Kuna rocket imetumwa huko angani ikagonge mwamba unaohatarisha kugonga dunia

Kuna rocket imetumwa huko angani ikagonge mwamba unaohatarisha kugonga dunia

Title yako imekaa kishabiki shabiki na kiumbea umbea mno. Unnecessary sensationalism!

Wanasayansi wanaamini kuwa huko nyuma dunia ilishawahi kugongwa na mawe haya makubwa (asteroids) na wana ushahidi huo. Jiwe la mwisho ni hili lililoua viumbe wengi duniani na kuondoa ufalme wa akina dinosaurs; na wanyama wengine lukuki.

Mawe haya yanasafiri kwa kasi ya ajabu na yanapopiga uso wa dunia yanavuvumua vumbi na uchafu mwingi ambao unaweza kubakia angani kwa miaka mingi. Vumbi na uchafu huu huenea dunia nzima na kuziba miali ya jua kabisa kabisa mpaka dunia inaingia katika kile wanachokiita deep freeze. Ina maana dunia inaganda kabisa na kutandwa na barafu kwa vile hakuna mwanga wa jua kwa muda mrefu. Na bila mwanga wa jua ina maana hakuna photosynthesis wala nishati ya aina yo yote. Matokeo yake ni vifo vya jumla kwa viumbe wengi.

Yapo mawe yanayoonyesha kuwa yatakuja kuipiga dunia huko mbele ya safari na NASA wana kitengo maalum kinachoshughulika na tatizo hili na mpaka sasa kuna nadharia tatu zilizopendekezwa kuweza kujiponya siku ikigundulika kuwa kuna jiwe linatujia huko:

1. Kurusha chombo chenye uzito na nishati maalum na kwenda kuligonga hilo jiwe huko angani likiwa mbali na dunia. Lengo hapa siyo kulisambaratisha bali ni kujaribu kulisukuma kidogo (nudge) ili liweze kuacha njia yake ya mzunguko (orbit) na hivyo kuliepusha kugongana na dunia.

2. Kurusha rocket yenye nguvu iliyobeba bomu kubwa la nyuklia na kwenda kulitandika hilo jiwe na kulisambaratisha. Hii hata hivyo inaweza tu kuishia kulimega hilo jiwe katika vipande vingi ambavyo vinaweza kuleta hatari zaidi duniani. Na kukitokea mushkeli wakati wa kurusha hiyo rocket hilo bomu linaweza kuturipukia hapa hapa duniani na kuleta madhara makubwa.

Ili kuepuka kulimega vipande vipande lipo pendekezo la kwenda kulipua bomu hilo karibu na jiwe hilo. Ile nguvu ya mripuko (boom) inaweza kutosha kulisukuma kidogo likiwa zima na kuliondoa katika orbit yake.

3. Kurusha chombo chenye monzi mikali ya laser na kwenda kujaribu kulimulika jiwe hilo na mionzi hiyo. Mawe haya mengi yana barafu iliyoganda na likipigwa na mionzi mikali kwa muda barafu inaweza kuyeyuka na hivyo kupunguza uzito wake na hii, wanadai, inaweza kusababisha liondoke kwenye orbit yake inayolifanya ligongane na dunia.

Hata bila kuyeyusha barafu yake, mionzi hii ya laser inaweza kufanya kazi sawa na utando wa buibui na hivyo kulisogeza jiwe hilo polepole nje ya orbit yake na hivyo kuepusha mgongano wake na dunia.

NASA leo wamerusha chombo kujaribu nadharia ya kwanza kama inafanya kazi kwa sababu dunia kupigwa na asteroid nyingine ni suala la muda tu. Elon Musk anarusha maroketi haya kila leo hatusikii cho chote lakini leo umeshusha ushabiki wa kufa mtu eti anga lilibadilika. Lilibadilika wapi? Labda kama ulikwenda kushuhudia wakati roketi hilo likirushwa huko California. Ni wazi hii habari hukuiandika mwenyewe na umefanya plagiarism mahali fulani (BBC Swahili) na sina uhakika kama una ufahamu wa kutosha na habari yenyewe pamoja na implications za kiujumla za kinachozungumziwa.

