Kumwambia mwanamke 'FANYA MAARIFA'

Kumwambia mwanamke 'FANYA MAARIFA'

Hahahahahahahaa Dilekeni dikeleni...... hehehehee looh acha nicheke kwanza sio kwa mabusu hayo..... asante best naona mabusu motomoto ujue mie ni Kasie Mahaba. ...... hehehehehe shauri lako...

Umenifanya nikumbuke busu alilopewa Mange na Roma Mkatoliki atii mmwaah. .. heheheheheee

Umemtaja James Jeddah mjeda akija hapa ujiandae kupigana shauri yako, mie simoo.

Karibu niko fildi kukusanya dodoso kumeanza tena.

Asante kunimiss ndo mie hapa nimejaa telee
hahaha yaani ulitakiwa ulipozaliwa uitwe Huba weye, Moyo wako wako,Stori zako,Sauti yako [emoji23] zimepambwa kwa manukato ya mahaba tu Kasie mahaba wee. Yaan ukiingia tu humu ndani ya Jf lazimia nisikie harufu ya huba lako.

[emoji23] [emoji23] Ya JJ tuyaache maana najua utanitetea, jicho lako tu latosha kushusha munkari wa yule bwana,

Daah habari ya madodoso umenikumbusha mbali sana,kuna experience unaipata huwezi kuipata kokote kule,ingawa watu hawawi wakweli sometimes ila ni kitu flani unique sana ktk kujifunza na kupata taarifa. All the best, usije walewesha wana kaya na hayo mahaba yako.......madodoso yatakosa udodosi [emoji23] [emoji23]
 
hahaha yaani ulitakiwa ulipozaliwa uitwe Huba weye,
Hahahahaaa inabidi uombe kibali cha kunibatiza niitwe Hubaa hehehehehe
Moyo wako wako,Stori zako,Sauti yako [emoji23] zimepambwa kwa manukato ya mahaba tu Kasie mahaba wee.

Ooh woow, umenifanya ning'are nijione mweupee kama cheupe dawa kumbee waalaa nimepakwa chocolate. Itabidi uninusishe hayo manukato ya mahaba maana mie hata sijui yananukiaje.....

Ila sauti umesikia wapi wewee.... mbona Kasie ana sauti ya bezi aka sauti ya zege hehehehe

Yaan ukiingia tu humu ndani ya Jf lazimia nisikie harufu ya huba lako.

Hahahahahaa huo ni uchochezi ujuee utanuniwa hehehehee shauri yako...

[emoji23] [emoji23] Ya JJ tuyaache maana najua utanitetea, jicho lako tu latosha kushusha munkari wa yule bwana,

Hahahahahahhaaaa Dikeleniiii oohooo shauri yakooo, haya macho ya mchina ya Kasie umeyaona wapii?
Daah habari ya madodoso umenikumbusha mbali sana,kuna experience unaipata huwezi kuipata kokote kule,ingawa watu hawawi wakweli sometimes ila ni kitu flani unique sana ktk kujifunza na kupata taarifa. All the best, usije walewesha wana kaya na hayo mahaba yako.......madodoso yatakosa udodosi [emoji23] [emoji23]
Yeah usemacho ni kweli kabisaa....
Hahahahaa hawawezi kulewa sana sana wao ndo watanilewesha mie. Udodosi lazima upatikane.

Mchana mwema.

Kasie Mahaba.
 
Hahahahaaa inabidi uombe kibali cha kunibatiza niitwe Hubaa

Moyo wako wako,Stori zako,Sauti yako [emoji23] zimepambwa kwa manukato ya mahaba tu Kasie mahaba wee. Yaan ukiingia tu humu ndani ya Jf lazimia nisikie harufu ya huba lako.

