Mkereketwa_Huyu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 9,836
- 7,231
Ndio maana mleta uzi alikuwekea mikatabaKuna muda huwa najiuliza kama kuna watu wengine hufikiri hata kidogo. Hiyo Geneva convention inayotaka tukatae mikataba iliyoingiwa na wakoloni ime classify ni mikataba ya aina gani? Kama huo utaifa tu ni mikataba ya kikoloni sasa tunaweza tukakataa nini? Tupo commonwealth halafu tukatae mikataba iliyoingiwa na waingereza. Aaaaa, ngoja nifanye mengine, maana kama huwezi kufikiri halafu ukataka uweze kufikiri kwa kusema tu 'mimi najua kufikiri' bila kujifunza kufikiri kamwe hutoweza kufikiri. Mungu atutetee!
Wewe mwenye akili umeongea nini zaidi ya utumbo tu
Ndio maana mleta uzi alikuwekea mikataba
na kwa nafasi yako na usomi wako naamini kuwa unaweza kuelewa imeleza nini
Na alilikomalia mpaka ikashangaza. "Kwanini tutumie maji ya Ziwa Victoria Wakati Misri hawana maji ?" aliuliza watanzania.
Hayo uliyosema yote tunayajua, point ni kwamba kwanini sisi watanzania tusifaidike na maji ya ziwa Victoria wakati wenzetu wanafaidika na maji yatokanayo na ziwa hilo?Ziwa victoria ni chanzo kinachopeleka maji river nile, Ambapo misri ni final destination kama mpokeaji maji kutoka ziwa victoria.
Hivyo basi sisi watanzania tukiwa na project (irrigation schemes) nyingi kama hzi kiwago cha maji kitakacho kua kinapotea kila siku kitakua kikubwa, Na kupelekea kiwango cha maji kupungua nchini misri.
Tukumbuke kwamba maji hadi yafike misri yanipita sudani na uganda ambapo pia yatatumika katika miradi mbalimbali.
Egypt ni nchi inayotegemea sana kilimo(large scale agriculture) kwa kutumia njia ya umwagiliaji.
Hitimisho.
Egypt ili wafanikishe kilimo cha umwagiliaji wanategemea maji kutoka victoria kupitia mto nile.
Kiwango cha wingi au uchache wa maji mto nile unategemea sana utumiaji wetu maji sisi watanzania.
Umeandika kuashiria una huruma sana na misri.Ziwa victoria ni chanzo kinachopeleka maji river nile, Ambapo misri ni final destination kama mpokeaji maji kutoka ziwa victoria.
Hivyo basi sisi watanzania tukiwa na project (irrigation schemes) nyingi kama hzi kiwago cha maji kitakacho kua kinapotea kila siku kitakua kikubwa, Na kupelekea kiwango cha maji kupungua nchini misri.
Tukumbuke kwamba maji hadi yafike misri yanipita sudani na uganda ambapo pia yatatumika katika miradi mbalimbali.
Egypt ni nchi inayotegemea sana kilimo(large scale agriculture) kwa kutumia njia ya umwagiliaji.
Hitimisho.
Egypt ili wafanikishe kilimo cha umwagiliaji wanategemea maji kutoka victoria kupitia mto nile.
Kiwango cha wingi au uchache wa maji mto nile unategemea sana utumiaji wetu maji sisi watanzania.
Mkuu huyo jamaa kwa hiyo comment yake, mimi imenipa wasiwasi kama kweli ni mtanzania.Kwani Misri iko Tanzania? au sehemu ya Tanzania? Ziwa Victoria liko Tanzania, matatizo yao sio sehemu yetu,hatuwezi kupata matatizo ili wao wanufaike.
Ningependa kuwa mbia wana jamii hebu fanyeni utafiti.
Kuna tuhuma kuwa baadhi ya viongozi wa awamu iliyopita na wengine wa awamu hii wako kwenye payroll ya serikali ya Egypt ili kuzima au ku sabotage kwa namna mbali mbali miradi ya kilimo cha Umwagiliaji na matumizi mengine ya maji toka ziwa victoria
Baadhi yao wako ndani ya idara mbali mbali za serikali na maslahi yao ni kwa ajili ya serikali ya Misri na sio Tanzania
Imefika mahala baadhi ya miradi imepigwa chini na watu wa idara ya mazingira kwa visingizio mbali mbali kuwa ili watanzania wasitumie maji ya aiwa victoria
Naomba wenye kujua undani wa haya madai watujuze kwa nini tumewekewa restriction kutumia maji wakati Ethiopia na Sudan wanaendelea na miradi mikubwa mikubwa ya Umwagiliaji na Mabwawa makubwa ya umeme na kadhalika huku sisi tunaambiwa kuwa maji kwenda Shinyanga na mikoa mingine haiwezekani kwa kiwango cha kutosheleza wananchi.
