Kuna tatizo mahali kwenye nafasi ya uongozi nchi hii. Je, kafara la Lindi linahusika?

Kuna tatizo mahali kwenye nafasi ya uongozi nchi hii. Je, kafara la Lindi linahusika?

Hivyo akina kinenes na ikwetwa kwa kushirikiana na watu wa nje wakaamua kumuua..huku wakiwahusisha watu waliikuwa karibu yake..[emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064]
Hapa Kuna mtu ameamini mtu Hadi denial inamtesa ,hakuna kitu hapo.
 
Inasikitisha sana uchawi na matamko ni laana mbaya sana, na ninafikiri wazee wote wa matambiko karibia waishe bila kutoa codes za kuondoa Hilo tatizo
Thus awataki katiba mpya na uraia pacha hivi vinafungua code.
Uraia pacha na katiba mpya ni sawa na dawa ya panya na panya.
Hivi viwili ndio code ya kuisambaratisha ccm.Ccm ikifa nchi itafunguka na maendeleo yataanza kuja.
 
Hakuna taifa lolote duniani lililosimama imara bila nguvu za mkuu wa anga! Kuanzia matambiko mpaka makafara na vyama vya kishetani.

Hivi vyote vimejenga madhabahu zao kwenye kila ardhi ya kila taifa. Wananchi wake wana dini na imani zao lakini mataifa yamesimikwa kwenye hizi madhabahu viapo na makafara.

Tanzania nj taifa kama mataifa mengine duniani, nayo ina makafara na madhabahu zake za kuifanya nchi itawalike iheshimike na iwe na 'stability' kwenye kila nyanja kuanzia kiuchumi, kijamii, kimaono mpaka kiulinzi nk

Kuna makafara ya kuilinda Tanzania yanatajwatajwa sana.. Kafara la Bagamoyo na kafara la Lindi! Kafara la Bagamoyo linaelezewa kwa ufasaha na wahusika wake wanajulikana.. Shida ipo kwenye usiri mkubwa unaotawala kwenye kafara la Lindi

Hili limebaki kuwa fumbo na tetesi isiyothibitishwa popote. Wanaolijua ni wachache na hulisimulia kwa tahadhari kubwa sana! Lina nini ndani yake hili?

Kafara la Bagamoyo ni la moto..na kiongozi wake ni Mzee mchawi marehemu Forojo Ganze na hiki ndicho alikisema kabla ya kukata roho

"Baba, sisi tunataka kuwasha mwenge na kuuweka juu ya mlima Kilimanjaro, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini mahala pasipo na tumaini, faraja palipo na huzuni, tumaini pasipo na tumaini, upendo penye chuki na heshima palipo na dharau"

Baada ya kutamka hayo mbele ya Mwl. Nyerere, Ganze alikata roho na ndipo ukaanzishwa Mwenge wa Uhuru. Kinachonishangaza hapa ni kile kipengele kisemacho"UMULIKE NJE YA MIPAKA YETU". Ina maana ndani ya nchi tubaki gizani kama tulivyo sasa?

Hli kafara la Bagamoyo tunaweza kuliita kafara la mambo ya nje na lile la Lindi tunaweza kuliita la mambo ya ndani...sasa hapa ndio penye shida...ni kafara la mambo ya ndani na limebaki ndani na kuwa siri kubwa

Mwalimu Nyerere Mchonga meno kwa hakika anayajua vema makafara yote mawili na miiko yake na pengine ndio maana katika tawala zote tangu uhuru ni utawala wake pekee ndio ukifanikiwa kwa kiwango cha juu kwenye
Kuweka misingi sahihi ya uongozi, uwajibikaji na uzalendo
Kuweka misingi sahihi kijamii, kisiasa na kiulinzi
Kuweka misingi sahihi ya kimtazamo na kimaono
Mipango endelevu na dira sahihi tangu tulipoanzia, tulipofikia na tunakoenda

Baada ya hapo waliofuatia wote kila mtu alikuja na MAGAZIJUTO YAKE na sarakasi zake
Baada ya hapo kila aliyeingia alianza vizuri lakini hakuchelewa kuharibu. Kama si kipindi cha kwanza basi cha pili cha uongozi wake
Baada ya hapo waliofuatia wote waliingia kwa upole na unyenyekevu lakini mara wakageuka wajivuni, wababe, na baadhi yao dharau kujikweza na kujimwambafai kwingi...bila kusahau vitisho na ugiligili mwingine mwingi
Baada ya hapo wengine wote watakanguliza maslahi binafsi, ya ndugu zao, jamaa zao na watu wote waliokuwa na maslahi nao

Mambo yanazidi kuharibika na pengine hawaoni wametiwa upofu.. Huu ugiligili sasa ni mpaka kwa viongozi wanaowateua kuwasaidia majukumu ya kiutendaji. Sasa hivi kiongozi akipewa kipaza sauti aongee mbele ya makamera asipotoa boko basi atatoa kituko cha karne ama kuongea yasiyowezekana

Matamko ni mengi mno
Maelekezo ni mengi mno
Makatazo ni mengi mno
Maonyo ni mengi mno
Yani haya ni mengi mno mpaka yanapishana barabarani na kupigana vibega

Kuna tatizo kubwa la kiuongozi na hili lina mizizi mirefu tangu ang'atuke mwalimu. Je, kwa mtazamo wa kiroho ni lile kafara la Lindi?
Wakati utaongea. Hebu tuupe muda!
Nchi imepoteza mwelekeo.
 
