Kupendwa sana na mtu ambaye humpendi ni moja ya kero ambayo haisemwi

Kupendwa sana na mtu ambaye humpendi ni moja ya kero ambayo haisemwi

Stephen Ngalya Chelu

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2017
Posts
8,252
Reaction score
18,335
Mahusiano yana mengi sana.

Kuna nyakati unakuwa na mtu anayekuonesha mapenzi ya dhati, anakufanyia kila kitu lakini haum'feel kabisa. Unajaribu kumkasirisha ili labda akasirike akuache lakini wapi, kila kosa lako analisamehe na mara nyingine yeye ndo anakuwa anaomba msamaha kwa makosa yako.

Unajaribu kupunguza kumjali ili pengine umfanye na yeye aanze kukaa mbali na wewe lakini haitokei hivyo. Atalia atalalamika lakini bado atabaki na wewe. Unatamani umwambie muachane lakini unakuwa unamuonea huruma. Unabaki kuendelea kupata mapenzi motomoto ambayo hauyahitaji na huku siku zikisonga ukiomba lolote litokee muachane...
 
Mahusiano yana mengi sana.

Kuna nyakati unakuwa na mtu anayekuonesha mapenzi ya dhati, anakufanyia kila kitu lakini haum'feel kabisa. Unajaribu kumkasirisha ili labda akasirike akuache lakini wapi, kila kosa lako analisamehe na mara nyingine yeye ndo anakuwa anaomba msamaha kwa makosa yako.

Unajaribu kupunguza kumjali ili pengine umfanye na yeye aanze kukaa mbali na wewe lakini haitokei hivyo. Atalia atalalamika lakini bado atabaki na wewe. Unatamani umwambie muachane lakini unakuwa unamuonea huruma. Unabaki kuendelea kupata mapenzi motomoto ambayo hauyahitaji na huku siku zikisonga ukiomba lolote litokee muachane...
Mkuu ni yule wa tokea 2020 ama?
 
Ilishawahi nitokea,aseee mbona nilitafuta dawa,sio kwa kuganda kule hata umpige tukio gani ye yumo tu
Adela popote ulipo unisamehe, nakumbuka ulivyonipenda kwa dhati, nakumbuka ulivyolia mbele yangu kwa uchungu.

Nilijaribu kuwa muwazi kwako kuwa nikikubali tuwe na uhusiano nitakuumiza bure...kumbe nilitia petrol kiberiti...ulilia sana lkn haikubadili kitu.

Nimejifunza kuepuka mapenzi yakumhurumia mtu kwani ni matesi ya kesho.
 
Adela popote ulipo unisamehe, nakumbuka ulivyonipenda kwa dhati, nakumbuka ulivyolia mbele yangu kwa uchungu.

Nilijaribu kuwa muwazi kwako kuwa nikikubali tuwe na uhusiano nitakuumiza bure...kumbe nilitia petrol kiberiti...ulilia sana lkn haikubadili kitu.

Nimejifunza kuepuka mapenzi yakumhurumia mtu kwani ni matesi ya kesho.
Kaka mbona hapo mwishoni kama Kuna namna unapambana na karma
 
Back
Top Bottom