Kuna anguko kubwa sana la kujua kuandika sentensi na herufi sahihi za maneno miongoni mwetu Watanzania

O Level mwlimu wangu wa kiswahili alikua Mhaya... actual wacha nizienderee zanna..!!
 
Soma hapa tena na tena.

" mawasiliano kwa njia ya maandishi, sms, chats etc."
 
Watoto wengi siku hizi kuandika kwa usahihi ni janga kubwa, inafika muda unajiuliza huko shuleni wanasoma nini?

Ukipita Facebook watu hawawezi kutofautisha hakuna na akuna, hela na ela na vingine vingi. Kuna muda huwa naona labda mimi nazeeka ndiyo maana nacomplicate mambo!
 
 
Darasa la saba ukimaliza unajua kuandika vizuri lugha ya kiswahili, tatizo ni watu kujiendekeza
 
Tatizo kuna maneno mengi sana ambayo watanzania hawajawahi kuyaona kwa ufasaha wake yakiandikwa.

INakuwa ni ngumu sana kujua usahihi wa neno ambalo haujawahi kuliona likiandikwa na hiyo inapelekea shida hata kwenye kulitamka.

Njia bora ya kuwa fasaha katika uandishi ni kusoma sana makala na maandiko mbalimbali,hiyo itamfanya mtu kujua maneno namna yanavyoandikwa kwa usahihi.

Watanzania sisi sio wapenzi wa kusoma bali ni wapenzi wa kuangalia na kusikiliza,na katika kusikiliza hauwezi kupata usahihi wa maneno kwa sababu haujui yanatamkwa vipi.
 
Unasikia ati:
"Analia machozi" badala ya "Analia" au "Amalia na kutoa machozi"
"Amefariki dunia" badala ya "Amefariki" au "Ameaga dunia"
Kuchanganya au kutumia vibaya maneno.
"Sio" panapostahili kutumia"Siyo"
"Ndio" panapostahili kutumia"Ndiyo".
Hawa "Mbashara" wengine " Mubashara".
 
Kuna akina xaxa naenda xokoni na jomoni xitaki.
Yaani utopolo tu.
 
Kama mtu anaandika xaxa badala ya sasa cna badala ya sina halafu ukimuangalia ni mtu mzima na ni kiongozi wa taasisi kwa kweli hali ni mbaya mkuu mabadiliko ya haraka yanahitajika
 
Ni kweli hali ni tete.Majina ya watu,miji nk siku hizi yanaanza kwa herufi ndogo.Huo muandiko ndo usiseme,"S" inakatwa na mstari katikati ndo inakuwa nane,"f" inachorwa kama mswaki.Nafikiri wale walimu waliotufundisha kuumba herufi huku wakitushika mkono walipostaafu kilikuja kizazi cha .com ikawa ndo mwisho wa kuumba herufi.Na vile vidaftari vyenye mistari mikubwa na midogo vya kujifunzia miandiko sijui kama bado vipo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…