Kuona Maiti ikizikwa na Manispaa kumenitafakarisha sana maisha yetu hapa duniani

Kuona Maiti ikizikwa na Manispaa kumenitafakarisha sana maisha yetu hapa duniani

Siwezi sikitika mtu kuzikwa na manispaa, siwezi sikitika mtu kukosa watu wa kumzika. Nasikitika mtu akifa tu, akishakufa mumzike kwa helicopter au toroli bado amekufa.

Mumzike kwenye jeneza au kwenye mkeka, amekufa. Na mazishi mazuri hayampi nafasi ya kwenda mbinguni wala kumuepusha na moto.

Kwangu mimi nikiona mtu anasikitika na kulilia maiti kuzikwa na manispaa huwa namuona weak, na taifa halijengwi na watu wa mioyo dhaifu kama huyo. Mkiwa vitani comrade akafa si lazima mbebe mwili kurudisha nyumbani kama logistics haziruhusu. Yani tuhangaike kubeba majeruhi kutoka frontline kisha tuhangaike kubeba miili ya waliokufa? Kama hakuna ceasefire ya kuchukua deceased mnachukua dogtags na vitambulisho ila miili mnazika ukouko frontline.

Nikienda sehemu kutafuta, sina ndugu wala jamaa nikatangulia ghafla bila yeyote kujua ni sahihi sana nizikwe na manispaa. Hakuna haja ya kutia huruma kwenye hilo
Sawa ila basi kuwe na utu kwenye hayo mazishi ya manispaa sio unazikwa kama upo vitani au ni mkimbizi..
 
Gerezani?

Sidhani. Kwa kadri nijuavyo, Gerezani wakati unaingizwa unaandika wosia. Si ya mali zako bali mwili wako. Kwamba endapo ukafariki mwili wako wakabidhiwe nani na wapi.

Maana yake, wanakuwa na taarifa zako zinakuwepo.

Hawa ni ndugu waliopata ajali ama kuuwawa. Na kwa bahati mbaya asiwepo anayemfahamu. Utazikwa kama mzoga.

Umetoka umeenda sehemu ya mbali. Kwa bahati mbaya mauti yakakukutia katikati ya harakati. Utazikwa na manispaa kama mbwa.

Inaumiza sana.
Hakuna muda Kama huo mzee wafungwa wengi wanazikwa na manispaa
 
iyo hela ya majeneza ni bora ungeongeza matunda kwaajili ya wagonjwa ambao wangali hai. mtu akifa hajui lolote kwahyo hawajatambua wema wako hamna ata mwenye uwezo wa kukuombea baraka, ila ungefanya kwa walio hai ungeombewa baraka coz wametambua wema na huruma yako kwao
 
Hao mara nyingi sio kama hawakuwa na ndugu ila unakuta wana deni kubwa hapo hospital na hupewi maiti mpaka ulipie sasa watu wanaona mtu ameshafariki halafu tutoe million tano au million 10 mtu anaamua liwalo naliwe.
 
Siwezi sikitika mtu kuzikwa na manispaa, siwezi sikitika mtu kukosa watu wa kumzika. Nasikitika mtu akifa tu, akishakufa mumzike kwa helicopter au toroli bado amekufa.

Mumzike kwenye jeneza au kwenye mkeka, amekufa. Na mazishi mazuri hayampi nafasi ya kwenda mbinguni wala kumuepusha na moto.

Kwangu mimi nikiona mtu anasikitika na kulilia maiti kuzikwa na manispaa huwa namuona weak, na taifa halijengwi na watu wa mioyo dhaifu kama huyo. Mkiwa vitani comrade akafa si lazima mbebe mwili kurudisha nyumbani kama logistics haziruhusu. Yani tuhangaike kubeba majeruhi kutoka frontline kisha tuhangaike kubeba miili ya waliokufa? Kama hakuna ceasefire ya kuchukua deceased mnachukua dogtags na vitambulisho ila miili mnazika ukouko frontline.

Nikienda sehemu kutafuta, sina ndugu wala jamaa nikatangulia ghafla bila yeyote kujua ni sahihi sana nizikwe na manispaa. Hakuna haja ya kutia huruma kwenye hilo
Binadamu ni tofauti na viumbe wote duniani ndio maana Mungu kamtofautisha na wanyama anahitaji kuzikwa ki starabu
 
Tatizo huku kwetu maiti inapewa thamani kubwa kuliko hata mgonjwa anayepambania afya yake.

Kilichokufa hakifi tena, kuna mamia ya raia wamekufa huko vitani Ukraine wamezikwa kwenye shimo moja zaidi ya mia lakini hakuna mtu yeyote wa huko aliyeona jambo hilo kama ni la ajabu.
Kwahio unataka na sisi tuwe kama Ukraine? acheni hizo mambo, let's say ikitokea familia yako wamepata ajari utakubali wazikwe watano shimo moja kisa Ukraine wamefanya hivyo?
 
Ndugu walikuwepo na wachungaji + mashehe ila hawakuhusika katika kumzika kwa sababu ya Kwanza toka akiwa kijana hakua akishiriki ibada ya kanisa wala msikiti japo alikuwa anafahamika kama mkristo.

Iliniuma aiseee yaani hata ile sala au dua ya mwisho hakusaliwa, yaani kama tumefukia mbwa aliyegongwa na gari.
Hii ndiyo silaha ya wanaofaidika wewe ukiwa muumini wa dini husika. Kukutisha na kifo, maisha baada ya kifo.
Kwa kawaida binadamu ni waoga wa kitu tusichokijua au mahali tusipopajua. Ni vile tunaoopa giza sababu linatufanya tusijua kama tupo mahali salama sababu hauoni vizuri adui au vitu hatari vinavyotuzunguka karibu yetu tukiwa gizani.

Hakuna uhakika wowote sala/dua za kuombea marehemu zitamfaidisha kwa lolote yule mfu. Hii iwe kuna MUNGU au hayupo maana dini zinasema hatima yako ukifa itategemea na matendo yako ukiwa hai. Unaweza kuonekana mtu wa dini sana kwa nje kumbe unatenda dhambi nyingi mbaya kwa siri.

Pili hakuna uhakika sana kwamba kuna maisha baada ya kifo au utasikia maumiu yoyote baada ya kukata roho.
Ushahidi uliopo ni wa simulizi tu toka kwenye vitabu na mapokeo ya simulizi za midomo. Hakuna aliyekufa akarudi, ila walipoteza fahamu na kurudi wanasema hawakusikia maumiu wala chochote kwa muda ambao walipoteza fahamu hadi pale walipo onesha dalili za kurejesha fahamu ndipo walipata hisia na kusikia watu kwa mbali wakiongea. Hii inatupa uhakika ukisha kufa hakuna maumivi wala nini.

Hivyo uzikwe kwenye jeneza, kaburi la peke yako au kaburi la wengi au uchomwe moto, uliwe na viumbe wengine hakuna tofauti katika hisia za mfu(marehemu).
Zile huduma zote za mazishi ni za kutufariji tulio hai tu na kulinda mazingira tusipate magonjwa ya kuambukiza toka kwa miiili iliyokufa.
Kaburi ni kwa faida ya waliobaki hai wanapata mahali pa kumbukumbu ya ndugu yao aliyekufa na usafi wa mazingira kusiwe na harufu na magonjwa kwa walio hai.
 
Maiti sio ya kuionea huruma, wa kumuonea huruma ni Pele ambaye anajua kuwa hana maisha marefu zaidi ya mwezi mmoja.
It's been 17 day since I wrote this shit
 
Back
Top Bottom