Kuota mambo ya shule ni nini tafsiri yake?

Kuota mambo ya shule ni nini tafsiri yake?

🤣 🤣 🤣 ajabu nilikuwaga mtabe wa Math, na Physics ila kwenye ndoto unashangaa pepa aliendi, mara ugomee pepa, mara ufike bado dk 10
Mkuu afadhali umefungua uzi tupate majibu. Hata mm huwa naota nipo shule mara nyingi sana. Na wakati wa mitihani siku zote huwa simalizi, ninashindwa kujibu maswali rahisi au nachelewa kuingia chumba cha mtihani. Nikifika ndio nakuta wanafunzi wenzangu wanamaliza kujibu mtihani Tusubiri wenyewe waje kututafsiria.
 
Na mimi huwa naota pia , tena naota nafanya pepa gumu sioni hata swali la kujibu, au naota nimechelewa kuingia kwenye chumba cha mtihani, nilishawahi kuota sina calculator hivo nikashindwa kusolve maswali kabisa na huwa roho inauma hadi nikishtuka hivi kwamba ilikua ni ndoto ndiyo nashukuru na kupata amani, sijui ni nini tafsiri yake 🤔
Mkuu yaani wewe ni mimi kaabisa. Katika ndoto zangu zote sijawahi kumaliza kujibu maswali ya mtihani na ku submit booklet. Sijui hii ina tasfiri gani ktk maisha yangu.
 
Maana yake umeshindwa au kuna jambo linakuja mbele yako utashindwa kwa hio utafute namna ya kuchomoka hapo umepewa alarm ndoto ni fumbo
Asante kwa tafsiri mkuu. Lakini kama jambo lenyewe linalokuja huko mbele silijui mitajipangaje kulikabili? Au ni hili life gumu ninaloishi ndilo natakiwa niweke bidii nitokemo?
 
Sijui hii ina tasfiri gani ktk maisha yangu.
Kuna Jambo umeshindwa kulikamilisha au utashindwa kulikamilisha mboni simple tu kuelewa sasa cha kufanya kaa chini jichunguze Jambo gani umeshindwa au unaona huko mbele utashindwa kulikamilisha unapewa alarm hio ni km alert unatahadharishwa kilichojiri na kitakachojiri jichunguze vizuri udhaifu wako ulipo ndio sehemu yako ya kushindwa jiimarishe hapo
 
Asante kwa tafsiri mkuu. Lakini kama jambo lenyewe linalokuja huko mbele silijui mitajipangaje kulikabili? Au ni hili life gumu ninaloishi ndilo natakiwa niweke bidii nitokemo?
Nimekujibu hapo tayari mkuu
 
Hii ya kufika bado dk kadhaa nishaiota sana mkuu au kushtuka kuna national ya drs la 7 zikiwa zimebaki siku 3 tu
Mimi mara nyingi naota kuna mtihani unakaribia (bado siku 2 au 1) lakini sijajisomea hata topic moja. Huwa hahaha sana hadi najikuta nimeamka kutoka usingizini huku nikitokwa na kijasho chembamba na moyo kwenda mbio. Nikibaini ilikuwa ndoto tu napata relief. Kusema kweli hii ndoto inanihenyesha sana usingizini.
 
Kwa ufahamu wangu: Ndoto za shule ni ndoto zinazosignify Retrogression Spirit. Roho ya kurudishwa nyuma, kunakuwa hakuna progress katika eneo flani la maisha yako au pia maisha yako kwa ujumla. Unakuta unaanza hili mara linakufa, mara aumwe mtu ile hela uitoe ikamtibie, mara msiba, mara kaja mcheps ukahonga au akakuibia, mara uibiwe na majambazi. Au ni kazini mara ufukuzwe, usimamishwe. Au ni kiwanja chako mara kiuzwe mara mbili basi ilimradi ukwame.

Na hii spirit inaoriginate from various places, mojawapo being generational curses. Baadhi yetu tunapenda sana kufanya ibada kwa mizimu tunasema tunaona wazee au kuaga kwenu kumbe unakabidhiwa huko kwenye hizo madhabahu. Mara ya kwanza utaona unafanikiwa and all but kiuhalisia kiroho ndo umedidimia sana. Na mafanikio ya kweli huanzia mtu kufanikiwa rohoni kwanza ndo mwilini. Lakini kuna cases pia kwamba yumkini kuna watu ulisoma nao way back hawakuwa wazuri as in wachawi au maagent wa kuzimu. Wakakamata nyota yako, destiny yako. Na kama ulikula nao, ulishare nao chochote, ama waliiba peni yako..hili nalo ni very possible. Na pia kuna baadhi ni ardhi ulikosomea. Kuna shule zimewekewa mambo yake kwenye ardhi.

Juzi hapa kuna mtu alileta uzi wa shule za watoto wa single sex kuwa na roho za uchafuzi (tafsida). Sasa pia ardhi za shule hizi mara nyingi zinadai haya maagano yatimizwe. Uwe na uhakika watu watafanya haya. Kwanini: unakuta mtu katoka na tabia mbaya kwao huko, anaenda shule anafanya hayo madude, tayari ardhi inabeba hiyo laana. Wewe unampeleka mwanao, huombei ardhi ya shule.

Kila uchafu, laana zilizopo zitamkumba very likely. Somo ni refu sana, ninaongea from personal experience, nilikuwa affected pia. Mpaka leo ninajifanyia maombi ya deliverance. Mifungo ya kavu, Daniel fast ihusike. Its not easy but utapona tu ukiamua. Pray and mean it kuchomoka hapo.
 
Back
Top Bottom