Kuna tatizo la kiufundi mahali kwenye kizazi hiki tukubali au tukatae au ni njia mpya ya siasa?

Tanganyika kuna fursa mpya ya ajira ijulikanayo km UCHAWA na wanaosifia kwa jina ni CHAWA wakati wanao sifiwa ndio makazi ya CHAWA (SEHEMU ZENYE UCHAFU au CHAFU)
 
Mkuu,
Mtu anasifu na kuabudu mwanadamu kama MUNGU

Cc. Lucas mwashambwa
 
Sehemu yoyote ambako watu wengi wana elimu duni na njaa basi unafiki, kujipendekeza, majungu na ushirikina ndio mtindo wa maisha.
Watanzania wengi ni watu washirikina sana, wanafiki, watu wa kujipendekeza sana na watu wa majungu sana!
Nenda maofisini, kwenye biashara , kwenye siasa na hata kwenye michezo hizo ndo sifa!
Yote hii ni kwa sababu ya elimu duni na umasikini uliopitiliza!
Watanzania wengi mtu akiwa na cheo au maendeleo kidogo ya kiuchumi basi huyo ndo Mungu wao!
 
Sio kwa ubaya ila nawe unachanganya madesa, kwa hiyo hapo kipengele ni kusifiwa au kuitwa dokta tu pia unaona jau???

Maana sidhani kama kuna issue hapo mtu kuitwa dokta, kwa kifupi umeanza vizuri ila umemaliza vibaya

Kusifia kulianza baada ya watu hasa wenye maslahi binafsi kama wanasiasa ni kuendekeza uchawa ila hakuna policy ambayo iliwekwa fulani asifiwe, ila watu kuwa na dhamira yao binafsi kama kuonwa na fulani ndio wakaja na hizo pigo, na ukiwa rais ni ngumu kuzuia hivyo kwa sababu hata ukisema watu hawaachi nakumbuka hata Magufuli aliwahi sema hivyo ye anachotaka ni kazi tu ila watu wakaendeleza


NB: hili siwezi kuliacha hivi hivi, na nikiri kwa imani yangu sijawahi kusikia Rais aliesifiwa mitaani kwenye mazungumzo yasiyo rasmi iwe ya mmoja mmoja au kikundi bila hayo ma-platform ya mubashara sijui redio, Runinga ama jukwaa la kisiasa kama Magufuli na nimekuwa active kuanzia utawala wa Mkapa mpaka sasa.
 
Nyerere kasifiwa na vimeingia kichwani Kama dini,ni Mungu mtu,kiasi hawezi kosolewa kwa baadhi ya watu,na ukimkosoa unatazamwa kwa jicho la malaika wa motoni

Watetezi wa Nyerere wanayo hoja. Kwamba, enzi hizo kweusi, angetumia nafasi yake ya Urais na Uenyekiti wake wa CCM Taifa. Muda huu tunavyojadili habari za Mwl Nyerere, watu wa kabila lake na watu wa dini yake ndio watu pekee ambao wangekuwa wamehodhi mifumo yote ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.

Itoshe kusema, migodi ya dhahabu, mafuta na gesi na rasilimali zinginezo hazikuanza kuvunwa wakati wa Mwl Nyerere. Hoja yake kipindi hicho ilikuwa ni kuwa na subra hadi kuwepo Watanzania wenye sifa na uwezo wa kushiriki ipasavyo kwenye ugemaji wa rasilimali hizi. Ukiniuliza ikiwa alikuwa sawa, nitasema ndio.

Maana baada Azimio la Arusha lililotaifisha mali za mabepari, Watanzania waliopokea hizo mali hawakuweza kuziendeleza. Hivyo Mwl Nyerere aliona amefanya kosa na hakutaka kurudia kosa.

Fast forward, waliopokea kijiti cha uongozi kwa Mwl Nyerere, mbona hawatangulizi maslahi ya nchi kama alivyofanya mtangulizi wao? Tafakuri ya swali hili ndio linarejesha sifa kem kem kwa yule Mzee.

Wakosoaji wa Mwl Nyerere pia sioni kama wanatatizo. Maana lengo lao ni kuibua madhaifu ya kiuongozi ya Mwl ili viongozi waliopo na wajao wasirudie makosa yale yale. Pengine no muhimu kwa wakosoaji kujenga hoja za kimazingira na nyakati ili kuibua mjadala chanya kuhusu viongozi waliopita (Mwl Nyerere et Al) versus viongozi waliopokea kijiti. Lengo liwe kujenga badala ya kudogodesha.
 
Watanzania Binadamu wengi mtu akiwa na cheo au maendeleo kidogo ya kiuchumi basi huyo ndo Mungu wao!

Mkuu Fumadilu Kalimanzila

Hii hoja umeibua hapa ni kama maelezo ya ziada ya kwenye amri ya kwanza Kati ya zile amri 10 za Musa. Binadamu anayewazidi wenzake kwa lolote anajikuta amekuwa Mungu wao.

Ni shida ipo Tanzania, ni shida ipo Duniani kote. NIAMINI!
 
For now it's disgusting. narudia alieasisi uchawa alaaniwe ila pia . Magu baada ya kuanza kuteua watu wanaolamba viatu Kasi ya wadudu chawa ilishika hatamu
 
Kwamba watu wa dini yake na kabila lake hawakushika hatamu za nchi!?..hivi wakatoliki hawajashikilia mifumo ya utawala wa nchi!?..watu wa Mara hawakutapakaa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama!?..watu wasivune rasilimali za nchi wangoje nini!?..watanzania wa Nyerere walimudu kununua vyombo vya moto na kujenga makazi Bora Kama wa Leo!?
 
