Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Naona wengi wenu hapa mnapuyanga tu. Sisi parokiani kwetu kuna sadaka mbili tu matoleo ya kawaida na ujenzi wa kanisa ambao infacts ni kweli.

Hata hivo hakuna mchango usiokuwa na maelezo na hii inategemea eneo na eneo.

Imagine parokia kama mavurunza wanajenga kanisa la ghorofa unadhani ni michango kiasi gani inahitajika?
 
Mkuu, hata ukitoa unaweza usipewe huduma vilevile!

Mimi mama yangu mzazi alikua kiongozi wa jumuia huko kijijini na alikua mtoa sadaka asie na kifani, shughuli zote za ujenzi wa kanisa alishiriki kikamilifu kwa maisha yake yote mpaka amezeeka.

Bahati mbaya akaja kupata tatizo la kiafya ambalo limemuweka kitandani zaidi ya miaka 10 sasa. Cha ajabu eti kila mwaka analetewa bahasha ya zaka na kanisa linatishia kwamba akifa halitamzika kama sisi watoto hatutakua tunatoa hela za kwetu na zake!

Sasa mimi najiuliza, mtu ambae amelala kitandani hilo fungu la 10 analitoa wapi? Tangu amelala kitandani, kanisa limemsaidia vipi? Michango yote aliyochanga tangu akiwa binti mdogo mpaka sasa ni mzee, haijatosha tu? Ni mpaka tone la mwisho??
Inasikitisha Sana[emoji26]
 
Zamani makanisa yalikuwa yanapata sana misaada toka nje lakini kwa sasa nje hawatoi sana misaada (wanasema mioyo yao kuhusu dini imepoa) so inabidi makanisa yajiendeshe yenyewe. Hapo ndipo uhitaji mkubwa wa hela unapoanzia
Ha ha ha....
Hapo ndo unapata picha kuanmakanjsa makanisa yaliletwa afrika kimchongo.

Mwendo wa
Explorers[emoji117] missionaries [emoji117]Traders[emoji117]colonialist
 
Mkuu kwa iyo situation ilokukuta haihitaji kufikiria mara 2 kua kanisa linakunyonya
Sasa kma anaumwa mbona kanisa halimsaidii kitu ila wao ndo wanataka?

Laiti angekua Muislamu huyo waislamu wangejichanga wangemuhudumia badala ya yy kudaiwa huduma

Uislamu ni dini ya haki
Nakazia[emoji106]
 
Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
Milele Amina !

Kuna muda tusiwe wapotoshaji, wewe kutoa/kutokutoa humpunguzi kitu mtu. Kutoa inapaswa iwe ni jambo lako na moyo wako.

Na hii ieleweke kwa dini zote, maana hulazimishwi wala hutatajwa wewe hukutoa/wala hutatukuzwa kuwa umepotea ni vema sasa ujifunze kwa kujiwekea utaratibu kutoa ni moyo anayejua ni Mungu wako.
 
Tumsifu Yesu Kristu mpendwa

Nadhani changamoto ipo kwenye ufahamu wa namna ufalme wa Mungu unavyofanya kazi. Sioni tatizo kwako wala mtizamo wako maana ninatambua unachohitaji wewe ni elimu na ufahamu wa jinsi Yesu anavyotenda kazi
Basi tutaanza na neno la Mungu ili iwe rahisi kupokea elimu hii
Tafadhali soma Mathayo 25:14-30
Nitachukuwa mstari 24-26 ili upate kuelewa ufalme wa Mungu unavyofanya kazi
24 - Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;
25 - Basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako
.
26 - Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;

Hoja yako kwa kanisa haina tofauti sana na hadithi hii
Kwani kinachokuumiza wewe ni kanisa kuwa na michango mingi angali wewe ndio unayefanya kazi.
Naamini kama ungali fahamu vyote ulivyonavyo sio vyako sidhani kama ungelalamika. Kitu kinachotugharimu kibinadamu ni ile hali ya kuamini kwamba hii fedha/mali ni YANGU. Pasi na kufahamu yote tuliyonayo ni matokeo ya upendo wa Mungu kwako. Kibinadamu kuamini falsafa hii ni ngumu sana maana Ipo kiroho wakati tunadhani yote tuliyonayo ni matokeo ya juhudi zetu pekee yetu.
Ukisoma mstari wa 28 utaona ni nini matokeo ya ubinafsi wa mtumwa yule.
Yesu anasema duniani kuna mabwana wawili ambao ni fedha na Mungu. Utachagua mwenyewe wa kumtumikia lakini huwezi kuwatumikia wote kwa pamoja, Ukishindwa kufahamu kama vyote ni mali ya Bwana hakika itakuwa ngumu sana kuachilia yote ulionayo kwa Mungu.

