Kuna vijana wajinga sana katika hii nchi

Kuna vijana wajinga sana katika hii nchi

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari!

Mimi ni mwajiriwa katika ofisi moja ya umma.

Sasa hapa kazini kuna watumishi wa kudumu, wa mkataba wa muda mfupi na wanafunzi waliokuja kufanya field na wengine wamezamia mazima wakisubiri huruma za boss huenda atawaajiri.

Yes. Wapo walioanza kama wanafunzi mpaka wakaajiriwa kwa mkataba mfupi (renewable). Wengine huu mwaka wa 5, 6, n.k hawana hata mkataba, wanaambulia kaposho kidogo tu ingawa ndio hutegemewa sana kwenye majukumu.

Wameshindwa kupata ajira kwasababu aidha vigezo vyao ni hafifu au uchache wa ajira. Kwa huruma nikawashauri vijana watatu waliobobea kwenye utaalamu tofauti ambao wakijumuisha nguvu wanaweza kufungua ofisi moja na wakawa na maisha mazuri au hata wakawa matajiri baada ya miaka kadhaa.

"Kwakuwa nyie karibu wote mna uzoefu wa kazi na hamjaajirwa kwa miaka zaidi ya minne sasa basi muwaze kujiajiri kwa kuunganisha nguvu, mtapata pesa nyingi huko mbele kuliko hata sisi wenye ajira" Niliwaambia.

Niliwasihii watafute milioni 3 ya kianzio (kukodi) ofisi au fremu na kununua vitendea kazi.

Jibu walilonipa kuwa hawana pesa.
Nikawaambia kila mmoja wenu akamwambie mzazi au mlezi wake ampatie milioni moja hata kwa mkopo. Kama hilo humu basi mumtafute mtu mwenye pesa mumpe wazo lenu awakopeshe au naye akubali kuwa sehemu ya ofisi.

Wakawa wagumu kuelewa. Nikawaambia hata Mimi kama mko tayari naweza kutoa hiyo pesa kwa masharti ya umiliki wa ofisi kwa 25% yaani mgawanyo sawa. Bado wamekuwa wazito.

Vijana wajinga sana hawa, tunafanya kazi tena wao hutumikishwa zaidi kwa malipo ya pesa ya nauli tu na kila siku kazini wanakuja.

Hii nchi ina vijana wajinga sana.
 
Tanzania ajira ya serikalini inaheshimika sana kuliko kujiajiri.

Unaweza kuta mtu anafanya kazi taasisi flani ya serikali yenye jina kubwa na analipwa lets say laki saba kwa mwezi na kuna mwingine ana duka lake la jumla anaingiza milioni 2 kwa mwezi .

Yule wa serikalini ataheshimika na kuogopwa zaidi ya huyo aliyejiajiri.

Ni mindset zetu tu ndio zinawafanya watu wateseke ilhali wanaweza endesha maisha hata huko kwingine pia.
 
Tanzania ajira ya serikalini inaheshimika sana kuliko kujiajiri.

Unaweza kuta mtu anafanya kazi taasisi flani ya serikali yenye jina kubwa na analipwa lets say laki saba kwa mwezi na kuna mwingine ana duka lake la jumla anaingiza milioni 2 kwa mwezi .

Yule wa serikalini ataheshimika na kuogopwa zaidi ya huyo aliyejiajiri.

Ni mindset zetu tu ndio zinawafanya watu wateseke ilhali wanaweza endesha maisha hata huko kwvijingine pia.
Inayoheshimika ni pesa tu siyo taasisi unayofanyakazi.

Wapo wengi tu kwenye taasisi nyeti lakini wanakimbizwa na vijana wa clearing and forwarding, wanacheza na dollar kila siku.
 
Mkuu kwanini wewe hujaenda kuanzisha hiyo ofisi ukapata hizo pesa zaidi na ungali hapo hapo?

Hapa ndipo unapowashangaa kina msoga boys na wengi wakiwashauri wengine kujiajiri lakini si wao.

Yaliwahi nikuta kama yako baada ya kupata ajira iliyokuwa na ka probation ka kiana. Da jamaa wa similar field wakawa wananiona kama ka threat fulani.

"Kutwa kuchwa ikawa ushauri kuwa pale si pazuri niende pengine wakati wao wamekomaa wapo tu."

Haya mambo ya kuwaona wengine wajinga wakati hamuwalishi, nadhani si sahihi sana.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Inayoheshimika ni pesa tu siyo taasisi unayofanyakazi.

Wapo wengi tu kwenye taasisi nyeti lakini wanakimbizwa na vijana wa clearing and forwarding, wanacheza na dollar kila siku.
Hao jamaa zako nao wamechoka siku hizi, kazi chache na malipo mengi yana control number wamevutwa shati.

Baadhi ya kazi zimehamia Tasac zilizopo nazo za kupigania.

Kwa ujumla sekta nyingi hali ni tete.
 
Tanzania ajira ya serikalini inaheshimika sana kuliko kujiajiri.

Unaweza kuta mtu anafanya kazi taasisi flani ya serikali yenye jina kubwa na analipwa lets say laki saba kwa mwezi na kuna mwingine ana duka lake la jumla anaingiza milioni 2 kwa mwezi .

Yule wa serikalini ataheshimika na kuogopwa zaidi ya huyo aliyejiajiri.

Ni mindset zetu tu ndio zinawafanya watu wateseke ilhali wanaweza endesha maisha hata huko kwingine pia.
We jamaa kumbe unaongeaga point hivi... kweli uccm unakuharibugu akili
 
Habari!

Mimi ni mwajiriwa katika ofisi moja ya umma.

Sasa hapa kazini kuna watumishi wa kudumu, wa mkataba wa muda mfupi na wanafunzi waliokuja kufanya field na wengine wamezamia mazima wakisubiri huruma za boss huenda atawaajiri.

