Tetesi: Kuna jambo baya linaendelea Mtwara...

Tetesi: Kuna jambo baya linaendelea Mtwara...

Hao jamaa inaonekana wamedhamiria na mfadhili wao hajatetereshwa kiuchumi na corona. Cha msingi na sisi tumvurugie huyo mfadhili wao kwa kutengeneza makundi kama hayo na kumtupia hao nyuki naye ajue machungu yake. Tukijifanya tunaendana nao sawa hao invisible army, itatukosti sana.
 
Hao jamaa inaonekana wamedhamiria na mfadhili wao hajatetereshwa kiuchumi na corona. Cha msingi na sisi tumvurugie huyo mfadhili wao kwa kutengeneza makundi kama hayo na kumtupia hao nyuki naye ajue machungu yake. Tukijifanya tunaendana nao sawa hao invisible army, itatukosti sana.
Mfadhili wao nani?
 
Nimepata habari, , kutoka kwa Jamaa yangu Hapa"" kwamba kaka yake"" Jana" jion ameletwa Lugalo Hosp"".... Yeye na wenzake.....
Wakiwa na majeraha"" baada ya Ambush!

Kutoka kwa waasi!
Japo" nduguye amezuiwa mawasiliano"" ila halipata simu'mara moja"" na kutoa Taarifa"kwao"

My take:
Kama kuna ukweli wowote juu ya hili jambo tuwekwe wazi!

N.B
Wazazi wameenda Lugalo Hosp""
Na wamezuiliwa kwanza mpka hatua za kijeshi zifuatwe!
 
BBC imetoa ripoti ikionyesha kuwa watu 20 wameuawa siku ya jumatano kati ya mpaka wa Tanzania na Msumbiji katika eneo la kijiji cha Kataya mto Ruvuma

https://www.bbc.com/news/topics/cjnwl8q4qdrt/tanzania

Screenshot_20201016-153842_Samsung Internet.jpg
 
Wasalaam wana Jf,

Tanzania na Nigeria ni nchi rafiki kwa zaidi ya miongo minne sasa. Urafiki wa nchi hizi mbili sio wa kutilia mashaka hata kidogo hususani katika masuala ya kiuchumi , siasa na mbinu za ulinzi na usalama. Inasemekana wakati fulani Tanzania ikiwa kwenye harakati za vita na Idd Amin kama sikosei au wakati wa vita vya ukombozi wa nchi za kusini mwa Afrika (wenye kumbukumbu sahihi mtanidokeza kwenye komenti) Nigeria ilitoa msaada mkubwa sana wa kiinteligensia kwa watanzania walipofanikiwa kunasa mawasiliano ndege iliyokuwa inakuja Tanzania kwa dhamira ovu na Tanzania waliutumia vizuri ushauri wao kuishugulikia ndege hiyo na kuishangaza dunia kwa weledi wao wa vita.

kwa kipindi cha wiki mbili nchi hizi zinapitia majaribu makubwa sana ya usalama wa nchi zao. Kule Nigeria kumeanza maandamano ambayo kama hawatachukua hatua huenda yakawa hayana ukomo. Maana walilalamika shida ni kikosi cha SARS, nasikia kimefutwa lakini wana nzengo bado wanatiririka ile mbaya mitaani kudai haki zao sielewi lini yatakwisha lakini uzoefu unaonesha hapa lengo sio SARS kuna mtu anatakiwa apakwe kinyesi anuke na aondoke ikulu au uwe mwanzo wa mapinduzi kama ya nchi za kiarabu.

Tanzania inapitia kipindi kigumu cha uchaguzi ndani ya siku 10 zijazo, nasikia eti kule kusini kuna chokochoko za wasiotupenda kushambulia wananchi wasio na hatia na kutoa lugha ya kejeli na dharau kwa jeshi letu. Kwangu zinabaki kuwa tetesi kwa sababu mamlaka husika hazijasema kuwa kuna baya linaendelea na kama lipo basi tuchukue tahadhari za usalama wa raia wetu na mali zao kwa sababu rafiki yetu kipenzi anapitia wakati mgumu na itakuwa ngumu kushauri na kutusaidia uzoefu wake wa kupambana na vikundi kama hicho kinacholeta chokochoko huko kusini sababu atakuwa bize na maisha yake.

Tusipuuze ushauri au mawazo watakayotupa Nigeria kwa sababu wao wanaishi navyo vikundi hivi na ukitizama kwa makini utagundua miji yenye gesi na mafuta ndio haswaa inasumbuliwa na shida hii.

