Kupinga Serikali Tatu; Natofautiana Na Profesa Issa Shivji...

Kupinga Serikali Tatu; Natofautiana Na Profesa Issa Shivji...

Maggid, nadhani utasikia rai yangu ya wewe kushiriki mijadala na si 'kutupa' kitu na kukimbia.

Kuna utata sana wa serikali 3. Aliyekuwa rais wa znz Aboud Jumbe alijiuzulu kwa sakata hilo.
Wznz waksema ameonewa.

G55 ilikuja na pendekezo hilo kama ilivyokuwa kwa tume ya Nyalali, Kisanga na Warioba(tume ya kwanza).CUF kina sera ya serikali 3. Profesa Shivji amekaririwa mara nyingi akitaka serikali 3.

Inashangaza wale waliokubali serikali 3 ndio hao hao wanaoonyesha mashaka nayo akiwemo Prof Shivji.

Prof Shivji ni mzanzibar na ametoa elimu ya znz katika muungano. Kama raia au msomi anayo haki ya kujiunga na taasisi kama maridhiano au Uamsho bila tatizo au kujificha.

Kisichopendeza ni kujificha nyuma ya uprofesa ili kuendeleza ajenda za akina Uamsho .
Hapa natofautiana naye sana na nabaki kumuheshimu sana.

Ukisoma mapendekezo yake, anasema mambo ya nje na uraia yasiwe ya muungano kama wanavyodai wale wa mkataba wa muungano.

Prof anashangaa kwanini Polisi lisiwe jambo la muungano wakati huo huo akitaka znz huru kama walivyo akina Maalim na Jussa.

Ukiondoa Uraia na uhamiaji hakuna serikali ya shirikisho. Rais wa shririkisho hawezi kuwepo kama hakuna raia na hapo Prof Shivji anaunga mkono hoja ya kuvunja muungano kiufundi.

Profesa anasema mapendekezo yaliyopo yatampa rais wa Tanganyika nguvu kubwa kwasababu ana eneo kubwa.Prof haelezi nguvu ya kiuchumi itakayotokana na mchango wa Tanganyika katika serikali kuu.
Kwamba kuwe na usawa hilo haliwezekani isipokuwa kama znz itakuwa na mchango sawa na Tanganyika.
''with great power comes responsibility''

Prof anasema wznz wengi wanataka mamalaka kamili. Juzi tu kulikuwa na kikao cha kamati ya kushughulikia kero za muungano chini ya Gharibu Bilal na Makamu wa pili wa rais Idd Seif alisema kuna.Ingawa sikubaliani na kamati hizi lakini kuna kitu kinachoonekana hapo.

Kinachoonekana ni kuwa wanaotaka mamlaka kamili ni wapemba ambao nadhani Prof Shivji ana sympathize nao kwa kusema ni wengi.
Lau isingekuwa hivyo akina Gharib na Idd Seif wangeungana na akina Jussa na Maalim kutaka mamlaka kamili.

Hofu ya profesa ni kuvunjika kwa muungano. Hapa amejificha tu katika usomi lakini ukweli ni kuwa hasimamii muungano.Znz imevunja katiba ya muungano mara zaidi ya 10, profesa hakuwahi kuonya kuwa kuna hatari ya kuvunja muungano.

Leo ujio wa Tanganyika anaona hatari hiyo! Ukimsoma vizuri profesa, anaunga hoja ya muungano wa mkataba lakini nafsi inamsuta

Ndugu yangu Kobelo, federation haiwezekani kwasababu znz inataka iwe znz kwa maana kuwa haitaki kutoa kuwa sehemu ya federation. Haikubali kupoteza utambulisho kama ilivyofanya Tanganyika.

