Kupima wanafunzi wa kidato cha pili kwa kutumia division ni kuharibu mfumo wa elimu

Kabla ya kufikia huku au sambamba na hili... Hivi kweli, wale wanafunzi wa "NguoKuchanika" unatungia na kuwafanyisha mtihani sawa na Feza au St. Francis ??
Kutunga mtihani mmoja sawa na hizo shule sio tatizo mkuu, maana wote wanatumia sylubas moja tatizo ni katika hizo shule za serikali walimu wameshajikatia tamaa kabisa
 
Mkuu umenikumbusha kuwa tangu mwaka 2013 hadi sasa tumepitia mifumo mitatu ya kutunuku matokeo ya kidato cha nnerna kidato cha sita.
Kama unavyosema hapo juu kuwa tunatakiwa kuwa na mpango wa muda mrefu, inaweza saidia kunusuru hali hii
 
Hiyo Division 4:33 imekujaje ndugu?

Mkuu ipo hivi, mwanafunzi wa kidato cha pili ili awe na sifa za kuendelea na kidato cha tatu inampasa apate kuanzia division 1.7 hadi division 4.33 yaani wanatumia ule mfumo wa kidato cha nne ambapo anaekuwa na sifa za kupata cheti ni katika hayo madaraja
 
Acha chuki na ufaulu wa watoto, kama unaona wanafaulu sana jua kuwa siku hizi materials ni mengi sana na walimu ni wengi wapo masuleni na wengine wapo mitaani so urahisi wa kufundishwa na kufaulu umeongezeka.

Tofauti na enzi zako ambapo walimu walikuwa adimu, materials za kufundishia na kujifunzia hayakuwepo ya kutosha.

Pia daraja D enzi hizo ilikuwa ni 20 sio 30.


Halafu kitaalamu ikiwa unatumia grade tofauti tofauti za upimaji utashindwa kujua uhalisia kama kiwango cha elimu kimekua au hakijakua so ilikuwa ni lazima kutumia kiwango kimoja cha grading system kwa wote, ndio maana kipindi flani walijaribu kutumia system ya chuo ya GPA,

Halafu, kama mtihani wa mwisho unamgrade mwanafunzi kwa division sasa ni ukichaa gani unakufanya utumie wastani kidato cha pili ikiwa mchujo wote tunaufanya kumuandaa mwanafunzi apate divisheni?
 
Ccm walishafeli zamani sana kwenye elimu.
 
Usiwe na wasi wasi likiharibika jambo tutarudia mfumo wa zamani
 
Form two kupata Division 4 ni kufaulu huko mkuu? mbona tunapenda kujidanganya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…