Kwa kumalizia jitahidi sana kujifunza kanuni za Mungu hasa kwa kusoma neno lake ili uongeze maarifa ya kimungu kuanzia namna ya kupata fedha/mali, kutumia na kuzalisha uli usipungukiwe ukamkufuru Mungu, maana kumcha Bwana ndio chanzo maarifa na hekima. Tena Suleiman anasema bora hekima na ujipatie hekima na kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.
Mwisho kasome Hosea 4 upate kufahamu nini kinachoangamiza Imani. Usilaumu kanisa jilaumu wewe kwa kuwa gizani.

Uwe na jumapili njema ya matawi na nikutakie kwaresma njema.

Tumsifu Yesu Kristu.
Nikisema nifuate ushauri wako na kufuata kanuni za Mungu basi hata sadaka ninayotowa sasa hivi hawataipata nitapeleka direct kwa yatima na wajane na kanisani sintokanyaga tena.

Siendi kanisani kuutafuta ufalme wa mbinguni haupatikani pale, nakwenda kanisani kuwa connected na jamii yangu ambao tunaamini katika kristu.

Mimi siamini katika kuuona ufalme wa mbinguni kwa kwenda kanisani au kunipa maandiko ili kuhalalisha uharamia wenu?

Mbona maandiko mnachaguwa ya kutumia wakati Timotheo wa pili imeandikwa wazi atamaniye kazi ya uaskofu basi atamani kazi njema, basi imempasa Askofu awe mume wa mke mmoja, sasa mbona kanisa katoliki limekumbatia useja kinyume na mafundisho wa biblia?
 
Huu uzi haujaandikwa na Mkatoliki, aliyeandika hapa anatoka kundi la wale wanaosababishaga biashara ya kitimoto izorote
 
Yule moigaji TU,
Anasema Hakuna sadaka, ila Kuna michango[emoji4]

Michango haina ishu hautoi...

Sadaka za makanisani nyingine zina hadi mkataba wa mwaka, unasaini kwamba mwaka huu jengo utatoa kiasi kadhaa, ahadi kiasi kadhaa...
 
Ukiona huko Katoliki na Lutheran sadaka zinakutisha na kukuchosha basi jaribu makanisa ya Pentekoste ndio utakiona cha mtema kuni.

Huko Pentekoste utatakiwa kutoa
1. 10% ya kipato chako chochote (kama una mshahara wa 1m kwa mwezi, basi kila mwezi laki moja lazima pastor aikunje mfukoni, na pastor atataka kuona mpaka salary slip)

2. Kuna sadaka za shukrani kila unapofanikiwa jambo lolote (na hii inapaswa kuwa sadaka nono fulani)

3. Kuna sadaka ya kusindikizia maombi yako kila unaposaka kuombewa mambo yako. (Hapo utapigwa mikwara kibao)

4. Kuna sadaka ya kuchangia shughuli mbali za kanisa (kuanzia ujenzi, vyombo vya muziki, uinjilisti, suti ya mchungaji, gauni la mama mchungaji nk)

Unaotaje sadaka ya shukrani kila unapofanikiwa. Mbona wao hatoi sadaka ya shukrani wakifanikiwa kupata magari au kujenga makanisa
 
Kumbuka hizi imani tuliletewa na wageni. Kipindi chote cha nyuma walikuwa kwenye matazamio. Vitu vingi walikuwa wanagharamia kwenye makanisa mengi. Hata ujenzi wa makanisa walikuwa wanahusika kwa kiasi kikubwa. Hata mishahara ya wachungaji walikuwa wanahusika. Kufupisha kwa sasa kila kitu wameacha kutoa,hata ruzuku zote wameacha kusaidia makanisa. Walikuwa wanasubiri tuwe addicted na hiyo imani. Kwa hiyo makanisa kwa sasa yanajiendesha yenyewe. Lazima wategemee hizo sadaka kwa kiasi kikubwa.
 
