Kupata maendeleo ya kweli, Watanzania ni lazima tujifunze kuukubali ukweli!. Hili la CCM kutawala milele ni kweli!.

Kupata maendeleo ya kweli, Watanzania ni lazima tujifunze kuukubali ukweli!. Hili la CCM kutawala milele ni kweli!.

Ni kiherehere changu tu kujiuliza swali la kimsingi kabisa la demokrasia ndani ya CHADEMA. Mimi si mwanachama wa chama hiki cha upinzani lakini ndio chama rasmi kinachoongoza kambi ya upinzani bungeni.

Huu ni usultani! Huwezi kuendesha demokrasia kwa kuwa na Mwenyekiti yule yule, timu ile ile, na uongozi ule ule katika upinzani, halafu tukajidai watatetea demokrasia ya nchi. Kama CHADEMA hawawezi ndani ya chama chao kurekebisha katiba kuweka ukomo wa uenyekiti, mtu anajiuliza kwa Taifa je? Si ni yale yale?
Mkuu Jidu, kwanza kuhoji jambo lolote kuhusu uendeshaji wa Chadema, sio kiherehere, bali ni haki yako kikatiba, kisheria, kikanuni na kiutaratibu kwasababu Chadema ni public party na sio private party, kitu chochote ambacho kinalipwa by taxpayers money, ni public entity, the public has the right to know its affairs na hakina ile kinga ya the rights to privacy kwa public monies.

Tena kwenye nchi za wenzetu, viongozi wote wa umma, their public and private conduct is public rights, hata akionekana tuu barabarani na mdada wa mtaani, ni disgrace to public office, Bill Clinton alitaka kufanyiwa impeachment kwa kosa la ku disgrace the oval office kwa kosa dogo tuu la kumpiga busu la mapenzi, intern Monica Lewinsky kwenye ofisi ya umma. Salama yake ni Monica Lewinsky mwenyewe ndie alimkingia kifua Clinton kwa kutoa ushahidi kuwa ni yeye Monica ndiye aliyatamani busu la Clinton na kula kiapo kuwa affair hiyo iliishia kwenye busu tuu na haukumaliziwa kwenye yale mambo!. Huku kwetu public officers paid by taxpayers money, sio tuu wanapiga mabusu watu wasio wenzi wao, bali hata kuwazalisha kabisa na kitu ambacho ni immorality lakini sis hukui kwetu ni ok kabisa, halafu watu wana preach morality!.

Hili la udikiteta Usultani wa Chadema, niliuzungumza hapa katika bandiko hili.

P
 
Bwana Mayalla, ccm kutawala milele siyo kesi, kesi ni namna ambavyo wanatawala kwa DHULUMA. Wangekuwa wanatenda HAKI upinzani ungekuwepo kwa asilimia chache mno mana upinzani ni kitu kisichozuilika. Sasa hivi chuki ni kubwa mno haimithiliki. Jaribu kuwaambia viongozi wasimamie HAKI waache kutengeneza UADUI baina ya watu, tunakoelekea siyo kwema.

Tamati, KILA CHENYE MWANZO KINA MWISHO.
 
Ndipo mwenyezi Mungu alipomuuliza paskali

Ewe paskali mbona unakengeuka na kuwa mpumbavu?

Ewe paskali hata lini Cha binadamu kikadumu milele?

Mwenyezi Mungu akageuza uso wake kwa hasira na paskali akatindikiwa yote yaliyo mema machoni pa bwana!
 
Wanabodi,

Leo tena naendelea na zile Makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa. Topic yangu ya leo ni kutuhusu sisi Watanzania, ili tupate maendeleo ya kweli, ni lazima tujifunze kuupokea na kuubali ukweli halisi, ukweli bayana, hata huo ukweli ukiwa mchungu vipi, ukweli ni ukweli tuu, na siku zote ndio husimama mpaka mwisho. Kali ya rais wetu Dr. John Pombe Magufuli, kuwa "CCM itatawala Milele " ni kauli ya ukweli kabisa kuwa ni ukweli halisi na ukweli bayana, katika mazingira ya sasa ya nchi yetu na uendeshaji wa siasa za vyama vingi, kama hakuna kitakachobadilika, then rais Magufuli yuko very right kuwa CCM itatawala milele!.