Lakini natoa rai kwa nchi hizi mbili kuchukua tahadhari ya hali ya juu na kuiuliza why sisi na wao kwa wakati huu mmoja? je kuna dalili na sisi kwetu watu wakayatumia vibaya matokeo ya uchaguzi kupata sababu, kisingizio na mwamvuli wa kuandamana? na kama wataandamana je, maandamano hao yatakuwa na kikomo au ndio style ile ya Arab regime, ndio maaana nasema wachukue tahadhari za usalama kwa raia wao.

karibuni kwa michango mawazo mazuri, weka ushabiki pembeni tufungue mjadala mpana na wenye fikra pevu.
 
Duh! Mbona hii hatari sasa, tatizo la Watanzania, huwa hawataki kuungana na majirani kwenye kupambana na haya magaidi, tuliwaambia uhusika wetu Somalia huwa tunapambana kuhakikisha mashababi hayaoti mapembe na kuvuruga ukanda wote wa Afrika Mashariki, tunawafuata hadi kwenye shina.

Watanzania wamekua wakichekelea na kukunja mikia kwa uwoga huku majirani wote wakiwemo Uganda, Rwanda n.k. wakipeleka majeshi yao Somalia wamesahau kuna vijana wa Kitanzania wengi tu wameenda kupata mafunzo ya ugaidi Somalia, na tunao ambao wamekamatwa Kenya wakifanya ugaidi.

Vivyo hivyo Tanzania imekua ikionyesha udhaifu na uzembe kwenye vurugu za Msumbiji, wanaambiwa kwamba raia wao Watanzania haswa ndio magaidi kule, wanachekelea na kunyamaza, sasa hayo magaidi yameanza kugeuza na kurudi nyumbani. Yanachoma vijiji na kukata watu vichwa, halafu huwa siyaelewi haya magaidi, unaua wanavijiji ili iweje, hovyo sana bladi mani na zao.

Magaidi wanapaswa kuuawa bila huruma, Watanzania acheni uwoga, uzembe na udhaifu, unganeni na wenzenu kwenye hili pambano, hawa vijana hawapaswi kuogopwa, wapewe moto kama dawa.
 
Katika siku mbili hizi kumetrend ktk mitandao video zikionesha wahuni wanaojita waislam wakivamia kijiji kule Mtwara na kuchoma moto kuua mmoja ya muathirika akikatwa kichwa,huku wahuni hao wakijigamba kuja kuleta dola ya kiislam.

Kwanza ieleweke wazi ktk uislam hakuna uhuni kama huu unaoelekezwa hivi kuwa ili mtu mwingine aweze kufuata imani yako mpaka atishwe kwa vipigo,kuuawa,kuharibu Mali na Mtume Muhammad ametuelekeza tuishi na watu wa imani nyingine kwa kuvumiliana na amani sambamba na hilo kuwalingania/kushawishi kwa maneno na matendo mazuri kuingia ktk imani yangu, sasa Duniani Leo pameibuka makundi kama boko haram,Isis, na vikundi vidogovidogo kama hivi kwa wahuni wa Mtwara vikijinasibu kwa kivuli cha uislam kwa hili Mimi kama Muislam nalipinga wazi kabisa.

UHUNI HUU USIINGIZWE KATIKA SIASA
Ningetoa rai Katika hili kwa uhuni huu uliotokea kama ni kweli basi pasijetokea Mwanasiasa akaanza kutafutia kiki za kisiasa kama Yale yaliyotokea kule kibiti,Askari wetu walikufa familia zao zimebaki bila ya wategemezi wengine walikuwa wanategemewa na ukoo wakaenda kwa ajili ya kutetea Taifa hili na hatua zilipoanza kuchukuliwa kwa walengwa wa uhuni ule Baadhi ya wanasiasa walipiga kelele za kupotea watu ambao ndio haohao wahuni wenyewe maana hata hizi clip ukiwasikiliza unaona wazi ni ndugu zetu waswahili wenzetu walioamua kukengeuka kwa kigezo cha Dini kwahiyo tutegemee majibu makali na tuvumilie tu na siasa ikae mbali ktk hili.

WITO KWA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA
Ningependa kuvipongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa mioyo yao ya kizalendo katika kupambana na matukio matukio mbalimbali ya kihalifu hasa la vikundi kama hivi kama kule Kibiti. Askari wetu wamejitolea roho zao hata kufa ili sisi tulale na wake, waume pamoja na familia zetu kwa amani, tunavishukuru vyombo hivi kwa kujitolea kwao, kama Serikali haikuwakumbuka katika Maslahi yao basi naamini wana ujira mkubwa hata Mbinguni, wasife Moyo kwa magumu na changamoto wanazopitia na kama lipo hili linalosambaa kwenye viclip naamini litapita haijalishi litagharimu roho ngapi katika kipindi hiki cha mpito naamini litakuwa na majibu makali sana, Kwenu mtakaokuwa mstari wa mbele katika mapambano hayo tunawaombea kheri.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Kuna habari na video zipo kila mahali kuonyesha Al-Shabab ya Central Africa wakiwa wanafyetua risasi ovyo kwenye makazi ya wananchi wa Tanzania ndani ya mpaka wa Tanzania,.

