Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna ile ya kuwataka waumini waliofiwa na wapendwa wao eti watoe sadaka kubwa kubwa kadri wawezavyo kama kikokotoo cha kuwawezesha hao wapendwa wao waliotangulia mbele ya haki kupata ahueni ya maisha huko kaburini. Yaani mimi hii haijawahi kuniingia akilini kabisa.
Ninapohudhuria misa za maziko kwa dhebu la mtoa mada napata hasira. Ati baada ya kuaga mwili wanaweka kikapu cha sadaka ya kumuombea marehemu (hii kiongozi aliyeendesha misa anaondoka nayo), kisha kinakuja kikapu cha rambirambi.
 
Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
imetabiliwa watu watapenda pesa kuliko kitu chochote
 
Usilalamike sana, chukua hatua zifuatazo.
1. Acha kutoa hizo sadaka (michango), au toa ile inayokugusa tu, mingine kaa kimya, hakuna mtu wa kukufanya lolote.

2. Tafuta chenji za kutosha ukiwa unakwenda kanisani. Kama ukikuta sadaka za kutoa ni tano na wewe ulipanga kutoa sadaka ya jumla ya shilingi mia tano tu, basi chenji hiyo mia tano ili kupata sarafu za mia mia ziwe tano, kisha kila ukitakiwa kutoa sadaka unadondosha jiti tu kwenye chombo cha sadaka.
Usisahau kanisani muhimu kuliko yote huwa tunafuata neno, sasa haiwezekani injili ihubiriwe dakika 20 halafu misa itumie masaa karibu matatu kuendesha harambee ndani ya kanisa.

Wewe hata kama ni mwislamu jaribu kusikiliza hotuba za mapadre wa kikatoliki halafu msikilize mtu kama Mwamposa hotuba yake utajuwa hapa naongea nini, wanaokwenda kwa Mwamposa wanashiba neno na ndio kitu muhimu zaidi.

Sasa ibada ya misa kipaumbele cha muda mwingi kikiwa ni sadaka mbalimbali na harambee mbalimbali kwangu ni useless ni bora hata nikikaa nyumbani nitune channel ya Arise and shine Mwampisa atanibariki sana kwa neno na anatowa hotuba kwa muda mrefu mpaka unashiba neno.
 
Ona waislam duniani kote wanajijua Kuna wale wajahidina na wasio wajahidina hata uende wapi duniani ukikuta muslam atakuwa kundi moja hapo ndio maana warabu wanawajengea misikiti, mda huu wa mwezi mtukufu Kuna misikiti Kila siku inatoa pesa kwa watu wasiojiweza kwenda kununua futari umeona hapo kwanini hawajaingiza ubinafsi na umimi kwenye Imani njoo kwetu Sasa

Kanisa la masanja mkandamizaji
Kanisa la mc pilipili
Kanisa la gwajima
Kanisa la mzee wa upako
Kanisa la mwamposa
Kanisa la kakobe
Na bado Kuna utitiri wa makanisa na bado wanapigana vijembe unasali wapi wewe ukisema kwa MC pilipili wanaanza kusengenya njoo uku yani

ingekuwa kula kitu moto inaruhusiwa uslam unaenda uko sema kiti moto kuacha dah ngumu, maana nishaionja Sasa kuacha ngumu
Chief mbona vitamu vipo vingi sana na vinaruhusiwa ndani ya dini ya kiislamu....unaweza ku giveup kitimoto na still uko fine tu! Karibu kwenye uislamu

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Mkuu, hata ukitoa unaweza usipewe huduma vilevile!

Mimi mama yangu mzazi alikua kiongozi wa jumuia huko kijijini na alikua mtoa sadaka asie na kifani, shughuli zote za ujenzi wa kanisa alishiriki kikamilifu kwa maisha yake yote mpaka amezeeka.

Bahati mbaya akaja kupata tatizo la kiafya ambalo limemuweka kitandani zaidi ya miaka 10 sasa. Cha ajabu eti kila mwaka analetewa bahasha ya zaka na kanisa linatishia kwamba akifa halitamzika kama sisi watoto hatutakua tunatoa hela za kwetu na zake!

Sasa mimi najiuliza, mtu ambae amelala kitandani hilo fungu la 10 analitoa wapi? Tangu amelala kitandani, kanisa limemsaidia vipi? Michango yote aliyochanga tangu akiwa binti mdogo mpaka sasa ni mzee, haijatosha tu? Ni mpaka tone la mwisho??
Hapo kwakweli hawajafanya vizuri.
Kwa kipindi hiki walitakiwa wao ndio wamsaidie hasa ukizingatia alikuwa muumini mzuri.
Wakati mwingine watu huvunjika moyo kwasababu ya mambo kama haya na kuwafanya kushuka kiimani au kuamua kubaki bila dini kabisa.
 
