Kurudi kwa UDA (daladala) hii maana yake nini?

Kurudi kwa UDA (daladala) hii maana yake nini?

Haya mabasi/daladala za UDA yalianza onekana kwa wingi sana kipindi cha uongozi wa Awamu ya 4 ila baada ya kuingia awamu ya 5 hizi daladala zilipotea zote moja baada ya nyingine na mwisho hatukuziona tena barabarani.

Tangu msiba uishe wa Aliyekua Rais awamu ya 5 Rais.Magufuli UDA zimeanza kurudi barabarani nimeshashuhudia UDA 3 mpya ruti ya MBEZI - MBAGALA/3, MBEZI-BUGURUNI,MBEZI-TEMEKE,nk

swali langu ni la mshangao,imekuaje tena haya magari kurudi wakati huuu? yalikua wapi? boss wake ni nani? kwanini alikua hayarudishi barabarani kipindi cha uhai wa magufuli na kwanini kayarudsha sasa hivi?

"Watanzania sisi sio wajinga,Tunaona"

Nimalizie kwa kusema "Anae stream youtube sasa hivi ni kidume", Ukimuona mtu yuko Online Muheshimu,Ma group yangu sioni cha admin wala member anatuma tuma vi meme leo ni kimyaaaaaa,WAZIRI WA NCHI MWANACHAMA WA DATA amejua kututembelea huu mwaka,halafu ndio kwanza April 2..

Kwani wewe unapata hasara ama faida gani yakifanya au yasipofanya kazi!?
Mengi ya mambo ambayo wananchi wanaona ni ya kifisadi wala hata hamna kikubwa kinachoweza kufanywa kikabadili sana maisha yao!
Hata hizo barabara n.k kuna janja nyingi ndani yake...
 
tusirudishane shule braza,hujawahi hata nilipia tuition
Mh hayati JPM aliamini kwenye STATE CONTROLED ECONOMY ndio maana hata mashirika ya ndege yaliwekewa vigingi, ruti za mabasi pia nyingi uliona hazikupewa trip za Kariakoo nk, aliamini sana kuwa serikali ikontroo kila kitu hali iliyopelekea uchumi mbovu. Hata tenda za ujenzi walipewa sana JKT ambao infact ni cheap labor tu. Ukiangila hii ERA ya mama SAMIA kama ameanza kurudisha hali ambayo inapaswa kufatwa na NCHI.
 
na kwa kurudi kwa UDA ndio JIPU litaendelea kukwiva maana naona kabisa namna ambavyo UDA wataanzisha ruti za K.koo - Mbezi na hakuna trafik ataeuliza wala kuzikamata hizo dala dala,hatima ya MWENDOKASI siijui ni ipi kwakweli

Tena itakuwa poa sana! Mwendokasi wanazingua sana, unakaa kituoni lisaa lizima zinapita bila kusimama na hazina abiria eti zipo sijui off service!
 
Afu we sales wa UDA nshakuona we endelea,tambeni huu wakati wenu
Wala hakuna anayetamba hapa, usually biashara yoyote ikishakosa ushindani lazima idorore na ndio kilichokuwa kinatokea kwa Mwendokasi.

Vituo vinajaa abiria gari hamna au gari zipo wamezi-park tu main terminal huku chache zikigombaniwa so acha wapewe changamoto ili wachague kuboresha au wakabidhi kandarasi kwa mwengine mwenye uwezo.
 
Haya mabasi/daladala za UDA yalianza onekana kwa wingi sana kipindi cha uongozi wa Awamu ya 4 ila baada ya kuingia awamu ya 5 hizi daladala zilipotea zote moja baada ya nyingine na mwisho hatukuziona tena barabarani.

Tangu msiba uishe wa Aliyekua Rais awamu ya 5 Rais.Magufuli UDA zimeanza kurudi barabarani nimeshashuhudia UDA 3 mpya ruti ya MBEZI - MBAGALA/3, MBEZI-BUGURUNI,MBEZI-TEMEKE,nk

swali langu ni la mshangao,imekuaje tena haya magari kurudi wakati huuu? yalikua wapi? boss wake ni nani? kwanini alikua hayarudishi barabarani kipindi cha uhai wa magufuli na kwanini kayarudsha sasa hivi?

"Watanzania sisi sio wajinga,Tunaona"

Nimalizie kwa kusema "Anae stream youtube sasa hivi ni kidume", Ukimuona mtu yuko Online Muheshimu,Ma group yangu sioni cha admin wala member anatuma tuma vi meme leo ni kimyaaaaaa,WAZIRI WA NCHI MWANACHAMA WA DATA amejua kututembelea huu mwaka,halafu ndio kwanza April 2..
Tunarudi kwa mzee ruksa kama Mwinyi
 
Wala hakuna anayetamba hapa,usually biashara yoyote ikishakosa ushindani lazima idorore na ndo kilichokuwa kinatokea kwa Mwendokasi.

Vituo vinajaa abiria gari hamna au gari zipo wamezi-park tu main terminal huku chache zikigombaniwa so acha wapewe changamoto ili wachague kuboresha au wakabidhi kandarasi kwa mwengine mwenye uwezo.
Kama UDA zimerudi unadhani mwendokasi anaweza shindana na UDA Mbezi to K.koo? hili ni pigo la KO kwa Mwendokasi, wengojea
 
Tena itakuwa poa sana! Mwendokasi wanazingua sana, unakaa kituoni lisaa lizima zinapita bila kusimama na hazina abiria eti zipo sijui off service!
Kuna siku nilishapasua kioo kwa ungese wao huo huo, nkarusha jiwe BUUUU nikaja upande wa pili nikateremka Ndukiiiiiii
 
na kwa kurudi kwa UDA ndio JIPU litaendelea kukwiva maana naona kabisa namna ambavyo UDA wataanzisha ruti za K.koo - Mbezi na hakuna trafik ataeuliza wala kuzikamata hizo dala dala,hatima ya MWENDOKASI siijui ni ipi kwakweli
Acha vijana wapate ajira wewe
 
Mh hayati JPM aliamini kwenye STATE CONTROLED ECONOMY ndio maana hata mashirika ya ndege yaliwekewa vigingi, ruti za mabasi pia nyingi uliona hazikupewa trip za kariakoo nk aliamini sana kuwa serikali ikontroo kila kitu hali iliyopelekea uchumi mbovu. Hata tenda za ujenzi walipewa sana JKT ambao infact ni cheap labor tu. Ukiangila hii ERA ya mama SAMIA kama ameanza kurudisha hali ambayo inapaswa kufatwa na NCHI.
Anatupoteza huyu mama, mi nawambia muda si mrefu mtaanza mnyooshea vidole
 
Back
Top Bottom