Kuna Basi la Mwendokasi lilikuwa linapita njia ambayo sio yake, limegonga mtu kwenye Zebra, amefariki Kimara

Kuna Basi la Mwendokasi lilikuwa linapita njia ambayo sio yake, limegonga mtu kwenye Zebra, amefariki Kimara

Mwendokasi zamani walikua wanaheshimu hizo zebra, siku hizi wanapita kishada.

Na watembea kwa miguu ni vizuri kuangalia pande zote, juzikati boda ilinikosa kwa hilo la kuamini gari zinatokea uapnde huu tu, kumbe kuna mwehu anapiaha na wenzie.
Hii ni kweli nimeshuhudia taa za Magomeni Usalama, ilipo DCB ,taa nyekundu jamaa anakanyaga tu Mafuta.
 
Aisee hizi gari zitamaliza watu sanaa wanendesha kama vile treni hawajali watembea kwa miguu wala wakatisha kwa boda bodaa ni kufagiaa tuuu...! Route ya mbagala ikianza kufanya kazi vifo vitazidi njia ya morogoro road watakufa wengi sana
 
Hawawezi kukubali hao wanaotoa hizi taarifa ni mashuhuda wewe kwasababu unaamin siasa unaenda kusikiliza wanasiasa wenzako, ndugu yangu aligongwa Magomeni akaambiwa maelezo aandike kagongwa na NOAH na sio Mwendokas
Nani amekuambia kuwa mimi ninaamini siasa? Hebu wacha utoto wako tafadhali🤣
 
Mwendokasi sijui wanashida gani
Hiyo tarehe nane niko kwenye bajaji, hapo korogwe, ghafla tunashtuka mwendokasi inaelekea kimara ipo upande wa kuelekea Ubungo, tena ipo kasi
Pengine ndo hiyo iligonga hapo kwenye Zebra🙌😓.
Wanajifanyia tu wanavyotaka, madai yao madereva ni wanajeshi.
Wawapeleke bukavu sasa
 
Kila anayegongwa na mwendokasi ni lazima afariki yule jamaa wa Kisutu tu ndio alipona, na siku hizi watu wanagongwa sana na Mwendokasi, juzi tu ilikuwa Magomeni bodaboda kachimbwa.. Mwaka jana kuna ndugu yangu kagongwa na mwendokasi kapewa ulemavu wa muda police wakawa wanamlazimisha aandike kagongwa na Noah
"police wakawa wanamlazimisha aandike kagongwa na Noah"
 
Habari, huku Mtaani kwetu kuna jamaa amefariki baada ya kupata ajali ya kugonjwa na basi la Mwendokasi jioni mida ya saa moja, Machi 8, 2025.

Mashuhuda wanasema kuwa kuna Basi la Mwendokasi ambalo lilikuwa linapita njia ambayo siyo ya kwake, ilikuwa ikitokea Ubungo kwenda Kimara lakini ikapita katika njia ya kutokea Kimara kwenda Ubungo.

Hivyo, jamaa wakati anavuka alikuwa ameelekeza macho upande mwingine, bahati mbaya ni kuwa basi hilo likamgonga kwa kuwa lilikuwa katika nia iliyokuwa yake na halikusimama baada ya hapo.

Marehemu alikuwa ni Dalali, zamani alikuwa muuza chipi mitaa ya Korogwe anafahamika kwa jina moja la Daniel, alibebwa na wenzake akapelekwa Hospitali ya Mwananyamala ambapo mwili wake upo huko mpaka sasa.

Wenyeji wa Kimara wanamjua na vizuri na wengi tupo hapa kwenye msiba mpaka muda huu naandika andiko hili.

Huyu mtu ni mwenyeji wa Singida lakini aliondoka kwao miaka mingi, hivyo ndugu zake wengi hawajulikani kiivyo, lakini msiba kwa sasa upo hapa Kimara Korogwe, kinachoendelea ni michango ili kukamilisha mchakato wa kufanikisha kumzika.

Ukifika Korogwe Baa au kwa Pati napo ndipo msiba ulipo, kwa anayehitaji kufika karibuni.