Hebu tuanze kuchangishana tupate hela sasa tukalinunue halafu tujenge hema kuu ya Mungu mkuu Muumba wetu tukusanye watu wa kiroho wanaosema na mungu wetu tukakemee hayo mashetani Taifa lipone!!!
Mwalimu Christopher Mwakasege (Arusha) na Omari Mnyeshani (Tanga) wanaweza kutusadia 0719 356206 na 0755 025821
 
HAKUNA JIPYA. HILI LIMESHAANDIKWA SANA. TENA NA TENA.

Ngoja nikupe Darsa kidogo la lugha na maana.
"Baba, sisi tunataka kuwasha mwenge na kuuweka juu ya mlima Kilimanjaro, umulike HATA nje ya mipaka yetu, ulete tumaini mahala pasipo na tumaini"

Mtu anapoaema umulike HATA maana yake ni nyongeza. Umulike ndani na hata nje ya mipaka yetu. Sasa wewe mwenyewe hapo juu ulicopy na kupaste maneno yaliyosemwa kama yalivyo. Ila chini umekuka ondoa neno HATA. umetukosea sisi wasomi.

Kabla hujaandika uwe unajua kuna watu mbalimbali humu ndani. Na uelewa umetofautiana.

Nikisema HATA mbwa anauma maana yake kuna mnyama mwingine yupo anauma. Tunataka kuwasha taa HATA za nje ziwashwe. Maana yake za ndani ni kawaida na kuna nyongeza ya taa za nje pia kuwashwa.

Habari za Makafara na ninii sijui ni uongo ule ule wa miaka yote. Tanzania inahitaji kuelimika ili iwe na mtizamo mpya zaidi.
Waambie mkuu yaan kuna mizee humu imekalia uchawii uchawii mada zao za kichawi kutwa kucha..nchi inahitaj maendeleo ya kielimu mijitu inawaza uchawii..
Wapuuzi sana hawaa
 
Mkuu wa anga ni aina za majini au fallen angels wanaozuia maombi yetu yasimfikie Mungu. Ni jini mkubwa na wenzie (wakuu wa anga). Kumbuka Lusifa ana wenzie 6 Malaika waasi na wao na wengine ni theluthi (moja ya tatu) ya Malaika na walipoasi walishushwa chini ni matrilioni ya viumbe vya kiroho vinavyotutesa.
Nitataja Hao 6 na baadae ila tukumbuke ulimwengu wa roho una madaraja 7 nayo ni physical realm (ulimwengu wa nyama) huu wa kibinadamu ,pili ni spiritual huko ndiko mizimu ,wachawi ,misukule,majini wa kati ,vibwengo n.k. yaani tofauti na WA nyama ,tatu ni Luciferian hawa ni majini wakubwa ambao wanaitawala dunia na watu wakubwa duniani wakipata ukuu wa spiritual realm wanaenda huku ili wawe wakuu kidunia kama vile tajiri wa dunia, kucontrol teknolojia na Sayansi za dunia,magonjwa na tiba kidunia,nne ni Fallen Angels realm yaani Lucifer na kaka zake 5 na dada Yao mmoja hawa ndiyo wameleta dini za uongo zote kuanzia uhindu, budha,tao,Shinto,Mashahidi wa Yehova na zingine pia wasioamini Mungunitaongelea siku ingine na maovu yote .Tano ni Angels realm, SITA ni Prophets and seers realm yaani manabii na waonaji Mungu huwaonyesha hawa vingi vinavyotokea .Daraja la 7 la Mungu ni la juu huko Mungu ana wenye uhai wanne na Wazee 24 yaani 12 wa zamani enzi za agano la kale na 12 wale wanafunzi wa Yesu ila Yuda Iskarioti hayumo.
Uongo mtupu
 
Hapana aliharibu alipolidharau kafara la kukimbiza moto...Ule moshi wa Ruangwa ndio ilikuwa alama ya onyo na karipio
Nachukia sana mwenge. Natamani aje atokee mwamba anaemuamini Mungu kikweli kweli atengue hilo tambiko. People have been praying over and over lakini wapii. Kuna tambiko lingine lilifanyika Zanzibar, ni baya zaidi kuliko haya yanayofahamika sana. Mungu atusaidie tu la sivyo hatutatoka hapa.
 
