Kuna kila dalili kuwa Putin kaanza kukata tamaa!

Tokea mwezi wa February mpaka sasa ivi tupo September bado miezi 4, mwaka ukamilike tokea Vita ianze. Kila siku majira ya baridi majira ya baridi tuuuu
Russia wanasema operation inakwenda kulingana na walivyopanga.

Labda wewe utuambie Russia kapoteza kiasi gani tangu vita ianze, au hata kama kuna kombora au bomu limerushwa toka Ukraine kuelekezwa kwenye ardhi ya Russia.
 
Kwahiyo unadhani kupanda Kwa gharama za nishati ndo kutabadilisha mtazamo wa Ulaya dhidi ya Russia?!
Huo mtazamo umebadilisha nini toka vita ianze?! Mbona wameshindwa kumfurusha mvamizi leo zaidi ya miezi 6!
 
Yale majimbo yalishajitenga na Ukraine tangu 2014 na walijitanga kama Jamhuri ya Donetsk na Lugansk.

Hayo majimbo yanakaliwa na raia wengi wenye asili ya Russia na wanaongea pia kirusi.
Kwahiyo Ukraine karidhia kuyaachia hayo majimbo?!
 
Hayo majimbo hajayamega Putin bali majimbo hayo raia wake wengi ni wale wenye asili ya Russia na wanaongea kirusi.

Walianza kujitenga tangu 2014 na walijitangaza kama Jamhuri ya Donetsk na Lugansk. Wala siyo Putin aliyeyatwaa majimbo hayo.
😀😀😀 Si ndicho alikitangaza Putin tangu mwanzo kwamba operesheni yake ya kijeshi ni kulinda uhuru wa hawa raia wa hayo majimbo? #Amani amani amani. Tuombeeni amani tunaoumia na hiyovita ni sisi.🙏🙏🙏
 
Huo mtazamo umebadilisha nini toka vita ianze?! Mbona wameshindwa kumfurusha mvamizi leo zaidi ya miezi 6!
Angalia ramani ya Ukraine kuanzia February 24 na Leo September 25 ndo utaelewa kwanini Babu Putin kaanza kutishia nuclear Kwa aibu aliyoipata kwenye uwanja wa Vita.
 
Urusi ana hathirika lakini Ulaya inaathirika zaidi ,
ndani ya Urusi bidhaa za chakula,mafuta ,gesi ziko chini Wakati ndani ya Ulaya ni tofauti kabisa.

Na vitu nilivyo vitaja hapo ndio vitu muhimu katika maisha ya mwana nchi wa kawaida.

Jana nilikuwa nasikliza kipindi cha maoni kwenye DWswihili wachambuzi yanasema uchumi wa Ulaya uko kwenye hali mbaya sana na iwapo hali itaendelea hivi basi uchumi wa Ulaya utasambaraka.

Wanasena nchi kama Ujerumani ambayo ndio yenye uchumi mkubwa barani Ulaya viwanda vingi vimefungwa na vingine vimepunguza wafanya kazi kutokana na ughari wa gesi hali kadharika wingereza ,Ufaransa na Italy.

Na kuna kipindi kama sikosei ulikuwa mwezi wa 3 tulibishana mm na ww nikawa nakwambia kuwa Ulaya haiwezi kuishi bila gesi ya Urusi ukanibishia ila sasa hivi nadhani umeshaliamini lile ulilo kiwa unalikataa.
 
Mushafikia huko tena 2024[emoji23][emoji16][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alitangaza Elensky mwenyewe sio RUSSIA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lini fini na swed walijiunga NATO [emoji16][emoji23][emoji16]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa partial na vikwazo mbona haihusiani dada angu
Halaf unasema hawana pakusemea huko wakat huo huo unasema wameingia mabarabarani
Kumbe RUSSIA kuna demokrasia haswa mpaka raia wanapinga amri ya amiri jeshi MKUU anbae ndio RAIS

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa inavyoendelea Donesk na Luhansk na Crimea zitarudi

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Russia anahilihitaji zaidi soko la Ulaya kuliko kitu kingine chochote katika kusurvive kwake.Ndiyo maana kila mara haishi kujiwekea vimasharti mara nitafunga bomba hili mara lile na hakuna anaejali.Hiyo German unayosema hao Wachambuzi wanasema viwanda vingi vimefungwa ndiyo hii hii ambayo Waziri wake wa Nishat anakwambia ina Gesi ya akiba 90% na kufikia December itakuwa na 95%.
Hiyo gesi Russia akae nayo kwa mwaka mzima iwe kwa matumizi yake mwenyewe tuone kama ataweza kusurvive na vita hii ambayo haiishi leo wala kesho

Hao wachambuzi waswahili wenye kuchambua uchumi wa Ulaya kusambaratika wakati wao wanaganga njaa huko huko West si ni kichekesho.Yani Mataifa yenye uchumi mkubwa Duniani yanatabiriwa anguko na 'wachambuzi waswahili' [emoji3]
 

Sikurazimishi ila hali halisi
inajionesha kwa hiyo ww kukubali au kutokukubali hakutabadilisha chochote.

Urusi inahitaji soko la Ulaya ila kumbuka pia na Ulaya inahitaji gesi ya Urusi ili isurvive na ndio maana wanasema wanataka kuacha gesi ya Urusi lakini vitendo ni zero.
Na leo waziri wa uchumi wa Italia amesema ya kuwa Italia aiwezi kuishi bila gesi ya Urusi na kauli kama hiyo imeongewa sana na viongozi wa Ujerumani ambayo ndio giant wa uchumi wa Ulaya.

Hao unao waita wachambuzi waswahili na kuwadhihaki wanaishi ndani ya nchi hizo hivyo wana shuhudia maisha halisi ndani ya Ulaya jinsi yalivyo magumu hivo wanaongea kitu wanacho kishudia tofauti na ww ambaye uko Tz saa nyingine hata hiyo Ulaya unaionaga kwenye TV tu na hautarajii kukanyaga huko.

Hata kipindi kile Ulaya anajitutua eti ataachana na gesi ya Urusi nilikuambia ya kuwa haiwezekani ukabisha hivi hivi lakini muda sasa unaongea na tuna shuhudia hali halisi.

Kipindi Urusi anaweka masharti ya kulipa kwa rubo ulisema haiwezekani lakini wakakuumbua kwa kukubali kulipa kwa rubo.
Na rudia tena Ulaya haiwezi kusurvive bila gesi ya Urusi.
 
Nimesema imefikia hatua watu wamepata ujasiri wa kuingia barabarani baada ya hiyo partial mobilization kuona wanasukumizwa wakafie vitani.Na sidhani kama wote walisalimika hata kurudi majumbani kwao salama
 
Ndiyo maana nikasema,hao wachambuzi wanaoganga njaa hizo Nchi za Magharibi na kufurahia maisha ndiyo wanajisemesha haya.Basi kwakuwa uchumi unakwenda kuanguka hebu warudi basi nyumbani kwenye Uchumi imara kama watakubali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…