Kura ya Maoni: Muundo upi wa Muungano unafaa?

Kura ya Maoni: Muundo upi wa Muungano unafaa?

Muundo upi wa Muungano unafaa?

  • Serikali 1

    Votes: 81 23.3%
  • Serikali 2

    Votes: 22 6.3%
  • Serikali 3

    Votes: 241 69.5%
  • Sijui

    Votes: 3 0.9%

  • Total voters
    347
  • Poll closed .
Serikali 3 ndiyo mpango mzima.... Mimi nashangaa CCM wanampango gani na WaTanganyika. Serikali Mbili ni Kichaka cha kugawana vyeo na Kuuza hovyo Resources za Tanganyika kwa Mgongo wa Muungano.

Hata Hivyo kama JK amemaliza Miaka yake miwili ama akiwa Angani au Nchifulani maana yake ni kwamba hatuna Rais wa kuhangaika na Mambo yetu watanganyika.

Ni mara ngapi maamuzi mazito yakawa yanasuburi ama Rais atue au Arejee kutoka nje? Je kwa nini tusiwe na Rais wa kufanya majukumu ya Tanganyika...
 
Hii serikali mbili stein pale nyumbani kwako zinafaida gain? Au mradi amesema kama na haturuhusiwe kumpinga ata bila kujali yeye anatafuta ulaji nyumbani kwakwe
 
Buchanan nakusikitia bure, hujui kwa nini bunge la katiba Limekaa Dodoma??
Kazi yake ni kutunga katiba mpya, zote ni process!!
Katiba ya kale ni kuu kuu, Serikali tatu ni jibu pande zote, wala muungano hauvunjiki!!
 
Last edited by a moderator:
serikali moja ile ambayo Zitto ameidadavua!
 
Ongeza mamba 4 kwa wasiotaka muungano.

Mkuu, mimi naona tatizo hapa ni neno muungano. Tutowe muungano tuweke ushirikiano, maana nchi jirani hatujaungana ila tunashirikiana. Hakuna Mtanzania anayezuiwa kwenda kenya, uganda, Zambia nk. nchi hizi zote hakuna malalamiko kwa sababu tunashirikiana tu. Hata Wachina wamejaa TZ ila hatujaungana. Kwa hiyo kukata mzizi wa fitina neno muungano 'toa'.
 
Serikali 2 ndo mpango mzima! Tukiendekeza 3 Serikali ya Muungano itakuwa haina hata ardhi (ardhi si suala la Muungano) na itakuwa ombaomba kwa nchi washirika kwa kuwa haina vyanzo vya mapato vya kwake!

Zikiwa mbili ziwe zanzibar na Tanganyika. Nchi 2 majirani wema...
 
serikal tatu kwan zenj hawapo tayar serkal moja hivyo watanganyika tumekandamizwa kwa kipindi kirefu bila ya kuwa na serikal inayotutetea
 
Hivi kero za Muungano zinazozungumzwa hapa kwa mwenye elimu ndogo km yangu Naomba kuelimishwa na nielimishwe pia kubadilika kwa namba za serikali toka 2 kwenda 3 kutazitatua vipi. Naomba viingereza msiweke wasomi Tafadhali.
 
WanaJF Kwa mda mrefu sasa kuelekea utungaji wa katiba mpya kumekuwa na mjadala mkali kuhusu muungano wetu uwe wa muundo upi sasa ningependekeza tuwe na kura ya maoni hapa JF kuhusu muundo wa muungano, upi ni muundo sahihi?

1.Serikali moja.
2. Serikali mbili.
3.Serikali tatu.