Waambie mkuu yaan kuna mizee humu imekalia uchawii uchawii mada zao za kichawi kutwa kucha..nchi inahitaj maendeleo ya kielimu mijitu inawaza uchawii..
Wapuuzi sana hawaa
Hatukatai ila usibishie masuala ya kiroho kwani ndiyo yanacontrol masuala ya mwilini .

Madhara ya hayo MATAMBIKO ndiyo maana Kuna shida kwenye vitu vifuatavyo Kwa Tanzania.
1. Nchi kuwa na rasilimali nyingi kama Tanzanite,Mlima Kilimanjaro, maziwa makubwa kama Victoria Tanganyika ,bahari ,makaa ya mawe,mbuga za wanyama,ardhi kubwa yenye rutuba,madini ,misitu na mbao na vingine vingi mno lakini hakuna sera Wala mipango madhubuti haijaonekana na Taifa Lina miaka 60 sasa [emoji24][emoji24][emoji24]

2. Wananchi kutokuwazia maendeleo au kutokuwa na Utamaduni wa kuyaleta maendeleo ila kubakia wanawaza vitu vidogo vya ajabu kama udaku, ukipata nafasi kufanya ufisadi na ubadhirifu na kuwavuta ndugu na washkaji kwenye nafasi.

3. Mfumo wa elimu kubakia ule ule wa kikoloni wa kutengeneza White collar jobs badala ya kutoa elimu na maarifa ya Sayansi, ufundi na vitendo , biashara na ujasiriamali.Hivyo vijana wanaanza awali Hadi Form 6 hawana ujuzi wowote. Elimu Kwa wananchi wa kawaida ni duni na wale wachache walionacho watoto wao hawasomi kwenye shule hizi zisizo na ubora. Hii inaongeza pengo la walionacho na wasionacho na watawala kuendelea kuwatawala watawaliwa milele.

4. Sera za nchi kwenye maendeleo kuwa mbovu mfano kwenye uwekezaji Tanzania hali ya kufanya biashara ni Mbaya . Kuanzia kuwavuta wawekezaji,kushughulikiwa vizuri na Kwa haraka Kuna bureaucracy za ajabu huko TIC,TRA na vyombo vingine vyote. Kupata mitaji ni shida,kupata ardhi ni shida,kupata umeme ni shida,miundo mbinu na mawasiliano ni shida,masoko ni shida.Sera zinabadilika muda wowote hata ukikadiria kuwa utalipa kiasi Fulani Kwa miaka 10 atakuja kuibuka mtu au watu watabadilisha sera ,taratibu na sheria hawatabiriki.

5. Mazingira ya kupata Ajira Kwa sekta binafsi na serikali ni mabaya sana.Wahitimu wamejaa mitaani Hadi wanazeeka hawajui wafanye nini.Sera ni mbaya na zilizopo utekelezaji sio mzuri.

6. Nchi kujaa rushwa na ufisadi kwenye maeneo yote iwe mahakamani na Polisi,ofisi za umma ,mamlaka zote. Kama humjui mtu huwezi kutoboa hili sio Tanzania tu bali nchi nyingi za kiafrika.Shida hii inasababisha tupate majengo,barabara,huduma na bidhaa zilizo na ubora wa hali ya chini au hafifu kabisa.Tofauti na nchi zilizoendelea ambapo hata rushwa ikihusika viwango Bora huzingatiwa.

7. Kuminywa Kwa uhuru wa kuzungumza na kuwasiliana na uhuru wa vyombo vya habari.Yaani mambo ya kukosoana hakuna ukikosoa wewe mbaya unatakiwa usifie tu.Wasifiaji wanapewa tuzo na watu kuogopa kuongea wengine wanakuja JF kuandika nyuma ya keyboard [emoji3491].Hii inaleta impunity state.

8.Kilimo pamoja na kuitwa UTI wa mgongo wa nchi hakuna jitihada za makusudi kisera,kibajeti ili kikukue Imebakia siasa tu . Wananchi wengi wapo vijijini na ni wakulima na wafugaji ila wanalima kijima tu jembe la mkono na mvua za misimu tu.Kuwezeshwa hakupo ni siasa tupu ndiyo maana unaona bajeti za matumizi ya kawaida na chai ofisini ni kubwa kuliko kuwezesha miradi ya maendeleo.

Kiufupi ni hivyo sio tunaongelea uchawi kwenye dunia ya kisasa ila tunawekea mkazo kuwa haya masuala yana mzizi wake kabla ya uhuru na baada ya Uhuru.
 
Nachukia sana mwenge. Natamani aje atokee mwamba anaemuamini Mungu kikweli kweli atengue hilo tambiko. People have been praying over and over lakini wapii. Kuna tambiko lingine lilifanyika Zanzibar, ni baya zaidi kuliko haya yanayofahamika sana. Mungu atusaidie tu la sivyo hatutatoka hapa.
Hebu funguka zaidi kuhusu tambiko la nchi la Zanzibar mkuu
 
Back
Top Bottom