Inaaminika kuna idadi kubwa ya wananchi wametekwa na kupelekwa kusikojulikana, Kwa maelezo ya mbunge wa zamani wa Tandahimba ambaye sasa anagombea jimbo la Mtwara anayeitwa Nachumu, ameeleza kuwa familia yake wametekwa watu tisa, kwa maelezo yake ni kuwa waliochukuliwa na wasichana wa miaka 18 na kuendelea na watoto.

Kinachosikitisha hatusikii lolote kutoka Police au msemaji wa JWTZ, au rais Magufuli. Hii habari ni ya kutisha na ya kuhuzunisha sana, Watanzania wengi tungependa kuona watoto wetu wanaokolewa na kurudishwa kwa wazazi au kwa familia zao. Kuna habari kuwa askari wawili wa JWTZ walichinjwa (beheaded)na kifaru chao cha aina ya WZ-551 au ZSL92 au maarufu kama T-92 kilitekwa na kuharibiwa.

Mwezi na nusu uliopita kulikuwa na habari kuwa kuna wanajeshi wetu wapatao 20 wameuawa huko Mocimboa da Praia kwenye jimbo la Cabo Delgado iliyopo Northern Mozambique, hao Al Shabab ambao wameteka mji huu ulio kwenye jimbo la utajiri wa gesi asilia walionyesha na vitambulisho kama viwili vya wanajeshi wetu kuonyesha hao wameuawa.

Bado serikali imenyamaza, JWTZ na polisi wamenyamaza, sasa yamekuja madai mengine yaliyothibitishwa na uchomaji moto wa nyumba za wananchi na watu kuuawa lakini hakuna tunalosikia kutoka serikalini ni KIMYA tu.

Je, ni utamaduni wa Rais Magufuli na serikali yake kukaa kimya inapotokea majanga kama haya yanayoathiri maisha ya watanzania? Wananchi tuna wasiwasi haya mauaji na utekaji hovyo wa raia.

Watanzania tungependa kujua yafuatayo:

1. Idadi ya raia walioathiri na shambulio hilo ikiwemo waliokufa na waliojeruhiwa
2. Vijana wetu na wananchi wengine waliotekwa, Serikali imeshawapata? au inawatafuta na imefikia wapi? na ni idadi gani wametekwa?
3. Je, Serikali yetu inayo majeshi yake ndani ya Msumbiji?
4. Serikali ina mikakati gani ya kuwatokomeza hao wauaji ili wasirudi ndani ya mipaka ya nchi yetu?
5 Je, serikali kwanini inaficha hili tatizo? Kuna sababu za msingi?
Haya ni mambo yanayohusu maslahi ya Taifa letu, Halina connection na uchaguzi.

Naomba MOD wa JF hili suala tulijadili
Asanteni sana
 
Kilichopo tu ni kwamba baada ya 'Wahuni' hawa 'Wanamgambo' kuondolewa na JWTZ kwa 'style' ambayo hawatakuja Kuisahau huko Mkuranga, Kibiti na Rufiji 'walipoichokoza' Tanzania baadhi yao hasa wale Waandamizi wao walikimbilia nchini Msumbuji ambako ndiko kuna Ngome yao Kuu na hata walipokuja huku Pwani na kule Amboni Tanga walitokea huko huko.

Taarifa nilizothibitishiwa na Chanzo kutoka katika 'Kikosi Maalum' ni kwamba hawa 'Wahuni' wanatamba na kusumbua sana tu huko nchini Msumbuji japo kwa miezi kama Saba ( 7 ) hivi iliyopita walikuja maeneo ya mpakani na Tanzania ila kutokana na 'Intelligence' imara ya Tanzania na ile ya Jeshini ( CMI ) waliweza 'Kudhibitiwa' na wakakimbilia huko 'Ngomeni' Kwao Msumbiji.

Na ni kweli kwamba 'Wahuni' hawa ( ambao ni Wanamgambo ) wana 'Vifaa' vikubwa tu na uwezo mkubwa wa Kivita hasa hii ya Msituni ( Guerrilla ) na 'Mafunzo' makubwa sana ya 'Kivita' hali ambayo imefanya mpaka wameweza 'Kupambana' vilivyo na 'Jeshi' dhaifu kwa sasa la Msumbiji na kuweza kuteka Bandari muhimu huko ambayo inawasaidia Kuwaingizia Kipato na 'Kutamba' pia.

