Kuona Maiti ikizikwa na Manispaa kumenitafakarisha sana maisha yetu hapa duniani

Kuona Maiti ikizikwa na Manispaa kumenitafakarisha sana maisha yetu hapa duniani

Dr Restart

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
4,949
Reaction score
24,046
Wasalaam!.

Kuna ndugu wa Mfanyakazi mwenzangu alipatwa na maradhi, akalizimika kulazwa ili kuendelea kupata matibabu zaidi katika moja ya Hospital za Rufaa hapa nchini.

Nilikuwa na ratiba ya kwenda kumuona baada ya ibada. Hivyo nilipotoka kanisani nilienda sokoni kununua baadhi ya vitu vya kumpelekea. Wakati nipo katika manunuzi, nikajisemea moyoni acha ninunue na vya ziada ili niwapelekee wakina mama wenye watoto wachanga. Napenda sana kutembelea wodi ya watoto. Nikavibeba na kuondoka kuelekea hospitali.

Kwa kuwa nilishawasiliana na mfanyakazi mwenzangu na kunitaarifu yupo, sikutilia maanani nitafikia wodi ipi nikishafika. Hivyo niliendesha bila wasiwasi wowote.

Mungu ni mwema nilifika salama. Lakini wakati naingia, niliona kitu cha kunistaajabisha na kunisononesha sana. Niliumia sana kiukweli.

Mlango niliongilia ni maarufu kama Mlango wa Mochwary. Na kwa hakika geti lipo karibu kabisa na chumba hicho cha kuhifadhia wapendwa wetu waliotutangulia. Geti la mochwari pia lilikuwa wazi. Kwa sababu gari lisingetoshea kuingia mazima. Hivyo ilinipa nafasi ya kuona barabara kile kilochokuwa kinafanyika.

Miili ya watu takribani mitano ilitolewa na kutupwa ndani ya gari (double cabin) hilo la manispaa. Waliwekwa kwa kupandanishwa. Kwa kweli niliumia sana.

Wakati nastaajabu kinachoendelea, watu hao wanatupiwa kwenye gari hilo kama takataka za muozo. Hawapangwi, wanarusha tu pwaa!.

Nilijisikia vibaya sana. Bahati mbaya nikapigiwa honi ikanilibidi nisogeze gari mbele. Nikasimama na kumruhusu mwenzangu apite.

Nikamuita mlinzi mmoja wa hapo hospitali. Kumuuliza, ndiyo akajibu ni miili ya watu iliyokosa ndugu na jamaa wa kuzika. Hivyo Manispaa inachukua jukumu la kwenda kuwafukia. Maana kule si kuzika.

Kumdadisi kiundani, akanieleza wanaenda kutupwa katika shimo moja lililokwishachimbwa na Caterpillar. Maumivu yake sijapata kuyaona. Nilisismkwa na kukosa raha. Kwa hakika niliumia sana.

Sikuweza tena kukaa ndani ya gari. Nikashuka na kuwafata wahusika. Wanadai ni mali ya manispaa. Wanajaza nafasi, wanapaswa wakaliwe na mbwa. Kwa maana ya kuwa hawafukiwi sana. Ni kidogo tu. Mbwa na paka wanapita kujipatia vitoweo.

Kiukweli nilisononeka kusipo kawaida. Hawana sanda, wamefunikwa tu na shuka la MSD. Nilipoanza kujifikiria maisha yangu ya ulimwenguni, machozi ya Utu uzima yalinitoka.

Nikawaomba walau hata niwanunulie jeneza wawekwe huko wakalazwe. Walikataa kabisa. Lakini baada ya kuwasihi, walikubali. Mungu ni mwema. Nje kidogo ya geti kuna wafanyabiashara wa majeneza. Nikanunua ya kuingizwa ndani. Nikanunua na Sanda, wakaviringishwa na kuwekwa yake. Wakapakiwa na kwenda kupumzishwa. Niliwalipa vijana kwa kazi ya ziada.

Sikuwa na raha siku nzima na hata sasa. Nina mawazo mengi mno. Lile tukio linaogofya na kuumiza sana.

Tuishi maisha ya kumpendeza Mungu. Wapendwa wetu kwa namna yeyote wapumzishwe kwa heshima..

Mungu atusaidie.
 
Upande wangu mwezi June mwaka huu nilihudhuria mazishi ya ndugu mmoja aliyefariki huko DSM akaletwa kuzikwa huko kwao nilipokuwepo kama mgeni tu. Yule ndugu aliniuma kwakweli maana alizikwa na Serikali ya mtaa imagine.

Ndugu walikuwepo na wachungaji + mashehe ila hawakuhusika katika kumzika kwa sababu ya Kwanza toka akiwa kijana hakua akishiriki ibada ya kanisa wala msikiti japo alikuwa anafahamika kama mkristo.

Iliniuma aiseee yaani hata ile sala au dua ya mwisho hakusaliwa, yaani kama tumefukia mbwa aliyegongwa na gari.
 