Wakati tunahangaika na tozo, ufisadi wa kutisha, kutengeneza madawati, kujenga nyumba za walimu, kujenga vyoo vya shimo vya kutosha mashuleni, ushirikina, ukosefu wa umeme na maji, siasa za hovyo za kuoneana hizi, wenzetu huko hawalali wanahangaika na mambo kama haya mazito. Tuombe wafanikiwe kwa sababu siku moja pengine wataweza kuokoa maisha ya viumbe hapa duniani. Hata wakishindwa wao pia wanahangaika kutafuta makazi katika sayari zingine huko wanaweza wakaondoka zao na kutuacha hapa siku mambo yakibumburuka!
Asante kwa mchango wako kaka mkubwa
 
Asante kwa mchango wako kaka mkubwa
Asante mkuu. Naona watu wanajadili jambo hili kwa ushabiki tu wakati hata leo ukienda hapo makao makuu ya NASA unaonyeshwa tu kitengo hicho kinachohangaika na kuchunguza kama kuna asteroid inayotulenga huko...na nini cha kufanya.

Tatizo hata hivyo universe ni kubwa na telescope zao zinaweza kutazama upande mmoja tu kwa wakati. Na maasteroid mengine hasa yale madogo madogo huwa hayaonekani katika makamera yao. Ndiyo maana wanajaribu kuhangaika kuona cha kufanya kama vu bin vu bonge la asteroid hili hapa linakuja moja kwa moja kutugonga....
Screenshot_20211125-040258_Chrome.jpg
 
Nimekukubali mzee.. Ukweli ni kwamba watu wapo serious na haya maisha, na hii dunia yetu.
Hakuna pengine pa kukimbilia. Kama asteroid ikija huko imeponyoka kutoka kwenye asteroid belt angalau Homo Sapiens tuwe na la kufanya na siyo kuangamia kibudu tu kama walivyoangamia akina dinosaur.

Tuwaache hawa jamaa wafanye mambo yao na sisi tubakie na ujuaji wetu usio na kichwa wala miguu...

Fikiria mwaka huu bajeti ya NASA ni dola bilioni 23.3. Hii si karibia bajeti yetu nzima kabisa? (Sina uhakika). Halafu utasikia mbongo anasema hawa jamaa wanataka kutupiga. Kuwapiga hela zenu za tozo ama? Au mnazopewa kila siku kama mikopo na misaada?
Screenshot_20211125-041625_Google.jpg
 
Hakuna pengine pa kukimbilia. Kama asteroid ikija huko imeponyoka kutoka kwenye asteroid belt angalau Homo Sapiens tuwe na la kufanya na siyo kuangamia kibudu tu kama walivyoangamia akina dinosaur.

Tuwaache hawa jamaa wafanye mambo yao na sisi tubakie na ujuaji wetu usio na kichwa wala miguu...

Fikiria mwaka huu bajeti ya NASA ni dola bilioni 24. Hii si karibia bajeti yetu nzima kabisa? (Sina uhakika)
View attachment 2022961
Deep Space Network.. Carlifornia, Madrid and Australia.. Walinishangaza sana wale jamaa wanavyomonitor anga kama wanavyomonitor ndege pale radar za airport..
Ukiachilia mbali kama execution yake itawezekana au lah, lkn ebu fikiria tu the thinking ya kwenda kuidiverge asteroid huko iliko millions of kilometres.. Halafu mpuuzi mmoja ambaye hata uwezo wa milo miwili kwa siku hana na ana miaka 40+ anakuja na hoja nyepesi za kubeza..

Nakumbuka wanasema hizo projects zimehamasishwa zaidi na kilichotokea Russia i think soon before or soon after WW1. Alfajiri vioo vya majengo ya mji mzima vilikuwa vinapigwa na punje ndogo ndogo za kokoto; wakarealize ilikuwa ni jiwe limesagwasagwa wakati linaingia anga la chini la dunia.
Wakaona lazima tuwe tunamonitor space tujue whats going on.
Baada ya kuweza kumonitor, next step ni tunafanyaje sasa kuzuia maafa?😴😴😴
 