Kwamba watu wa dini yake na kabila lake hawakushika hatamu za nchi!?..hivi wakatoliki hawajashikilia mifumo ya utawala wa nchi!?..watu wa Mara hawakutapakaa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama!?..watu wasivune rasilimali za nchi wangoje nini!?..watanzania wa Nyerere walimudu kununua vyombo vya moto na kujenga makazi Bora Kama wa Leo!?
 
Asante sana Mkuu !
Sisi wengine ni wahenga 😂😂🇹🇿🙏🙏🙏
 
Katika Uongozi wote huo sikuwahi kuona vijana na Viongozi wakisifiwa Kama wanavyosifia kwenye uongozi wa Magufuli na Rais Samia.
Ukosefu wa ajira umefanya Ma Rais wa kizazi cha leo kuwafanya vinana watumwa.

Ikiwa Chawa ndio anapewa ulaju hata kama hana sifa za ulaji huo tafsiri yake ni kuwa hii Pool ya vijana wasio na mbele wala nyuma wanapata ujumbe kuwa Rais anataka wapiga zumari ili akukumbuke.

Hii kasumba imepenya sana kwa Wasomi karibu woote wa ngazi zoote kama unavyojua kila mtu anapenda maisha mazuri.

Sasa sisi tuliojitambua Enzi za Kikwete tuliona Vijana wakipamba kwa hoja kwenye maswala mbali mbali ya Kitaifa.

Enzi za magufuli uliona mambo yalivyokuwa mabaya sana. Na Dr Samia naye anapita mule mule hana jinsi.
 

Context matters mkuu
 
Kwa nchi hii Tanzania watu wameacha uwajibikaji. Watu kupigania matumbo yao tu,hata viongozi wameiga huo mkumbo. Mtu akimsifia sana kiongozi anateuliwa kwenye nafasi fulani. Hizi media kwa Tanzania zimekuja kuua kabisa uwajibikaji.

Hapo umesema Mkapa ndio amefanya makubwa ktk nchi hii. Ndio yapo yake nae. Lakini hajamzidi Magu. Unajua hata yeye ameondoka duniani anajisikia vibaya kwa ubinafshishaji mkubwa usio na manufaa yoyote kwa Mtanzania zaidi ya kuwaneemesha zaidi wenye nacho na kuendelea kuwadidimiza masikini na anaondoka anaiacha nchi ikiwa masikini. Na sasa tuna watu wengi wameongezeka masikini wa fikira. Miaka 20 ijayo kwa mwendo huu usishangae Tanzania ikawa mwishoni kabisa kwa watu wake kuwa masikini. Tatizo mfumo.

Nyerere pia ameondoka akisikitikia kuwafukuza haraka wazungu. Japo Uhuru ulikuwa muhimu lakini angewaacha tuchanganyikane nao tu tudumu nao hata kwenye uongozi. Bahati mbaya akawafukuza mpaka kwenye mashamba,ambayo baadae yalishindwa kuendelezwa.

Mtu aliefanya yakaaanza kuonekana na alikuwa na na maono ya mbali ni Magufuli tu. Aliyoyafanya yanaonekana na aliyoyaacha yangemaliziwa yana maana sana kwa maendeleo ya nchi yetu. Mfano mdogo ni umeme. Magu aliwafanya watu wote waingiziwe umeme kwa 27000 tu. Huko ndio kuwasaidia masikini. Kipindi chake tu umeme ulianza kuwa historia kwa Tanzania kukatika. Watu waliuza majenereta walivyokuwa wanayatumia ksbb yalikuwa hayana kazi tena. Ona barabara alivyozitanua,fry over. Barabara mkoa kwa mkoa. Alikuwa na malengo na alithubutu kufanya.

Nini kifanyike sasa ni T.R.A ifumuliwe,iundwe upya,kodi zifanane na nchi tulizo jirani nazo. Usalama pia ifumuliwe iundwe upya,kuwe na vitengo. Viwepo vinavyoangalia biashara kati ya nchi nyingine na yetu unaendaje kuna kuna mahala pa kurekebisha mapema wanarekebisha juu kwa juu bila sisi wananchi kutufikia. Kuwe na kitengo cha ushushushu wa kiuchumi. Mambo ya kuchunguzana wenyewe kwa wenyewe hayo wangeachiwa polisi.
Vinginevyo kuwe na kitu kikubwa. Hasa hasa kiwepo kitengo cha kushughulikia na kujipanga upya mfumo mzima wa uongozi nchini,mfumo mzima namna ya uendeshaji wa nchi. Hayo mambo ya kusifia Sifia tu wao ndio wataya-cancel yenyewe kutokana na mfumo.
 
Unastahili kukalia chupa ndio akili yako itarudi mahali pake
 
May be niulize, udokta wako mi wa nini? Labda ulisomea kutibu mapaka pale SUA na ma-mbwa
 
Waasisi wa tatizo wanajulikana na wafusi wa tatizo ni sisi

Tusisingizie siasa…. Ni culture yetu ya hovyo

Ya kupenda dezo
 
KIzazi chawa...
Kizazi lamba miguu...
Kizazi kiliponzwa na vitisho vya mwendazake magu na wabunge wake wajinga,wamchongo na waoga sifiasifia ili upate cheo.
Niupepo mchafu but utapita tukipata prezdaa msomi, mwenye akili na anayejiamini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…