Na mwisho wale wanaosema hawataki muungano wa serikali 3 inabidi waende mbali na kusema wanataka ipi?Wakisema mbili, je watawatendea haki Watanganyika.Wakisema moja je znz wapo tayari kutoa sehemu ya uhuru na mamlaka yao?

cc.JokaKuu, Jasusi, Mwanakjiji, Kichuguu, Mchambuzi
Nguruvi3, Nakubaliana nawe kwa baadhi ya hoja ulizozitowa kuhusu Muungano huu na nakubaliana nawe kuwa serikali tatu haziepukiki.
Kwanza nafikiri utakubaliana nami kuwa kushindwa kwa Jumbe na G55 hakuletwa na mtu mwengine yeyote bali Nyerere katika harakati zake za kunusuru kizawa chake (Muungano). Pia utakubaliana nami kuwa sababu za harakati hizi mbili zilikuwa tofauti kwani wakati Jumbe sababu yake ni kule kubaini kuwa alidanganywa na Nyerere kwa uchu wake (jumbe ) wa madaraka. G55 sababu zao zilikuwa ni kulipa dharau walionyeshwa na Salmin (Komandoo) na kauli yake ya "kutingisha kibiriti". ukiangalia sababu zote mbili hazikuwa na nguvu za wananchi, lakini hili la sasa ni kuwa wananchi wenyewe wameshabaini kuwa kunahitajika mabadiliko.
Kuhusu Issa Shivji na wasiwasi wake si chengine bali ni yaleyale ya maslaha binafsi, Shivji, CCM bara, CCM Zanzibar na wazanzibari wachache wenye kumiliki mali Bara wote wanaangalia maslaha yao binafsi. Shivji anaamini kuwa ameshajijenga Bara na anaogopa kuvunjika kwa Muungano ( anajuwa vilivyo kuwa mpaka sasa nia hasa ya muungano kwa upande mmoja( Bara) haipo. CCM bara wanajuwa kuwa kujitenga kwa Zanzibar kuna maana ya kupoteza madaraka na pia wagombeaji wa chaguzi wanajuwa kuwa watapoteza ngome muhimu katika harakati za kura za maoni (hasa wakijitangaza kuwa wanauinga mkono serikali 3, jambo litakalowakasirisha CCM zanzibar). CCM zanzibar wao masilahi yao ni kuwa fedha zote za uhai wao kichama zinatoka Bara hivyo kutofautisha serikali ni kuenda kwenye utengano (wanajuwa kuwa hakuna nia thabiti ya Muungano hivyo serikali mbili ni turufu. Na ukija kwa wenye mali kule Bara sababu zao ziko wazi na hofu yao Watanganyika wataamuaje ikiwa sasahivi kila wakati wako midomoni?
Sasa hili la kutumia nafasi na miundo mbinu ambayo itawafanya wananchi wazidi kuchanganyikiwa nsdio silaha yao makundi haya na hapo utapat sababu kwanini Shivji na wenziwe wanafanya wanachofanya.
 
Mkuu hapa nakupa salute

Unaposema serikali unamaanisha nini?? Kuna mpaka serikali za mtaa ambazo zina legislature (halmashauri), Executive (mayor) na Judiciary (mahakama za jiji). Hizi nazo ni serikali.

Dola!! .. kutakuwa na dola ngapi? Au nchi ngapi? .. Hapo ndiyo tunapokataa kuwa na nchi mbili zilizoungana, ambapo kila moja ina madaraka kamili.Na serikali ya muungano ambayo madaraka yake kikatiba hayashurutishi nchi shirikishi kuyafuata.\

Yaani ukiangalia mfano, unaweza kuona kuwa Zanzibar ina uwezo wa kufanya gerrymandering na kuanzisha wilaya mpya ishirini, just to balance or to even have more votes thAn Tanganyika.

Ni bora kuwe na federation ya Tanzania ambapo Tanganyika na Zanzibar ni states. Na federal legislature pamoja na Judiciary ziwe independent and above the laws of the states. The legislature needs to be bicameral with the senate evenly distributed among the member states.

Ila hii serikali ya Muungano waliyopendekeza hawa jamaa is Bogus to say the least.
 