Waache kujipa kiki hao jamaa!!Dunia italindwa na yule alieitengeneza Dunia ilivyo!!!!Tena wasije wakafanya yao wakidhani wanatengeneza kumbe ndio majanga yakazidi kwa Dunia!!Hekima ya Binadamu ni upumbavu kwake yeye alieitengeneza Dunia!!WATAJUAJE KAMA HILO JIWE NDIO NGUZO YENYE KANI ISABABISHAYO UTULIVU KWA SAYARI ZOTE???
Mkuu huyo aliyeitengeneza dunia alikuwa wapi wakati dinosaurs wakisambaratishwa na kile kimondo?
Mkuu hii dunia hauishi peke yako wewe unajali kuhusu wewe sasa hivi na unaona chini ya miguu yako wenzako wanaona miaka 1000 mbele juu ya survival ya race yao na vizazi vyao au leo kungekuwa hakuna simu, magari wala umeme kama wangekuwa na akili kama zako.

Yaani kijiwe kimoja saizi ya mpira ukilinganisha na ukubwa wa dunia ndio kinaweza kushikilia sayari zote seriously?
Trust me bila hawa jamaa wewe usingejua kabisa kwamba unaishi juu ya jiwe kubwa linaloelea kwenye empty space wala usingejua uwepo wa gravity wala uwepo wa sayari so cha kufanya ni kuachia wataalamu na wawaanzilishi wa elimu uliyosoma kufanya wanachokijua.
Wewe endelea kupambaba na tozo na bei za vifurushi.

Hapa ni sawa na mwanafunzi kumwambia mwalimu jinsi ya kufundisha au mgonjwa kumwambia daktari jinsi ya kutibu.
 
Dunia kuzunguka kote huko lakini bado ipo kwenye hatari ya kugongwa...
 
Kuna faida gani katika kuwekeza katika maigizo zaidi ya kujitekenya na kucheka mwenyewe. Maana ya maigizo ni kuongeza au kupunguza katika uhalisia bora uendelee kuwa maskini na nyuma kimaendeleo ila ukaishi katika uhalisia kuliko kuishi katila maigizo na kufurahisha mioyo yao.

Katika Sayansi iliyo feli na iliyo kaa kimaigizo ni Sayansi ya anga,kwayo mtu unakuwa na maswali ambayo hayajibiki wala wanaofanya tafiti za anga hawajahi kufikiria.

Endapo mtu ukiwa ni mwenye tabis ya kufikiri japo kidogo utapata maswali ambayo hayajibiki. Shida ya wengi wanapenda kuona wenye mambo yao washajua ya kuwa watu wanapenda kuona sana kuliko kuhoji,basi wahusika wanawaonyesha tu. Teknolojia imefika mbali sana na watu hawahoji juu ya teknolojia,mtu akifanya animation utajuaje akitengeneza picha utajuaje ila ukiwa mtu wa kuhoji uongo lazima ujitenge.

Ukiijadili hii mada kwa jicho la uhojaji na elimu hutapata uhalisia hata mmoja zaidi ya sanaa tu.
Wewe hayo maswali unayojiuliza leo na kushindwa kujibu wenzako walishajiuliza miaka 200 nyuma na kupata majibu.

Ukiona hivyo basi tambua wewe siyo Albert Einstein, Nikola Tesla wala Isaac Newton hivyo hayo maswali achana nayo na undelee kutafuta ugali sababu hicho ndio pekee waafrika wanaweza fanya kwa usahihi bila kukosa majibu.
 
Title yako imekaa kishabiki shabiki na kiumbea umbea mno. Unnecessary sensationalism!

Wanasayansi wanaamini kuwa huko nyuma dunia ilishawahi kugongwa na mawe haya makubwa (asteroids) na wana ushahidi huo. Jiwe la mwisho ni hili lililoua viumbe wengi duniani na kuondoa ufalme wa akina dinosaurs; na wanyama wengine lukuki.

Mawe haya yanasafiri kwa kasi ya ajabu na yanapopiga uso wa dunia yanavuvumua vumbi na uchafu mwingi ambao unaweza kubakia angani kwa miaka mingi. Vumbi na uchafu huu huenea dunia nzima na kuziba miali ya jua kabisa kabisa mpaka dunia inaingia katika kile wanachokiita deep freeze. Ina maana dunia inaganda kabisa na kutandwa na barafu kwa vile hakuna mwanga wa jua kwa muda mrefu. Na bila mwanga wa jua ina maana hakuna photosynthesis wala nishati ya aina yo yote. Matokeo yake ni vifo vya jumla kwa viumbe wengi.