Huko juu Ethiopia wao wameamua kujenga na KUMALIZA kujengaBwawa la umeme kubwa kuliko yote Africa kwenye mto Nile ambao chanzo cha maji yake ni huku kwenye ziwa Victoria
SHERIA
Kuna watu watakuja hapa kukujazeni ujinga wao kuwa kuna mkataba wa 1929 ambao lazima sisi tuuheshim
Ukweli ni kuwa:
1. MKATABA ulikuwa kati ya serikali ya kikoloni ya UINGEREZA na MISRI
2. Kuna mkataba wa Vienna wa The Vienna Convention on Succession of States in Respect of Treaties, ibara ya 16, inasema kuwa mataifa huru au yaliyopata uhuru kama TANGANYIA/TANZANIA hayahitaji kurithi treaty obligations of its colonial power.
Someni mkataba wa Vienna ambao sisi ni signatory na link hii hapa:
http://legal.un.org/ilc/texts/instruments/english/conventions/3_2_1978.pdf
ndio, nenda mwanza kaone jamaa wanavyo yatumia hayo maji. Mimi natumia maji ya ziwani kumwagilia mazao.Unauhakika na unacho"comment"?
Lowasa tu ndie kiboko ya longolongo aliyatupilia mabali madai yao na kuamuru maji yatumike, now shinyanga wanafaidi maji ya ziwa victori.
Your out of focus by half lamda,kumbe hujui unazungumzia nini?Bora wewe una akili zako timamu kwa sababu umekuwa Mtanzania kwa vile Mungu kapenda! Kenya nchi jirani kwako kwa vile Mungu kapenda na hayo maneno unayoyatumia ya Slavery mentallity na colonial hangover umeyapata kwa kuwa Mungu kapenda. Jeunalifahami jina lako? Nalo hilo Mungu kapenda. Dini yako? Hiyo ndiousiseme ulishushiwa kwako mwenyewe direct na Sir God Himself. Congratulations. Mkataba upo, mumeamua kuwa wanyama wa kufugwa kwa kufuata taratibu zao basi heshimuni taratibu zao ndizo zinazoendesha maisha yenu, kurukaruka pasipo kujua unafanya nini ni kupoteza muda, once a slave, always a slave!
Does Egypt have monopoly over Nile waters?Ningependa kuwa mbia wana jamii hebu fanyeni utafiti.
Maji ya lake victoria ya vynazo viwili
kuna maji yanayo toka kwa ajili ya mto nile
na kuna maji ya nayo jaza ziwa victoria.
Majiya victoria haya husiani kabisa na maji ya nile
Fanyeni utafiti na matajua hayo.
Haya ya kuwa tume ambiwa tusitumie lake victoria sisahii. tusi je kuchafua chanzo cha nile au kukibadilisha njia.
Fanyeni utafiti
Kuna tuhuma kuwa baadhi ya viongozi wa awamu iliyopita na wengine wa awamu hii wako kwenye payroll ya serikali ya Egypt ili kuzima au ku sabotage kwa namna mbali mbali miradi ya kilimo cha Umwagiliaji na matumizi mengine ya maji toka ziwa victoria
Baadhi yao wako ndani ya idara mbali mbali za serikali na maslahi yao ni kwa ajili ya serikali ya Misri na sio Tanzania
Imefika mahala baadhi ya miradi imepigwa chini na watu wa idara ya mazingira kwa visingizio mbali mbali kuwa ili watanzania wasitumie maji ya aiwa victoria
Naomba wenye kujua undani wa haya madai watujuze kwa nini tumewekewa restriction kutumia maji wakati Ethiopia na Sudan wanaendelea na miradi mikubwa mikubwa ya Umwagiliaji na Mabwawa makubwa ya umeme na kadhalika huku sisi tunaambiwa kuwa maji kwenda Shinyanga na mikoa mingine haiwezekani kwa kiwango cha kutosheleza wananchi.
Huko juu Ethiopia wao wameamua kujenga na KUMALIZA kujengaBwawa la umeme kubwa kuliko yote Africa kwenye mto Nile ambao chanzo cha maji yake ni huku kwenye ziwa Victoria
SHERIA
Kuna watu watakuja hapa kukujazeni ujinga wao kuwa kuna mkataba wa 1929 ambao lazima sisi tuuheshim
Ukweli ni kuwa:
1. MKATABA ulikuwa kati ya serikali ya kikoloni ya UINGEREZA na MISRI
2. Kuna mkataba wa Vienna wa The Vienna Convention on Succession of States in Respect of Treaties, ibara ya 16, inasema kuwa mataifa huru au yaliyopata uhuru kama TANGANYIA/TANZANIA hayahitaji kurithi treaty obligations of its colonial power.