Kweli michango imezid na inakera. Unatoa sadaka kabla hata kanisani hujafika na kabla hujashiriki mtiririko mwingine wa ibada.
Japo siwez hama kwa hizo sababu lakin inabid warekebishe mahali wanatukwaza waumini.
Huku uchaggani picha linaanza kwanza Padri anaheshimika Kama mungu.

Yaani mtu anaweza kuitwa kwenda kea Mtendaji wa Kijiji au Police aisende lakini akiitwa kwa Padre. Kwanza anapata hofu kubwa kuwa tatizo ni nini🤣

Na ukifiwa Padre akija ile sadaka ya ibada ya mazishi anabeba anaondoka nayo. Na kwako ni masikini hata ibada ya mazishi hamalizi, anafanya nusu akimaliza naaepa anawaachia waumini waendelee.

Ila binafsi naona utamaduni wa uchaggani ndio umepelekea tatizo kuwa kubwa sana. Maana huku ukipata MSIBA usitegemee kabisa ushirikiano kutoka kwa watu.

Hata Kulia Wala maombolezo Wala huzuni. Kwahiyo kinachofanyika ukipata MSIBA, inabidi uwe na pesa ukodi VITI, MAHEMA, POMBE, NYAMA na MUZIKI.

Muziki ndio utaomboleza pamoja na watu wa kukodiwa ( TARUMBETA).

Bila kufanya hivi Hakuna mtu atajua kwako Kuna msiba. Na kibaya zaidi na kanisani ukiwa umetengwa, utazikwa Kama mzoga was mbwa Koko.

Hii ndio hali HALISI.
 
Nikisema nifuate ushauri wako na kufuata kanuni za Mungu basi hata sadaka ninayotowa sasa hivi hawataipata nitapeleka direct kwa yatima na wajane na kanisani sintokanyaga tena.

Siendi kanisani kuutafuta ufalme wa mbinguni haupatikani pale, nakwenda kanisani kuwa connected na jamii yangu ambao tunaamini katika kristu.

Mimi siamini katika kuuona ufalme wa mbinguni kwa kwenda kanisani au kunipa maandiko ili kuhalalisha uharamia wenu?

Mbona maandiko mnachaguwa ya kutumia wakati Timotheo wa pili imeandikwa wazi atamaniye kazi ya uaskofu basi atamani kazi njema, basi imempasa Askofu awe mume wa mke mmoja, sasa mbona kanisa katoliki limekumbatia useja kinyume na mafundisho wa biblia?
Kama hauamini kwamba utapata ufalme wa Mungu kanisani basi taka sana kuzifahamu kazi za roho mtakatifu. Yesu Kristu Katika mafundisho yake neno kanisa alilitaja mara moja tuu Rejea
Mathayo 16:13-17
Na wakati anaondoka aliwaachiwa mitume kazi ya kufundisha juu ya ufalme wa Mungu kwa msaada wa roho mtakatifu.

Mtakatifu Paulo ndio mwalimu wa mwanzo wa kanisa na mifumo mingi imeasisiwa nayeye jitahidi kumsoma kwa kina na uelewe hoja ya kwanini imempasa kasisi kuishi useja. Ukristo ni kazi tena ni nguvu jibidiishe kujifunza ili kujenga Imani yako juu ya mwamba imara
 
Ninapohudhuria misa za maziko kwa dhebu la mtoa mada napata hasira. Ati baada ya kuaga mwili wanaweka kikapu cha sadaka ya kumuombea marehemu (hii kiongozi aliyeendesha misa anaondoka nayo), kisha kinakuja kikapu cha rambirambi.

Hapo kumleta padri kuja kuombea marehemu unatozwa pesa. Akifika lile kapu pale wanaondoka nalo la kwenda parokiani mambo ya ajabu sana.

Niliwai udhuria msiba wa msabato mmoja. Ile watu wamemaliza kutoa yule mchungaji akachukua pesa akampa mume alifiwa mke. Itamsaidia mbele ya safari na dharura atakapokua ana mpumzisha mkewe.

Nilijutia sana kwa nini sikunyanyuka kutoa sadaka. Ila nipendezwa na jambo lile.

