Kununua hisa Tanzania ni kucheza kamari

Bora hata wewe CRDB wanasikika, nilinunuaga precision air, tangu nilivyonunua miaka mitano iliyopita sijawahi hata kuwasikia wanaongelea habari za hisa, ila kiukweli hali ni mbaya
Duh pole sana mkuu. Umenikumbusha mambo ya precision air...hatari sana, hapo ndo ujue nchi yetu bado changa sana.
 
Mkuu wake wa kitengo alikuwa pale BOT akiongoza kurugenzi ya 'Risk management', sasa sijui kwa nini hamshauri!
Tatizo naamini anaona anajua kila kitu.anafanya anachokiona kinafaa kwa mda na ku win cheap rating ya mda huo na kusahau long term impact and damages! nchi yetu yenyewe imegeuka risk kwa investors wa ndani na nje.
 
Hisa sio kamari kama misingi ya biashara na uwekezaji inazingatiwa. Kikubwa hapa ni matamko yenye kuathiri biashara za watu tofauti na kwingineko ambako biashara zinaathiriwa na sababu za kibiashara na si siasa.

Utanunua hisa za kampuni ya simu ikiwa kuna kampuni moja pinzani inapigiwa upatu na mamlaka kukamata soko?

Utanunua hisa za kampuni ya cement ikiwa kuna kampuni mojawapo pinzani inawekewa mazingira pendelezi ya kuwezesha uzalishaji kwa unafuu zaidi ya kampuni nyingine?

Utanunua hisa za benki ya kilimo na maendeleo vijijini ikiwa tayari mamlaka zinapendekeza amana ziwekwe kwenye benki nyingine pinzani?

Shida hapa sio BUSINESS TREND, shida ni POLITICAL FLAMES
 
Duh pole sana mkuu. Umenikumbusha mambo ya precision air...hatari sana, hapo ndo ujue nchi yetu bado changa sana.
Yap kweli namimi hao jamaa wa Precision niliwasahau.toka wakose mtaji zaidi na kupata hasara wamewatia umaskini wanahisa wao
 
Bora hata wewe CRDB wanasikika, nilinunuaga precision air, tangu nilivyonunua miaka mitano iliyopita sijawahi hata kuwasikia wanaongelea habari za hisa, ila kiukweli hali ni mbaya
mkuu uwekezaji kwa nchi yetu unaathiriwa na serikali inayokuwa madarakani.Serikali haina mtizamo wa kuwasaidia wanahisa na wenye kampuni.wao ni kupata chao na kukaa pembeni.hata stimulus package ili kampuni iendelee kusimama hawatoi.hawa Precision nakumbuka waliomba hela serikalini takribani 50bn mpaka kesho hawajapewa.
 
Binafsi kwa sasa siwezi nunua hisa hata watangaze nyumba kwa nyumba.

Ni kitu kipo wazi, Drop iliyoonekana DSE pekee inatosha kuonesha picha ya miezi inayokuja
unabusara na upo smart. watu wanaingia kichwakichwa kunyolewa
 
kweli nchi zinazojari wananchi angekubali kujiuzuru kuwa amekosa mkakati wa kunusuru uwekezaji wa wananchi.wao kwa akili zao ndogo wanadhani wanaumiza wale big investors wenye big shares kumbe wahanga pia ni sisi tunaochagizwa kumiliki uchumi wa nchi kupitia hisa.
 
exactly. shida ipo ikulu
 
Hashauriki yule, yeye ni kila kitu, pale mjengo kuna washauri wa kila sekta lakini anajifanyia anayoyajua yeye tu
kibaya amekusanya wasomi waliobobea wamezunguka serikali yake nzima lakini anayaamini mawazo yake wasomi kawaweka pale kupunguza ukosoaji mitaani.
 
Hiyo CRDB Jamaa hataki hata kuisikia anaona anamkomoa C.E.O kumbe anangamiza wananchi wanaomiliki hisa kule.Haachi huduma na nguvu ya soko iamue ubora wa benki.
 
Watanzania msiwe wajinga. Hisa zina faida kwenye nchi zilizo imara kiuchumi na hasa kisiasa. Mnapoteza fedha zenu bure shauri yenu. Rais anaua uchumi nyie mnanunua hisa.
 
Niwatetee watanzania walio Wengi mkuu haya tunayoyapigia kelele ndo yanachangia kushuka kwa soko hisa .mtu anaweza asilalamike direct kuhusu DSE lakini anacholalamika kina impact kwenye kuporomoka kwa soko la hisa.
 
Kwenye uzi kama huu hauwezi kumuona Lizaboni.
Nilikuwa najadiliana na mdau mmoja wa soko la hisa, alionesha wasiwasi wake kuwa hizo hisa zilizo katika Initial Public Offer (IPO) kwa sasa, ziko "over-priced". Wanunuzi wanaweza kuwa wananunua brand, lakini huko mbele hakutabiriki. Nadhani ni kampuni ya kwanza katika DSE iliyomwaga shares nyingi kiasi hicho!
 
One man show inaenda kuangusha nchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…