Moja kati ya sifa kubwa za rais Magufuli, ni kusema ukweli Daima tena bila kukopesha, wala kurembaremba, japo kuwa mkweli sana sometimes sio nzuri sana kidiplomasia katika baadhi ya maeneo, ambapo diplomasia hutumika, haya mambo ya diplomasia ndio yametufikisha hapa tulipo, sasa ili tutoke hapa na kusonga mbele kimaendeleo, Watanzania ni lazima tujifunze kuubali ukweli jinsi ile ulivyo, bila kurembwa rembwa, hivyo hili la CCM kutawala milele ni ukweli mtupu ambao lazima tuukubali.

Kuna wengi wanadhani siasa ni kupiga blah blah tuu, hivyo kwao, kila kinachosemwa na wanasiasa, wanakiona kama ni blah blah!, no!. Siasa sio blah blah tuu, japo blah blah zipo, ila pia kuna ukweli bayana, dhahir, shahir!. Siasa ni sayansi, social science, hivyo sayansi ya siasa ni political science, inafuata kanuni zile zile za kisayansi za Newton's laws of motion, ile kanuni ya "a body in motion" or
" a static body", itaendelea kubaki hivyo hivyo milele, hadi kutokea nguvu nyingine itakayoibadilisha, hivyo kwa hali hii ilivyo sasa, CCM is the body in motion, itaendelea kutawala milele, kwa sababu watu wenye uwezo wa Kimungu, wameishaona kuwa kwa Tanzania, hakuna kabisa uwezekano wa kutokea nguvu nyingine ya kuizuia CCM isitawale milele nchi yetu ya Tanzania, hivyo CCM, itatawala milele!.

Japo kila lenye mwanzo, huwa lina mwisho, na CCM kama chama, ina mwanzo hivyo ni lazima nayo iwe na mwisho, unless CCM ndie Mungu mwenyewe, ambaye Yeye ndiye Pekee Alfa na Omega hivyo CCM hii iliyopo sasa nayo ni CCM Alfa na Omega, haina mwisho, hivyo pia katika utawala wa Tanzania, CCM ndio alfa na omega wa siasa zetu, ndicho chama pekee chenye hati miliki ya kuitawala Tanzania milele!, huu ni ukweli bayana ambao lazima sote, tuupokee, tuukubali na tuutekeleze. Wale wote wasioukubali ukweli huu, ni kweli kabisa watapata taabu sana!.

Jee Milele ni Muda Gani?.

Kuna aina mbili za milele, milele ya kwanza ni milele ya kiroho, eternal ambayo inaongozwa na Mungu, na hata sisi binadamu, tutaishi milele, hivyo hapa duniani tuko tuu safarini kuelekea kwenye ama uzima wa milele mbinguni au peponi kwa Mungu kwa watenda wema, au kwenye jehanum ya ziwa la moto wa milele kwa shetani kwa watenda maovu.

Milele ya pili ni life span ya kudumu mpaka mwisho. Hii ni milele ya kidunia, ukizaliwa ukaishi, siku utakapokufa hiyo ndio milele yako na hapo ndipo mwisho wako. Life span zinatofautiana, mtoto akizaliwa na kuishi siku moja, hiyo siku moja, ndio milele yake, na mtu mwingine ukiishi miaka 100, hiyo ndio milele yake, kama ilivyo nyumba, ukizaliwa na kuvikuta vitu fulani, ukaishi navyo mpaka ulipokufa na kuviacha, vitu hivi vitasemwa vimeishi milele. Hivyo kwa wale wote walioishuhudia CCM ikizaliwa, kisha wao ndio wamekufa na kuiacha CCM, kwao CCM imedumu milele. Hivyo hata hawa waliopo sasa, ambao wamezaliwa na kuikuta CCM, na watakufa na kuiacha CCM, kwao CCM ni chama cha milele.

