Kuna sababu gani Tundu Lissu kukaa kimya kabisa kwenye kesi ya Ugaidi ya Mbowe?

Kuna sababu gani Tundu Lissu kukaa kimya kabisa kwenye kesi ya Ugaidi ya Mbowe?

Je ndio ameamua kuwa kimya ili Mbowe akifungwa aje Kama Mwenyekiti mpya wa chama?!!.

Je ameamua kufuata mkondo wa Swahiba wake Zitto Zuberi Kabwe aliyekaribia kumsajili ACT-Wazalendo kuwa tusitegemee kuona akikosoa Kama Awamu iliyopita.

Nilimsikia kuwa alishawahi kupigiwa simu kwamba Mama anataka kuongea nae ila akashangaa ukimya. Je walishaongea na kumaliza tofauti zao hivyo hawezi kuiongelea kesi hii sababu anaweza kumuudhi mama. Au ni sehemu ya maongezi yao kuwa akae kimya.

Au Tundu Lissu anaamini Mbowe ni Gaidi kweli na ameona ushahidi unajitosheleza hivyo anaogopa kuongea hukumu ikaja kinyume akaumbuka.

Au amekumbuka kurudi home na amechoka kukaa uhamishoni hivyo anajitahidi kutouudhi utawala mpya kabla ya kurudi.

Au ndio fadhila ya kesi zake kufutwa.

Sipendi aongee kashfa zake hapana. Natamani atoe uchambuzi na maoni kwa Serikali na dunia Nini kifanyike kumnasua Freeman haraka kwenye huu mtego utakaomuweka maabusu mwaka mzima.

Naona Mbowe ananigwa na kugalagala pekeyake. Sio Salum Mwalimu, Zitto, Mbatia, Shibuda, Viongozi wa dini wanaoshugulika ata kumuongelea au kusisitiza haki kufuata mkondo wake.

Tundu kaa kimya hivyohivyo tusubiri mawe yaongee.
Tundu Lissu ni Wakili msomi, anajua madhara ya kuongelea kesi iliyoko mahakamani. Madhara ya Lissu kuongelea kesi hii ni makubwa sana. Itoshe tu hadi hapo kusema, tusubiri maamuzi ya mahakama.
 
Ikiletwa hapa kauli na msimamo wa Lissu kuhusu kesi ya Mbowe utaufunga huu uzi au utazima data?
HAKUNA KITU LISSU NDIYO ANA MONITOR HIYO KESI IWE NGUMU KWA MBOWE ANAONGEA NA KIBATALA KILA SIKU NDIYO MAANA KIBATALA ANAIKOROGA TU HII KESI HAKUNA POINT YA MAANA ANAYOIONGEA YA KUMNASUA MBOWE KIBATALA LISSU WAO LAO MOJA MBOWE AFUNGWE WACHUKUE UENYEKITI MAANA KILA ALIYETAKA KUWA MWENYEKITI ALIPOTEZWA AKAPONA SUMAYE ALIYEAMBIA ANATAKA KUONJA SUMU
 
HAKUNA KITU LISSU NDIYO ANA MONITOR HIYO KESI IWE NGUMU KWA MBOWE ANAONGEA NA KIBATALA KILA SIKU NDIYO MAANA KIBATALA ANAIKOROGA TU HII KESI HAKUNA POINT YA MAANA ANAYOIONGEA YA KUMNASUA MBOWE KIBATALA LISSU WAO LAO MOJA MBOWE AFUNGWE WACHUKUE UENYEKITI MAANA KILA ALIYETAKA KUWA MWENYEKITI ALIPOTEZWA AKAPONA SUMAYE ALIYEAMBIA ANATAKA KUONJA SUMU
rudi shule.
 
Ameona mziki mnene.
Amejifunza pia, kubwabwaja akizunguka dunia yote Tanzania iwekewe vikwazo lakini kaangukia pua.
 
