Tetesi: Kuna tetesi kwamba Marekani inapanga kutangaza vikwazo kwa Serikali ya Tanzania

Tetesi: Kuna tetesi kwamba Marekani inapanga kutangaza vikwazo kwa Serikali ya Tanzania

Umeandika kinazi...utakuwa ni CUF au CHADEMA...unafurahia Tanzania kuwekewa vikwazo...dah...Watanzania wengine bwana kazi ipo...haya endeleeni kuandika hivyo...tutaona mwisho wake utakuwaje...Lakini lililo wazi ni kuwa Maalim Seif hawezi kuwa Rais wa Zanzibar na haitatokea kuwa hivyo...


Wewe umeandika kizalendo maana umetokea ccm na wana ccm ndio wazalendo pekee nchi na ndio waliumbwa na Mungu kutawala nchi. Hongera sana wewe unayefurahia kuvunjwa kwa haki na sheria za nchi
 
Marekani mmeifanya kuwa Mungu,wenu unakaa unaabudu mtu fanya kazi acha fikra mfu,kwani kama wao waliendelea sisi tutashindwa nini.
Misaada yenyewe ni ukoloni mtupu halafu mnaleta ngonjera hapa.
Leo ndio mmeanza kubeza misaada ya wahisani wakati mmeshazingua katika terms zao hasa masuala ya kidemokrasia
 
KIBURI, JEURI NA ULIMBUKENI HAVIJAWAHI KULETA NEEMA WALA KUWA SEHEMU YA UTATUZI WA MATATIZO YALIYOPO.
 
Ni kweli kabisa. Watu waliofirisika kifikra wanadhani nchi hii itajengwa na Marekani. Kama Marekani wangekuwa na dhamira ya kweli kuiletea maendeleo nchi yetu, Tanzania isingekuwa hapa ilipo.
Kutegemea misaada ni sawa na MME ALIYEOA MKE, LAKINI HELA YA KUMTUNZIA MKE WAKE ANATEGEMEA MSAADA KUTOKA KWA MWANAUME MWENZIE.
Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe kama Marekani ilivyojengwa na wamarekani wenyewe.
 
Unafikiri Marekani wapo kwa ajili ya kutetea demokrasia ya Tanzania? Kama kuna yeyote nu mwenye wazo hilo anahitaji maombi!
 
Umeandika kinazi...utakuwa ni CUF au CHADEMA...unafurahia Tanzania kuwekewa vikwazo...dah...Watanzania wengine bwana kazi ipo...haya endeleeni kuandika hivyo...tutaona mwisho wake utakuwaje...Lakini lililo wazi ni kuwa Maalim Seif hawezi kuwa Rais wa Zanzibar na haitatokea kuwa hivyo...
Kwani kila anayeandika ni CUF au CDM??
 
Umeandika kinazi...utakuwa ni CUF au CHADEMA...unafurahia Tanzania kuwekewa vikwazo...dah...Watanzania wengine bwana kazi ipo...haya endeleeni kuandika hivyo...tutaona mwisho wake utakuwaje...Lakini lililo wazi ni kuwa Maalim Seif hawezi kuwa Rais wa Zanzibar na haitatokea kuwa hivyo...
Ata ww inaonekana ni gamba
 
Unajuaje kama siyo sera ya Trump.
Mkuu haiwezi kuwa sera ya Trump maana HAJAAPISHWA rasmi. Na mara nyingi yule Waziri atakayechukua wizara ya nje STATE Department ndiye ataketoa SERA na MABALOZI wapya wa Trump.
Kuna wachache wanaweza kubakizwa ama kuondolewa kabisa.

Kwa sasa KISHERIA Obama ndiye rais wa Marekani.
Hata amiri jeshi mkuu ni Obama hata kama zimebakia siku mbili
Bado Trump anaitwa ni rais mtarajiwa.
Hivyo kwa kigupi hana sauti wala sera ya mambo ya nje ambayo yaweza kutekelezwa.
labda KUTWEET pekee!
 
Ni kweli kabisa. Watu waliofirisika kifikra wanadhani nchi hii itajengwa na Marekani. Kama Marekani wangekuwa na dhamira ya kweli kuiletea maendeleo nchi yetu, Tanzania isingekuwa hapa ilipo.
Kutegemea misaada ni sawa na MME ALIYEOA MKE, LAKINI HELA YA KUMTUNZIA MKE WAKE ANATEGEMEA MSAADA KUTOKA KWA MWANAUME MWENZIE.
Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe kama Marekani ilivyojengwa na wamarekani wenyewe.
Kama hadi rambirambi tunazitegemea kujengea miundombinu unategemea lini Tanzania itajitegemea.
 
na underson ndambo.