Ndugu Majid swala la serikali tatu bado ni kizungumkuti kingine ambacho waZanzibar hawataki kusikia. Unajua wazenji wanataka kuona bendera yao ikipepea pale UN. Wanaamin maisha waliyonayo sasa hiv nimagum ukilinganisha kabla ya muungano, Lakin tujiulize tena kwa Tafakuri kubwa saana 1) Nani alimuua Karume na kwa nini 2) unadhani muungano ukivunjika Zanzibar itabaki kuwa Zanzibar ama itatokea Unguja na Pemba! 3) Ni kwa nn Kambarage aliutaka muungano kwa udi na uvumba na alilaani atakae uvunja???? 4) ni kwa nn baada ya kumfukuza sultani na zanzibar kupata uhuru yule mwanamapinduzi Okello alitimuliwa!. Tutafakari nadhani kuna jambo muhimu sana na sio hiz blah blah sijui garama sijui ujinga gani.. Mr Majid hebu fuatilia hata baadh ya hayo machache nadhan twaweza pata mwanga.

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Shivji anatumika kwa matakwa ya magamba.

Prof. Shivji nimemshangaa sana, sidhani kama yale ni maoni yake binafsi bila chembechembe za magamba. Hivi kama tukiungana na nchi ya tatu let say Kenya, serikali zitakuwa 3 kwa maana Zanzibar na Kenya watakuwa na za kwao, na ya Jamhuri?, Je tukiungana afrika mashariki yote serikali zitakuwa 5? yaani kila nchi itakuwa na serikali yake na ya Jamhuri isipokuwa Tanganyika! Huu utakuwa wendawazimu! Mi nadhani Prof. SHIVJI ni vizuri kustaafu kila kitu maan utaanza kuharibu sifa nzuri uliojijengea katika Jamii! SISI WANANCHI TUNATAKA SERIKALI TATU Jaji WARIOBA amekusanya na kuwasilisha mawazo yetu.
 
Prof. Shivji nimemshangaa sana, sidhani kama yale ni maoni yake binafsi bila chembechembe za magamba. Hivi kama tukiungana na nchi ya tatu let say Kenya, serikali zitakuwa 3 kwa maana Zanzibar na Kenya watakuwa na za kwao, na ya Jamhuri?, Je tukiungana afrika mashariki yote serikali zitakuwa 5? yaani kila nchi itakuwa na serikali yake na ya Jamhuri isipokuwa Tanganyika! Huu utakuwa wendawazimu! Mi nadhani Prof. SHIVJI ni vizuri kustaafu kila kitu maan utaanza kuharibu sifa nzuri uliojijengea katika Jamii! SISI WANANCHI TUNATAKA SERIKALI TATU Jaji WARIOBA amekusanya na kuwasilisha mawazo yetu.

Serekali tatu labda ni maoni ya wananchi wa tanganyika,huku zanzbr maoni yetu ni mamlaka kamili ya z'br ikifuatiwa na muungano wa mkataba,kinyume na hapo kaunganeni na kenya.
 
Kwa yeyote aliesoma rasimu kwa nia safi akaielewa utakubali kabisa kuwa Serikali tatu hazikwepeki. Sababu iko wazi kabisa kuwa hatuna Muungano bali tuna ushirikisho la mambo 12 ya nchi 2. mambo mengine yooooote kila nchi kivyake. Sasa huwezi ukasema serikali ya moja isimamie mambo hayo 12 na ya nchi mojawapo, halafu nyingine ijisimamie yenyewe kwenye mambo yake. Hii inchi inayojisimamia lazima itaona kuna fursa ambazo huyu anaesimamiwa na Muungano anazipata chini ya kapeti kidhuluma dhuluma, na inakuwa sio rahisi kuisimamia hiyo serikali maana mipaka ya kiutendaji haieleweki. Kwa hiyo moja futa Zanzibar ibakie serikali moja [Muungano uvunjike papo hapo] kitu ambacho bara hawawezi kuthubutu kufanya au Serikali tatu, ili serikali ya SHIRIKISHO aka Muungano iweze kuwa wazi na kudhibitiwa na hizo za nchi shirika. CCM haitaki serikali tatu lakini Rais anataka ndio maana ametoka Baraka tuendelee na mjadala sasa kazi kwao, kimewageukia wakawashawishi wananchi wapige kura ya hapana.
 
