Kupigwa Marufuku Makanisa ya Kilokole, Gwajima amjibu mkuu wa mkoa wa Arusha, ni mtoto wa Dawa

Kupigwa Marufuku Makanisa ya Kilokole, Gwajima amjibu mkuu wa mkoa wa Arusha, ni mtoto wa Dawa

We umeelewaje hiyo kauli? mie sikuona tatizo na kauli hiyo imejaa hekima.. MTOTO WA DAWA ina maana yake sema ufafanuzi wake tumeelewa tofauti; wenye hekima ya kimungu wameipata loud and clear. USINIULIZE MANA KWA MITAZAMO YETU TUTABISHANA MPAKA KESHO!!
kuna hekima gani kwa kiongozi wa dini kumuita kiongozi wa serikali(ambaye ni kiongozi wa watu wa dini zote na wasio na dini)JINI MTU?Ni hekma za kabila gani hizo kumuita kiongozi jini au mtoto wa dawa?Inawezekana kwamba amefanya utafiti na amejiridhisha kwamba ni mtoto wa dawa lakini sio hekima kumtangazia kila mtu,na kama anamtangaza kuwa ni mtoto wa dawa bila utafiti wowote hapo amekosea zaidi kwa principle ya "NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK"
 
Na yule aliyedanganya Shinyanga akatimuliwa alitutaka radhi? Kiongozi akikosea arekebishwe, sema Lugha ya Gwajima hujaielewa. Viongoz wengine bila stail zao hawakusikii NG'O. kAMA KAZOEA KUROPOKA, ATAREKEBISHWA KWA STAILY ILEILE. Kiongozi ukitoa maamuzi yawe sawa kwa jamii yote usilalie upande mmoja. Kelele usiku wanaopiga wengi, weka muongozo kwa wote, HAPO NANI KATELEZA ATUTAKE RADHI
Acha kuchanganya mambo kiongozi. Tunaemjadili hapa ni mtu anayejitambulisha kwa jamii kama kiongozi wa dini, mtu anayehamasisha maadili na tabia njema. Kwa nafasi yake hayuko sawa kabisa kuongea sentesi zenye viwango vya chini kabisa tena nyepesi za udhalilishaji na zisizozungukwa na busara. Maana tunaamini bibilia humbadilisha mtu na kuwa muungwana sio kwa utaratibu wa huyu. Ninasema na kwa nia njema kabisa
 
kuna hekima gani kwa kiongozi wa dini kumuita kiongozi wa serikali(ambaye ni kiongozi wa watu wa dini zote na wasio na dini)JINI MTU?Ni hekma za kabila gani hizo kumuita kiongozi jini au mtoto wa dawa?Inawezekana kwamba amefanya utafiti na amejiridhisha kwamba ni mtoto wa dawa lakini sio hekima kumtangazia kila mtu,na kama anamtangaza kuwa ni mtoto wa dawa bila utafiti wowote hapo amekosea zaidi kwa principle ya "NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK"
Kwa uzoefu wake Gwajima anafahamu kuwa ni shetani na watoto wake ndio wanapingana katika pilika za kufanya kazi za mungu. Sasa akatokea mtu akajiingiza kwenye 18 bila hata kuangalia na wengine atamuelewaje? Gwajima atamfananisha na nani? Hata hawa jamaa akimuita kiongozi flani Kafiri sababu tu mkristo, hiyo sawa
 
kwingineko duniani: Gwajima acha ubishi tanguliza busara
Pastor Gets Jail Time for Noisy Church
Gospel church fined because singing and preaching was too loud for neighbours
California Church Threatened With $500 Per Day Fine After Gospel Choir Accused of Excessive Noise — but They’re Fighting Back
Church Noise – Welcome to the Church of Noise
Is this Louisiana church's service too loud? Yes, authorities say
Oakland church gets warning after neighbors complain of choir noise
Lagos shuts religious houses, hotels over noise pollution
NEMC bado hawajatoa sheria ya kupambana na huu usumbufu, ila lazima itakuja na kunakuwa na maximum tolerable Volume kwa makanisa,night clubs,misikiti, viwanda,mikutano,matangazo ya barabarani na nje ya hapo unashtakiwa na kulipa faini au kufungwa.

inabidi kuwa na kiasi,
waislamu wanawaita wenzao waje kuswali sioni shida(ila kama wanakera pia wawemoderated). Mabar yapigwe marufuku au wawekewe limit ya sauti,
Kuhusu walokole inabidi wawe na kiasi, Kama unamuomba na kumsifu Mungu wako aliye sirini kuna haja gani ya kupaza sauti kwa wasiohusika. Tena saa nane usiku masaa kadhaa non stop.

