Kundi kubwa la watu wenye fedha ambazo hawajui watazitumiaje, ndio mtaji wa matapeli

Kundi kubwa la watu wenye fedha ambazo hawajui watazitumiaje, ndio mtaji wa matapeli

Akilindogosana

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2020
Posts
4,303
Reaction score
12,679
Habari wakuu.

Siku za karibuni pamekuwa na utapeli wa aina nyingi na aina mbalimbali unaohusiana na fedha. Kama bahati nasibu, kamari, network marketing, pyramid scheme, ponzi schemes, "online business" na aina nyinginezo za utapeli.

Hao matapeli wanakuaminisha kuwa utapata faida kubwa na fedha nyingi harakaharaka. Na wanacheza na akili yako kujiona utakuwa tajiri mkubwa sana ndani ya muda mfupi. Tena watakuaminisha kwa kupitia vibali halali, washindi feki, hata matangazo mengi sana na mbinu nyingi sana kushawishi watu. Kwa hiyo wanamgeuza mtu anakuwa kama mjingamjinga hivi. Ile ukiwekeza tu 😂 😂😂 hupati kitu 😂😂😂.

Chanzo cha huo utapeli ni sababu mbili

1. Uwepo wa wajinga weeeeeeeengi katika jamii yetu wenye hamu ya utajiri wa haraka. Hapo ndipo matapeli wanacheza na akili za watu kuona watapata utajiri wa haraka sana.

2. Sababu ya pili ni mtu kuwa na hela ambazo hujui ufanyie nini ili zizalishe fedha zaidi. Hapa matapeli wao wanacheza na akili kukuaminisha kuwa utapeli wao ni uwekezaji utakao kupa faida tena wanasema hauna risk kabisa 😂😂😂. Hii ni kuanzia watu wenye pesa ndogondogo mpaka kubwakubwa. Na unakuta mtu ametapeliwa laki tano, 1m mpaka wengine unakuta kaweka 30m mpaka 100m. Hatimaye pesa inaondoka yote na matapeli.

Sasa ni muda wa watu kutoa ushari kwa watu wa sehemu sahihi ya kuwekeza hela. Ama sivyo matapeli wataendelea kutapeli watu. Na serikali iwafatilie na jeshi la polisi lifatilie matapeli kupitia miamala ya simu, benki na selcom.

Watu wasio na mipango ya pa kuipeleka hela ndio hasahasa wanatapeliwa kwa kutafuta utajiri wa haraka.
 
Sio kweli,

Ni Serikali imeshindwa kuwazuia au kuna baadhi ya viongozi wa serikali wanahusika
- Kutokana wana vithibisho vyote kutoka serikalini na wanatambulika lakini mamlaka haiwafatilia

Ingekuwa enzi za Magufuli hili lisingetokea
 
Sio kweli,

Ni Serikali imeshindwa kuwazuia au kuna baadhi ya viongozi wa serikali wanahusika
- Kutokana wana vithibisho vyote kutoka serikalini na wanatambulika lakini mamlaka hawafatilia

Ingekuwa enzi za Magufuli hili lisengetokea
Huu utapeli ni wa siku nyingi. Hata enzi ya magufuli matapeli wa "wekeza utajirike" walikuwepo. Ishu ni kuwepo wajingawajinga weeeeeeeengi ambao hawajui wawekeze katika kitu gani ili wafaidike.
 
Huu utapeli ni wa siku nyingi. Hata enzi ya magufuli matapeli wa "wekeza utajirike" walikuwepo. Ishu ni kuwepo wajingawajinga weeeeeeeengi ambao hawajui wawekeze katika kitu gani ili wafaidike.
Sasa kama umeanza enzi za Magufuli, kwa nini serikali isizuiwe?

Kuna mtu ambaye ni kigogo serikalini anahusika
 
Sasa kama umeanza enzi za Magufuli , kwa nini serikali isizue?

Kuna mtu ambaye ni kigogo serikalini anahusika
Utapeli wa aina hiyo upo enzi na enzi ila wanabadili mfumo. Ila wazo ni kutapeli watu. Enzi hizo palikuwa na DECI. Kwa hiyo ni utapeli wa siku nyingi sana
 
Mm nawapongeza matapeli kwa kuchangamsha nchi hasa groups za wasup.