N:B ukiweza kutoa sababu za muundo wa muungano unaoutaka itakuwa vizuri zaidi

Moja tu
 
ili kujua muundo gani ni sahihi turudi kwenye asili ya muungano huu tulionao.
Muungano huu umepatikana kwa kuunganisha nchi mbili:

  1. Jamhuri ya watu Zanzibar
  2. Jamhuri ya Tanganyika
kabla ya tarehe 26 April 1964 kulikua na serikali Mbili nazo ni :
  1. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
  2. Serikali ya Tanganyika

na baada ya tarahe 26 April 1964 Takawa na Nchi mbili( kwa mujibu wa katiba zote za znz na Muungano)nazo ni
  1. Zanzibar
  2. Tanzania
ukiangalia kwa makini utaona Tanganyika ni kama imebadilsha jina na kuwa Tanzania.lakini baada ya muungano nchi zimebaki mbili na serikali mbili.
kili chobadilika ni Serikali ya Tanzania kuchukua baadhi ya mambo ya upande wa zanzibar kuwa chini ya himaya yake,mfano :
  1. anga
  2. mambo ya nje
  3. mambo ya ndani
  4. elimu ya juu
  5. ulinzi
  6. posta nk
mambo mengine yaliyobaki bado yapo ndani ya serikali ya mapinduzi:
  1. kilimo
  2. uvuvi
  3. maji
  4. barabara
  5. umeme
  6. michezo n.k
ukiangalia kwa makini utaona muundo huu kuhalisia hakuna muungano....kwani serikali zimebaki mbili na ile ya mapinduzi ipo pale pale.Tanganyika wao wamebadili jina na kujinyakulia mambo fulani ya zanzibar.
hapa hakuna muungano kuna kubabaisha...
nchi mbili zikiungana kunakua na mambo mawili yanatokea:
  • zinaungana nchi na serikali zao na kufanya serikali na nchi moja tu yaani union au muungano.
  • au zinaungana na kutengeneza federation system of goverment , hapa kunakuwa na

  1. Serikali kuu itayo simamia mambo mnayo kubaliana
  2. kunakua na serikali za state zinazofanya federation.
serikali kuu inakua na turufu juu ya mambo ya states.
kwa vile inaonekana zanzibar ni wazi haako tayari kupoteza utaifa wao basi option iliyopo ni kufanya federation.
kila state itasimamia shughuli zake za uchumi...kutkana na vyanzo visivyo ndani ya federal control
mjii mkuu wa federation unaweza kuwa ni Dar es salaam au Zanziabr. Na mjii mkuu wa Tanganyika ukawa Dodoma.
 
Methali: KILA PENYE ZANZIBAR PANA TANGANYIKA - Aidha kiwaziwazi au kiwiziwizi.
 
umetunyanyapaa sie tusioupenda huu muungano.
Mimi binafsi siupendi huu muungano jinsi ulivyo na ningependa kuona unavunjwa halafu mchakato wa muungano kama ulazima utakuwepo uanze upya.
 
Serikali 3 ndo mpango mzima!
WanaJF , upi ni muundo sahihi?
1.Serikali moja.
2. Serikali mbili.
3.Serikali tatu.
4. Sujui
6.Zanzibar iwe Nchi Huru
N:B ukiweza kutoa sababu za muundo wa muungano unaoutaka itakuwa vizuri zaidi

Hebu iacheni Zanzibar iwe Nchi Huru kwa nini Tusiungane na Burundi Malawi au Rwanda
Zanzibar wameshatukataa iwe Inchi 1 iwa Inchi 2 iwa Inchi 3 hata futi 900 hawataki wanachotaka ni NCHI YAO
Ujerumani mashariki na Ujerumani Magharibi walitengana sembuse RUSSIA na bado Korea Kaskazini na Kusini
tanganyuka turidhike na hata ninyi Wabunge wa BUNGE LA KATIBA wapeni kisiwa chao chokochoko zitaisha
 
ili kujua muundo gani ni sahihi turudi kwenye asili ya muungano huu tulionao.
Muungano huu umepatikana kwa kuunganisha nchi mbili:

  1. Jamhuri ya watu Zanzibar
  2. Jamhuri ya Tanganyika
kabla ya tarehe 26 April 1964 kulikua na serikali Mbili nazo ni :
  1. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
  2. Serikali ya Tanganyika

na baada ya tarahe 26 April 1964 Takawa na Nchi mbili( kwa mujibu wa katiba zote za znz na Muungano)nazo ni

