Kuna genge limejipanga kuharibu kwa makusudi sifa na hadhi ya Rais Samia

Unatetea ujinga unasema hakuwa kuwa na Genge kwenye chama,Lile Genge la msoga umelisahau si la huyu Mama?
weka ushahidi wako na kama lile genge lake basi wale wananguvu kuliko genge lolote unalolijuwa.
 
Huyu poisonous hana anachojua, ni chawa wa mama anachojua yeye ni kumfichia Samia madhaifu yake yakutoa bure bandari zetu.
Bandari zetu na wajomba zako au? una bandari wewe tafuta pesa ujengee watoto wako nyumba acha kujimilikisha mali isiyokuhusu. Eti Bandari zetu..... tafuta pesa
 
Acha kutuletea ujinga wewe. Eti genge wakati mtu mwenyewe kashaonesha hafai kua rais wa tanzania. Kazi anashindwa kufanya and the anaamini nje tu ndio wataweza kuendesha nchi yetu? Au pengine ni mpigaji mpenda rushwa. Waliyovujisha haya maelewani ni wazalendo kabisa. Eti dubai ndio wawe na hati miliki kujenga miradi na kuendesha bandari zetu zote? Sasa hii nchi ni yetu au ya sultani wa dubai. Tuna uwezo kuendesha nchi yetu mtu asituletee mchezo hapa.
 
Sa 100 amechoka Yaani naona anajikongoja tu Kabla ya 2025 anaweza jiudhuru cheo
 
Sasa ndo wauze Bandari,embu tumia basi walau akili kidogo?
Usikariri na wewe basi tumia akili kidogo, kama wameuza basi hakuna haja ya ku contact ingekuwa hati ya mauzo sasa hamueleweki mara mkataba hauna kikomo, mara wameuza, mara miaka 100 mara vifungu vibaya hujui shida nini mara waarabu. Kama watu wanataka kujadili issue tujadili issue kwa ushahidi. Investor yoyote akija kuna vitu lazima apate kumpa confidence hiyo ni kawaida duniani kote. Na mkataba ni pande mbili una malengo tofauti ya kimaslahi. Sasa muwe wa wazi shida hatutaki wawekazaji au waarabu au nini hasa tunahitaji? sisi kama sisi ufanisi zero, shida ya sisi wa Tz tunadhani bandari kama mlima kilimanjaro tumeshushiwa na Mungu, bandari imejengwa na itaendelea kujengwa sababu biashara ya port inabadilikika na tech kila siku, meli sio ndogondgo tena ni meli kubwa sisi hatuna uwezo huo. Na hapa sio lazima DP aje kama mnaye mwekezaji bora kuliko DP apendekezwe ila ni lazima tuondoke kwenye ukiritimba wa bandari.
 
Awatoe kwenye system aweke wengine
 
Mpambe sana lakini ukweli ni kwamba mama amejihalibia sifa yeye mwenyewe. Kwa mambo haya huoni kama mama ameamua kujihalibia mwenyewe?

1. KIKOKOTOO (kilio kikubwa sana)
2. BANDARI [Kwa tz bara tu!!]
3. CIG REPORT (Hakuna hatua)
4. HUDUMA OFISI ZA SERIKALI (tumerudi kulekuleee)
 
Naiamini issue ya bandari baada ya kuysoma ule mkataba mbovu mlioingia na mwarabu, simsubiri Lissu wala mwingine yeyote aje kunitafsiria yaliyoandikwa kwenye ule mkataba, najielewa.

Unapodai tunakosa classified data, hebu wewe tuwekee hapa hizo data zako classified tuzione, kinyume na hapo wewe ni tapeli tu, eti unazo hizo data lakini unazificha, wewe ni chawa wa Samia, simple.
 
Wote akili zenu zinafanana, Samia wakati anahangaika kuwaondoa kina Lukuvi alikuwa anatengeneza kitu gani?

Anyway, ukiandika kwanza jifunze kuweka paragraph.
 
Uzuri wamezoeya kupiga wamekosa pakupiga wanapigana waokwawao wacha waendelee vinamwisho mfupi sana visivyo haki
 
Wote akili zenu zinafanana, Samia wakati anahangaika kuwaondoa kina Lukuvi alikuwa anatengeneza kitu gani?

Anyway, ukiandika kwanza jifunze kuweka paragraph.
Wewe soma unataka kufanya mitihani ya paraghraph kajiunge shule. Hapa soma elewa move on....
 
Naomba kukuuliza huo mkataba ukomo wake ni lini,na kwann hakuna sababu yyte ya kuvunja mkataba ata ikitoea bahari ikakauka...huu si Ujuha kabsa wa viongozi wetu kuanzia huko juu?
 
mamako ana hadhi gani tuanzie hapo. Pumbavu kabisa yule yuko kati ya wanawake 100 bora duniani, ana uwezo mkubwa sana. Unataka kumlinganisha na mamako aliyezaa kima km wewe? Shenzy lisilo na aibu
inaonekana uliteswa sana ulipokua mtoto
 
Bandari kwanza mambo mengine baadae
 
Rais yupi anaharibiwa, kizuri huwa kinajiuza kibaya kina jizurulisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…