Kuna uwezekano Watanzania tuna tatizo la uelewa? Nikimsikiliza Polepole, namuona Mwl. Nyerere. Nyie msiomuelewa Polepole, je Nyerere mngemuelewa?

Mwl alieichukua nchi ikiwa kwenye mfumo wa chama kimoja ila alivumilia kuona ikiwa ya vyama vingi.
Wewe Mkuu VinJoe , ni mjinga!.
Kuwa mjinga sio tusi, ni ile hali tuu ya kutokujua jambo, ukifundishwa unafundishika, ujinga unakutoka, unakuwa mwerevu!.

Nyerere aliichukua nchi ikiwa na mfumo wa vyama vingi, akaifanya kuwa nchi ya chama kimoja. Ni Mwinyi ndiye aliyerudisha vyama vingi ile 1992.
Now you know, sasa wewe sio mjinga tena!.

Kuna wengi wasiomuelewa Polepole, ni wajinga tuu!. Waerevu tunamwelewa, kuna vitu anasema kweli.
P
 
Hakuna pahala ambapo watu walizuiliwa wasiseme, isipokuwa watu walizuiliwa kutoa matusi na vijembe na kejeli kwa wengine au kwa serikalii.
Waliohoji zilipokwenda 1.5Trilion unajua waliambiwa nn? Kina Ben Saanane walimtukana nani? Je Azory? Na wengine kibao? Musiba alikuwa anatisha wakosaji na hafanywi kitu
 
Kaka Pasco.

Nikuambie jambo fulani hapa.

Mimi binafsi nimewahi si mara moja kuwa karibu na Polepole.
Nimewahi mara kadhaa kutoa ushauri mzuri tu namna ya kuweka mustakabali mzuri wa kisiasa lakini seems alikuwa hayupo tayari kwa hilo

Kibaya zaidi, yeye kama Mwenezi Taifa ambaye ndiye anayesimamia intelejensia ya Chama, tulimfikishia taarifa nyingi with evudences kuonesha namna ambavyo rushwa imetamalaki kuelekea mchakato wa kura za uteuzi wa wagombea..

Rafu zilichezwa sana na hata kupelekea wengi maisha yao kuathirika na Humphrey anajua hilo..

Hizi porojo anazoongea sasa hivi ni kujaribu kutengeneza survival stream asije kufa njaa mbeleni.

Unajua walichokuwa wanapitia Wapinzani na wadadisi wengi wa kisiasa... Humphrey alikuwa anajua na usikute aliidhinisha projects mbalimbali za kipuuzi dhidi ya Watanzania wenzake.

Sikubaliani na Bulembo na shosti wake Nape lakini naona huyu kimbwenelehi wanayemuita Kiroboto alipaswa kwanza kukiri hadharani ushiriki ama kutoshiriki kwake kwenye madhila ya kubinafsisha siaza kipindi chote alichokuwa Mwenezi.

Humphrey anaongea kana kwamba anataka kuikomboa CCM, unaikomboa CCM kutoka wapi? Mimi na wenye akili waliosalia tungemuona ana mantiki pale ambapo angeizungumzia Tanzania kuliko lichama lililoifikisha Tanzania miaka 60 ya Uhuru huku ikiuhodhi bila kuupeleka uhuru huo kwa Watanzania kama dhamira ilivyotakiwa kuwa.

Humphrey hawezi kuwa katika lines unazomnadi kwa sababu alifikia kwenye nafasi za kuonesha uwezo huo anaouongelea leo, tutathmini nini alifanya na alifeli wapi na kwa nini.
Humphrey anasumbuliwa na tatizo la MNYONG'ONYO linalotokana na sonona
 
Pamoja na kumuelewa Polepole lakini kumlinganisha na Nyerere, HAPANA!!!!!!!!!!!
 
Nyakati hizi watu wanaopambana kwa hoja wamepungua sana.. Sasa hivi ni 'full' vitisho na siasa chafu tu..
Mtu anauliza 'awamu' inabadilikaje? Si uchaguzi mkuu ukifanyika? Watu wanaanza kumrushia mawe..
 
Ibara ya 8(a) ya katiba inasema.
Wanaichi ndio msingi wa mamlaka yote, na serikali itapata mamlaka yake yote kutoka kwa wanainchi kwa mujibu wa katiba hii.

Serikali inapata mamlaka yake kupitia uchaguzi, na uchaguzi ulifanyika Nov 2020 na kuiweka serikali ya awamu ya 5. Hii awamu ya 6 imepata mamlaka yake wapi?

Hii ni Serikali ya awamu ya 5 na raisi wa 6 Full stop.

Km tunataka serikali ya awamu ya sita inabidi tuitishe uchaguzi serikali ya awamu ya 6 wapate hayo mamlaka yaliainishwa na katiba.

watu wakiambiwa hii ni serikali ya awamu ya 5 wanatokwa mapovu...[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Ongeza sauti, huku backbenchers bado hatujasikia .


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Gobole , asante sana kwa mchango huu. Wewe ni miongoni mwa watu wachache humu waelewa, Polepole ameusema ukweli mchungu supported by facts za kwenye katiba, lakini humu, tuna mijitu mijinga ajabu!, akili zao finyu haziwezi kumwelewa Polepole!.

Kama Mwalimu Nyerere aliwahi kusema serikali yetu imeacha mambo mema na kukumbatia mambo ya kijinga, ndicho hiki hiki Polepole anachokifanya sasa.
P
 
Ni aidha kiroboto au punda anayepiga mateke wakati wa kuchinjwa
 
Nilishawahi kusema na nitarudia tena, ONLY GREAT THINKERS HUMWELEWA POLE POLE

TIME HEALS ALL WOUNDS
Mkuu Ajaye , asante sana kwa hii.
JF was meant to be the home of great thinkers, na kweli kule mwanzo we had lots of great thinkers, but as times go by, JF imezidi kupendwa na wengi, sasa jf ni ya wote, not only is a home of great thinkers, with great minds who discusses ideas, but is a home to some ordinary minds, who discusses events and simple minds who discuss people.
Bandiko hili sio la kumjadili mtu anayeitwa Humphrey Polepole, bali ni kujadili the idea ya mfanano kati ya Humphrey Polepole na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
P
 
Ahsante pia mkuu, paschal mayalla, kwenye jamii ya watu waliostaarabika katika nyanja za muhimu hoja hujibiwa kwa hoja na si vitisho... ukiona mawazo na michango isiyo mizuri humu! Unapata picha ya watu wa namna gani tulionao katika taifa linalotegemea kupiga hatua mbele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…