Kuna shida gani Tanzania ikitangaza rasmi kuisaidia Congo kupambana na M23? Tuna Viongozi wa namna gani?

Kuna shida gani Tanzania ikitangaza rasmi kuisaidia Congo kupambana na M23? Tuna Viongozi wa namna gani?

Congo hana hela?

Ungejua kuna Mercenaries wa kirusi na kichina wanalipwa na Serikali ya Congo ku provide ulinzi maeneo strategically hata usingeongea hayo mashudu hapo!

Kama wanalipa mercenaries kinawashinda nini kulipa kurudisha amani na usalama nchini mwao hadi waingiliwe na TZ?
 
Congo hana hela?

Ungejua kuna Mercenaries wa kirusi na kichina wanalipwa na Serikali ya Congo ku provide ulinzi maeneo strategically hata usingeongea hayo mashudu hapo!
Hao mercenaries kwa nini wasitumike pia kwenye mgogoro huo!? Ni wazi hawana fedha. By the way, hao wanyama unaokula wengi wanakula mashudu. Kwa hiyo indirectly hata wewe unakula mashudu.
 
Hakuna faida yeyote ile. Changamoto za kufanya biashara Congo ni sawa na changamoto za Zambia au Uganda so kuingilia internal affairs zao hakuna uhakika wowote ule kwamba TZ itafaidika kiuchumi.

Kama Congo kuna faida nchi zingine wangeweza kwenda sio lazima TZ. Kenya, Angola zenye uchumi mkubwa wanaweza kwenda kupata hizo faida ila hakuna mtu anajishughulisha that speaks volume.

TZ iliyoshindwa ku maximize potential zake za ndani kukimbilia kuingilia nchi za watu ni ujinga na ufinyu wa kufikiri. Madini, bandari, mbuga, kilimo, viwanda vimewafikisha wapi ambavyo havihitaji anything to do Congo? Wewe kama mfanyabiashara biashara yako mwenyewe inakushinda kuingilia za mwingine utaweza vp?

Your notions doesn't make no sense.
Naheshimu mawazo yako.

Pamoja na kukuheshimu kama one of great thinkers wa siku nyingi ila nikiri tu hii mada imekuzidi uwezo.

Kwani 2012 hatukwenda Congo? Kama tulienda mwaka ule kwa mawazo ya kufanta liberation tu kwa nini tusiende saivi kwa mawazo na akili za kufaidika kiuchumi?

Tuseme hujui faida ya kiuchumi zilizopo Mashariki mwa Congo? Unadhani nchi ya Uganda na Rwanda kwa miaka mingi saivi zinaendesha chumi zao kwa fedha za wapi?

Mada hii inaweza kuanza kuziamsha mamlaka za Tanzania on how to start benefiting from conflict areas.

Tukitanua akili zetu kuanza kuwaza mambo makubwa namna hiyo its obvious tutawaza mambo makubwa hadi kwenye masuala yetu ya ndani.

Asante.
 
Leo tunajenga reli ya SGR kwa dhumuni ifike Mashariki mwa Congo. Swali ni Je hiyo reli itakuwa na faida kama Mashariki mwa Congo kukiendelea kuwa vitani namna hii?

Tuache suala la reli. Hivi Je Viongozi wetu hawajui tunaweza faidika kiuchumi endapo leo hii tukiwasaidia wazi Congo kwenye vita yao dhidi ya M23?

Marekani, Uingereza na Ujerumani wanatoa msaada mkubwa kwa Ukraine kupambana na Urusi. Msaada ule sio msaada kama msaada ni mkopo ambao Ukraine watazilipa nchi zile kwa miaka mingi ijayo!

Tuseme Viongozi wetu hawa hawaoni kuwa tunaweza kutoa msaada wa kijeshi kwa Congo sisi kama Tanzania ( Sio chini ya mwamvuli wa SADC au AU au EAC) na tukautumia kama mkopo kwa nchi ya Congo ambapo baadae watatulipa hata kwa karne nzima na tukafaidika kiuchumi?