Mkuu wa mkoa amekuwa biased kwa kusahau wapaza sauti wengine, hii haiwafanyi walokole wanaopiga kelele sana usiku kuwa na uhalali wa kuwazuia wananchi wengine wasilale. Hekima inahitajika. Sheria iwekwe yenye limit ya sauti. na ukivunja uwe ni mlokole,muislamu,disko,mdundiko mimi kama jirani nikushtaki unilipe fidia ya kunisumbua usiku nishindwe kupumzika kesho nifanye kazi kwa ufanisi offisini.

Pia bibilia inawataka watu wa dini kuwaheshimu viongozi wa serikali hata kama wanamapungufu. kumuita muwakilishi wa rais kwa kejeli mtoto wa dawa au kumfananisha na jini Mungu hakubaliani na udhaifu huo. Hapo mtumishi kateleza atutake radhi.
Hauna adabu,acha watu waabdu km wanavyo taka
 
Acha kuchanganya mambo kiongozi. Tunaemjadili hapa ni mtu anayejitambulisha kwa jamii kama kiongozi wa dini, mtu anayehamasisha maadili na tabia njema. Kwa nafasi yake hayuko sawa kabisa kuongea sentesi zenye viwango vya chini kabisa tena nyepesi za udhalilishaji na zisizozungukwa na busara. Maana tunaamini bibilia humbadilisha mtu na kuwa muungwana sio kwa utaratibu wa huyu. Ninasema na kwa nia njema kabisa
Na je kama kweli huyo mkuu katumika kama mototo wa dawa, kauli ya Gwajima ni sawa? angetumia njia ipi ili ujumbe ufike (waswahili wasema mwake mwake). Kuna msitari kwenye biblia unasema kuwa "mpumbavu utamjibu kutokana na upumbavu wake" (siukumbuki) vinginevyo hatakuelewa. Gwajima anapenda kutumia staili hiyo kuwajibu kwa jinsi anavyowaona hao. Nakumbuka namna alivyomuongelea speaker aliepita, DAA.
 
Kwa uzoefu wake Gwajima anafahamu kuwa ni shetani na watoto wake ndio wanapingana katika pilika za kufanya kazi za mungu. Sasa akatokea mtu akajiingiza kwenye 18 bila hata kuangalia na wengine atamuelewaje? Gwajima atamfananisha na nani? Hata hawa jamaa akimuita kiongozi flani Kafiri sababu tu mkristo, hiyo sawa
Iwapo kila mtu ataongea na public kwa mujibu wa uzoefu wake bila hata kupima matokeo ya kile anachoongea itakuwa vurugu,na matokeo ya kutenda kwa mujibu wa uzoefu mara nyingi ni kujikuta unajigonga kwenye sheria na kujeruhiwa.
Yako mambo ameyasema hapo naungana nae,mfano kabla ya kufika hatua hiyo zipo baa kwenye makazi ya watu zina usumbufu may be kuliko hayo makanisa,lakini kwa hili la kumuita binadamu mwenzio jini nadhani amepotoka.
 
Iwapo kila mtu ataongea na public kwa mujibu wa uzoefu wake bila hata kupima matokeo ya kile anachoongea itakuwa vurugu,na matokeo ya kutenda kwa mujibu wa uzoefu mara nyingi ni kujikuta unajigonga kwenye sheria na kujeruhiwa.
Yako mambo ameyasema hapo naungana nae,mfano kabla ya kufika hatua hiyo zipo baa kwenye makazi ya watu zina usumbufu may be kuliko hayo makanisa,lakini kwa hili la kumuita binadamu mwenzio jini nadhani amepotoka.
Kamuita mtoto wa dawa sio jini. ukimwambia ajitete atasema watenda zambi wote anawaita ni watoto wa shetani. Mkuu katenda zambi ya upendeleo, kaacha kule anakoshiriki kagusa kwingine.
 
