DOKEZO Kuna Mama anauza gongo na bangi wazi kata ya Moshono mtaa wa Mtoni, karibu na chuo cha uhasibu Arusha. OCD Arusha Mjini tusaidie

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kuna kipindi alikatamatwa na polisi akatoka ndani ya nusu Saa.Aliporudi alikuja na speed mpya huku akidai hakuna mtu wa kumfanya kitu.
 
Ikiwa watawala wanakwiba mali za umma.....matrafiki wanakula rushwa hadharani......na mama Abdul anagawa fedha kununua magoli badala ya kuboresha maisha ya walipa kodi......waache wananchi wajipambanie wenyewe......uadirifu unatakiwa uanze na watawala kama mfano......
 
Kama ana uswahiba na geshi la polisi mwacheni apige hela tu. Ndio Tanzania yetu ilivyo, kama huna mtu wa kupangua kikosi kazi cha kutoka CCP basi usijaribu kabisa biashara za haramu. Utaozea jela!
 
Una matatizo ya afya ya akili.
Gongo na bangi ajabu yake na madhara yake ni nini?
Gongo unaweza fananisha na pombe feki zilizojazana mitaani?
Hiyo bangi inamadhara gani? Hao waheshimiwa wazuia bangi ndio wanaoharibu vijana na unga.
Wewe ni mtoto wa mama
 
Mtoa hoja ulishawahi kujiuliza Bangi inavutwa viwanjan na Polisi wapo lkn wavutaji hawakamatwi
Na huwa wanajukwaa lao maalumu la kukaa na kuvuta
 
Acha kujaribu biashara za watu...
 
Nataka nitengeneze network nzuri na Mimi niuze hivi vitu haviitaji gharama za tra au adv cost... We ni kimalizana na wakubwa wa kazi ....
 
Wengi wanafanya biashara hizi hawafanikiwi kivile,laana nyingine zipo hapa hapa duniani
 
Ukisikia kusagiwa kunguni ndiyo huku sasa.

Lingekuwa ni suala la nia njema kuwatakia heri vijana wa huo mtaa, ungejumuisha na mitaa mingine yote nchini Tz.

Namaanisha hivii?: mtaa huo wakifungiwa kupika gongo, walevi wa mtaa huo watahamia mtaa mwingine kwenda kunywea na kuvutia huko.

Gongo na bhangi yamekuwa ni mapato haramu ya Polisi tangu enzi za Nyerere.

Huyo Polisi uliyemchomea utambi hapo akiacha kupika yeye, ataenda kukamata iliyopikwa mitaa mingine, ataendelea kula haramu za gongo na bhangi vile vile.

Kikubwa hapo ni kushauri sheria inayoharamisha matumizi ya gongo zaidi ya miaka 50, huku gongo hiyo ikiendelea kupikwa na kunywewa iangaliwe upya ama ifutwe.

Imekuwa ikiwanufaisha Polisi kwa mlango wa nyuma tangia itungwe.
 
Arusha na Moshi huwezi zuia gongo na bangi. Kuna polisi huchukua gawio kila kila wiki kutoka kwa wauzaji. Piga kimya mkuu, ukileta mdomo utajikuta uko matatani.
 
kama ni hvo nibora waipitie sheria upya ihalalishwe kwa wote.
 
Acheni kwenda kununua.Ataacha.Au mumwambie Daudi Albert Bashite.Kwani amehama?Au anaandaa marathon na waduduz?
 
 

Attachments

  • 5919305-ec605a136bd2bee9b52fbc92e106fc6e.mp4
    7.4 MB
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…