Hivi nchi hii kuna Think Tanks? Ni kina nani hao Think Tanks? Wana Mchango gani positively kwa maendeleo ya Taifa?
Hata kama hakuna ushahidi, kwani ni kosa? Wapo wengi wanaosema eti hatuwezi kuwakung'uta M23 kwa vile wanaungwa mkono na Rwanda. Kama Kagame alimshindwa Habyarimana hadi akamtungua, atatuweza sisi tuliomtandika nduli? Kama hamuwezi Museveni tuliyemtengeneza, atatuwezaje sisi? Hawa ni wa kuchapwa na kutwaa kiinchi kama Rwanda na kukifanyia tuliyoifanyia Uganda na ikatulia.
 
Naheshimu mawazo yako.

Pamoja na kukuheshimu kama one of great thinkers wa siku nyingi ila nikiri tu hii mada imekuzidi uwezo.

Kwani 2012 hatukwenda Congo? Kama tulienda mwaka ule kwa mawazo ya kufanta liberation tu kwa nini tusiende saivi kwa mawazo na akili za kufaidika kiuchumi?

Tuseme hujui faida ya kiuchumi zilizopo Mashariki mwa Congo? Unadhani nchi ya Uganda na Rwanda kwa miaka mingi saivi zinaendesha chumi zao kwa fedha za wapi?

Mada hii inaweza kuanza kuziamsha mamlaka za Tanzania on how to start benefiting from conflict areas.

Tukitanua akili zetu kuanza kuwaza mambo makubwa namna hiyo its obvious tutawaza mambo makubwa hadi kwenye masuala yetu ya ndani.

Asante.
Unaweza kwenda kwenye conflicts kwa lengo la kupata benefit lakini huo mgogoro ukakuzidi uwezo na wote mkawa kwenye migogoro,leo Tz ikienda yenyewe kama yenyewe kupambana na M23 huoni kwamba tayari mgogoro wa kidiplomasia na Rwanda utakuwa mkubwa?
 
Unaweza kwenda kwenye conflicts kwa lengo la kupata benefit lakini huo mgogoro ukakuzidi uwezo na wote mkawa kwenye migogoro,leo Tz ikienda yenyewe kama yenyewe kupambana na M23 huoni kwamba tayari mgogoro wa kidiplomasia na Rwanda utakuwa mkubwa?
What did we loose mwaka 2012 tulipoenda kuwasaidia Congo?

Kila biashara ina risks zake. Kama tulienda mwaka 2012 bila ya kuwa na mawazo ya kiuchumi na tulifanikiwa kwa nini tushindwe saivi?

Hatujui uwezo wetu wa kijeshi?
 
Unaweza kwenda kwenye conflicts kwa lengo la kupata benefit lakini huo mgogoro ukakuzidi uwezo na wote mkawa kwenye migogoro,leo Tz ikienda yenyewe kama yenyewe kupambana na M23 huoni kwamba tayari mgogoro wa kidiplomasia na Rwanda utakuwa mkubwa?
Rwanda inatakiwa atangazwe kama adui wa EAC sio wa kuchekea
 
What did we loose mwaka 2012 tulipoenda kuwasaidia Congo?

Kila biashara ina risks zake. Kama tulienda mwaka 2012 bila ya kuwa na mawazo ya kiuchumi na tulifanikiwa kwa nini tushindwe saivi?

Hatujui uwezo wetu wa kijeshi?
Hatujapoteza kitu! Je migogoro imeisha? Kama ni rahisi hivo Kwanini wahusika wenyewe ambao ni Congo wameshindwa kupambana na kundi ndogo la waasi?
 
Leo tunajenga reli ya SGR kwa dhumuni ifike Mashariki mwa Congo. Swali ni Je hiyo reli itakuwa na faida kama Mashariki mwa Congo kukiendelea kuwa vitani namna hii?

Tuache suala la reli. Hivi Je Viongozi wetu hawajui tunaweza faidika kiuchumi endapo leo hii tukiwasaidia wazi Congo kwenye vita yao dhidi ya M23?