Hizi kauli za CCM kutawala milele, hazikuanza leo, na wala hazikuanza na rais Magufuli.
Hebu tembelea bandiko hili, umsikilize mwana CCM huyu alisema nini na uangalie alisema
lini na alisema wapi!, kwa wavivu wa kufungua links, kauli hii ya CCM kutawala milele, ilitolewa na Mhe. Pinda ndani ya Bunge letu tukufu na hakuna aliyetia neno!.
PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

Nilidhani Mhe. Pinda amekosea, kumbe mimi ndiye niliyekosea baada ya ukweli huu kuzidi kuthibitishwa na kutamkwa wazi wazi na bayana, itabidi tuu nimtafute Mtoto wa Mkulima, nimuombe msamaha kwa kudhani he was wrong, kumbe mimi ndio I was very wrong.

Humu jf, mtu wa kwanza kusema kuwa CCM itatawala milele ni mwana jf huyu
Je, CCM Itatawala Milele Au?
Na nilipokutana naye, nilifanya nae mahojiano haya.
lini
Watch TBC Live!. " William Malecela na Ndoto ya CCM Kutawala Miaka 50!.

Wenye Matumaini na Upinzani Kushika Dola!, Sahauni! CCM Inajiandaa Kuua Kabisa na Kuuzika Jumla !.

Kuhusu hili la CCM kutawala milele, pia niliwahi kulisema hapa
CCM kutumia Hooks & Crooks Kushinda Chaguzi, Inajua Ikishindwa Ndio Itakufa Jumla, Itakubali?

Katika awamu hii, viongozi wa upinzani walipoamua kujiengua kwenye vyama vyao kujiunga CCM, japo walibezwa, nikasisitiza humu, wasibezwe, wanaona mbali
Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja?

Jee Umilele wa CCM Kutawala Tanzania Milele, Unatokana na Nini?.

Umilele wa CCM kuitawala Tanzania, unatokana na mungu kuiteua CCM na kuipatia hati miliki ya milele kuitawala Tanzania, ndio maana katika baadhi ya makala zangu za nyuma, niliwahi kushauri tuifute ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, tuifute ruzuku kwa vyama vya siasa, Tanzania turejee kuwa nchi ya chama kimoja cha milele, CCM.
Ruzuku kwa vyama vya Siasa: Mnaonaje tumshauri Rais Magufuli aifutilie mbali ruzuku hii? Ni ufisadi
Kidumu Milele Chama Cha Mapinduzi.
Pascal

Rejea matukio ya Malawi na Zimbabwe, Hastings K. Banda na Robert Mugabe hawa wote walikuwa marais wa milele na wote walibebwa sana na majeshi yao na polisi, Mugabe ilifika mke wake akasema hata maiti yake itatawala Zimbabwe! Lakini wote wawili ilichukua siku moja kuondolewa madarakani na majeshi yao ambayo hawakutegemea yangeweza kuwageuka na ndipo umilele wao ulipoishia. Kama zilivyokuwa nchi hizo ndivyo na Tanzania ilivyo kwa majeshi kuibeba CCM lakini tujue kila siku damu nzee huondoka na kuingia damu mpya na fikra mpya hivyo lolote litaweza kutokea.
Mwisho, nani aliweza kufikiria kuwa makaburu wa Afrika Kusini wangeweza kuondoka pamoja na jeshi lake la polisi lilivyokuwa katiri! Kulingana na andiko lako unamwamini mungu lakini mimi ninamwamini Mungu hii ndiyo tofauti yetu ya mawazo.
 
Kulingana na andiko lako unamwamini mungu lakini mimi ninamwamini Mungu hii ndiyo tofauti yetu ya mawazo.
Mkuu Elvis Chirwa, to a devout Catholic kumwambia anaamini mungu, is blasphemous comment.

