Zanzibar 2020 Kuna kijungu kinapigwa Visiwani, ni Uchaguzi wa hatma ya Zanzibar

WanaCCM tunaopenda ukweli, basi ni huu " MAGUFULI UMEMPA USHINDI MAALIM SEIF KWENYE SAHANI YA DHAHABU"

Magufuli unaiuwa CCM yetu, huna dhamira nzuri na chama chetu, tunajua hadi yako kwa mzee mwinyi, na sasa Ahadi yako kwa Lowassa.
Huyu baba ana matatizo makubwa kama kweli aliwaahidi
 
Nani mwenye habari za uhakika kukamatwa Serukambi Dodoma na pesa njingi sana ambazo zilitumika katika operation za uchaguzi wa Hussein Mwinyi.

Pia Inasemekana hizo pesa zimetoka kwa Rostam
oooohhhh
 
Tunaendelea kuwapeni habari zetu za tathmini. Bado timu iko visiwani ikitupatia tathmini mbali mbali za kisiasa na kijamii.

Huko visiwani kuna kijungu chapagwa...
shehe, mwaka huu Wazanzibari mmeletewa tena Mndengereko wa pale Mkuranga.

mnaloo!
 
Tujiandae saa tatu kamili kutazama mahojiano mahsusi Kati Dr. Hussein Mwinyi(Rais mtarajiwa wa Zanzibar) na Tido Muhando UTv(Channel 108 azam tv)
 
Ukisema hivyo unamaanisha hao wengine hawakupata kura hata moja kutoka kwa wajumbe wa bara? Huoni hesabu zako zinakataa?

Mungu Ibariki Tz - MITz
 
Ukisema hivyo unamaanisha hao wengine hawakupata kura hata moja kutoka kwa wajumbe wa bara? Huoni hesabu zako zinakataa?

Mungu Ibariki Tz - MITz
 
Ukisema hivyo unamaanisha hao wengine hawakupata kura hata moja kutoka kwa wajumbe wa bara? Huoni hesabu zako zinakataa?

Mungu Ibariki Tz - MITz
Hapana hesabu hazijakataa ni ukweli usopingika mgombea pekee katika wagombea watatu aliyekuwa anakubalika pande zote mbili za ccm bara na zanzibar ni dk Hussein.

Ninaamini bila Shaka yoyote kura 95 za wajumbe wa nec bara zilienda Kwa Hussein Mwinyi. Kwa sababu wao pia walikuwa wanaamini mgombea bora katika watatu alikuwa mh Hussein na Kwa siasa zanzibar zilivyo ni rahisi sana hussein kupata upinzani zanzibar kuliko bara na hiyo hesabu ipo wazi kabisa.

Na ndio hata mh mwenyekiti wa ccm mh rais Magufuli aliwaponda wale walokuwa wanasema Hussein hatoshi wanaosema hivyo wanatoka zanzibar. Laiti ingekuwa kura zile zinapigwa wajumbe wa bara peke yao na zanzibar peke yao ungethibitisha maneno yangu.
 
WanaCCM tunaopenda ukweli, basi ni huu " MAGUFULI UMEMPA USHINDI MAALIM SEIF KWENYE SAHANI YA DHAHABU"

Magufuli unaiuwa CCM yetu, huna dhamira nzuri na chama chetu, tunajua hadi yako kwa mzee mwinyi, na sasa Ahadi yako kwa Lowassa.
Mkuu mbona unaota ndoto za jioni,Maalim katu hataweza kushinda na kuwa raisi wa Zanzibar .
 
Kama kweli amekataliwa na znz wote ina maana atapata kura moja ambayo ni yake. Nasubiri hili litokee ili uwe right otherwise ni unafiki wa kisiasa tu. Yaani hata baba yake na mkewe?

Muda utaongea.
Unauhakika kuwa baba yake ni mpigakura wa Zanzibar?
 
Kwani nani mwenye asili ya Zanzibar wengi wana asili ya Bara
 
Chadema mnahangaika Sana kuanzisha mada za Zanzibar ya kwenu yanawafodea Zanzibar hamna chenu hamna hata mtia Nia mmoja wa ubunge!!

Pambaneni na hali zenu ya Zanzibar waachieni wenyewe ambao wawe CCM wawe vyama vya Upinzani hawako tayari kumpa kura hata moja mgombea wa ubunge wa chadema.

Kwa hilo CCM na Upinzani Zanzibar tuko pamoja .Tuna tofauti zetu lakini likifika Swala la Chadema tuko pamoja .Ya Zanzibar yaacheni nyie chadema.Hamna chenu kule
 
Achana na chadema hizo mada Wala waanzilishi sio Wana CCM Ni Chadema.Hakuna chama kikichojaa wambeya Kama Chadema
 
Propaganda hizi
Nimejaribu kupitia comments. Bado hakuna hoja za kubainisha ushindi wa dr Hussein isipokuwa kwa kujiegemeza kwenye historia tu ya kutumika vyombo vya dola.

Katika mazingira huru ya uchaguzi Zanzibar, hakuna CCm yoyote anapenya kwa sasa.

Mara hii kumeongezeka kibwagizo "Hatma ya Zanzibar" bado nasema kuna mvumo uko chini chini.
 
Kwani nani mwenye asili ya Zanzibar wengi wana asili ya Bara
As long as Mwana CCM hawezi kuitetea Zanzibar kwa njia yoyote ile basi hilo ni pengo kwa mazingira ya Zanzibar na ni turufu kwa upinzani. Kwa sababu ya maelekezo ya chama, Wazanznibari walio CCm wameprove failure kuthubutu kupigania maslahi ya Zanzibar.

Kosa walilolifanya CCM ni kujisahau kuwa wenzao wana malengo ya kwenda serikali moja. Sasa imefika wakati instruments za chama upande wa Zanziubar zinashikiliwa na wazanzibari wenye maslahi ya Bara moja kwa moja. Hili ni kosa.

walidhani kuondowa nafasi ya Rais wa Zanzibar kuwa makamo wa rais JMT kwamba wanamkomoa Maalim Seif ambaye walihofu atakuwa rais kwenye chaguzi zas nyuma. Wenzao wakatumia mwanya kupeleka ajenda zao mbele.

Leo hii wanaugumia maimivu kimya kimya. kila chaguo lao linazimwa kwa maamuzi ya chama ambayo yako strategically.

Kila wakitafakari si CCM asili Zanzibar wala nani wote wanaelekea kupoteza ushawishi ni suala la muda TU.

Muungano oyeeeeeeeee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…