Kinachosikitisha ni kuwa Mwendokasi hawajatoa tamko lolote na wanaweza kukaa kwa kuwa basi lenyewe halikusimama.

Tunaomba Uongozi wa Mabasi ya Mwendokasi mje mtoe hata rambirambi, kama nikivyoeleza msiba upo hapa Korogwe Baa au mnaweza kuulizia Kwa Pati.


DART WASEMA SIO KWELI
JamiiForums imewasiliana na Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) kupitia kwa Ofisa wa Kitengo cha Habari DART, Elias Malima, awali alisema anafuatilia baada ya kupewa taarifa hiyo.

Baadaye akarejea na kusema “Nimefuatilia taatifa hizo sio za kweli, hakuna popote ambapo imeripotiwa juu ya tukio hilo na wakati huu ambapo kuna watu wengi wnaweza kuripoti ingekuwa imeshajulikana tu.

“Huku kwetu hatuna ripoti ya aina hiyo, pia suala la kusema basi lilikuwa linapita njia ambayo siyo yake sijawahi kusikia.”
.
Inasikitisha sana.

Mifumo yetu yote imekaa shagala baghala. Ukiona boda zinavyoendeshwa ni hovyo kabisa. Ukiona baadhi ya magari yanavyoendeshwa, yakiwemo ya Serikali na taasisi zake, ni hovyo kabisa. Kila siku ni misiba na ulemavu, na kwa kiasi kikubwa ni kwa sababu mifumo yetu ni ya hovyo, usimamizi ni wa hovyo kabisa, na hivyo kufanya kila kitu kiwe cha hovyo.

Wasimizi wa sheria na mifumo, hakuna wanachofanya zaidi ya kuelekeza nguvu zao kwenye mambo ya kisiasa, kuwalinda watawala na CCM hata katika mambo ya hovyo.

Turudi kutoka pale tulipopotoka. Polisi wasimamie sheria zote za barabarani kikamilifu, bila ya kubagua aina ya chombo (iwe gari, pikipiki, baiskeli au mwenda kwa miguu: kila mmoja afuate sheria) mmiliki wake (iwe mmiliki binafsi, kampuni au Serikali).
 
Angalau wewe umejisemea Ukweli, wengi hapa JF uongo mtupu. Uangalifu wakati wa kuvuka Barabara ni shida hapa mjini. Imagine mtu anaamini Zebra siku hizi! Wakati wa JPM sawa ila sasa wakati wa mama, kuamini zebra ni kukitafuta kifo
Nimewahi simama Zebra nikiwa na gari..kidogo niwe sababu ya watoto watu kutolewa uhai.Yule Boda hatosahau maisha yake.Sijui nilipata wapi nguvu ya kushuka haraka na utoa dozi iliyokamilika kwenye lile tukio.
Mpaka kesho nikisimama na gari kwenye zebra,nisipokuwa na mtu upande wa abiria nakosa amani 100%
 
Kuanzia saa 12 jioni kuanzia Kimara Baruti Hadi Kimara SUKA lazima uwe Makini.
Hicho kipande sio Rafiki Kabisa kwa watembea kwa Miguu. Ni Hatari Sana.

Imekuwa kawaida gari kutumia upande usiowao wakati wa jioni hasa zinazotokea Mjini.
 
Kuanzia saa 12 jioni kuanzia Kimara Baruti Hadi Kimara SUKA lazima uwe Makini.
Hicho kipande sio Rafiki Kabisa kwa watembea kwa Miguu. Ni Hatari Sana.

Imekuwa kawaida gari kutumia upande usiowao wakati wa jioni hasa zinazotokea Mjini.
Hivi wameruhusiwa?
Manake nimeona tena leo gari za jesho zinapita upande siyo wake
 
Mkuu boda wamezidi hiyo kwao kawaida niliwahi isema humu nikaonekana mjinga , jamaa wanaacha nji.a sahihi hivyo ni vyema kucheck pande zote mimi nilisikia tu shati inagongwa KUCHEKI hivi kumbe boda kicha kapita kwa Kasi niloshukuru Mungu tu
Kabisa mkuu, yani ni kua makini tu aisee
 
Back
Top Bottom