[emoji23] [emoji23] Ya JJ tuyaache maana najua utanitetea, jicho lako tu latosha kushusha munkari wa yule bwana,

Daah habari ya madodoso umenikumbusha mbali sana,kuna experience unaipata huwezi kuipata kokote kule,ingawa watu hawawi wakweli sometimes ila ni kitu flani unique sana ktk kujifunza na kupata taarifa. All the best, usije walewesha wana kaya na hayo mahaba yako.......madodoso yatakosa udodosi [emoji23] [emoji23]
[/QUOTE] hahaha haya niambie hiko kibali naende kukiombea wapi,najitoa muhanga mie @Hubaa
 
hahaha haya niambie hiko kibali naende kukiombea wapi,najitoa muhanga mie @Hubaa

Weeweee shauri yakooo, nime update hapo juu angalia quote nimeirekebisha.

Mtafute mtoa kibali yupoo....
 
Weeweee shauri yakooo, nime update hapo juu angalia quote nimeirekebisha.

Mtafute mtoa kibali yupoo....
hahaha yule hana nguvu kwako,ahemi,hapumui wala hakooi,chezea kumbato la huba lako [emoji23] [emoji23] Idhin yako ndio jambo la msingi zaidi kwangu kuliko chochote,afu si unajua mi na yeye damu zetu haziendani kabisaa [emoji23] [emoji23] Kasie umeniuzia kesi ujue.

Jion njema
 
Habari za jumapili wapendwa,

Leo nina kisa kioja swali...

Kwenye pilika pilika zangu za umesenja nikiwa fildi huko kukusanya dodoso kwa ajili ya miradi kadha wa kadha inayofadhiliwa na watu wa Mashariki ya mbali ndo nilikutana na kioja hiki.

Nilikaribia nyumba ya nne tangu nianze kukusanya dodoso nikiwa nimeambatana na mwenyeji wangu baada ya kunitambulisha yeye aliondoka kuendelea na shughuli zake na kuniacha mie niendelee na dodoso.

Baada ya dodoso kuisha nikiwa nataka kumuaga yule mwenye nyumba nirudi nilipofikia - nyumba ya kulala wageni... yule baba akaniambia mwanangu nina maswali.... nikamsikiliza na kumjibu kwa ufasaha. Akaniambia amejisikia tuu kunisimulia kisa alichokumbana nacho kwenye maisha yake na kumfanya hadi wakati huu hana familia. Ni babu mzee ambaye anajiweza kujimudu ila ndo anaishi mwenyewe na hana mtoto wala mke.

Basi mpenda masimulizi mie nikarudi kuketi nimsikilize babu ananisimulia nini.

Mwanangu, usemi wa kumwambia aliyekuwa mke wangu kipindi hicho umenifanya hadi leo sina familia Maana niliumia sana na sikuwa nimemaanisha alichokielewa mwanamke yule.

Huo mwaka hali ilikuwa ngumu mazao shambani hayakukubali biashara ya samaki mtoni pia ilikuwa ngumu. Nakumbuka siku hiyo nilirudi nyumbani saa kumi alasiri nikiwa sina kitu kwa ajili ya familia kula, nikamwambia mke wangu "FANYA MAARIFA BASI LEO TULE "nimerudi mikono mitupu.

Mke wangu aliguna na kubinjua midomo huku akinitizama kwa jicho la upande.... nakumbuka hakuniambia anaenda wapi ila alijitanda khanga na alitoka. Nilisikia harufu ya marashi aliyopaka baada ya kupiga hatua takriban tatu hivi. Nikakaa uani kusubiri maarifa ya mke wangu, kweli saa 12 jioni alirudi na kibaba cha mahindi, unga na choroko na usiku ukapita. Hilo ndo lilikuwa kosa langu tangu hapo mke wangu alianza kutembea na wanaume pale kijijini akisingizia anafanya maarifa tusilale njaa hata kama nikirudi na kitoweo nyumbani. Hali ile sikuweza kuivumilia nilimrudisha kwao na hatukuwa tumebarikiwa watoto. Tangu hapo sikutaka tena kuishi na mwanamke.

