Kupitia mafanikio ya Diamond Platnumz nimegundua Watanzania wengi wana roho mbaya

Kupitia mafanikio ya Diamond Platnumz nimegundua Watanzania wengi wana roho mbaya

Youngblood

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2014
Posts
19,433
Reaction score
56,810
Habari zenu,

Kwakweli kama wote mnavyojua kijana Diamond Platnumz ni moja ya vijana wapambanaji sana katika nchi hii,ni wale vijana waliotoka from the bottom huko chini kabisa na wakafanikiwa kupata mafanikio makubwa kutokana na juhudi binafsi.

Kinachonishangaza sasa ni trend kubwa ya Watanzania hasa vijana kumchukia huyu ndugu yetu hata bila sababu za maana kabisa badala ya kujifunza kutoka kwake.

Mbaya zaidi Watanzania tumejikita kumfanya ashuke pale alipo au aonekane hana chochote wala lolote, ukipita mitandaoni huko huoni hata wanaompongeza kwa mafanikio yake, wengi utaona wanapambana kumshusha inasikitisha sana, nakumbuka hata mimi mwenyewe kuna kipindi mkumbo huo ulinipitia kutokana na habari za mitandaoni, lakini nikagundua ni majungu tu.

Vijana wa Kitanzania tuache Majungu na fitina tuchape kazi, umbea hauna posho, hatuwezi kufanikiwa kwa kipiga majungu bila kupambana.

Asanteni.
 
Youngblood naomba niseme haya machache

Mti wenye matunda ndio hupopolewa mawe. Kuchukiwa ni ada ya mwanadamu. Hapa duniani kila kitu kina uwili! Kukiwa na wanaokupenda basi wanaokuchukia hawakosekani, kukiwa na wanaokusifia basi wanaokukosoa hawakosekani pia.

Watu duniani kote hufurahia mabaya ya mtu kuliko mafanikio yake na ndio maana habari mbaya za watu huvuma kwa kishindo kuliko habari zake nzuri.

Diamond kijana asiye na elimu lakini mwenye mafanikio makubwa naye ana mapungufu yake..hakuna mkamilifu la hata mmoja chini ya jua.

Chuki kubwa kwa Diamond ukiachana na ile ya wivu wa wasanii wenzake na vijana washindwa wengine. Imekolezwa na yeye kuambatana na KAYAFA. Mtu aliyetajwa kwa ukatili upendeleo na roho mbaya! Kumbuka ukiwa karibu na waridi nawe utanukia lakini pia ukiwa karibu na harufu mbaya nawe utanuka!

Uzuri wa Diamond anajitambua nakuitambua nafasi yake katika jamii hivyo hazipi nafasi chuki zinazomuandama kwa namna zote.. Ukimya ni silaha maridadi sana kwa haters. Kamwe usijaribu kujibishana na hater kwakuwa hiyo ndio nafasi pekee anayoitafuta kukuumiza na kupunguza machungu yake, mnyamazie azidi kuumia.

DIAMONDS ARE FOREVER!
 
Nikiwa tajiri nikaa kimya na utajiri wangu na watu wakaona pia na juhudi zangu za kutafuta sidhani kama kuna mtu atanichukia au kuhangaika kunishusha ila tatizo litakuja pale nitakapo anza kujigamba Nakuanza kusema hapa "Hakuna Mwana JF tajiri kama mimi"
 
Ilikuwa muhimu kujiuliza kama ni huyu tu aliyefanikiwa Tanzania? Kwanini kumekuwa na kampeni zenye mwelekeo wa kumchukia? Kwani wanaoendesha kampeni hizo hawajadadavua sababu hata moja?

Wapumzike kwa amani akina Ben, Azory, Mawazo, wa kwenye viroba nk. Kweli magu alikuwa baba lao!
 
@Youngblood naomba niseme haya machache

Mti wenye matunda ndio hupopolewa mawe. Kuchukiwa ni ada ya mwanadamu. Hapa duniani kila kitu kina uwili! Kukiwa na wanaokupenda basi wanaokuchukia hawakosekani..kukiwa na wanaokusifia basi wanaokukosoa hawakosekani pia...
Maneno mazuri kabisa
 
Nikiwa tajiri nikaa kimya na utajiri wangu na watu wakaona pia na juhudi zangu za kutafuta sidhani kama kuna mtu atanichukia au kuhangaika kunishusha ila tatizo litakuja pale nitakapo anza kujigamba Nakuanza kusema hapa "Hakuna Mwana JF tajiri kama mimi"
Kabisa
 
Siyo Almasi wako tu anayechukiwa; mafanikio yoyote, hata tu zile process za mafanikio kabla ya mafanikio yenyewe, huchukiwa sana na both vichochole na vibosire. This is the nature of a corrupted human soul. Until watu wagundue hawakuja na kitu chochote hapa duniani, na kwamba hawataondoka na kitu chochote, hii hali ya kuhodhi mali na hulka ya materialism na capitalism na struggle of the fittest vitaendelea kwa kasi ya ajabu na kushamiri na kuhamiri mioyoni mwa wanadamu hadi pale atakapokuja tena Fundi Seremala ili kufanya usafi wa mwisho wa haki duniani.
 
Back
Top Bottom