Kwa vile ni Mungu ndiye anaweka serikali za mataifa, baada ya Tanzania kufanywa ni shamba la bibi kwa muda mrefu, tukamuomba Mungu kwa kusali, kufunga na kuomba atupatie mkombozi wa kulikomboa taifa letu, Mungu akaisikia sala yetu, akajibu maombi na kutupatia rais Magufuli, hivyo rais Magufuli ni chaguo la Mungu kwa Tanzania, hivyo Magufuli atayaweza yote katika YEYE amtiaye nguvu!.


P
 
Mkuu Elvis Chirwa, to a devout Catholic kumwambia anaamini mungu, is blasphemous comment.

Kwa vile ni Mungu ndiye anaweka serikali za mataifa, baada ya Tanzania kufanywa ni shamba la bibi kwa muda mrefu, tukamuomba Mungu kwa kusali, kufunga na kuomba atupatie mkombozi wa kulikomboa taifa letu, Mungu akaisikia sala yetu, akajibu maombi na kutupatia rais Magufuli, hivyo rais Magufuli ni chaguo la Mungu kwa Tanzania, hivyo Magufuli atayaweza yote katika YEYE amtiaye nguvu!.


P
Kweli upumbavu umetamalaki kwa wasomi dah eti huyu Ni mwanagreat thinker p
 
Ndio maana walevi hawateuliki Leo wa bluu kesho wa kijani angalia deogratius rweyunga wa itv anazeeka bichwa tu
 
Kweli upumbavu umetamalaki kwa wasomi dah eti huyu Ni mwanagreat thinker p
Ni kawaida, hata Galileo Galilei alipokundua dunia ni duara, aliuliwa kwa kumkufuru Mungu!.
Hata Archimedes alipogundua the law of flotation, alitoka bafuni mbio kama alivyozaliwa na kuingia mtaani, huku akipiga kelele "eureka eureka " watu wamdhania ni kichwa!.
P
 
P
Ni kawaida, hata Galileo Galilei alipokundua dunia ni duara, aliuliwa kwa kumkufuru Mungu!.
Hata Archimedes alipogundua the law of flotation, alitoka bafuni mbio kama alivyozaliwa na kuingia mtaani, huku akipiga kelele "eureka eureka " watu wamdhania ni kichwa!.
P
Pasko unaakili ila ni mpumbavu utanisamehe ila wewe sidhani Kama uko sawa kichwani na matangazo ya frilensa hutapata ngoo kuanzia sasa !!! Toka siku ile nakuona unaingia geti la kijitonyama mkabala na ile pub opozit a getini nilikuona kirusi.
 
P
Pasko unaakili ila ni mpumbavu utanisamehe ila wewe sidhani Kama uko sawa kichwani na matangazo ya frilensa hutapata ngoo kuanzia sasa !!! Toka siku ile nakuona unaingia geti la kijitonyama mkabala na ile pub opozit a getini nilikuona kirusi.
Mtu ambaye hayuko sawa kichwani, akafanye nini Kijitonyama, wakati huwa wanachukua the top cream?.

Sasa wewe umeniona naingia Kijitonyama tuu ukaniona kirusi, ambapo ni eneo la makazi na kuna public hospital mule, anybody can go, jee siku ukigundua ofisi yangu iko Eagle Wing pale St. Peter's, utasemaje?.
P
 
Mkuu Elvis Chirwa, to a devout Catholic kumwambia anaamini mungu, is blasphemous comment.

Kwa vile ni Mungu ndiye anaweka serikali za mataifa, baada ya Tanzania kufanywa ni shamba la bibi kwa muda mrefu, tukamuomba Mungu kwa kusali, kufunga na kuomba atupatie mkombozi wa kulikomboa taifa letu, Mungu akaisikia sala yetu, akajibu maombi na kutupatia rais Magufuli, hivyo rais Magufuli ni chaguo la Mungu kwa Tanzania, hivyo Magufuli atayaweza yote katika YEYE amtiaye nguvu!.


