Kuna Video iliyokuwa ikionesha Polisi/traffic wa Inyala, Mbeya wakimshusha kwa nguvu dereva wa lori. Polisi wadai amekufa kwa homa ya mapafu

Kuna Video iliyokuwa ikionesha Polisi/traffic wa Inyala, Mbeya wakimshusha kwa nguvu dereva wa lori. Polisi wadai amekufa kwa homa ya mapafu

Uandishi gani huu wa habari!
====
Toa details za wahusika, mazingira yalikuwaje, ndipo utoe taarifa ya tukio zima. Siyo wote wanaelewa unayoelewa juu ya mkasa huu. Hata hivyo asante sana mleta mada kwa kutujuza uwepo wa mkasa huu.
====
Moderators, mkiwa mnapata wasaa muwe 'mnatupiga shule', namna ya kuwasiliza taarifa hapa JF.
Si kazi yetu kukuamsha usingizini , taarifa hii ipo humu jf tena kwa upana sana , hatuwezi kuirudia , hata hivyo hata utaratibu wa jf hauruhusu kurudia kuleta habari , tumeleta tamko la polisi tu , ni kazi yako kutafuta habari zilizotangulia .

Tunatambua gharama ya bando kwa sasa imefanya wengi muwe nje ya mtandao , poleni sana , #Mitano tena .
 
Homa yamapafu ndyo ugonjwa gani si waseme tu covid na aliwwzaje kuebdesha gar akiwa na hali mbaya kiasi kile
 
Nikikumbuka RPC njombe alivomdanganya waziri kuhusu mauaji ya watoto njombe.tangu siku ile sina imani na polisi aisee.iviagonge magari.halafu gari lake lisikwaruzwe hata kidogo.kwamba alikimbia ni gari la kukimbia hilo?
 
Hili tukio halina tofauti na lile la mauji ya Mwangosi enzi za Kikwete na msishangae kuona hakuna askari ataechukuliwa hatua.

Nashangaa sana watu wanapomkubuka Kikwete na si ajabu watakuja tena kumkumbuka Magu kwani wanadamu tumeumbwa kusahau.
Mkapa hakukumbukwa Kwa mema ujue
 
Wamemshambulia kwa ngumi au mateke au virungu haionyeshi hapo! Naona wanambeba na kumuondoa ktk gari alikuwa mgonjwa na hakupaswa kuendesha gari lilikuwa linayumba. Polisi wameokoa maisha ya watu wengi hapo. Na kumbeba na kumuondoa kwa nguvu ilikuwa very proper.
Ukifungwa akili omba Mungu usifungwe na utu.
 
Kuna kitu kwenye sheria kinaitwa causation/chanzo....hata mtu kama alikuwa vakiumwa marelia kali ukampiga/ukamuangusha kwa makusudi akafa......!!
huzo tuhuma unawajibika nazo
 
20201224.jpg
54321076.jpg
 
Kuna kitu kwenye sheria kinaitwa causation/chanzo....hata mtu kama alikuwa vakiumwa marelia kali ukampiga/ukamuangusha kwa makusudi akafa......!!
huzo tuhuma unawajibika nazo
Umesoma sheria gani?Mbona mwandiko mbaya na hausomeki!
 
Hilo lilikuwa wazi polisi wasingeweza kukubali kuonekana wao ndo wenye makosa so wametafuta kisingizio kinachoweza kukubalika
 
Kwa hiyo walikuwa wanamtibu kwa kumrusha toka juu ya gari?
Majibu rahisi kwenye tuhuma nzito kama hii
Dhulma hii ya kiumbe huyo haitawaacha salama
 
Daah, naomba nijibu kitaalam zaidi. Katika saikolojia ya binadamu kuna kitu kinaitwa ‘Compensation behavior’, hii huonyeshwa hata na mtoto wa shule ambae anashindwa kung’ara katika masomo na badala yake anaamua kung’ara kwa njia zingine, mfano kupiga kelele darasani, kuwa mkorofi darasani, kujifanya comedian nk.

Tukirudi kwa hao form 4 failure, nadhani sasa inaeleweka why wanafanya hivyo..
Nimekupata.
 
Muda Mwingine nguvu wanazo tumia Police Mhhh ni bora Tupewe chanjo ya CORONA tuu
 
ila binadamu tujitahidi kuwasemea mabaya watu, maelezo yanasema dereva aliambiwa na daktari karibia anafika Mbeya( yaani hospitali ya Chimala) 1. anatakiwa kulazwa , 2. baadae akawa anaendesha gari na kuyagonga magari kadhaa kutokana na udhaifu3. watu wakapiga simu kwa askari kulalamika uendeshaji wake,. naomba tuwe na subira, kuna madhara kuchochea mambo kama haya; mfano mke wako au mama yako mwalimu, akiwa shuleni akamchapa mtoto (adhabu ya kawaida ) bila kujua akafariki, watu bila kujua undani wakaja hapa kusema , '' aaah walimu wamezidi saaana , huyo ni kkufunga tu ! tutakuwa tunaharibu mfumo wa haki
 
Na kwamba walipomkamata waligundua kwamba anaumwa ambapo madereva wenzake walipompeleka kwenye hospitali ya Chimala aligundulika kuwa na homa ya mapafu, hayo yamesemwa na Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Jerome Ngowi

View attachment 1689757


Natoa pole kwa wafiwa na Namuomba Mwenyezi Mungu aipokee roho ya Marehemu Dereva , Amina
Mbona kauli zinafanana na za Aquilina,hizi kauli wanazihifadhi kwenye kofia?
Kama madereva wenzake walimpeleka! Inamaana wao hawahusiki ila madereva wenzake ndio wakuhojiwa, sungura mjanja.
 
Back
Top Bottom