Kuna tatizo mahali kwenye nafasi ya uongozi nchi hii. Je, kafara la Lindi linahusika?

Hivyo akina kinenes na ikwetwa kwa kushirikiana na watu wa nje wakaamua kumuua..huku wakiwahusisha watu waliikuwa karibu yake..[emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064]
Hapa Kuna mtu ameamini mtu Hadi denial inamtesa ,hakuna kitu hapo.
 
Inasikitisha sana uchawi na matamko ni laana mbaya sana, na ninafikiri wazee wote wa matambiko karibia waishe bila kutoa codes za kuondoa Hilo tatizo
Thus awataki katiba mpya na uraia pacha hivi vinafungua code.
Uraia pacha na katiba mpya ni sawa na dawa ya panya na panya.
Hivi viwili ndio code ya kuisambaratisha ccm.Ccm ikifa nchi itafunguka na maendeleo yataanza kuja.
 
Nchi imepoteza mwelekeo.
 
Hebu tuanze kuchangishana tupate hela sasa tukalinunue halafu tujenge hema kuu ya Mungu mkuu Muumba wetu tukusanye watu wa kiroho wanaosema na mungu wetu tukakemee hayo mashetani Taifa lipone!!!
Mwalimu Christopher Mwakasege (Arusha) na Omari Mnyeshani (Tanga) wanaweza kutusadia 0719 356206 na 0755 025821
 
Unachoongea upo kwenye upofu nisingependa mada iingie kwenye malumbano ya kidini.Nafunga mjadala kati yangu na wewe.
Sasa unaaminije laana za kishetani bila kujua uwepo wa dini? Hakuna malumbano ya kidini nazan ww ndo mpofu wa kifikraa.
 
Waambie mkuu yaan kuna mizee humu imekalia uchawii uchawii mada zao za kichawi kutwa kucha..nchi inahitaj maendeleo ya kielimu mijitu inawaza uchawii..
Wapuuzi sana hawaa
 
Uongo mtupu
 
Hapana aliharibu alipolidharau kafara la kukimbiza moto...Ule moshi wa Ruangwa ndio ilikuwa alama ya onyo na karipio
Nachukia sana mwenge. Natamani aje atokee mwamba anaemuamini Mungu kikweli kweli atengue hilo tambiko. People have been praying over and over lakini wapii. Kuna tambiko lingine lilifanyika Zanzibar, ni baya zaidi kuliko haya yanayofahamika sana. Mungu atusaidie tu la sivyo hatutatoka hapa.
 
Waambie mkuu yaan kuna mizee humu imekalia uchawii uchawii mada zao za kichawi kutwa kucha..nchi inahitaj maendeleo ya kielimu mijitu inawaza uchawii..
Wapuuzi sana hawaa
Hatukatai ila usibishie masuala ya kiroho kwani ndiyo yanacontrol masuala ya mwilini .

Madhara ya hayo MATAMBIKO ndiyo maana Kuna shida kwenye vitu vifuatavyo Kwa Tanzania.
1. Nchi kuwa na rasilimali nyingi kama Tanzanite,Mlima Kilimanjaro, maziwa makubwa kama Victoria Tanganyika ,bahari ,makaa ya mawe,mbuga za wanyama,ardhi kubwa yenye rutuba,madini ,misitu na mbao na vingine vingi mno lakini hakuna sera Wala mipango madhubuti haijaonekana na Taifa Lina miaka 60 sasa [emoji24][emoji24][emoji24]

2. Wananchi kutokuwazia maendeleo au kutokuwa na Utamaduni wa kuyaleta maendeleo ila kubakia wanawaza vitu vidogo vya ajabu kama udaku, ukipata nafasi kufanya ufisadi na ubadhirifu na kuwavuta ndugu na washkaji kwenye nafasi.

3. Mfumo wa elimu kubakia ule ule wa kikoloni wa kutengeneza White collar jobs badala ya kutoa elimu na maarifa ya Sayansi, ufundi na vitendo , biashara na ujasiriamali.Hivyo vijana wanaanza awali Hadi Form 6 hawana ujuzi wowote. Elimu Kwa wananchi wa kawaida ni duni na wale wachache walionacho watoto wao hawasomi kwenye shule hizi zisizo na ubora. Hii inaongeza pengo la walionacho na wasionacho na watawala kuendelea kuwatawala watawaliwa milele.

4. Sera za nchi kwenye maendeleo kuwa mbovu mfano kwenye uwekezaji Tanzania hali ya kufanya biashara ni Mbaya . Kuanzia kuwavuta wawekezaji,kushughulikiwa vizuri na Kwa haraka Kuna bureaucracy za ajabu huko TIC,TRA na vyombo vingine vyote. Kupata mitaji ni shida,kupata ardhi ni shida,kupata umeme ni shida,miundo mbinu na mawasiliano ni shida,masoko ni shida.Sera zinabadilika muda wowote hata ukikadiria kuwa utalipa kiasi Fulani Kwa miaka 10 atakuja kuibuka mtu au watu watabadilisha sera ,taratibu na sheria hawatabiriki.

5. Mazingira ya kupata Ajira Kwa sekta binafsi na serikali ni mabaya sana.Wahitimu wamejaa mitaani Hadi wanazeeka hawajui wafanye nini.Sera ni mbaya na zilizopo utekelezaji sio mzuri.

6. Nchi kujaa rushwa na ufisadi kwenye maeneo yote iwe mahakamani na Polisi,ofisi za umma ,mamlaka zote. Kama humjui mtu huwezi kutoboa hili sio Tanzania tu bali nchi nyingi za kiafrika.Shida hii inasababisha tupate majengo,barabara,huduma na bidhaa zilizo na ubora wa hali ya chini au hafifu kabisa.Tofauti na nchi zilizoendelea ambapo hata rushwa ikihusika viwango Bora huzingatiwa.

7. Kuminywa Kwa uhuru wa kuzungumza na kuwasiliana na uhuru wa vyombo vya habari.Yaani mambo ya kukosoana hakuna ukikosoa wewe mbaya unatakiwa usifie tu.Wasifiaji wanapewa tuzo na watu kuogopa kuongea wengine wanakuja JF kuandika nyuma ya keyboard [emoji3491].Hii inaleta impunity state.

8.Kilimo pamoja na kuitwa UTI wa mgongo wa nchi hakuna jitihada za makusudi kisera,kibajeti ili kikukue Imebakia siasa tu . Wananchi wengi wapo vijijini na ni wakulima na wafugaji ila wanalima kijima tu jembe la mkono na mvua za misimu tu.Kuwezeshwa hakupo ni siasa tupu ndiyo maana unaona bajeti za matumizi ya kawaida na chai ofisini ni kubwa kuliko kuwezesha miradi ya maendeleo.

Kiufupi ni hivyo sio tunaongelea uchawi kwenye dunia ya kisasa ila tunawekea mkazo kuwa haya masuala yana mzizi wake kabla ya uhuru na baada ya Uhuru.
 
Hebu funguka zaidi kuhusu tambiko la nchi la Zanzibar mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…