Kundi Hili la Watumishi wa Umma lina Upeo Mdogo? Nini kifanyike?

Umesema walimu ni janga and yet wanaofundishwa na hao walimu wana IQ kubwa..!! Tafakari na uchukue hatua
 
Leo naungana na wewe. Hilo kundi limejaa watu wenye roho mbaya sana, sana... sijui Kwa sababu wengi wanatokea familia masikini.

Case study ni mwendazake kiongozi wa malaika, naye alitokea kundi Hilo.
Umejawa ujinga mwingi.
 
Mleta mada umeleta uzi ambao nachangia huku roho inauma. Kiukweli karibu familia nyingi za kitanzania huwa kunakuwa na mwalimu. Hawa watu ni muhimu sana ila ni wachache ambao hushtuka na kwenda sawa na dunia inavyoenda hasa kiuchumi. Rekodi nyingi za TAKUKURU inaonyesha waalimu ni wahanga wakubwa wa utapeli na matukio yanayofanania utapeli. Wastaafu wengi wa ualimu wamekuwa wakidhulumiwa kirahisi. Huwa najiuliza huko vyuoni kunakuwaga na mafunzo tofauti? Mbona wote tulipita form six salama na kuingia vyuoni kwa alama za kutosha sasa inakuwaje huku mtaani ghafla mwalimu anakuwa nyuma?

Inabidi semina nyingi sana za ujasiriamali na maisha kwa ujumla zitolewe kwa waalimu ili nao wachangamke.
 
Sasa wewe kwanini ulikubali kubeba mimba ya mtumishi wa hiyo kada unayoilalamikia wakati unaamini kuwa watumishi wa kada hiyo hawana akili?
Pole sana subili ujifungue nadhani atakusaidia kulea mtoto.
Punguza stress mama kijacho..
 
Na Mimi baadhi ya walimu wananikera Kama wewe ulivyokereka, shida hawaijui thamani Yao, we mtu huwezi kuwa unaburuzwa Hadi na wajumbe wa CCM....upo tu Kama sio professional....hujipendi, usupojijali hakuna WA kukujali.
Mbona Kada nyingine wanajibeba, hawadharauliki Kama walimu?
 
Una umri gani?
 
Tuseme ukweli serikali ndiyo imeanza kuwadharau Kwa maslahi madogo, imejitahidi kuwanyanyasa na kuwagombanisha na jamii.
Kila kitu lawama Kwa mwalimu, ubaya na wao wamepokea manyanyaso hawajisimamii, mtu anakuwa muoga muoga Hadi unajiuliza huyu hajiamini hivi Hana cheti au? Halafu unakuta ni mwanaume, Ila ni lioga...likipewa maelekezo hata na mjumbe wa CCM linafata, haliact professional.
 
Kila eneo lenye mwanadamu nchi hii lazima mwalimu apelekwe haijalishi ni chaka kiasi gani,anafanya kazi bila posho yeyote tofauti na mshahara,hana semina za kutosha wala motisha akiwa kazini,kila mwenye kacheo serikalini hata awe diwani jicho kwa mwalimu.Akishastaafu anatoka huko kijijini ambako hapakuwa na watumishi wengine zaidi yake anahamia mjini,Mtu wa hivi kwanini asipate tabu?
 
Hamkuelewa walisema ni asilimia 3 nyie hio 23 itoke wapi kwa uchumi wa wa kukopa badala ya uzalishaji
 
Hao wote uliowaorodhesha hapo wamepatikana kutoka kwa huyo mwalimu unayemtukana,nadhani na hiyo ndio sababu yao kuu ya kuwa walalamikaji wakubwa nchini kwa kuona kuwa hawapati wanachostahili.....

Mwalimu
Mwalimu
Mwalimu


Ipo siku utakuja kugundua kuwa wewe uliyeweka bandiko hili ndio una shida mahala....

Sent from my PBBM00 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…