Kuna tahadhari za kuongezeka matukio ya ujambazi na unyang'anyi, mamlaka husika zimeshindwa?

Kuna tahadhari za kuongezeka matukio ya ujambazi na unyang'anyi, mamlaka husika zimeshindwa?

Bepari la bariadi

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2016
Posts
420
Reaction score
671
Pasipo kumung'unya maneno Hali ya usalama wa raia na Mali zao imetikiswa kwa kipindi hiki, matukio ya ujambazi, unyang'anyi, ukwapuaji, na ukabaji yameendelea kushamiri sasa licha ya kuwepo na matamko mbali mbali kutoka kwa wenye dhamana na usalama wa raia.

Kama halijakukuta Basi fanya simple research kwa kuulizia watu maeneo yako ya kazi au kwenye Daladala au hata kijiweni tu uwaulize maoni yao kuhusu hali ya usalama mtaani kwao,kila kukicha utasikia hapa kama siyo pale.

Kuna huu ukwapuzi wa simu au bag na bodaboda unarudi nao kwa kasi. Tena hawa washenzi wanafunika plate number za pikipiki zao.

Polisi anzeni na hawa, wanaharibu Jina la bodaboda wengine walio raia Wema.

Lakini pia ile spirit na kasi ya kutokomeza ushenzi huu imeishia wapi? Je, nayo imezikwa na mwendazake? Watu hawana amani kabisa hasa jua linapozama.

Mama yetu, kwa hili nakuomba usilegeze sauti mama.

Punda haendi bila mijeredi na ukicheka na nyani utavuna mabua.
 
Kwanini mnakuza mambo bila sababu? Weka hapa majina ya ndugu zako waliouwawa na majambazi ndani ya wiki hii. Mama Samia yuko mioyoni mwa watanzania never try to distort her image; hamtoweza kwa sasa.
 
Hizo tahadhari zimetolewa wapi? Na nani?

Hivi Mo Dewji aliyetekwa kipindi cha Magufuli na kwenda kutupwa karibu na Ikulu, hii ingetokea kipindi cha Samia sijui mgesemaje nyie watu?

Ujambazi ulikuwa ukifanyika awamu zote brother, tena kuna hadi wakuu wa wilaya na mikoa waikuwa wakifanya huo ujambazi awamu iliyopita huku wakilindwa na Rais.
 
Hapa ndipo great thinker nawategemea,siyo wapambe wa kigogo, diamond na mpambaz😃
 
Kwanini mnakuza mambo bila sababu? Weka hapa majina ya ndugu zako waliouwawa na majambazi ndani ya wiki hii. Mama Samia yuko mioyoni mwa watanzania never try to distort her image; hamtoweza kwa sasa.
We jamaa moron kabisa,na wewe weka majina ya ndugu zako na majirani waliokufa kwa Corona.
 
Hizo tahadhari zimetolewa wapi? Na nani?

Hivi Mo Dewji aliyetekwa kipindi cha Magufuli na kwenda kutupwa karibu na Ikulu, hii ingetokea kipindi cha Samia sijui mgesemaje nyie watu?
Soon itakufikia brother Kama haijakufikia mpk Sasa
 
Sasa hivi wana relax na kuenjoy naonaa.
 
1622920687162.png
 
Waloshangilia kipindi mwendazake kwenda sasa tutawaona wizi utakithiri adi serikalini sio tuu mtaani. Yajayo yanafurahisha hii nchi bila ukali wa kujali maslahi mapana na usalama wa wanachi kuuweka mbele tutarudishwa hatua mia nyuma.

Ni bora uonekana katili kwa washenzi wachache kuliko kupoteza amani ya wananchi wengi mbaya zaidi naogopa inawezekana wengine wako wamevalia vazi la usalama.
 
Ujambazi ulikuwa ukifanyika awamu zote brother, tena kuna hadi wakuu wa wilaya na mikoa waikuwa wakifanya huo ujambazi awamu iliyopita huku wakilindwa na Rais
Kwa hiyo unabariki kosa lihalalishe kosa.

Toa hoja ki great thinker uitendee haki JF
 
Back
Top Bottom