Kuna taarifa tulipewa kuwa Wanajeshi wa Tanzania ( JWTZ ) sijui 'wametekwa' na Kukimbia hadi Kukiacha 'Kifaru' huku tukiaminishwa kwa 'Video' ila ukweli ni kwamba kilichoonekana siyo 'Kifaru' bali ni 'APC' nadhani wale Watu wa 'Medani' hapa mtakuwa mnaelewa na si vibaya pia mkija kutusaidia zaidi 'Kutuelimisha' juu ya hiki Chombo.

Kuhusu Picha ( Poster ) ya Mgombea Urais wa CCM ( sasa ni Rais ) Dkt. Magufuli kuonekana kwa hawa Wahuni ( Wanamgambo ) ni sehemu tu ya 'Propaganda' ya Watu wenye 'Chuki' na Tanzania na hasa ikiwa inaelekea katika Uchaguzi Mkuu huu ujao kama 'Kuichafua' na hata Kuzua 'Hofu / Tafrani' miongoni mwa Watanzania na hasa hasa Wakazi wa huko Mtwara.

Tumeambiwa kuwa kuna Watanzania 'waliokufa' huko na kwamba hali ni ya 'wasiwasi' mno huko Mkoani Mtwara hasa eneo la Nanyamba ila ukweli ni kwamba eneo liko salama kabisa tena 100% na hakuna 'Mauwaji' yoyote yale isipokuwa Jeshi la Tanzania ( JWTZ ) kwa Kushirikiana na Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama vimeendelea tu 'Kuimarisha' Usalama huko.

Kilichonishangaza zaidi GENTAMYCINE ni kwamba nina Ndugu zangu huko na nimefanya 'Jitihada' za 'Kudadisi' kama kuna 'sintofahamu' ya aina yoyote ile inayohatarisha Amani huko ( kama tunavyoaminishwa ) nilichojibiwa tu ni kwamba Mtwara iko salama. Na nawaombeni nanyi wana JF pia mjaribu Kuwasiliana na Watu wenu huko ili muweze 'Kujihakikishia' juu ya hili.

Nimalizie tu kwa Kuishukuru Serikali ya Tanzania chini yake Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt. Magufuli pamoja na Vikosi vyote vya Ulinzi na Usalama nchini Tanzania kwa 'Kupuuza' na Kuunyamazia 'Uzushi' huu ambao 'unaratibiwa' vyema kabisa na wale wasioitakia mema nchi yetu na kutaka kuleta 'taharuki' hasa wakiwa na lengo la Kuitia nchi 'Doa' la Kiusalama na Amani yake.

Asante sana na mno Wewe 'Chanzo Changu' kutoka hapo 'Kikosi Maalum' juu ya hili na Mimi nimeamua 'Kushea' hapa na Watanzania wenzangu.
 
Hali si nzuri na watu wanachinjwa kama kuku na Al shabab toka Msumbiji. Video ziko 3 lakini moja inatisha sana mtu anachinjwa live

 
Idhaa ya kiswahili ya CRI Kiswahili imeripoti hivyo kupitia ukurasa wao wa Facebook
 
Wazee leo katika mishe mishe Sina hili Wala lile nikapokea simu ya dogo wangu ni mwanajeshi kambi flani akaniambia bro niko safarini naelekea Mtwara.

Katika kunieleza akasema kule kuna Hawa Islamic State wameingia na mbaya zaidi walimkamata mwanajeshi wamemuua na wakamkata kichwa. Pia kuna habari kwamba wameteka watu zaidi ya 30. Sasa basi juzi waliitisha kikao kambini na kupewa maelekezo na wameanza safari ya kuelekea mtwara huko kupambana na hawa magaidi.

Katika kumuuliza zaidi na kuomuombea kwamba Mungu amlinde na wamelize zoezi salama huku nikiwa na mshituko kidogo dogo akaniambia usiwe na wasiwasi tuko vizuri na tumejipanga pia tumebeba siraha nzito nzito yani tukifika ni Moto tu paka waelewe yani kimsingi tuko vizuri

Daah hili nalo linakichanganya kwamba wamebeba siraha nzito na za kutosha huko kuna nini?

Kwa wanaojua je huko kumetokea Nini na kwa Nini serikali Kama hakuma taarifa za haya matukio?

Yote kwa yote nawaombea Askari wote wanaoenda huko na dogo pia Mungu awe nao na warudi salama
In God we trust[emoji123]
 
Hali ni tete huko Mtwara,,,tuwaunge mkono majeshi yetu.. Vita havina macho... Kama mtu hana shuguli maalum ya kufuata huko Mtwara, asiende.
 
Back
Top Bottom