Hauna adabu,acha watu waabdu km wanavyo taka
acha hisia na kupanic bila sababu, tunamwabudu Mungu kwa roho na Akili.
huko mtaani kuna wapagani,wasioamini Mungu,Watu wa kila aina. Hakuna mtu aliyemkataza mwenzake kusali.

Kama ushauri wa RC hukuuelewa fuata basi hata huu wa yesu.
mathayo 6:1-8
1wafaLME 19:11-13
1KORINTHO 14:33
 
Wakuu hapa suala la msingi ni Sauti hatarishi kutoka katika vyanzo tofauti tofauti. Je, tunatambua kuwa vyanzo vya sauti kwenye mazingira ya nje havitakiwi kutoa Sauti zaidi ya 60 hadi 65dB ?
 
Wewe acha ufala!

Yesu, mitume na manabii wake hawakuwa WANAFIKI kama wewe. Kwenye upumbavu walikemea viongozi au wenyewe kwa wenyewe tena kwa maneno makali.

Nitakupa MIFANO michache;

1. Wewe na YESU nani Mtakatifu?! Yesu aliuona UPUMBAVU wa Mfalme Herode, mtu mkubwa kwenye nchi alipozuia INJILI, na akamfananisha na MBWEHA.

"Akawaambia (Yesu), Nendeni, mkamwambie yule MBWEHA (Herode), Tazama, leo na kesho natoa pepo na kuponya wagonjwa, siku ya tatu nakamilika." - Luka 13:32

2. Wewe na Masihi wa Mungu, YEHU nani Mtakatifu?! Hakuona soni kumwambia ukweli Mfalme Yoramu juu ya UKAHABA wa kiroho wa mama yake aitwaye YEZEBELI.

"Ikawa, Yoramu alipomwona Yehu, akasema, Je! Ni amani, Yehu? Akajibu, Amani gani, maadamu UZINZI wa MAMA yako Yezebeli na uchawi wake ni mwingi?" - 2 Wafalme 9:22

Acha ufala, narudia tena. Umenikwaza, na mimi nimeamua kukupa za uso.

Mtu yeyote anayejifanya kuzuia kazi za Mungu, ni kama Mbweha tu.
Hahahaaaaa Mungu ana kazi ya ziada kama wamwabuduo ndo wako hivi..Mungu hufurahi kuabudiwa na wanyenyekevu...
 
Napenda Hii Style Mkuu Na Nimeizoea So Sioni Tabu.
Kila Kitu Changu Hapo Bro Sioni Haja Ya Kuficha ID Yangu Na Picha Coz Am Not A Criminal Na Nipo Jf Kujadii Na Kujifunza.
Pia Kutumia Jina Na Picha Halisi Huleta Nidhamu, Hekima Na Busara, Huwezi Kumtusi Mtu Ama Kuandika Habari Za Kichochezi Badala Yake Utajikita Kuielimisha Jamii Na Kujiimisha Mwenyewe.
Tupo Pamoja Mkuu.
Nimekupata mkuu. Tusonge mbele!
 
Mimi ni mkristo safi ila kuna baadhi ya makanisa yanaboa kwa kweli inabidi na Mkuu wa mkoa wa Mbeya naye atoe tamko.Kuna staff mwenzangu anaishi karibu na kanisa moja dogo yaani mbele ukumbi wa kanisa nyuma nyumba za kupanga.Wakianza kupiga kelele inabidi uondoke hadi wamalize.Mbona misikiti ipo hadi uswahilini lakini hii kero hakuna?
Wewe utakua mwislam una hide identity
 
Askofu Gwajima amesema aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo aliwakatalia walokole kufanya matamasha ya mkesha kwa madai kuwa wanapiga kelele.

Gwajima amesema Gambo ni " mtoto wa dawa" au Jini mtu nasi baada ya kusikia kufuru zake tulimlaani na kumshtaki mbele za Mungu wa mbinguni.

Maendeleo hayana vyama!
 
Back
Top Bottom