Yapo mawe yanayoonyesha kuwa yatakuja kuipiga dunia huko mbele ya safari na NASA wana kitengo maalum kinachoshughulika na tatizo hili na mpaka sasa kuna nadharia tatu zilizopendekezwa kuweza kujiponya siku ikigundulika kuwa kuna jiwe linatujia huko:

1. Kurusha chombo chenye uzito na nishati maalum na kwenda kuligonga hilo jiwe huko angani likiwa mbali na dunia. Lengo hapa siyo kulisambaratisha bali ni kujaribu kulisukuma kidogo (nudge) ili liweze kuacha njia yake ya mzunguko (orbit) na hivyo kuliepusha kugongana na dunia.

2. Kurusha rocket yenye nguvu iliyobeba bomu kubwa la nyuklia na kwenda kulitandika hilo jiwe na kulisambaratisha. Hii hata hivyo inaweza tu kuishia kulimega hilo jiwe katika vipande vingi ambavyo vinaweza kuleta hatari zaidi duniani. Na kukitokea mushkeli wakati wa kurusha hiyo rocket hilo bomu linaweza kuturipukia hapa hapa duniani na kuleta madhara makubwa.

Ili kuepuka kulimega vipande vipande lipo pendekezo la kwenda kulipua bomu hilo karibu na jiwe hilo. Ile nguvu ya mripuko (boom) inaweza kutosha kulisukuma kidogo likiwa zima na kuliondoa katika orbit yake.

3. Kurusha chombo chenye monzi mikali ya laser na kwenda kujaribu kulimulika jiwe hilo na mionzi hiyo. Mawe haya mengi yana barafu iliyoganda na likipigwa na mionzi mikali kwa muda barafu inaweza kuyeyuka na hivyo kupunguza uzito wake na hii, wanadai, inaweza kusababisha liondoke kwenye orbit yake inayolifanya ligongane na dunia.

Hata bila kuyeyusha barafu yake, mionzi hii ya laser inaweza kufanya kazi sawa na utando wa buibui na hivyo kulisogeza jiwe hilo polepole nje ya orbit yake na hivyo kuepusha mgongano wake na dunia.

NASA leo wamerusha chombo kujaribu nadharia ya kwanza kama inafanya kazi kwa sababu dunia kupigwa na asteroid nyingine ni suala la muda tu. Elon Musk anarusha maroketi haya kila leo hatusikii cho chote lakini leo umeshusha ushabiki wa kufa mtu eti anga lilibadilika. Lilibadilika wapi? Labda kama ulikwenda kushuhudia wakati roketi hilo likirushwa huko California. Ni wazi hii habari hukuiandika mwenyewe na umefanya plagiarism mahali fulani (BBC Swahili) na sina uhakika kama una ufahamu wa kutosha na habari yenyewe pamoja na implications za kiujumla za kinachozungumziwa.

Wakati tunahangaika na tozo, ufisadi wa kutisha, kutengeneza madawati, kujenga nyumba za walimu, kujenga vyoo vya shimo vya kutosha mashuleni, ushirikina, ukosefu wa umeme na maji, siasa za hovyo za kuoneana hizi, wenzetu huko hawalali wanahangaika na mambo kama haya mazito. Tuombe wafanikiwe kwa sababu siku moja pengine wataweza kuokoa maisha ya viumbe hapa duniani. Hata wakishindwa wao pia wanahangaika kutafuta makazi katika sayari zingine huko wanaweza wakaondoka zao na kutuacha hapa siku mambo yakibumburuka!
hawana kitu hao bado watoto sana, kama tu dawa ya covid, ukimwi na vijigonjwa vingine kama hivyo imewashinda wataweza kubadili nini au kufanya lipi la ajabu ktk dunia hii?

kwa kifupi hao wa.she.nzi ni wazee wa kiki na misifa tuu, hawana jipya.
 