P
Naona niliposema ninamwamini Mungu nilikuwa ninagofautisha kati ya mungu (uliyoitumia wewe) na Mungu (niliyemsema mimi) ni vigumu kuelewa. Inawezekana jina mungu ulilitumia kimakosa badala ya Mungu.
Hilo la kufunga na kumuomba Mungu sijui tulilifanyia wapi! Na kama watanzania tulilifanya kama usemavyo sijui kwanini tuliingia kwenye uchaguzi. Haya mambo ya kudanganya eti tuliomba yako kwenye nchi za wanyonge na masikini tu, Kenya hauwezi ukayakuta.
 
milele ina maana mbili na zote ni za kidini na sio za mtu kuishi siku moja na kufa ndio kuwa milele yake acha kudanganya watu labda useme huo ni uelewa wako, unasema watu watapona kwa kuujua ukweli wakati we unadanganya watu,.
KWA TAARIFA YAKO HAKUNA MAHUSIANO YA MWANADAMU KWENDA MBINGUNI HATA AKIWA MTAKJATIFU. KAMA UNA ANDIKO NIPE NISOME. HATA MWISHO MUNGU ATAUMBA MBINGU MPYA NA NCHI MPYA WANADAMU WATAENDELEA KUKAA KWENYE NCHI MPYA KAMA HUELEWI MAMBO YA UFALME WA MUNGU USIDANGANYE WATU. WE ENEDELEA KUSAKA UTEUZI KWA KUDANGANYA WATU NA KUMFANANISHA MUNGU NA CCM. MUNGU HAFANANISHWI KWA NAMNA YOYOTE ILE
 
Naona niliposema ninamwamini Mungu nilikuwa ninagofautisha kati ya mungu (uliyoitumia wewe) na Mungu (niliyemsema mimi) ni vigumu kuelewa. Inawezekana jina mungu ulilitumia kimakosa badala ya Mungu.
Hilo la kufunga na kumuomba Mungu sijui tulilifanyia wapi! Na kama watanzania tulilifanya kama usemavyo sijui kwanini tuliingia kwenye uchaguzi. Haya mambo ya kudanganya eti tuliomba yako kwenye nchi za wanyonge na masikini tu, Kenya hauwezi ukayakuta.
kama niliandika mungu badala ya Mungu, sorry ni typo!. Maombi tuliyafanya humu jf wakati tukimuita JK, dhaifu!.

2020 ndiyo ushafika, kwa hiyo ni wito wangu kwa vyama vya upinzani kutumia fursa hii adimu, kwa kufanya mikutano ya kisiasa, ambayo itaratibiwa kisayansi zaidi, ili hatimaye ifikapo mwezi wa Oktoba mwaka huu wa 2020, wananchi tukafanye maamuzi kwenye sanduku la kura kwa kuking'oa chama hiki cha CCM ambacho kimedumu kukaa madarakani tokea tupate Uhuru wetu, kwa "mbeleko" ya vyombo vya dola vya Jeshi la Polisi na TISS, kuwalinda watawala wetu na kujigeuza kuwa vitengo vya CCM ili watawala hao wasing'olewe madarakani
Mkuu Mystery karibu mitaa hii,
Hakuna wa kuitoa CCM madarakani kwasababu Tanzania hapa tulipo hatuna upinzani kabisa, huu upinzani uliopo ni upinzani uchwara, not serious not credible hivyo CCM itaendelea kutawala milele
P
 
Hii ya kutawala milele inaukakasi kidogo Mkuu. Hao watu wametawala kwa zaidi ya miaka 50 yenye mambo mengi ya kujiuliza. Bado mpaka leo hatujaweza kuondoa maaadui watano wa Taifa letu, UMASIKINI, UJINGA, MARADHI, UNAFKI NA NJAA. Wakati mwingine huwa najiuliza maswali mengi sana kuhusu aina za siasa za nchi yetu, nadhani matumizi ya akili zetu hayana nafasi kabisa. Naomba tufanye objective analysis tuongozwe na facts na siyo ushabiki au mapenzi. Muheshimiwa Raisi anatimiza wajibu wake kama Raisi na hayo ndiyo mategemeo ya waajiri wake ambao ni sisi wapiga kura.