Marekani, Uingereza na Ujerumani wanatoa msaada mkubwa kwa Ukraine kupambana na Urusi. Msaada ule sio msaada kama msaada ni mkopo ambao Ukraine watazilipa nchi zile kwa miaka mingi ijayo!

Tuseme Viongozi wetu hawa hawaoni kuwa tunaweza kutoa msaada wa kijeshi kwa Congo sisi kama Tanzania ( Sio chini ya mwamvuli wa SADC au AU au EAC) na tukautumia kama mkopo kwa nchi ya Congo ambapo baadae watatulipa hata kwa karne nzima na tukafaidika kiuchumi?

Hivi nchi hii kuna Think Tanks? Ni kina nani hao Think Tanks? Wana Mchango gani positively kwa maendeleo ya Taifa?
Uko sahihi kabisa.
 
Utazishawishije Kenya na Uganda ziiwekee Rwanda vikwazo? Wao huo mgogoro wa M23 unawapunguzia fursa gani?
Ukiachilia mbali fursa mkuu, kuwepo kwa kundi kama M23 ni tishio kiusalama kwa nchi zote kusini mwa bara la Africa, leo ni Congo wakifaulu itakuja uganda, mara Tanzania , Kenya n.k.

Makundi kama hayo yanaweza fanya sabotage za miundombinu, machafuko na vita itakayorudisha maendeleo nyuma.

Jirani zako wanapokuwa kwenye machafuko na vita hizo athari zinakuja hadi kwako kiuchumi na kiusalama, utapokea wakimbizi, utashindwa fanya biashara za kuuza mazao ya chakula n.k...

Madhara ni mengi..
 
Kagame and M7 are a byproduct of Nyerere's failed diplomacy and lack of political acumen. TZ installed these monsters to power, and handed them UGANDA which was used as launchpad against governments of Rwanda, Burundi and Zaire.

This time, Kagame is bringing was at your doorstep, and you're freaking out. Just deal with it 🤣🤣🤣​
 
Tulifanya hivyo mwaka 2012 tulipata shida gani?

Unaongelea Diplomasia kwani Congo sio mwanachama wa EAC?

Kuhusu rasilimali pia hizo fedha Congo anazolipwa vikundi vya mercenaries kwa nini asitulipe sisi tukanunua silaha kuwapambania?

Sikubaliani na hoja zako! Zaidi naona faida zaidi kwetu kiuchumi endapo tuki liberate Mashariki mwa Kongo kwa makubaliano maalum na nchi ile na hata tukiwa na Military Base pale.
Ni kweli Congo ni mwanachama wa EAC sasa (kuanzia 2022), lakini hoja ya diplomasia inahusu tahadhari na usawa wa kushughulikia maslahi ya nchi wanachama wote, hasa Rwanda ambayo inatajwa mara kwa mara kuhusika na M23.
 
Vita ni hasara Tupu Trump imegundua Hilo

Jenga uchumi achana na mawazo ya vita.
 
hoja yako ina msisimko lakini haina mashiko hebu tuiangalie kwa ukaribu. Rwanda inaingilia Congo kwa njia za kificho, na mara nyingi inakosolewa kimataifa. Tanzania, kwa heshima yake, haiwezi kutumia mbinu za "kuvizia" kama Rwanda. Sisi tuna historia ya kuheshimu sheria za kimataifa, na hatutaki kujifananisha na taifa linalotuhumiwa kufadhili waasi ili kufyonza rasilimali kwa njia za kifisadi.

Kuhusu "wafuga vitambi," tunaweza kuwa nao, lakini uamuzi wa kupeleka jeshi Congo si suala la kula madini tu. Tukifanya hivyo bila mipango madhubuti, tunaweza kuishia kuonekana kama wavamizi badala ya waokozi. Kujenga msingi wa kijeshi Congo ni rahisi kusema, lakini ni ghali kwa vitendo, hasa bila ushirikiano wa kweli wa Congo na jamii ya kimataifa.