1. Mbingu itapo chanika,�

2. Na nyota zitapo tawanyika,�

3. Na bahari zitakapo pasuliwa,�

4. Na makaburi yatapo fukuliwa,�

5. Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.�

6. Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?�

7. Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,�

8. Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.�

9. Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.�

10. Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,�

11. Waandishi wenye hishima,�

12. Wanayajua mnayo yatenda.�

13. Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,�

14. Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;�

15. Wataingia humo Siku ya Malipo.�

16. Na hawatoacha kuwamo humo.�

17. Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?�

18. Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?�
S

19. Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
(suratul AL - INFIT'AAR)
Sijui watazuia vingapi hawa hili kupingana na maandiko ya muumba
Hayo maandiko yameandikwa na haohao unaoona wanayapinga.
Hivi hujui kama dini zililetwa afrika na wakoloni au ukristo na uislamu ulianzishwa na babu zako wa kiafrika?
Je ulishawahi kuona mwafrika mweusi kwenye vitabu vyako vya dini zaidi ya watu weupe?
 
hawana kitu hao bado watoto sana, kama tu dawa ya covid, ukimwi na vijigonjwa vingine kama hivyo imewashinda wataweza kubadili nini au kufanya lipi la ajabu ktk dunia hii?

kwa kifupi hao wa.she.nzi ni wazee wa kiki na misifa tuu, hawana jipya.
Hiyo simu unayotumia unajua ilipotengezwa?

Au uliitengeneza wewe mkuu?
Kama uliitengeneza wewe sema ndio ili nikuulize maswali juu ya huo uvumbuzi wako wa simu.
 
Kongole na Mimi pia nilikuwa na mawazo kama yako, ingekuwa ni jiwe linaelekea kuidhuru Dunia nafikiri lingeshafika siku nyingi, Kama wanaweza kutuma chombo kulifuata jiwe maana yake jiwe pia linaweza kuja Duniani, lakini mpaka sasa liko kwenyemzunguko, Hii inaashiria kuwa huenda jiwe linaikinga Dunia na athari tusizozijua.
Hiyo wanayofanya ni experiment na sio kwamba hilo jiwe linakuja straight duniani.
Hilo jiwe lipo kwenye orbit yake halina madhara yoyote na dunia.
 
Hao wazungu waliokulisha haya maneno waambie waache ujinga
 

Dart: Mpango wa kulishambulia jiwe kubwa la Dimorphos linalokaribia kugonga dunia wazinduliwa​

23 Novemba 2021
Imeboreshwa 24 Novemba 2021

jiwe kubwa

CHANZO CHA PICHA,NASA / JHUAPL / STEVE GRIBBEN
Chombo cha anga za juu kinachotarajiwa kugonga jiwe moja kubwa linalokaribia dunia kwa kasi kimezinduliwa .

Chombo hicho cha Nasa kwa jina Dart kinataka kubaini ugumu uliopo katika kuzuia jiwe hilo kugongana na dunia.

Chombo hicho kitaligonga jiwe hilo kwa jina Dimorphos ili kujua ni kiwango gani cha kasi yake kinaweza kubadilika.

Iwapo miamba iliopo angani ilio na ukubwa wa mita chache ingegongana na dunia , ingesababisha athari kubwa.

Falcon 9 - roketi inayobeba chombo hicho cha Dart ilipaa mwendo wa saa mbili alfajiri siku ya Jumatano kutoka kambi ya angani ya Vandenberg mjini Carlifonia.

Safari hiyo ya NASA itatathimini pendekezo la muda mrefu la kumaliza mwamba huo ulioko katika anga za mbali unaoelekea kwenye dunia.

Chombo hiki cha anga za mbali kitaanguka kwenye kitu kinachoitwa Dimorphos kuangalia ni kwa kiasi gani kasi na njia yake inaweza kuharibiwa.

Kama kifusi cha cosmic chenye urefu wa mita mia moja kitagongana na sayari yetu, inaweza kusababisha maafa makubwa.

Hili ni jaribio la kwanza la kuzuwia mwamba huu unaozunguka dunia kwa melengo ya kujifunza jinsi ya kuilinda dunia, ingawa aina hii ya mwamba unaolengwa wakati huu sio tisho.