Mimi ni miongoni wa watu wanaochukua tahadhari sana katika kuelewa maandiko ya Pascal Mayalla sababu ndani yake huwa kuna falsafa yenye kuhitaji tafakuri ya kina. Kwa mfano U MILELE wa Mayalla unaohusishwa na imani za ki Uungu inanifanya kutambua U-Milele huu sio ule niitambuayo kwa tafsiri ya kiswahili ya Kingazija, "INFINITY" Bali yaweza kuwa ni U milele kwa maana ya muda mrefu sana.

Lakini hata Marehemu Kingunge Ngombale Mwiru, akimpigia debe mgombea Urais 2015 alitoa maono juu ya mstakabali wa mabadiliko ya kisiasa nchini alipotuambia kuwa CCM isipotoka madarakani kwa vuguvugu hili la sasa haitatoka tena madarakani. Na hakika hakumaanisha Milele kwa maana hii ya tafsiri ya Kingazija.

Na tusitarajie CCM kuondoka madarakani kwa kushindwa kuwaondoa maadui zetu watatu UMASIKINI, UJINGA na MARADHI. Kwani maadui hawa wamejengwa kwa misingi ya kanuni za uumbaji. Ni maadui ambao wapo na wataendelea kuwepo isipokuwa kwa taswira tofauti kulingana na hali na wakati unaoendana na mabadiliko ya maendeleo na uumbaji. Kudhani maadui hawa iko siku watakwisha ni kujidanganya na Kwa maana hiyo ni vita ya kudumu inayobidilika kulingana na mabadiliko ya kimaendeleo.

Ndio maana napoangalia Maamuzi, mienendo na mifumo ya vyama vyetu Vikuu vya Upinzani (Mf. Chadema na CUF) vinatoa mashaka ya kutwaa madaraka siku za Karibuni. vinajiingiza kwenye migogoro inatakayo wachukulia muda wao katika kuirekebisha na hatimae kurejea kwenye malengo ya kuchukua uongozi wa nchi.

Huwezi kujitoa kwenye uchaguzi wa muhimu wa Serikali za Mitaa (Wapiga Debe) na mara ukaingia kwenye mgogoro wa Demokrasia ndani ya Chama chenyewe na muda mfupi huu uliobakia ukatarajia kuchukua uongozi wa Nchi. Haya ni majeraha yatakulia muda wa kujipanga upya kwa ajili ya miaka kumi ijayo.
 
Hiki nilichokisema kwenye bandiko hili, leo kimewekwa wazi na Katibu Mkuu wa CCM
Dkt. Bashiru katika bandiko hili

Dkt. Bashiru: Aliye na dola ndiye ananufaika nayo kubaki madarakani, hata CHADEMA ikiingia madarakani ikaondolewa kwenye dola ni uzembe wao

Dr. Bashiru amesema
aliye na dola ananufaika na dola hiyo kubaki madarakani, huo ni ukweli hata CHADEMA ikiingia kwenye dola kuiondoa kwenye dola utakuwa ni uzembe wake kwa sababu ana nafuu na faida yakuwa na dola.

Wanaosubiri sisi tulegelege kwenye kutumia dola kubaki kwenye dola watasubiri sana, hata Trump kumuondoa ngumu, kuna nafuu kubwa na faida kubwa chama kilichopo madarakani kutumia nguvu za dola kufanya mambo ya kujenga imani kwa wapiga kura ili kiweze kubaki madarakani. Aliye na dola ndiye ananufaika na dola ile kubaki madarakani, huo ni ukweli na hata CHADEMA ikiingia madarakana ikaondolewa kwenye dola ni uzembe wake. Kwasababu ana nafuu na faida ya kuendelea kubakia.

tumetumia vizuri dola kubaki madarakani
Hivyo tunapo waeleza humu kuwa CCM itatawala milele, naomba mtuelewe!, huu ndio ukweli wa siasa zetu.
P
 
Mada yako Ni Moto unaounguza,nasikitika watu wa ajabu Kama mtu anejiita Mzee Mwanakijiji na Pascal Mayala wangekua na wao walimsikia Bashiri Ali Katibu Mkuu wa CCM alipokua akiyatamka hayo kwa kinywa chake.Lakini bahati mbaya hawakumsikia.
Huwa ananikumbushia sana Pascal Mayalla , wamefanana sana uandishi nk.
Pascal Mayala hawezi kuja kwa uzi huu na yule mtu Mwanakijiji.

