Kuna kila dalili kuwa Putin kaanza kukata tamaa!

Kuna kila dalili kuwa Putin kaanza kukata tamaa!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Sio siri tena kwa sasa vita vya Ukraine imeshika kasi huku Russia ikipitia kipindi kigumu zaidi huenda kuliko kipindi kingine chochote tangu kuanza kwa hii vita.

Kuna dalili fulani ambazo zinazoonyesha kama vile Putin pumzi inaelekea kukata. Hizi hapa chini ni baadhi ya sababu muhimu zenye kueleza hayo;

1. Kitisho cha kutaka kutumia Nyuklia ili kumaliza vita.
Sote tunajua Russia ni taifa kubwa kijeshi likiwa na shehena za kila namna za kivita na kiteknolojia, kitendo chochote cha Russia kupiga mkwara kuwa huenda wakaanza kutumia nyuklia ili kuishinda Ukraine, hiyo ni dalili ya kukata tamaa kwa 100%. Ni sawa sawa na serikali ya Tz itangaze kutumia mizinga, makombora na vifaru ili kuwaliza panya road wa Dar!

2. Kuita wanajeshi wa akiba wasiopungua laki tatu ili kwenda vitani Ukraine.
Hawa wanaoitwa wanajeshi wa akiba kumbe ni raia wanaume wa kawaida wa Russia ama kwa hiari yao au kwa nguvu wanashurutishwa kwenda vitani sasa.
Mantiki yake ni nini na kwanini iwe sasa?
Je, wanajeshi rasmi wa Russia wamepungua sana?
Je, vita imekuwa kubwa na nzito kwa Russia kiasi cha kuokoteza vijana mtaani ili kuipigania Russia?

3. Putin kulalamika kuwa sasa amegundua NATO na USA wanaisaidia Ukraine kisiri kwa hali na mali.
Hili ndio limenishangaza zaidi. Sote tunajua (sio siri) kuwa USA na NATO wapo bega kwa bega na Ukraine tangu awali. Na tangu awali Putin alishaonya kuwa yoyote atakayeisaidia Ukraine moja kwa moja kwenye hii vita atakiona cha mtema kuni mara moja (immediately military reaction from Russia). Sisi tulitegemea Russia ateremshe kichapo cha chap chap kizito kwa USA na nchi za NATO halafu ndio aje kwa umma kusema hizo blah blah. Ama basi atangaze kuitisha special military operation against USA and NATO ili tumuelewe.

4. Russia kutangaza kuwa kwa sasa inataka zaidi mazungumzo ya kumaliza vita!
Wakati vita hii inaanza Russia ilikuwa haioni kivilee faida ya kumaliza mzozo huu kwa mazungumzo ya mezani na Ukraine, Russia ilikuwa mwendo mdundo kufurumusha mabomu katika ardhi ya Ukraine. Wakati huu ambao Russia inatamani mazungumzo zaidi ili kumaliza vita, upande wa Ukraine wao hawataki sana mazungumzo kama ilivyokuwa awali.
 
Sio siri tena kwa sasa vita vya Ukraine imeshika kasi huku Russia ikipitia kipindi kigumu zaidi huenda kuliko kipindi kingine chochote tangu kuanza kwa hii vita.

Kuna dalili fulani ambazo zinazoonyesha kama vile Putin pumzi inaelekea kukata. Hizi hapa chini ni baadhi ya sababu muhimu zenye kueleza hayo;

1. Kitisho cha kutaka kutumia Nyuklia ili kumaliza vita.
Sote tunajua Russia ni taifa kubwa kijeshi likiwa na shehena za kila namna za kivita na kiteknolojia, kitendo chochote cha Russia kupiga mkwara kuwa huenda wakaanza kutumia nyuklia ili kuishinda Ukraine, hiyo ni dalili ya kukata tamaa kwa 100%. Ni sawa sawa na serikali ya Tz itangaze kutumia mizinga, makombora na vifaru ili kuwaliza panya road wa Dar!

2. Kuita wanajeshi wa akiba wasiopungua laki tatu ili kwenda vitani Ukraine.
Hawa wanaoitwa wanajeshi wa akiba kumbe ni raia wanaume wa kawaida wa Russia ama kwa hiari yao au kwa nguvu wanashurutishwa kwenda vitani sasa.
Mantiki yake ni nini na kwanini iwe sasa?
Je, wanajeshi rasmi wa Russia wamepungua sana?
Je, vita imekuwa kubwa na nzito kwa Russia kiasi cha kuokoteza vijana mtaani ili kuipigania Russia?

3. Putin kulalamika kuwa sasa amegundua NATO na USA wanaisaidia Ukraine kisiri kwa hali na mali.
Hili ndio limenishangaza zaidi. Sote tunajua (sio siri) kuwa USA na NATO wapo bega kwa bega na Ukraine tangu awali. Na tangu awali Putin alishaonya kuwa yoyote atakayeisaidia Ukraine moja kwa moja kwenye hii vita atakiona cha mtema kuni mara moja (immediately military reaction from Russia). Sisi tulitegemea Russia ateremshe kichapo cha chap chap kizito kwa USA na nchi za NATO halafu ndio aje kwa umma kusema hizo blah blah. Ama basi atangaze kuitisha special military operation against USA and NATO ili tumuelewe.

