Kupima wanafunzi wa kidato cha pili kwa kutumia division ni kuharibu mfumo wa elimu

Kupima wanafunzi wa kidato cha pili kwa kutumia division ni kuharibu mfumo wa elimu

Kabla ya kufikia huku au sambamba na hili... Hivi kweli, wale wanafunzi wa "NguoKuchanika" unatungia na kuwafanyisha mtihani sawa na Feza au St. Francis ??
Kutunga mtihani mmoja sawa na hizo shule sio tatizo mkuu, maana wote wanatumia sylubas moja tatizo ni katika hizo shule za serikali walimu wameshajikatia tamaa kabisa
 
Hakuna wizara inayochezewaga kama elimu Tanzania. Yaani kila waziri akija, kila rais akija kila badiliko lolote la waziri hata kama ni wawili au watatu katika awamu moja ya miaka mitano au kumi anaweza au atakuja na mabadiliko yake, sera zake sijui hakunaga nwongozo wa elimu angalau wa miaka 10 au hata 20 huko.

Kila siku tume haziishi, kuna uhuni mwingi sana huko hadi kubadilisha masomo, mfumo wa ufaulu mitihani hiyo ,vitabu nk nk.halafu hao wanaobadilisha na kuuchezea mfumo wa elimu na wizara sasa wala hkuna hata mmoja ambaye mwanae anasoma katika shule hizo za serikali. Nasema tena hakuna awe rais, waziri sijui katibu wa hiyo wizara HAKUNA, wao wako saint saint academia huko international na kwenye curicullum za camridge huko ism ist na feza feza.

Sasa hiyo inaonyesha jinsi gani mfumo wetu ulivyotoboka na kudharaulika wao wapo kutengeneza sera za kuhesabu per diem na madawati. Kwa kuongezea pia ndio moja ya wizara inayoongoza kwa kujengwa na kubomolewa kama kuunganishwa na kutenganishwa na wizara ama idara nyingine.
So expect the unexpected.
Mkuu umenikumbusha kuwa tangu mwaka 2013 hadi sasa tumepitia mifumo mitatu ya kutunuku matokeo ya kidato cha nnerna kidato cha sita.
Kama unavyosema hapo juu kuwa tunatakiwa kuwa na mpango wa muda mrefu, inaweza saidia kunusuru hali hii
 
Hiyo Division 4:33 imekujaje ndugu?

Mkuu ipo hivi, mwanafunzi wa kidato cha pili ili awe na sifa za kuendelea na kidato cha tatu inampasa apate kuanzia division 1.7 hadi division 4.33 yaani wanatumia ule mfumo wa kidato cha nne ambapo anaekuwa na sifa za kupata cheti ni katika hayo madaraja
 
Kwa miaka kadhaa sasa baraza la mitihani ya taifa linatoa matokeo ya kidato cha pili kwa kutumia mfumo wa division tofauti na ule wa miaka ya nyuma wa wastani.Hii tasfiri yake kuwa mwanafunzi akiwa amepata D mbili na F saba au 9 basi anakuwa amefaulu kuendelea na kidato cha tatu na hatimae kuja kuhitimu kidato cha nne, tofauti na miaka ya nyuma ambapo mwanafunzi alitakiwa kupata walau wastani wa D ambayo ilikuwa ni wastani wa 30 ndipo aweze kuendelea na kidato cha tatu.

Sijui ni nani alishauri matumizi ya mfumo huu, kiukweli kuendelea kutumia mfumo huu ni kuandaa wanafunzi watakao kuja kupata division sifuri nyingi katika matokeo ya kidato cha nne, inawezekana vipi mwanafunzi apate D mbili na F zote maana yake anakuwa na division 4.33 akafanana na yule wa miaka ya nyuma aliyepata wastani wa 30? Nini chanzo cha matumizi ya division kwa mitihani ya kidato cha pili? au ndio mpango wa BIG RESULT NOW? au ni ni ile program ya EDUCATION FOR ALL iliyohasisiwa huko Indonesia iliyopelekea kuanzishwa kwa shule za kata?

Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda najua upo makini ni vyema sasa ukaanza na ili kwanza, hawa ni watoto wetu/wadogo zetu kuwapima kwa mfumo wa division ni kujidanganya sisi wenyewe ni heri wafaulu wachache ila matokeo yawe katika ubora unaotakiwa.Tusiogope wanafunzi kukariri madarasa kwa kuhofia kushuka kwa ufaulu wakati tunaharibu mfumo wa elimu kwa kuweka vitu visivyo hakisi maendeleo ya elimu.

Kuandika hapa haitoshi nitakupigia simu na kukuandika ujumbe mfupi Mh Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda na kukueleza hili ,najua fika mtalifanyia kazi.

#ElimuNiYetuSisi
Acha chuki na ufaulu wa watoto, kama unaona wanafaulu sana jua kuwa siku hizi materials ni mengi sana na walimu ni wengi wapo masuleni na wengine wapo mitaani so urahisi wa kufundishwa na kufaulu umeongezeka.

Tofauti na enzi zako ambapo walimu walikuwa adimu, materials za kufundishia na kujifunzia hayakuwepo ya kutosha.

Pia daraja D enzi hizo ilikuwa ni 20 sio 30.