Yes. Wapo walioanza kama wanafunzi mpaka wakaajiriwa kwa mkataba mfupi (renewable). Wengine huu mwaka wa 5, 6, n.k hawana hata mkataba, wanaambulia kaposho kidogo tu ingawa ndio hutegemewa sana kwenye majukumu.

Wameshindwa kupata ajira kwasababu aidha vigezo vyao ni hafifu au uchache wa ajira. Kwa huruma nikawashauri vijana watatu waliobobea kwenye utaalamu tofauti ambao wakijumuisha nguvu wanaweza kufungua ofisi moja na wakawa na maisha mazuri au hata wakawa matajiri baada ya miaka kadhaa.

"Kwakuwa nyie karibu wote mna uzoefu wa kazi na hamjaajirwa kwa miaka zaidi ya minne sasa basi muwaze kujiajiri kwa kuunganisha nguvu, mtapata pesa nyingi huko mbele kuliko hata sisi wenye ajira" Niliwaambia.

Niliwasihii watafute milioni 3 ya kianzio (kukodi) ofisi au fremu na kununua vitendea kazi.

Jibu walilonipa kuwa hawana pesa.
Nikawaambia kila mmoja wenu akamwambie mzazi au mlezi wake ampatie milioni moja hata kwa mkopo. Kama hilo humu basi mumtafute mtu mwenye pesa mumpe wazo lenu awakopeshe au naye akubali kuwa sehemu ya ofisi.

Wakawa wagumu kuelewa. Nikawaambia hata Mimi kama mko tayari naweza kutoa hiyo pesa kwa masharti ya umiliki wa ofisi kwa 25% yaani mgawanyo sawa. Bado wamekuwa wazito.

Vijana wajinga sana hawa, tunafanya kazi tena wao hutumikishwa zaidi kwa malipo ya pesa ya nauli tu na kila siku kazini wanakuja.

Hii nchi ina vijana wajinga sana.
Sio wajinga kama ulivyowaelezea ila wanakosa uthubutu, na hili ndilo tatizo kuu nchini kwetu .
Hata wewe mwenyewe huo uthubutu huna pia , kama unaona hao vijana wakijiajiri watapata pesa na utajiri kwa nini wewe mwenye mtaji kabisa usichukue hiyo route?
 
Tanzania ajira ya serikalini inaheshimika sana kuliko kujiajiri.

Unaweza kuta mtu anafanya kazi taasisi flani ya serikali yenye jina kubwa na analipwa lets say laki saba kwa mwezi na kuna mwingine ana duka lake la jumla anaingiza milioni 2 kwa mwezi .

Yule wa serikalini ataheshimika na kuogopwa zaidi ya huyo aliyejiajiri.

Ni mindset zetu tu ndio zinawafanya watu wateseke ilhali wanaweza endesha maisha hata huko kwingine pia.
Biashara hazina uhakika ndugu amin na kwambia tumefanya tukaona Kodi ,garama za uendeshaji,ushindani ni kubwa mno mno ni ngumu kupata hizo faida unazo Dhani!!ndio maana watu wanauona bora kuajiriwa Kuna taasisi za serikali Zina mishahara mikubwa Sana mpaka mil 10 bado Kuna access ya mikopo huduma za afya nk!! Ajira tam asikwambie mtu !!
 
Inayoheshimika ni pesa tu siyo taasisi unayofanyakazi.

Wapo wengi tu kwenye taasisi nyeti lakini wanakimbizwa na vijana wa clearing and forwarding, wanacheza na dollar kila siku.
Story tuu c&forwarding Kuna watu wanasota TU sio Kila mtu anapiga
 
Tanzania ajira ya serikalini inaheshimika sana kuliko kujiajiri.

Unaweza kuta mtu anafanya kazi taasisi flani ya serikali yenye jina kubwa na analipwa lets say laki saba kwa mwezi na kuna mwingine ana duka lake la jumla anaingiza milioni 2 kwa mwezi .

Yule wa serikalini ataheshimika na kuogopwa zaidi ya huyo aliyejiajiri.

Ni mindset zetu tu ndio zinawafanya watu wateseke ilhali wanaweza endesha maisha hata huko kwingine pia.
Duka la jumla kutengeneza net profit ya mil 2 labda uwe peke Yako wilaya nzima ushindani ni mkubwa Sana asikwambie mtu
 
Biashara hazina uhakika ndugu amin na kwambia tumefanya tukaona Kodi ,garama za uendeshaji,ushindani ni kubwa mno mno ni ngumu kupata hizo faida unazo Dhani!!ndio maana watu wanauona bora kuajiriwa Kuna taasisi za serikali Zina mishahara mikubwa Sana mpaka mil 10 bado Kuna access ya mikopo huduma za afya nk!! Ajira tam asikwambie mtu !!
Watanzania kwa asili yetu sio aggressive kama watu wa mataifa mengine.

Hatuwezi mikiki mikiki ya maisha tunaridhika na mambo madogo madogo wanaopambana ni wachache sana.

Ndio maana wengi kwa udhaifu wao hukimbilia ajira za kudumu kwakua wao hawatafuti wanaletewa tu.

Raia wa nchi nyingine wanakuja hapa hawaajiriwi na wanatoboa.
 
Ebu mkuu acha Upumbavu kujiajiri sio Rahisi

Unajua nyie. Wajinga wenye dharau nikiangaliaga Maisha yenu nabaki kucheka connection hamna mjini hapa Magari mnaendesha mabovu nyumba za kushare vyoo na bado mnawadharau wengine Kama kujiajiri ni Rahisi acha hiyo kazzi uje mtaani.
 
Back
Top Bottom