Kuna watu makatili kweli kweli, achoma paka moto akiwa hai

Nikiwa mtoto na wadogo zangu wawili wa kiume tuliyaua mno mapaka shume aka vimburu
 
Huyo jamaa haya MTU anaweza kuua sababu ya mali
 

Paka hujiona mfalme
 
Huyo mshenzi ataandamwa na mikosi na mabalaa maisha yake yote, na wote ambao mmeshaua Paka msijishangae mambo yenu hayaendi sawa ni kile kivuli cha Paka ulichokiua kinakuwinda,

Binaadam hua tunafikiri hii Dunia ni yetu peke yetu, tunasahau kuna viumbe wengine tunachangia nao, tuache ubinafsi, tuache ukatili, Dunia ni mahala salama kama tukipaweka salama.
 
Yupo mwingine alimtwanga paka kwenye kinu hadi akawa uji[emoji1787]
 
Vifaranga vilirudi baada ya kumtesa vile? Angepiga rungu moja la kichwa kwisha habari
 
Paka wezi wanakera sana. Kuna jirani yetu enzi nipo shule kidato cha pili alikuwa amefuga paka wengi na wengine wakawa wezi, ukiacha mlango wazi wanaingia kudokoa chochote. Ikafikia mahali wanakaa karibu na dirishani, ukifungua tu baada ya dk 5 unakuta ameingia yupo uvunguni mara huyoo jikoni au kufungua friji ale chochote atachokikuta.

Basi kuna siku tukiwa na rafiki yangu tukamtegeshea kipande cha nyama kwenye mtego wa panya ule wa spring. Tukauweka chini kidogo ya dirisha pale wanapopenda kuingiliaga. Si tukawa chumba cha pili tunaendelea kupiga msuli, kama dk 30 mara tukasikia mtego umefyatuka na paka analia mauuuuuuuuu mauuuuuu kucheki kumbe amenaswa mguu wa mbele na mtego ameshindwa kuutoa, alivyotuona akapanic zaidi akajaribu kuruka kupita dirishani anashindwa, tukamfungulia mlango akatoka na mtego wake huku analia, nyama kaidondosha chini, tukamwacha. Akaingia kwao sijui hapakuwa na mtu maana tuliendelea kumsikia analia muda mrefu, badae akatoka tena hatukujua alipoenda, ila ulipita muda mrefu sana hatukuona paka mle ndani, na kile kipande kilibaki chini mpaka sisimizi wakakiandama tukafagia. Sema bi mkubwa hakupendezwa sana aliposikia tulichokifanya. Si unajua hofu za ushiriki na.
 
Kuna Waziri Mmoja alichomaga Vifaranga yaani ni roho mbaya ya ukatiri...
 
iwe fundisho, ukila na wewe huliwa
boko wala wenzioooo
 
Sisi tuliofuga njiwa ndio tunaijua vizuri adha ya haya mapaka shume.
Likifanikiwa kuingia ndani ya banda linaweza kuua hata njiwa 10 halafu linachua mmoja linaondoka, njaa ikimshika tena anakuja kuua wengine mpaka njiwa wote wanaisha au wanahama.
Ila yote kwa yote kwa imani yangu amelaaniwa binaadamu yoyote anaetesa au kuua kwa kutumia moto, hukumu ya kuadhibu kwa moto ni ya MUNGU pekee sio binaadamu.
 
hawa wadudu hamuwajui nyinyi,usione hawaishi na msela ukadhani ni bahati mbaya.wanajua.

enzi hizo niko kijijini huko,imechinjwa kuku ikaungwa rost imeliwa robo mchana,inatakiwa iliwe na usiku na kesho yake maana tulibaki watoto 3 tu,wazazi waliondoka mchana huo kwenda seminar mjini.

huwa kuna meza kubwa sana iko nyuma ya nyumba,hiyo tunaweka vyombo na vifaa vingine vya chakula na hata mboga sometime,siku hiyo kwa kuogopa paka hatukuweka sehemu nyingine yoyote isipokuwa sufuria husika iliwekwa juu ya hiyo meza,kisha ikafunikiwa ndoo kubwa juu ya ndoo ikawekwa tofali ya block.

tukaenda kisimani kuchota maji[emoji23].
wakati tunarudi tunashangaa kwa mbaaali kuna kama kuku wanakimbizana kunyang'anyana vitu,kumbe wamegawana nyama ya kuku aliyechinjwa,kuku nao tulikuwa nao kama 130 hivi wa kienyeji,kucheki ndoo juu ya meza iko chini,tukajua hapa tayari tumeshapigwa.

kufika pale paka tuliyekuwa tunamfuga,analamba mchuzi chini na wanaye kujipongeza kwa kazi aliyoifanya huku matumbo yanakaribia kugusa chini,kwa hasira nilipiga mmoja shuti hakuinuka na roho zake 7[emoji1787].
wengine walitawanyika mbiooo.
 
kuna paka ananilia vifaranga, siku nikimdaka namchoma kama huyu jamaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…