Sasa mwanangu hebu niambie. .. kwanza wewe una watoto? Nikamwambia hapana, umeolewa? Nikamwambia hapana...

Ila hivi mwanaume akamwambia mwanamke wake FANYA MAARIFA huwa mnaelewa kuwa amekutuma ukatembee na wanaume ndo ulete chakula nyumbani? Nikamwambia baba hapana si unaona mie niko kazini hapa ndo nipate mlo wangu japo sina wanaonitegemea.
Wewe unaelewaje?

Nikamwambia ningekuwa mie ningeenda kwa mwanamke mwenzangu pale kijijini aniazime kibaba cha unga na maharage au kunde kisha ukipata namrejeshea na si kwenda kukiuza kwa wanaume.

Haya mwanangu nakutakia kazi njema. Nikamjibu asante baba.

Swali kwa wakaka.....

Huwa inatokea siku hauna kitu na unaomba mwenzi wako aku assist? Anapokeaje ombi lako? Je ni fedheha kwako?

Swali kwa wadada na wamama....

Kufanya maarifa unaelewaje hasa ukiambiwa na mwenza wako siku anapokuwa hana kitu. Ni sawa au unaona si sawa?

Wiki moja baadae nikiwa kwenye sehemu ya umma wa watu wengi, mschana mmoja akiwa anaongea na wenzie akasema... mie bwana angu akiniambia mke wangu leo sina kitu fanya maarifa.... naenda kutembea na bwana nyuma yake tuu hapo mtaa wa pili wala siendi mbali....

Unafikiri kwanini huyu mschana amewaza hivi?

Kasie Mahaba.



Kumwambia mwanamke 'FANYA MAARIFA'
 
Hahahahahaaa wee babu umeibukia wapi? Hivi upoo? Nilijua nawe umekumbwa na gonjwa la kuogopa uhenga na kuja na NEW ID. .....

Maana humu unashangaa ID huijui na ni ngeni ila utasikia... Kasie za siku nyingi... nimekumiss....

Nashukuru kukuona bado upo japo si kama enzi zako zile ulikuwa akitivu hadi rahaa...




Back to the topic, kiukweli hata sikujua kama ulishaweka bandiko linalofanania na alikoweka Kasie.

Mie nilikutana na huo mkasa nikiwa fildi kukusanya dodoso wiki kadhaa zilizopita.

Wasalimie .........

Kasie Mahaba.
 
Hahahahahaaa wee babu umeibukia wapi? Hivi upoo? Nilijua nawe umekumbwa na gonjwa la kuogopa uhenga na kuja na NEW ID. .....

Maana humu unashangaa ID huijui na ni ngeni ila utasikia... Kasie za siku nyingi... nimekumiss....

Nashukuru kukuona bado upo japo si kama enzi zako zile ulikuwa akitivu hadi rahaa...




Back to the topic, kiukweli hata sikujua kama ulishaweka bandiko linalofanania na alikoweka Kasie.

Mie nilikutana na huo mkasa nikiwa fildi kukusanya dodoso wiki kadhaa zilizopita.

Wasalimie .........

Kasie Mahaba.

Nipo ...id ni hii hii tu
Magufuli anatukimbiza....
 
the boss maarifa mengi mnoo, siku hizi kuna akina mama wanapiga daiwaka anakuja anakufulia na kusafisha nyumba unampa elfu tano yake , watoto wanakula
 
..

Sasa 'haya maarifa' ya wanawake ni yapi?
The Boss Wanawake wana maarifa mengi sana,Muuza genge anafahamiana naye, muuza bucha anataniana naye, Kwa mangi ndio usiseme, Vibubwi ndio wenyewe, Kwenye michezo ya kina Mama anacheza michezo Mitatu majina mawilimawili yote anapokea,VICOBA ndio anakowekeza, Vyama vya wamama mitaani huko nako wamo. Maarifa ya mwisho ni yeye mwenyewe.
 
Back
Top Bottom