Someni mkataba wa Vienna ambao sisi ni signatory na link hii hapa:
http://legal.un.org/ilc/texts/instruments/english/conventions/3_2_1978.pdf
Hili ni jambo muhimu sana. Ila kabla hatujaenda mbali nikukumbushe kwamba mradi wa umeme wa Ethiopia ulioutaja uko kwenye tawi la mto Nile kutoka milima ya nchini Ethiopia nadhani mto wao unaitwa White Nile; ambapo tawi la pili (Blue Nile) ndilo linaanzia Lake Victoria etc.
Pili ni vema wataalamu waje na takwimu kuhusu athari za kila mradi wa matumizi ya maji ya ziwa Victoria (kwa nchi zote za Afrika Mashariki na kueleza jinsi outflow ya maji itakavyopungua katika mto Nile pale Jinja kuelekea Misri.
Nasema hivi kwasababu enzi za Wajerumani kulikuwa na mpango wa kuchimba mfereji kupeleka maji sehemu za Shinyanga na Tabora. Kwa mahesabu yao Wajerumani walionyesha kwamba mradi huo sio tu, usingeathiri kiasi cha maji kinachotoka ziwa Victoria kwenda mto Nile; bali hesabu zao zilionyesha kwamba maji yanayopotea kwa mvuke wa jua (L. Victoria surface evaporation) kwa mwaka mzima ni mengi kuliko maji ambayo yangeondolewa kupitia mfereji huo. Ambao volume ya maji iliyokusudiwa ilikuwa mara kumi na zaidi ya mradi wa bomba la Kahama!
Lakini pia zipo taarifa kwamba kina cha ziwa Victoria nacho kinazidi kupungua kutokana na siltation, inayosababishwa na deforestation kwenye catchment area ya ziwa na maeneo mengine. Kwahiyo future ya Lake Victoria inategemea mambo mengi pamoja na matumizi ya maji kwa umwagiliaji.
Tusingoje Wamisri watusemee au waje na data zao kupinga miradi yetu halafu sisi tusiwe na zetu. Ikiwa hivyo itabidi tuwe tunasalimu amri za watu wengine.
Au ni double agent nini?Nilishangaa kuona Membe anataka tusiyatumie maji ya Ziwa victoria eti kwa sababu Misri itaathirika. Akaenda mbele hata k kuzishawishi nchi za Maziwa makuu kuifikiria Misri zaidi kwa madai eti sisi nchi za ukanda huu wa kusini mwa mto nile tunapata mvua za kutosha! Huyu Membe mtu wa ajabu sana!.
Wao Misri wana bahari ya mediteranian, wanaweza kufanya desalination.
Misri wana Jangwa la Sahara. Ambayo chini yake huenda kuna maji mengi kama ambayo Libya waligundua.
Isitoshe sisi tuna mgogoro wa Ziwa Nyasa, sasa inakuwaje anagive up rights za Watanzania kuyafaidi Maji ya Ziwa hilo la Victoria?
Huyu Membe hatufai,angetuuza!!
Tumwambie akafunge mita pale kwenye tundu yanapopitia, hao wa ethiopia na misri walipe kodi kulingana na units wanazotumia, itengenezwe Victoria Revenue Authority (VRA) bila shaka mkuu atakusanya matrilion ya madolari hapo. Jamaa wakizingua kulipa bili anayapiga KUFULI. Full stopNgoja tusubiri JPM anasemaji kuhusu hili, tumpe mda au tumkumbushe juu ya hili maana naona kama halimo kwenye sera yake.
Kwani ziwa nyanza linategemea mvua? Hakuna siku ziwa lile litakuaka waache ujinga wao. Kwanza si wajiulize yale maji yanatoka wapi? Wanakijua chanzo chake?sasa Egypt wakilima sisi tunafaidikaje? ni vyema tulime sisi wenyewe kwa kutumia maji ya ziwa victoria. kikubwa na cha msingi ni kuboresha vyanzo vyetu vya maji na kuvilinda kwa nguvu zote ili tuvitumie kwa muda mrefu.
Tunao uwezo wakuzalisha tani milioni 100 za chakula na mazao ya biashara kwa mwaka. Kwa ardhi tuliyonayo na vyanzo vya maji vilivyopo hakika tunaweza kuilisha dunia nzima. Matumizi ya ardhi kwa nchi hii hata 1/8 hatujafika. Nchi kubwa hii hadi hatari. Mipori imejazana kila kona, unaweza kutembea kwa gari 80km/hr kwa muda wa masaa 8 ni msitu na mapori tu.Tukilitumia ziwa Victoria kwa kilimo cha umwagiliaji tutajiongezea uhakika wa chakula toka akiba ya sasa tani 1.5 million za sasa mpaka tani 4 million na kusahau njaa