Huo msimamo wa Jana au ule wakati kesi inaanza? Mimi maoni yake ya kila siku wakati kesi ikiwa inaendelea. Yawe ya ndani ya siku tatu hizi
Unafahamu bunge la makabwela linaloitwa Club house au Maria Space? Kama hujui itafute hata leo na utasikia Lissu anasema nini kuhusiana na mwenendo mzima wa hii kesi.
 
Una UMRI GANI??

Jambo likiwa mahakamani halipaswi kuropokwa hovyo.

Yeye anawasiliana na mawakili wengine wa utetezi ili kuweza kushinda kesi hii dhidi ya Jamhuri.
 
Mushumbus ktk ubora wake. Mwiraqw mwenzangu Slaa kala hasara ya kudumu. Unadhani wanasheria wa CDM hawana mawasiliano Lisu? Kwanini Lisu aongelee kesi iliyopo mahakamani huku akijua utaratibu wa sheria?
Sio hulka yake kukaa kimya. Na Kama kunakitu Lissu anasaidia Jopo la mawakili ingekuwa wazi kwa wakili yoyote kumtambua mchango wake kwenye kesi hii. Siasa ya Afrika ngumu hasa ukiwa huna Ela. Ukimtoa Jamsi Mapalala na Mchungaji Mtikila wabishi wote walishapotezaga msimamo. Unamkumbuka Mrema, Mwanasheria Masumbuko Lamwai, Julius Mtatiro, Moses Machari, Zitto yula wa 2006 Hadi 2008.

Ukimiya wake Sasa unatia Shaka ngoja tuone mwisho wake.
 
Nenda kwenye hopeless space yao uko Kila alhamis utaona anaongea wakiwa na wale kina dada ambao wamesomeshwa na pes aza ccm na mpaka leo wazazi wao wanahudumiwa na ccm na ndipo wanapata kiburi cause wanajua hata wakikosa kazi ccm ipo inatunza wazazi wao so Wana uhakika wa kula na kulala bure so wanakuja walisha matango pori kina mdude ambao wakizingua tu dakika mbili defender zipo mlangoni mwao
Muwe mnatunza akili hata kidogo. CCM ina hela ya kuwasomesha watu au za kupora?
 
Je ndio ameamua kuwa kimya ili Mbowe akifungwa aje Kama Mwenyekiti mpya wa chama?!!.

Je ameamua kufuata mkondo wa Swahiba wake Zitto Zuberi Kabwe aliyekaribia kumsajili ACT-Wazalendo kuwa tusitegemee kuona akikosoa Kama Awamu iliyopita.

Nilimsikia kuwa alishawahi kupigiwa simu kwamba Mama anataka kuongea nae ila akashangaa ukimya. Je walishaongea na kumaliza tofauti zao hivyo hawezi kuiongelea kesi hii sababu anaweza kumuudhi mama. Au ni sehemu ya maongezi yao kuwa akae kimya.

Au Tundu Lissu anaamini Mbowe ni Gaidi kweli na ameona ushahidi unajitosheleza hivyo anaogopa kuongea hukumu ikaja kinyume akaumbuka.

Au amekumbuka kurudi home na amechoka kukaa uhamishoni hivyo anajitahidi kutouudhi utawala mpya kabla ya kurudi.

Au ndio fadhila ya kesi zake kufutwa.

Sipendi aongee kashfa zake hapana. Natamani atoe uchambuzi na maoni kwa Serikali na dunia Nini kifanyike kumnasua Freeman haraka kwenye huu mtego utakaomuweka maabusu mwaka mzima.

Naona Mbowe ananigwa na kugalagala pekeyake. Sio Salum Mwalimu, Zitto, Mbatia, Shibuda, Viongozi wa dini wanaoshugulika ata kumuongelea au kusisitiza haki kufuata mkondo wake.

Tundu kaa kimya hivyohivyo tusubiri mawe yaongee.
Ama mambo ya maana ya kufanya kwenye chama...hao jamhuri wache wapambane na Kibatara hadi wanabeba madesa kizimbani mchezo.
 
Back
Top Bottom