Tukimaliza serikali tatu tunaanza mchakato wa Sera ya Majimbo, watakoma mwaka huu
 
Kwa maneno yako haya unakosea.....Shivji huwa hapelekeshwi na huongea kile anachoamini yeye na haya ni mawazo yake siku zote...
Fuatilia kongamano la Kwanza akitoa hotuba kuhusu Katiba mpya na kwa nini katiba mpya.....maoni yake kuhusu muungano yalikuwa ni hayo hayo....
Tunaweza kumpinga sio kosa....ila kuwa na serikali tatu ni ngumu kiutendaji kwa serikali ya muungano!
SI kweli kwamba hapelekeshwi, ni kibaraka mzuri wa mtazamo wa mwalimu Nyerere wakati hata chama alichokiasisi yeye (Mwalimu) kimebadilika.
 
Prof kivyake yeye huwa anaongea tu anayaacha hakuna mbadala wake tumemzoea, siku hizi hata makala zake na matamko yake na michango yake naona ipite tu
 
Serekali tatu labda ni maoni ya wananchi wa tanganyika,huku zanzbr maoni yetu ni mamlaka kamili ya z'br ikifuatiwa na muungano wa mkataba,kinyume na hapo kaunganeni na kenya.

Tupige kura, ninyi mko wangapi na sisi Bara tuko wangapi. hamuwezi kuunga mkono Serikali tatu kwa sababu na ninyi itabidi mchangie kwenye serikali kuu ya shirikisho, siyo kama sasa hivi mnakula vya ubwete toka Serikali ya Jamhuri.

Vinginevyo, LIWALO NA LIWE kwani tunanufaika na nini toka Zanzibar? Kila mtua ashike kipande chake atambaye kwani wasio ungana kama Kenya, Uganda, Rwanda, Msumbiji, Malawi nk. tunawazidi nini zaidi ya ufisadi na uroho wa madaraka?
 
Sijui kama Majid alimuelewa Prof. Shivji. Prof hakupinga serekali tatu, alichokiongelea mwanzo mpaka mwisho ni haja ya kuipa mamlaka zaidi katiba ya serekali ya muungano basi
 
Usisahau kuwa wapo wahamiaji kule Zenji wakitoka Tanganyika, sasa status yao iwe vipi?
Ngekewa,

..wa-Znz ndiyo wenye mamlaka ya kuamua watafanya nini na wa-Tgk waliohamia huko.

..pia napendekeza wa-Znz wapewe ukaazi hata kama Zanzibar itaamua kuwarudisha makwao wa-Tanganyika walioko huko.

..mimi kwa upande wangu nadhani tukiweza kuli-handle vizuri, kwa ustaarabu na upendo, suala la wa-Znz walioko huku Tanganyika, then we will be fine moving forward.

..wengi wanazungumzia masuala ya Yugoslavia, Serbia, Bosnia, lakini tunaweza kujiepusha na yaliyotokea huko kama tutayashughulikia matatizo yetu mapema kabla hayajageuka kuwa uhasama wa waziwazi.

cc: Kubwajinga, Kibunango, Nguruvi3, Jasusi, GHIBUU, Foum Jnr, maggid
 
Last edited by a moderator:
Ngekewa,

..wa-Znz ndiyo wenye mamlaka ya kuamua watafanya nini na wa-Tgk waliohamia huko.

..pia napendekeza wa-Znz wapewe ukaazi hata kama Zanzibar itaamua kuwarudisha makwao wa-Tanganyika walioko huko.

..mimi kwa upande wangu nadhani tukiweza kuli-handle vizuri, kwa ustaarabu na upendo, suala la wa-Znz walioko huku Tanganyika, then we will be fine moving forward.

..wengi wanazungumzia masuala ya Yugoslavia, Serbia, Bosnia, lakini tunaweza kujiepusha na yaliyotokea huko kama tutayashughulikia matatizo yetu mapema kabla hayajageuka kuwa uhasama wa waziwazi.

cc: Kubwajinga, Kibunango, Nguruvi3, Jasusi, GHIBUU, Foum Jnr, maggid

Mbona sifikiri kuwa wananchi wana matatizo kwa mtu anaefuata taratibu na mwenendo wa wenzake waliowakuta.
Wazanzibari hawajawahi kuwa na matatizo na wenzao wa Bara kiasi kwamba uzalendo wa kizanzibari unajengeka miongoni mwa wahamiaji kutoka nje ya Zanzibar. Tatizo la kubaguwana mara zote unaletwa na viongozi wanapotumia uzawa kwa maslaha yao.