"Dart itakuwa ikibadili kipindi cha uzio(obiti) ya Dimorphos kwa kiasi kidogo.

Na hilo kusema kweli ndio tu linalohitajika katika tukio ambapo mwamba utagundulika kabla ya muda ,"anasema Kelly Fast, kutoka ofisi ya uratibu wa ulinzi wa sayari ya Nasa.
Jumatano, roketi ya Falcon 9 iliyobeba chombo cha anga za mbali cha Dart itapaa kutoka ngome ya anga za mbali ya Vandenberg Space Force Base iliyopo California.

Infographic

Miamba inayozunguka jua ni mabaki yanayosalia katika ujenzi wa mfumo wa jua, huku mingi ikiwa haina tisho lolote la hatari kwa sayari yetu. Lakini wakati njia ya mwamba inapoziba njia inayozingira jua inapita ile ya dunia ili vitu viwili viweze kupita kwa wakati mmoja, na hivyo mgongano wa vitu hivi viwili unaweza kutokea.

Safari ya chombo hicho -Dart inayogarimu dola milioni 325 (£240m) italenga miamba miwili ambayo uzio wake unakaribiana - inayofahamika kama binary.

Mwamba mkubwa zaidi kati ya miamba hiyo miwili, unaitwa Didymos , ukiwa na ukubwa wa karibu mita 780 , huku mdogo zaidi ukiitwa Dimarphos-wenye upana wa mita mita 160.

Ukubwa wa Dimorphos unaweza kulipuka kwa kiwango cha nguvu sawa na bomu la nyuklia mara nyingi, na kusababisha maafa katika eneo linalokaliwa na watu wengi na kuwajeruhi makumi ya maelfu ya watu.

Miamba hii inayozingira dunia, mithili ya sayari ndogo(Asteroids) yenye milimita za ujazo 300 na mikubwa zaidi inaweza kusababisha uharibifu mkubwa katika sayari, huku miamba mikubwa zaidi ya kilomita 1 inaweza kusababisha athari kote duniani.

Roketi

CHANZO CHA PICHA,NASA
Baada ya kusafiri Dart , kwanza kitaepuka sumaku ya dunia, na kufuata uzio wake kulizingira jua.

Halafu kitazuwia binary kitakapokaribia umbali wa katika eneo la maili milioni 6.7 za dunia Septemba 2022.

Dart kitapasua na kuingia ndani ya Dimorphos kwa kasi ya karibu mita 15,000 kwa saa (6.6 kilomita kwa sekunde). Hii inatarajiwa kubadili kasi ya mwamba huo kwa kasi ya milimita moja kwa sekunde-na matokeo yake kuharibu uzio wake unaozingira Didymos.

Ni mabadiliko madogo sana, lakini inaweza kutosha tu kugonga kitu kinachoenda kugongana na dunia.

Infographic

Kuna miamba mingine mingi midogo inayozingira jua kuliko mikubwa na kwa hiyo kuwa na uwezekano wa tisho ambalo tumewahi kukabiliana nalo -kama tutawahi kukabiliana nalo-huenda litakuwa ni kutoka kwa mwamba wenye ukubwa wa aina hii ,"amesema Tom Statler, mwanasayansi anayesimamia safari hii katika Nasa.

Dart kinabeba kamera inayoitwa Draco ambayo itatoa picha za miamba yote inayozingira jua na kusaidia chombo kujiendeleza katika mwelekeo sahihi ili kugongana na Dimorphos.

Takriban siku 10 kabla ya Dart kugonga shabaha yake, chombo cha anga za mbali cha Marekani kitatuma setilaiti ndogo, iliyotengenezwa Italia inayoitwa LiciaCube. Setilaiti hiyo ndogo itatuma duniani picha za tukio, kuondolewa kwa kifusi na shimo lililotokea kutokana na athari ya tukio hilo.

Mabadiliko madogo katika njia ya Dimorphos karibu na Didymos yatapimwa kwa kutumia darubini duniani.

Chombo hicho kina maabara asilia muafaka kwa ajili ya kipimo cha aina hiyo. Kugongwa kwa chombo hicho kutabadili uzio wa Dimorphos uliopo karibu na Didymos kwa takriban 1%, badiliko ambalo linaweza kugunduliwa kwa darubini ya ardhini kwa wiki au miezi kadhaa.