Mimi nipo Tabora, mbona hakuna huu mfumo?
Kila Askofu ni mkuu katika jimbo lake, itakuwa Askofu wenu hapendi upumbavu kama yule Askofu wa KKKT Askofu Bagoza.

Hongera zenu, jimbo kuu la Dar kumeharibika Askofu mkuu mchaga.
 
Even Muslim but , waislam ni bahili sana,
Waislam sio bahili, sema waislam wanajitambua sana, na wanaitambua dini yao na mafundisho yao.
Waislam hawalazimishwi kuchangia kama mtu hana kitu. Wapo radhi kumchangia myu asiye na kitu na sio kumlazimisha achangie.
Pia waislam wapo huru kuhoji juu ya mapato na matumizi ya sadaka zao.
Na kingine wanaruhusiwa kuchangia kulingana na mradi husika mfano kwenye ujenzi sio lazima utoe pesa unaweza kutoa bati, tofali, nondo, sementi na vitu vingine kama hivyo.
 
Utazikwa na ndugu na majirani, si lazima kiongozi wa dini awepo.
...Hata ndugu yako yoyote anayeweza kusoma TU anaweza kuongoza Misa ya Wafu Kwa ajili Yako!
Hakuna, rudia, Hakuna aliyepewa Mamlaka ya kukusalia wewe ukifa ili uingie peponi!
 
Mavuno nadaiwa laki mbili mwisho mwezi wa sita.....
Nadaiwa zaka sijarudisha bahasha hii lazima nitoe.......
Leo jpili lazima nizame kanisani na sadaka 3
Nadaiwa laki mbili mchango wa gari la Paroko...nili-pleadge......
nisipotekeleza haya nitaonekana sio mkristo
Kidogo akili imeanza kutuingia. Dhehebu langu niliyaona mengi yanayokwaza kupitia michango. Ugumu ni kuwalisha somo hawa wafia dini wanaojiita wasaidizi kama wazee wa kanisa, wakuu sijui viongozi wa vigango hadi waumini wa kawaida. Wataanza kukushambulia na kukuona pepo mchafu. Nikaona isiwe taabu, nikawaachia watoto na mama yao. Kazi kubwa kwangu ni kuandaa sarafu za Sunday school kwa watoto ilihali mama ajitafutie hiyo michango kadri atakavyobarikiwa.

Ni kama viongozi wakuu hawatafakari nasi tuna mahitaji binafsi ya kuzitunza familia zetu! Wao wanatembelea magari, watoto wao wanapewa elimu za viwango vya juu, wake na waume zao wanatunzwa kupitia jasho letu lilibatizwa 'kutegemezwa' sijui na taka taka gani.

Kimsingi sadaka ililengwa itoke kwa hiari sio shuruti kama ilivyo madhehebu mengi ya kileo.

Nashukuru sana GT kwa kuliona hili na ukatupia uzi.

Wengi wako nyuma yako, tunakuunga mkono kupaza sauti hadi huu uharamia upungue au wabaki kusali viongozi wa kanisa na familia zao. [emoji34][emoji34][emoji34][emoji34]
 
Waumini wa makanisa wanakamuliwa sio poa, Ila kwa vile ni ridhaa yao hakuna shida kabisa.

*Kujenga makanisa ni kazi ya waumini.
*Kujenga mashule.
*Kujenga hospitali/vituo vya afya/dispensary ni kazi ya waumini.
*Kujenga nyumba za watendakazi wa makanisa.
*Kuwanunulia magari huku sisi tukipiga mihuri.

Bado tutoe zaka na sadaka kwa uaminifu.

Sisi tunapata nini?
*Tunawapeleka watoto wetu kwenye shule tulizojenga wenyewe na ada tunalipa sawa na wengine.

Anyways, mimi siendi kanisani Ila nikipigiwa simu ya kuchangia kitu natoa tu, nilipatwa na msiba hawakunibagua, labda kwa vile hivyo vimchango nashiriki.
Nakazia[emoji106]
 
Back
Top Bottom