Halafu kitaalamu ikiwa unatumia grade tofauti tofauti za upimaji utashindwa kujua uhalisia kama kiwango cha elimu kimekua au hakijakua so ilikuwa ni lazima kutumia kiwango kimoja cha grading system kwa wote, ndio maana kipindi flani walijaribu kutumia system ya chuo ya GPA,

Halafu, kama mtihani wa mwisho unamgrade mwanafunzi kwa division sasa ni ukichaa gani unakufanya utumie wastani kidato cha pili ikiwa mchujo wote tunaufanya kumuandaa mwanafunzi apate divisheni?
 
Kwa miaka kadhaa sasa baraza la mitihani ya taifa linatoa matokeo ya kidato cha pili kwa kutumia mfumo wa division tofauti na ule wa miaka ya nyuma wa wastani.Hii tasfiri yake kuwa mwanafunzi akiwa amepata D mbili na F saba au 9 basi anakuwa amefaulu kuendelea na kidato cha tatu na hatimae kuja kuhitimu kidato cha nne, tofauti na miaka ya nyuma ambapo mwanafunzi alitakiwa kupata walau wastani wa D ambayo ilikuwa ni wastani wa 30 ndipo aweze kuendelea na kidato cha tatu.

Sijui ni nani alishauri matumizi ya mfumo huu, kiukweli kuendelea kutumia mfumo huu ni kuandaa wanafunzi watakao kuja kupata division sifuri nyingi katika matokeo ya kidato cha nne, inawezekana vipi mwanafunzi apate D mbili na F zote maana yake anakuwa na division 4.33 akafanana na yule wa miaka ya nyuma aliyepata wastani wa 30? Nini chanzo cha matumizi ya division kwa mitihani ya kidato cha pili? au ndio mpango wa BIG RESULT NOW? au ni ni ile program ya EDUCATION FOR ALL iliyohasisiwa huko Indonesia iliyopelekea kuanzishwa kwa shule za kata?

Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda najua upo makini ni vyema sasa ukaanza na ili kwanza, hawa ni watoto wetu/wadogo zetu kuwapima kwa mfumo wa division ni kujidanganya sisi wenyewe ni heri wafaulu wachache ila matokeo yawe katika ubora unaotakiwa.Tusiogope wanafunzi kukariri madarasa kwa kuhofia kushuka kwa ufaulu wakati tunaharibu mfumo wa elimu kwa kuweka vitu visivyo hakisi maendeleo ya elimu.

Kuandika hapa haitoshi nitakupigia simu na kukuandika ujumbe mfupi Mh Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda na kukueleza hili ,najua fika mtalifanyia kazi.

#ElimuNiYetuSisi
Kwa miaka kadhaa sasa baraza la mitihani ya taifa linatoa matokeo ya kidato cha pili kwa kutumia mfumo wa division tofauti na ule wa miaka ya nyuma wa wastani.Hii tasfiri yake kuwa mwanafunzi akiwa amepata D mbili na F saba au 9 basi anakuwa amefaulu kuendelea na kidato cha tatu na hatimae kuja kuhitimu kidato cha nne, tofauti na miaka ya nyuma ambapo mwanafunzi alitakiwa kupata walau wastani wa D ambayo ilikuwa ni wastani wa 30 ndipo aweze kuendelea na kidato cha tatu.

Sijui ni nani alishauri matumizi ya mfumo huu, kiukweli kuendelea kutumia mfumo huu ni kuandaa wanafunzi watakao kuja kupata division sifuri nyingi katika matokeo ya kidato cha nne, inawezekana vipi mwanafunzi apate D mbili na F zote maana yake anakuwa na division 4.33 akafanana na yule wa miaka ya nyuma aliyepata wastani wa 30? Nini chanzo cha matumizi ya division kwa mitihani ya kidato cha pili? au ndio mpango wa BIG RESULT NOW? au ni ni ile program ya EDUCATION FOR ALL iliyohasisiwa huko Indonesia iliyopelekea kuanzishwa kwa shule za kata?

Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda najua upo makini ni vyema sasa ukaanza na ili kwanza, hawa ni watoto wetu/wadogo zetu kuwapima kwa mfumo wa division ni kujidanganya sisi wenyewe ni heri wafaulu wachache ila matokeo yawe katika ubora unaotakiwa.Tusiogope wanafunzi kukariri madarasa kwa kuhofia kushuka kwa ufaulu wakati tunaharibu mfumo wa elimu kwa kuweka vitu visivyo hakisi maendeleo ya elimu.

Kuandika hapa haitoshi nitakupigia simu na kukuandika ujumbe mfupi Mh Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda na kukueleza hili ,najua fika mtalifanyia kazi.

#ElimuNiYetuSisi
Ccm walishafeli zamani sana kwenye elimu.
 
Usiwe na wasi wasi likiharibika jambo tutarudia mfumo wa zamani
 
Acha chuki na ufaulu wa watoto, kama unaona wanafaulu sana jua kuwa siku hizi materials ni mengi sana na walimu ni wengi wapo masuleni na wengine wapo mitaani so urahisi wa kufundishwa na kufaulu umeongezeka.

Tofauti na enzi zako ambapo walimu walikuwa adimu, materials za kufundishia na kujifunzia hayakuwepo ya kutosha.
Form two kupata Division 4 ni kufaulu huko mkuu? mbona tunapenda kujidanganya
 
Back
Top Bottom