CHANZO CHA PICHA,NASA / JHUAPL / ED WHITMAN
Maelezo ya picha,

Picha ya wakaguzi wamtambo wa miale ya jua wa chombo cha anga za mbali mwezi Agosti
Hatahivyo, iwapo Dart kingejigonga katika mwamba wa wenyewe, muda wake wa uzio unaozunguka Jua ungebadilika kwa karibu 0.000006%, jambo ambalo lingechukua miaka mingi kulipima.

Mwamba wa binary ni mdogo sana kiasi kwamba hata kwa darubini zenye uwezo mkubwa wa kuvuta picha za mbali, huonekana kama nukta ya mwangaza.
Hilo jiwe lije tu tena lianzie Tanzania maana maisha yamekuwa magumu, kila kitu bei
 
Waache kujipa kiki hao jamaa!!Dunia italindwa na yule alieitengeneza Dunia ilivyo!!!!Tena wasije wakafanya yao wakidhani wanatengeneza kumbe ndio majanga yakazidi kwa Dunia!!Hekima ya Binadamu ni upumbavu kwake yeye alieitengeneza Dunia!!WATAJUAJE KAMA HILO JIWE NDIO NGUZO YENYE KANI ISABABISHAYO UTULIVU KWA SAYARI ZOTE???
wishfull thinking
 
Hivi katika hii mada ulivyo isoma hujajiuliza chochote kuhusu ukweli wa mada husika au umependa stori na picha ?

Mimi nilivyo soma hii mada cha kwanza nilianza kuhoji au kujiuliza juu ya picha ukiangalia kwa umakini hizo picha ni picha bunifu hakuja picha hata moja ambayo ni halisi.

Kingine kuhusu vipimo na utoaji wa majina na maelezo ya jambo husika,maelezo yanaonyesha ya kuwa wahusika hawana maarifa sahihi juu ya anga na vilivyomo. Swali la msingi nililo jiuliza ni kuwa wametumia mchakato gani kujia ukubwa wa hilo jiwe ?

Nani wa kwanza kutambua uwepo wa jiwe hilo na ilikuwa lini na alijuaje kuhusu jiwe hilo ?
Hivi unafahamu kwamba annual budget ya NASA ni 22,000,000,000 dollars?
Hiyo ni 22 US billion dollars sawasawa na trilion 45 za kitanzania.
Wewe unazo trilion 45 kwa ajili ya kupata majibu unayoyataka? kama huna kaa kimya.
Na hili andiko halijaandikwa na NASA bali limeandikwa na mtu mmoja mwenye uelewa hafifu na haya mambo hivyo bila shaka hawezi kujua chochote kuhusu jinsi gani NASA wamefanya mpaka kuja na majibu.
Usitumie google bali jifunze kutumia WIKIPEDIA, kule kuna majibu yote kama utakuwa na kichwa cha kuelewa kilichoandikwa.

Otherwise you're manchild asking childish questions.
 
Wewe hayo maswali unayojiuliza leo na kushindwa kujibu wenzako walishajiuliza miaka 200 nyuma na kupata majibu.

Ukiona hivyo basi tambua wewe siyo Albert Einstein, Nikola Tesla wala Isaac Newton hivyo hayo maswali achana nayo na undelee kutafuta ugali sababu hicho ndio pekee waafrika wanaweza fanya kwa usahihi bila kukosa majibu.
Sababu nimepewa akili na hakuna aliyejibu maswali hayo si wakina Eistein wala kina Tesla.

Huu udhaifu wa kutokuhoji wameshaujua Wanasayansi ndiyo maana wanafanya wanayo yataka sababu wanajua watu hawana muda huo.

Soma habari za kina Albert Einstein na Albert Michelson katika issue ya "How Einstein Kept the Stationary Earth Moving and Took Physics Away From Empiricism to the Fantasies of Imagination". Ujue ni kwa namna gani Einstein alivyo kilaza, kwahiyo suala la kuhoji hatuwezi kuacha sababu uhalisia upo na tunaishi nao.
 
Back
Top Bottom