Kwa mfano wazanzibari walikuwa ndio wahudumiaji wa shughuli za kibiashara kwenye miji mingi Bara kabla ya wenyeji kuamuwa kufanya shughuli hizo baada ya kuona mafanikio ya wageni.Hali kadhalika kuja kwa wamachinga Zanzibar kumerahisisha shughuli nyingi ndogo ndogo zanzibar. Tatizo linakuja pale tabaka la viongozi linapowatumia wananchi kwa maslahi yao.
 
Rodrick Alexander, gharama gani za zaidi? Kwani hizo shughuli zilizopendekezwa ziwe za muungano hivi sasa hazigharamiwi hata iwe gharama mpya? Halafu unaposema serikali tatu kwani hujuwi kuwa kule zanzibar wanajihudumia serikali yao? Hili watu wengi hawalioni wanachoona kuwa Watanganyika sasa watalazimika kujigharimia kwenye serikali yao. hivyo Serikali ya watanganyika wenyewe hawako tayari kuigharamia?
zanzibar wana eneo la ukubwa karibu sqm 2000 sawa na mji wa kahama tanzania bara wana eneo la ukubwa wa sqm karibu 800000 juzi juzi watu wameshituka kusikia mafao wanayolipwa viongozi wastaafu bado kuna gharama za uendeshaji wa serikali ambayo ni kiasi kidogo cha bajetikinatengwa kwa shuguri za maendeleo huku sehemu kubwa ikienda kwenye kulipa mishahara na gharama nyingine za kuendesha serikali ni heri tuvunje muungano kuliko kung'ang'ania muungano ambao unatutia umasikini nafikiri hili kenyata aliliona mapema ndio maana akakataa muungano
 
Serikali 3 jawabu tutapata serika mbili huru, Zanzibar huru na Tanganyika huru.
 
Kweli watanganyika mnapenda vya bure,mmezoea mawaziri wa muungano kuwafanya ndio hao hao watanganyika,mpango wa sasa ni kuwa kila moja ahudumie mawaziri wake na kila kitu chake,zanzbr ina kila kitu chake kwanini nyie muone taabu kuwa na vyenu?tukutane EAC na UN,zanzbr kwanza.
 
Tupige kura, ninyi mko wangapi na sisi Bara tuko wangapi. hamuwezi kuunga mkono Serikali tatu kwa sababu na ninyi itabidi mchangie kwenye serikali kuu ya shirikisho, siyo kama sasa hivi mnakula vya ubwete toka Serikali ya Jamhuri.

Vinginevyo, LIWALO NA LIWE kwani tunanufaika na nini toka Zanzibar? Kila mtua ashike kipande chake atambaye kwani wasio ungana kama Kenya, Uganda, Rwanda, Msumbiji, Malawi nk. tunawazidi nini zaidi ya ufisadi na uroho wa madaraka?

Mupige kura nyie kama nani?watanzania au watanganyika?rujisha tanganyika yako kwanza (kama una ubavu huo)ndipo uropokwe.
 
zanzibar wana eneo la ukubwa karibu sqm 2000 sawa na mji wa kahama tanzania bara wana eneo la ukubwa wa sqm karibu 800000 juzi juzi watu wameshituka kusikia mafao wanayolipwa viongozi wastaafu bado kuna gharama za uendeshaji wa serikali ambayo ni kiasi kidogo cha bajetikinatengwa kwa shuguri za maendeleo huku sehemu kubwa ikienda kwenye kulipa mishahara na gharama nyingine za kuendesha serikali ni heri tuvunje muungano kuliko kung'ang'ania muungano ambao unatutia umasikini nafikiri hili kenyata aliliona mapema ndio maana akakataa muungano

Kumiliki kitu kuna gharama na iwapo mnataka kuimilik Zanzibar basi msijali gharama. Nakubaliana nawe kuwa hiyo haja ya muungano hasa haipo hasa ilivyokuwa Tanganyika wameshagunduwa mafuta yao!
 
Back
Top Bottom