Matapeli hawatoki mbali ni wanaijeria,wakenya na wasouth waliojanjaruka
 
Habari wakuu.

Siku za karibuni pamekuwa na utapeli wa aina nyingi na aina mbalimbali unaohusiana na fedha. Kama bahati nasibu, kamari, network marketing, pyramid scheme, ponzi schemes, "online business" na aina nyinginezo za utapeli.

Hao matapeli wanakuaminisha kuwa utapata faida kubwa na fedha nyingi harakaharaka. Na wanacheza na akili yako kujiona utakuwa tajiri mkubwa sana ndani ya muda mfupi. Tena watakuaminisha kwa kupitia vibali halali, washindi feki, hata matangazo mengi sana na mbinu nyingi sana kushawishi watu. Kwa hiyo wanamgeuza mtu anakuwa kama mjingamjinga hivi. Ile ukiwekeza tu [emoji23] [emoji23][emoji23] hupati kitu [emoji23][emoji23][emoji23].

Chanzo cha huo utapeli ni sababu mbili

1. Uwepo wa wajinga weeeeeeeengi katika jamii yetu wenye hamu ya utajiri wa haraka. Hapo ndipo matapeli wanacheza na akili za watu kuona watapata utajiri wa haraka sana.

2. Sababu ya pili ni mtu kuwa na hela ambazo hujui ufanyie nini ili zizalishe fedha zaidi. Hapa matapeli wao wanacheza na akili kukuaminisha kuwa utapeli wao ni uwekezaji utakao kupa faida tena wanasema hauna risk kabisa [emoji23][emoji23][emoji23]. Hii ni kuanzia watu wenye pesa ndogondogo mpaka kubwakubwa. Na unakuta mtu ametapeliwa laki tano, 1m mpaka wengine unakuta kaweka 30m mpaka 100m. Hatimaye pesa inaondoka yote na matapeli.

Sasa ni muda wa watu kutoa ushari kwa watu wa sehemu sahihi ya kuwekeza hela. Ama sivyo matapeli wataendelea kutapeli watu. Na serikali iwafatilie na jeshi la polisi lifatilie matapeli kupitia miamala ya simu, benki na selcom.

Watu wasio na mipango ya pa kuipeleka hela ndio hasahasa wanatapeliwa kwa kutafuta utajiri wa haraka.
IMG-20221011-WA0191.jpg
 
Serikali iingilie kati hili suala la utapeli,,
Isisubiri wanainchi tuibiwe ndy watoke mafichoni na matamko uchwara.

Kuna hawa jamaa wa TALA na BRANCH.
Kampuni za mikopo ya mitandaoni.

Walikuwepo kipindi fulani,na wakatimuliwa na MAGUFULI baada ya kuonekana kuna vitu havipo sawa.


Baada ya MAGUFULI kufa,
hizi kampuni zimeibuka upya,
Na mbaya zaidi ,wamekabidhi madeni Kwa kampuni ambayo inasema ndy yenye mamlaka ya kudai madeni ya BRANCH,

Hii kampuni imekuwa ikitoa sms za vitisho na kupiga simu mfululizo bila kujali kiasi unachodaiwa,
Hata Kama ulikuwa unadaiwa sh 22000.
Kinachonipa ukakasi sio pesa wanazodai,
Bali je hawa wanaosema weka pesa kwenye account hii,
Ni Branch wenyewe au ni wahuni wa NAIROBI?

Kuna siku nilihoji ofisi za hao kampuni ya kudai madeni,
Wakasema wao wapo Arusha,na ndy walioingia mkataba na branch kudai madeni ya BRANCH,
Ila branch wenyewe wpo NAIROBI,,

Nikasita kulipa hizo pesa,
Kwa hofu huenda nikawa ni fursa Kwa wengine..

Hii branch iweje ikimbie wakati wa MAGUFULI,
Miaka 6 baadae ije inidai deni la 22000?
Hivi hawa sio wahuni wa NAIROBI kweli?
 
Back
Top Bottom