Tanzania ina fursa ya kusaidia kwa mkataba, lakini sio kwa njia za "Rwanda style." Tunahitaji mipango thabiti, si haraka za kuchota madini huku tukihatarisha amani yetu wenyewe. Tukishindwa, hatutakula madini; tutakula aibu.

huu

huu ni uwoga tu mbona Rwanda hajawa shabaha ya mashambulizi ndio kwanza anavuna madini hapo congo, hata kule Central Africa Rwanda anavuna madini.

huu ndio wakati sasahihi Hawa wafuga vitambi waenda congo kuchota utajiri iwe kwa mkataba na serikali ya congo au kama kama Rwanda afanyavyo.
 
hoja yako ina msisimko lakini haina mashiko hebu tuiangalie kwa ukaribu. Rwanda inaingilia Congo kwa njia za kificho, na mara nyingi inakosolewa kimataifa. Tanzania, kwa heshima yake, haiwezi kutumia mbinu za "kuvizia" kama Rwanda. Sisi tuna historia ya kuheshimu sheria za kimataifa, na hatutaki kujifananisha na taifa linalotuhumiwa kufadhili waasi ili kufyonza rasilimali kwa njia za kifisadi.

Kuhusu "wafuga vitambi," tunaweza kuwa nao, lakini uamuzi wa kupeleka jeshi Congo si suala la kula madini tu. Tukifanya hivyo bila mipango madhubuti, tunaweza kuishia kuonekana kama wavamizi badala ya waokozi. Kujenga msingi wa kijeshi Congo ni rahisi kusema, lakini ni ghali kwa vitendo, hasa bila ushirikiano wa kweli wa Congo na jamii ya kimataifa.

Tanzania ina fursa ya kusaidia kwa mkataba, lakini sio kwa njia za "Rwanda style." Tunahitaji mipango thabiti, si haraka za kuchota madini huku tukihatarisha amani yetu wenyewe. Tukishindwa, hatutakula madini; tutakula aibu.
Rwanda haiingii Congo kwa kificho. Kuna hadi taarifa ya UN iliyo confirm kuwa Rwanda ndo M23 wenyewe.

Marekani aliisaidia Kuwait ilivyovamiwa ba Iraq ndipo tukawa na Gulf War. Hadi leo Marekani ana maslahi ya kudumu Kuwait.

Kuna faida kubwa kiuchumi tuliingia Congo tena kipindi hiki kwa akili hizi za kufaidika kiuchumi kuliko wakati wowote ule.
 
Rwanda haiingii Congo kwa kificho. Kuna hadi taarifa ya UN iliyo confirm kuwa Rwanda ndo M23 wenyewe.

Marekani aliisaidia Kuwait ilivyovamiwa ba Iraq ndipo tukawa na Gulf War. Hadi leo Marekani ana maslahi ya kudumu Kuwait.

Kuna faida kubwa kiuchumi tuliingia Congo tena kipindi hiki kwa akili hizi za kufaidika kiuchumi kuliko wakati wowote ule.
Taarifa ya UN kuhusu Rwanda na M23 ni kweli, lakini hiyo inathibitisha kuwa Rwanda inaingilia Congo kiharamu na inalaumiwa kimataifa. Tanzania haiwezi kufuata mkondo huo, lazima tuwe mfano wa heshima kwa makubaliano rasmi na serikali ya Congo.

Kuhusu mfano wa Marekani na Kuwait, ni sahihi: Marekani ilitumia nguvu za kijeshi kulinda maslahi yake na kuimarisha uwepo wake wa kudumu. Tanzania inaweza kufanya hivyo, lakini siyo kama mkoloni mpya bali kama mshirika wa Congo. Tukiliberate Mashariki mwa Congo kwa mkataba wa wazi, tunapata maslahi ya madini, biashara, na hata kambi za kijeshi za kudumu.

Hii ni nafasi ya kipekee, lakini si lazima tuiingilie kwa haraka bila mipango. Faida ya kiuchumi inakuja, lakini lazima tufanye kwa ustaarabu ili kulinda taswira yetu na amani ya kikanda.
 
Back
Top Bottom