  1. Zanzibar
  2. Tanzania
ukiangalia kwa makini utaona Tanganyika ni kama imebadilsha jina na kuwa Tanzania.lakini baada ya muungano nchi zimebaki mbili na serikali mbili.
kili chobadilika ni Serikali ya Tanzania kuchukua baadhi ya mambo ya upande wa zanzibar kuwa chini ya himaya yake,mfano :
  1. anga
  2. mambo ya nje
  3. mambo ya ndani
  4. elimu ya juu
  5. ulinzi
  6. posta nk
mambo mengine yaliyobaki bado yapo ndani ya serikali ya mapinduzi:
  1. kilimo
  2. uvuvi
  3. maji
  4. barabara
  5. umeme
  6. michezo n.k
ukiangalia kwa makini utaona muundo huu kuhalisia hakuna muungano....kwani serikali zimebaki mbili na ile ya mapinduzi ipo pale pale.Tanganyika wao wamebadili jina na kujinyakulia mambo fulani ya zanzibar.
hapa hakuna muungano kuna kubabaisha...
nchi mbili zikiungana kunakua na mambo mawili yanatokea:
  • zinaungana nchi na serikali zao na kufanya serikali na nchi moja tu yaani union au muungano.
  • au zinaungana na kutengeneza federation system of goverment , hapa kunakuwa na

  1. Serikali kuu itayo simamia mambo mnayo kubaliana
  2. kunakua na serikali za state zinazofanya federation.
serikali kuu inakua na turufu juu ya mambo ya states.
kwa vile inaonekana zanzibar ni wazi haako tayari kupoteza utaifa wao basi option iliyopo ni kufanya federation.
kila state itasimamia shughuli zake za uchumi...kutkana na vyanzo visivyo ndani ya federal control
mjii mkuu wa federation unaweza kuwa ni Dar es salaam au Zanziabr. Na mjii mkuu wa Tanganyika ukawa Dodoma.

Hapo kwenye red mkuu patamu kweli zimeungana nchi eti baada ya muungano bado tuna nchi mbili tena
 
Kwa mfano mambo ya serikali mbili ni shida sana Katiba ya zanzibar ya mwaka 1984 ilipobadilishwa hii ya Tanzania ambayo hiyo hiyo inaitwa ya Tanzania bara/Tanganyika yenyewe haikubadilishwa matokeo yake Hadi sasa Katiba ya Tanzania inamtambua waziri kiongozi huku katiba ya Zanziba ikiwa haimtambui Kufuta huu mkanganyiko bora tuwe na Serikali moja tu

SEHEMU YA PILI
BARAZA LA MAPINDUZI LA ZANZIBAR

Ibara ya 105.

Ibara ndogo ya (1),
Kutakuwa na Baraza la Mapinduzi la Zanzibar litakalokuwa na wajumbe wafuatao:
(a) Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi;
(b) Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;
(c) Mawaziri wote wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;
(d) Wajumbe wengine watakaoteuliwa na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa mujibu wa masharti ya Katiba ya Zanzibar.

Ibara ndogo ya (2),
Bila ya kuyaingilia madaraka ya Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kama kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Baraza la Mapinduzi litakuwa ndicho chombo kikuu cha kumshauri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya mambo yote yanayohusika na utekelezaji wa madaraka yake ya uongozi na usimamizi wa shughuli za Serikali ya Zanzibar na pia utekelezaji wa madaraka yake juu ya shughuli zote za Serikali kuhusu mambo yote yasiyo mambo ya Muungano, kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii na yale ya Katiba ya Zanizbar.
Huu ni mfano tu
 
Mimi hapa pamoja na viungo vyangu vyote nachagua serikali tatu!nimechoshwa sana na muungano hauna faida.tena ikibidi wazanzibari wote warudi kisiwani kwao watuachie Tanganyika yetu!
 
Back
Top Bottom