Taifa la Marekani linatarajia kushusha rungu la aina yake kwa serikali ya Tanzania kufuatia hali ya sintofahamu inayoendelea nchini kutokana na sakata la uchaguzi mkuu wa Zanzibar.
Habari zinadokeza kuwa taifa hilo kubwa duniani litaweka vikwazo vya kiuchumi kwa Tanzania hali itakayopelekea Tanzania kuandika historia nyingine mbaya mbele ya uso wa dunia.

Serikali ya Marekani tayari imezuia misaada mbalimbali kwa Tanzania na pia ndiyo iliyoshinikiza Tanzania kunyimwa fedha za MCC, pamoja na kuzishawishi nchi zengine. Serikali ya Tanzania ipo hatarini kukumbwa na janga la njaa, ikiendelea kupuuza juhudi za kimataifa kuitaka kuumaliza kwa haraka mgogoro wa Zanzibar unaofukuta kwa kuacha haki itendeke kabla ya Febr 2017.

Habari zinadokeza kuwa balozi wa Marekani nchini atatoa msimamo unaoelezwa kuwa 'mkali' ili kuishinikiza serikali ya Tanzania kuheshimu maamuzi ya wananchi kwenye uchaguz mkuu wa Zanzibar uliofanyika 25th Oct 2015.
Acha wawekee hivyo vikwazo nchi ngap wamewekewa vikwazo lakin maisha yanaendelea
 
Uzushi tu huu, Yaan vyombo vikubwa vya habari vya kimataifa vishindwe kupata hizi tetesi wewe ambaye upo Tanzania ndo uipate?

Hakuna kitu kama hicho, na Obama hawezi kufanya kitu kama hicho, kama TUME ya uchaguzi ingelikuwa imemtangaza rasmi Maalim Seif kama Rais afu CCM ikashinikiza matokeo yafutwe hapo kweli vikwazo vingewekwa, lakini kwa namna ilivyotokea ni ngumu sana hatua kama hizo kuchukuliwa, labda useme kuwa, MAREKANI ilazimishe mazungumzo kati ya CUF na Serikali yafanyike lakini si vikwazo.
We mpuuzi sana kama CCM wenzio....sasa obama na Feb 2017 anahusika nini? Mwisho wake Jan 20....baada ya hapo ni isiempenda kaja
 
Ni Nchi gani duniani imeshawekewa vikwazo duniani kwa ajili ya mambo ya uchaguzi ??hv mnajua maana ya vkwazo vya uchumi?au kusitisha misaada kuna vikwazo na kusitisha misaada vikwazo vinatolewa na UN si nchi moja moja na vikwazo unawekewa kwa idadi ya moja ya tatu ya kura zote zitakazo pigwa na wanachama wa UN

Tanganyika imesitisiwa misaada na taasisi za misaada si serikali ya Marekani leo NSSF wakikataa kukupa misaada si kwamba serikali ya Tanganyika ndo imekataa kukupa misaada Millennium Development Goals (MDGs) ni taasisi ya kimarekani si serikali ya marekani
Marekani ni zaidi ya UN. Kama hujui muulize sadam Hussein Kama anaweza kukwambia
 
Mkuu haiwezi kuwa sera ya Trump maana HAJAAPISHWA rasmi. Na mara nyingi yule Waziri atakayechukua wizara ya nje STATE Department ndiye ataketoa SERA na MABALOZI wapya wa Trump.
Kuna wachache wanaweza kubakizwa ama kuondolewa kabisa.

Kwa sasa KISHERIA Obama ndiye rais wa Marekani.
Hata amiri jeshi mkuu ni Obama hata kama zimebakia siku mbili
Bado Trump anaitwa ni rais mtarajiwa.
Hivyo kwa kigupi hana sauti wala sera ya mambo ya nje ambayo yaweza kutekelezwa.
labda KUTWEET pekee!
Mkuu elewa wakati wa kampeni kila mgombea huwa ananadi sera zake, chama huwa na ilani yake, kwahiyo hata kabla ya kuapishwa wananchi wanajua anakwenda kufanyanini.

Pia kumbuka Secretary of states ni appointee wa rais.

Juzi Obama kasema atalifunga gereza la gwantanamo jana Trump kasema yeye hana haja ya kulifunga, unaona sera zinavyopishana hata kabla ya Trump kuapishwa.

Hata Magufuli tulijua sera yake ya viwanda hata kabla ya kuapishwa.
 
Kama tuliweza kuishi baada ya vita vya kagera hii ya sasa haitishi, wakitaka waweke vikwazo bado hatutawasujudu.
 
Acha wawekee hivyo vikwazo nchi ngap wamewekewa vikwazo lakin maisha yanaendelea
Inategemea ni nchi gani inawekewa, North Korea na Zimbabwe zote zina vikwazo ingawa maisha wanaendelea lakini angalia tofauti ya maisha kati ya wananchi wake, vipi Tanzania ikiwekewa.
 
Back
Top Bottom