Kupigwa Marufuku Makanisa ya Kilokole, Gwajima amjibu mkuu wa mkoa wa Arusha, ni mtoto wa Dawa

Huyu mkuu wa mkoa ameyataka mwenyewe. Acha Gwajima amlipue.
 
Ni haki ya msingi kwa kila raia kuishi bila bugudha. Uhuru wa kuabudu usiwe kigezo cha kwenda kinyume na Sheria na Kanuni zinazomlinda mwananchi kutokana na Uchafuzi wa Mazingira ukijumuisha matumizi hatarishi ya sauti.
 
Ni haki ya msingi kwa kila raia kuishi bila bugudha. Uhuru wa kuabudu usiwe kigezo cha kwenda kinyume na Sheria na Kanuni zinazomlinda mwananchi kutokana na Uchafuzi wa Mazingira ukijumuisha matumizi hatarishi ya sauti.
Kila siku kuanzia saa 10 hadi 11 alfajiri kuna kelele za.adhana lakini kwa kujua ni hitaji la imani za watu hakuna anayejali. Kulikoni huyu mtoto wa dawa?
 
Awazuie na hawa waliouza kengele kila siku wanaita watu wa kuita
 
Amtake radhi au atutake radhi
 
dawa ni ndogo sana,mwambie arudishe family kijijini kwa mda hata miezi 6,kisha anunua vifaa vya mziki vile heavy duty,aanzishe kakanisa hapo kwake,ka masela kujumuika na kumwabudu jah raasfari na kupiga miziki ya akina alpha blondy usiku kucha.
Watajisoti wao wenyewe
 
Mbona unaandika kwa kuanza kila neno na herufi kubwa? Ndo swaga na kitambulisho chako hapa JF kama alivyokuwa Pdidy ama? Huchoki na kupoteza muda kubofya CAPS key mara kwa mara?

Samahani mkuu. I am just curious hasa ukizingatia kuwa we siyo mdot.com (kama hiyo picha ni yako na uko verified user). Otherwise all is well!
 
Kulinda uhuru wa kuabudu ni muhimu lakini ni vyema tulinde tusiingilie uhuru wa wengine. Uhuru wako unaishia pale wangu unapoanzia. Ni vyema tukajiwekea utaratibu wa misikiti, makanisa n.k vinapokuwa maeneo ya makazi tusikwazane. Leo mtu jirani yako anaokoka na kuanza kusali kwa Walokole then ndani ya miaka miwili anaamua kufungua kanisa lake ndani ya eneo lake anafunga spika kubwa ni mwendo wa mapambio na kukemea usiku kucha huku upande wa pili ni familia na watoto wadogo hawawezi kulala zaidi ya kushtuka muda wote. Ni jambo jema lakini lazima lifanywe kwa hekima.
 
yule ni kiongozi wetu watanzania sio arusha tu(muwakilishi wa rais), kumdhalilisha kwa maneno yasiyo na staha katukosea wote. Hatutake radhi.
mtumishi kateleza
Ukinikana mbele za watu namii ntakukana mbele za watu!!
Ivi hawa viongoz hawana washauri had wanakurupuka" hata kama alikua sahihi jinsi ya utoaji taarifa!!
Kwanza jina lake nani ili tujue tatizo lake
 
Napenda Hii Style Mkuu Na Nimeizoea So Sioni Tabu.
Kila Kitu Changu Hapo Bro Sioni Haja Ya Kuficha ID Yangu Na Picha Coz Am Not A Criminal Na Nipo Jf Kujadii Na Kujifunza.
Pia Kutumia Jina Na Picha Halisi Huleta Nidhamu, Hekima Na Busara, Huwezi Kumtusi Mtu Ama Kuandika Habari Za Kichochezi Badala Yake Utajikita Kuielimisha Jamii Na Kujiimisha Mwenyewe.
Tupo Pamoja Mkuu.
 
Sipo huko, tunazungumzia hoja ya Gwajima
 
Mtoto wa dawa ni mtoto wa kutengenezwa kwa mganga, hiyo hasikii wala haelewi, neno la MUNGU kwake ni moto, hataki hata kulisikia.
 
yule ni kiongozi wetu watanzania sio arusha tu(muwakilishi wa rais), kumdhalilisha kwa maneno yasiyo na staha katukosea wote. Hatutake radhi.
mtumishi kateleza
Na yule aliyedanganya Shinyanga akatimuliwa alitutaka radhi? Kiongozi akikosea arekebishwe, sema Lugha ya Gwajima hujaielewa. Viongoz wengine bila stail zao hawakusikii NG'O. kAMA KAZOEA KUROPOKA, ATAREKEBISHWA KWA STAILY ILEILE. Kiongozi ukitoa maamuzi yawe sawa kwa jamii yote usilalie upande mmoja. Kelele usiku wanaopiga wengi, weka muongozo kwa wote, HAPO NANI KATELEZA ATUTAKE RADHI
 
Mtoto wa dawa ni mtoto wa kutengenezwa kwa mganga, hiyo hasikii wala haelewi, neno la MUNGU kwake ni moto, hataki hata kulisikia.
lugha za dharau na kujikina kidini. hayo mambo mmemconsult na kuthibitisha hilo au mnatumia uhuru wa dini kupachikia viongozi sifa mlizokuwa nazo kabla ya wokovu
 
Kwani vilabu na mabaa na disko hazipigi kelele mbona ajapiga marufuku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…