Ukatoliki wetu ni changamoto
 
Ona waislam duniani kote wanajijua Kuna wale wajahidina na wasio wajahidina hata uende wapi duniani ukikuta muslam atakuwa kundi moja hapo ndio maana warabu wanawajengea misikiti, mda huu wa mwezi mtukufu Kuna misikiti Kila siku inatoa pesa kwa watu wasiojiweza kwenda kununua futari umeona hapo kwanini hawajaingiza ubinafsi na umimi kwenye Imani njoo kwetu Sasa

Kanisa la masanja mkandamizaji
Kanisa la mc pilipili
Kanisa la gwajima
Kanisa la mzee wa upako
Kanisa la mwamposa
Kanisa la kakobe
Na bado Kuna utitiri wa makanisa na bado wanapigana vijembe unasali wapi wewe ukisema kwa MC pilipili wanaanza kusengenya njoo uku yani

ingekuwa kula kitu moto inaruhusiwa uslam unaenda uko sema kiti moto kuacha dah ngumu, maana nishaionja Sasa kuacha ngumu
[emoji23][emoji23] haya masihala sasa mtani. Kiingiacho halimtii mtu najisi bali kitokacho
 
Toa ndugu toa ndugu..ulichonacho..halafu unataka usitoe hilo kanisa litapelekaje injili..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje wahudumu..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje bills tofauti kama umeme na maji...unataka usitoe hilo kanisa litafanyeje logistics mbali mbali...unataka usitoe maintaince na repairs ya vifaa na miundombinu mbalimbali utatoa wewe.??

Acha kulalamika sana kama huna hela kaa kutulia

Uzuri hujalazimishwa..ila mkristo wa kweli hawezi kuona kama ni wizi mana hayo ndio mahitaji muhimu ya kuendesha taasisi.

Kingine kutoa ni upendo..kiwango itachojaliwa kutoa kinatosha sana.

Kama unaona hufiti nenda huko ambako hawatoi sadaka..hakuna aliyekushikiria unabaki kanisani.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote.

#MaendeleoHayanaChama
Hizo huduma za kiroho ni ngumu tatizo sisi tunaenda kanisani na mitizamo ya kibinadamu/kipagani. Huyu Mungu tunayemtafute/tuitafute kweli mioyoni mwetu na tuijue. Huduma za kiroho ni gharama hakuna cha bure isipokuwa kusali tu unapokuwa wewe mwenyewe.
 
Hahah, mzee baba siku hizi nasikia kuna kanisa linaitwa sijui Free Church la yule jamaa wa Ze Comedy, ukitaka kusali unaibuka tu hakuna sadaka za mafungu mafungu...
Alizisoma nyakati akabaini taabu na kero za machangizo
 
Alie design hiyo business model ya church business ni genius ndio maana alihakikisha kuna njia za kukubana ili usiache kutoa hela maisha yako yote.

Kwanza kabisa wanaanzia mbali kwa kukuingiza kwenye system tangu ukiwa mtoto mchanga kwa ubatizo. Pili unaaminishwa kwamba bila kubatizwa kanisani na kupewa sakramenti wewe si mkristo. Hiyo yote unajengwa kisaikolojia ili uje upigwe vizuri. Baadae unaaminishwa kwamba ili uwe mkristo lazima utoe sadaka na michango yote ili "kueneza injili" na kusaidia jamii wakati kiuhalisia hamna kitu kama hicho. Mwisho unaambiwa usipotoa michango hautazikwa na kanisa na unatishiwa usipozikwa na kanisa unaenda motoni..!!! Yaani system ipo self contained mwanangu kila kitu ni mumo kwa mumo..!

Yaani mtu unafika mahali unajua kabisa hapa napigwa, ila huna pa kutokea dadeki..!
[emoji851][emoji851][emoji851][emoji851]
 
Usipotoa ni Bora hata kanisani usiende kwasababu huduma za kanisa hutapewa.

Hata kuzikwa Padre anaweza asije
Uzuri padri hashiko septu wala jembe wala habebi jeneza na mfu hayatambui yanayojiri. Sasa sijui hofu i wapi?

Okonkwo atabaki kuwa shujaa wangu japo ni fixious myth!
 
Uzuri padri hashiko septu wala jembe wala habebi jeneza na mfu hayatambui yanayojiri. Sasa sijui hofu i wapi?

Okonkwo atabaki kuwa shujaa wangu japo ni fixious myth!
Padre hashiki Jembe lakini ana uwezo wa kuwaambia watu wasishike wakakubali.
 
Back
Top Bottom