Watu hao wa mochwar nadhan mioyo ishakuwa chuma
Hata kama wanazikwa na manispaa serikali hawawezi shindwa kuwazika vizuri
Kama Serikali zinaruhusu mtu anakufa kwa kukosa dozi ya Tsh 20, 30, 50 ndio wataweza kugharamikia mazishi yake?

Afrika ndio motoni, ukiona umezaliwa Afrika ujue ndio adhabu yako hiyo pindi ulipokufa from your past life
 
Hatari sana, na inawezekana walipofika mazikoni walitoa jeneza wakaweka pembeni halafu wakawachukua marehemu na kuwatupia wote kwenye shimo hilo moja ili watosheleze maana ukiwazika na majeneza wasingetosha shimo moja. Yale majeneza wanayauza kwa watengezaji hata wakipata elfu 20 kwa kila jeneza wao huridhika tu....cha muhimu wewe ulifanya upande wako Mungu akubariki na akukumbuke siku ya umwisho wako
 
Kama serikali zinaruhusu mtu anakufa kwa kukosa dozi ya Tsh 20,30,50 ndio wataweza kughalamikia mazishi yake??
Afrika ndio motoni, ukiona umezaliwa afrika ujue ndio adhabu yako hiyo pindi ulipokufa from your past life
Mkuu kwa hiyo hapa tupo jehanam..!?
Sikuwahi kujutia kuzaliwa Afrika na sitokaa nijutie.
 
wengine unakuta wamekaa gerezani miaka na miaka hata ndugu zao wamewasahau. ila kuzika watu kaburi moja sio sawa kabisa.
Gerezani?

Sidhani. Kwa kadri nijuavyo, Gerezani wakati unaingizwa unaandika wosia. Si ya mali zako bali mwili wako. Kwamba endapo ukafariki mwili wako wakabidhiwe nani na wapi.

Maana yake, wanakuwa na taarifa zako zinakuwepo.

Hawa ni ndugu waliopata ajali ama kuuwawa. Na kwa bahati mbaya asiwepo anayemfahamu. Utazikwa kama mzoga.

Umetoka umeenda sehemu ya mbali. Kwa bahati mbaya mauti yakakukutia katikati ya harakati. Utazikwa na manispaa kama mbwa.

Inaumiza sana.
 
hatari sana, na inawezekana walipofika mazikoni walitoa jeneza wakaweka pembeni alafu wakawachukua marehemu na kuwatupia wote kwenye shimo hilo moja ili watosheleze maana ukiwazika na majeneza wasingetosha shimo moja. Yale majeneza wanayauza kwa watengezaji hata wakipata elfu 20 kwa kila jeneza wao huridhika tu....cha muhimu wewe ulifanya upande wako Mungu akubariki na akukumbuke siku ya umwisho wako
Kama kweli wamefanya hivyo, nawaombea Msamaha kwa Mungu. Yeye ndiye anayejua zaidi.

Aamin na ahsante kwa dua yako Mkuu..
 
Upande wangu mwezi june mwaka huu nilihudhiria mazishi ya ndugu mmoja aliyefariki huko dsm akaletwa kuzikwa huko kwao nilipokuwepo kama mgeni tu. Yule ndugu aliniuma kwakweli maana alizikwa na serikali ya mtaa imagine. Ndugu walikuwepo na wachungaji + mashehe ila hawakuhusika katika kumzika kwa sababu ya Kwanza toka akiwa kijana hakua akishiriki ibada ya kanisa wala msikiti japo alikua anafahamika kama mkristo.

Iliniuma aiseee yaani hata ile sala au dua ya mwisho hakusaliwa, yaani kama tumefukia mbwa aliyegongwa na gari.
Sala haina maana yoyote kwa mtu aliyekufa. Zile ibada lengo lake ni kuwakumbusha walio hai kuenenda katika njia inayopaswa.
 
Siwezi sikitika mtu kuzikwa na manispaa, siwezi sikitika mtu kukosa watu wa kumzika. Nasikitika mtu akifa tu, akishakufa mumzike kwa helicopter au toroli bado amekufa.

Mumzike kwenye jeneza au kwenye mkeka, amekufa. Na mazishi mazuri hayampi nafasi ya kwenda mbinguni wala kumuepusha na moto.

Kwangu mimi nikiona mtu anasikitika na kulilia maiti kuzikwa na manispaa huwa namuona weak, na taifa halijengwi na watu wa mioyo dhaifu kama huyo. Mkiwa vitani comrade akafa si lazima mbebe mwili kurudisha nyumbani kama logistics haziruhusu. Yani tuhangaike kubeba majeruhi kutoka frontline kisha tuhangaike kubeba miili ya waliokufa? Kama hakuna ceasefire ya kuchukua deceased mnachukua dogtags na vitambulisho ila miili mnazika ukouko frontline.

Nikienda sehemu kutafuta, sina ndugu wala jamaa nikatangulia ghafla bila yeyote kujua ni sahihi sana nizikwe na manispaa. Hakuna haja ya kutia huruma kwenye hilo
 
Back
Top Bottom