Mzee Mwanakijiji pamoja na Pascal Mayalla , hata mimi kiukweli wamenishangaza sana. The latter yeye ni muumini wa ccm kutawala milele na rais kuongezewa muda! Tena yeye ana wish kwamba baada ya Maghufuli ni zamu ya Makonda!!

The former yeye ameshangaza sana kwasababu pamoja na kwamba ni mwandishi na mtu ambaye amekuwa akijinadi kwamba ni mtu mwenye kupenda mijadala ya hoja badala ya viroja, usemi ambao yeye ndiye aliyeufanya kuwa maarufu humu, ndiye sasa amekuwa champion wa viroja! Ni kweli kabisa humu JF ungekuta yeye ndo mwenye thread ya nguvu kuhusiana na haya yanayoendelea. Anaishi marekani na anafahamu umuhimu wa midahalo na uwezo wa viongozi kujenga hoja ulivyokuwa muhimu mbele ya wapiga kura! Halafu sidhani kama alishawahi hata kulaani ya member mwenzetu humu, ndugu yetu na comrade wetu Ben Saanane. Sijawahi kumsikia akipingana na ukandamizaji wa habari, uvunjwaji wa katiba na mengineyo mengi.

Kweli kuishi kwingi ni kuona mengi. Leo hii Mwanakijiji ni muumini wa ccm!!🤦🏾‍♂️
Hii ni sawa tu na kuyabugia matapishi yako ukijiaminisha ni mlo wa ukweli!
Pascal Mayalla hawezi kuleta pua hapa. Hana hoja ya kuweza kupambana. Atakuja na hoja gani? Na wakati yeye mwenyewe yuko kwenye mission? Ni mwandishi ambaye hata ushirikiano wake na waandishi wenzake una utata. Mfano nchi za wenzetu, wana habari wanashirikiana sana inapokuja kwenye maslahi ya kazi zao, hata kama wana mitazamo ya tofauti.
Wengi wenu ndio mmefunguliwa macho na Dr. Bashiru, angalie akina sisi hili tuliliona lini na tukalizungumza, hivyo hakuna kipya Dr. Bashiru alichozungumza, only to confirm something that was already there and already known.
CCM ni chama dola, kitatawala milele!.

P
 
Wengi wenu ndio mmefunguliwa macho na Dr. Bashiru, angalie akina sisi hili tuliliona lini na tukalizungumza, hivyo hakuna kipya Dr. Bashiru alichozungumza, only to confirm something that was already there and already known.
CCM ni chama dola, kitatawala milele!.

P
Pascal naomba nikushauri kitu kimoja ndugu yangu,kwa ruhusa yako Mkuu.
 
Wengi wenu ndio mmefunguliwa macho na Dr. Bashiru, angalie akina sisi hili tuliliona lini na tukalizungumza, hivyo hakuna kipya Dr. Bashiru alichozungumza, only to confirm something that was already there and already known.
CCM ni chama dola, kitatawala milele!.

P
Ndo maana hausapoti tume huru?
 
Ndo maana hausapoti tume huru?
Tume huru ipi wakati hii iliyopo ni huru?, inahitaji tuu kuwa Shirikishi. Tatizo la uchaguzi Tanzania sio Tume huru bali uwanja sawa wa kufanya siasa.

Aliyezuia mikutano ya siasa sio NEC, ni mtu kajizuilia tuu, katiba ipo, waliozuiwa kinyume cha katiba wapo na wanaangalia tuu!.

Pamoja na matatizo mengine yote, Tanzania hatuna any serious and credible opposition.
P
 
Back
Top Bottom