4. Russia kutangaza kuwa kwa sasa inataka zaidi mazungumzo ya kumaliza vita!
Wakati vita hii inaanza Russia ilikuwa haioni kivilee faida ya kumaliza mzozo huu kwa mazungumzo ya mezani na Ukraine, Russia ilikuwa mwendo mdundo kufurumusha mabomu katika ardhi ya Ukraine. Wakati huu ambao Russia inatamani mazungumzo zaidi ili kumaliza vita, upande wa Ukraine wao hawataki sana mazungumzo kama ilivyokuwa awali.
Unajua kama Kuna kitu referendum kinaendelea ndani ya huko wanakosaidia mabeberu wote na yule anayetumiwa na mabeberu na wote Hawajui nini Cha kufanya🤔
 
Haamini macho yake
FB_IMG_1664033478376.jpg
 
Unajua kama Kuna kitu referendum kinaendelea ndani ya huko wanakosaidia mabeberu wote na yule anayetumiwa na mabeberu na wote Hawajui nini Cha kufanya🤔
Mpango wa Referendum ulikuwepo muda mrefu, na sio issue tena kwenye majimbo 'yaliyojitangaza' kujitenga kutoka Ukraine huku Russia ikitangaza kuyatambua rasmi muda mchache kabla ya kutangaza vita dhidi ya Ukraine.
 
Sio siri tena kwa sasa vita vya Ukraine imeshika kasi huku Russia ikipitia kipindi kigumu zaidi huenda kuliko kipindi kingine chochote tangu kuanza kwa hii vita.

Kuna dalili fulani ambazo zinazoonyesha kama vile Putin pumzi inaelekea kukata. Hizi hapa chini ni baadhi ya sababu muhimu zenye kueleza hayo;

1. Kitisho cha kutaka kutumia Nyuklia ili kumaliza vita.
Sote tunajua Russia ni taifa kubwa kijeshi likiwa na shehena za kila namna za kivita na kiteknolojia, kitendo chochote cha Russia kupiga mkwara kuwa huenda wakaanza kutumia nyuklia ili kuishinda Ukraine, hiyo ni dalili ya kukata tamaa kwa 100%. Ni sawa sawa na serikali ya Tz itangaze kutumia mizinga, makombora na vifaru ili kuwaliza panya road wa Dar!

2. Kuita wanajeshi wa akiba wasiopungua laki tatu ili kwenda vitani Ukraine.
Hawa wanaoitwa wanajeshi wa akiba kumbe ni raia wanaume wa kawaida wa Russia ama kwa hiari yao au kwa nguvu wanashurutishwa kwenda vitani sasa.
Mantiki yake ni nini na kwanini iwe sasa?
Je, wanajeshi rasmi wa Russia wamepungua sana?
Je, vita imekuwa kubwa na nzito kwa Russia kiasi cha kuokoteza vijana mtaani ili kuipigania Russia?

3. Putin kulalamika kuwa sasa amegundua NATO na USA wanaisaidia Ukraine kisiri kwa hali na mali.
Hili ndio limenishangaza zaidi. Sote tunajua (sio siri) kuwa USA na NATO wapo bega kwa bega na Ukraine tangu awali. Na tangu awali Putin alishaonya kuwa yoyote atakayeisaidia Ukraine moja kwa moja kwenye hii vita atakiona cha mtema kuni mara moja (immediately military reaction from Russia). Sisi tulitegemea Russia ateremshe kichapo cha chap chap kizito kwa USA na nchi za NATO halafu ndio aje kwa umma kusema hizo blah blah. Ama basi atangaze kuitisha special military operation against USA and NATO ili tumuelewe.

4. Russia kutangaza kuwa kwa sasa inataka zaidi mazungumzo ya kumaliza vita!
Wakati vita hii inaanza Russia ilikuwa haioni kivilee faida ya kumaliza mzozo huu kwa mazungumzo ya mezani na Ukraine, Russia ilikuwa mwendo mdundo kufurumusha mabomu katika ardhi ya Ukraine. Wakati huu ambao Russia inatamani mazungumzo zaidi ili kumaliza vita, upande wa Ukraine wao hawataki sana mazungumzo kama ilivyokuwa awali.
Sitashangaa kumwona Putin akikokotwa kuelekea mahakamani siku moja kama ana bahati nzuri vinginevyo atauawa kwa staili ya akina Saddam na Ghaddafi.
 
Kura inapigwa katika majimbo manne. Asilimia 15 ya ardhi ya Ukraine kaimega tena na NATO ipo bado mnambeza Putin?😀Kujiimarisha kijeshi ni kutokana na mipaka kuongezeka baada ya siku mbili majimbo manne yanajiunga Urusi. Mnajua nchi za NATO zitafanyaje? Pia Urusi tangu vita ianze anapambana na NATO. Kuelekea msimu wa baridi Ulaya, jamaa kapiga vita ya uchumi wa gesi. Hii vita ni kuombea imalizike. Msimchukulie Putin kirahisi. #Tuombe amani amani...🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom