Kusema hakuna mtu wa kuvaa viatu vya Urais baada ya Dkt. Magufuli ni kukosa akili

YES Banaaa!!!
 
Mwandishi ndiyo mashamba na limbukeni wa kutupwa!!

Ijapokuwa kuna vitu vingi vya maana katika andiko lako, Jambo moja tu ambalo linalokufanya kuonekane wewe ni mshamba na mjinga,

Nikikuuliza kwamba, Unatumia vigezo gani vya kumfananisha Magufuli ambaye ni Binadamu awe kama Mungu?

Pengine utasema ni zile sifa anazopewa za utendaji na usimamizi wake!!

Lakini Je, kuwa mtu makini na kusimamia mambo yako Kwa makini na ukasifiwa kwa umaskini wako, kunakosa gani kwako binafsi na Kwa wasifiaji?

Mimi ni mfanyabiashara, Kunakosa gani kutaka Viwango vya Mo kwamba nami siku moja ningependa kufika huko?

Au Kunakosa gani kumsifia Mo jinsi alivyomtafiti mzuuri ktk masoko na pengine kusema huwezi kumfananisha na wengine?

Na ieleweke, Mungu alituumba kila mtu awe wa tofauti na Viwango vya tofauti, na lazima hata darasani awepo mtu wa kushika no moja darasani ingawa walimu ni walewale na masomo ni yaleyale, Darasa ni lilelile, masomo ni yaleyale, walimu ni walewale, Ila kuna mwanafunzi atatoka kapa!

Kinachokusumbua ni wivu wa kike, fanya vema na wewe utapata kibali machoni pa watu, na usipende kutafsri kupendwa na kusifiwa eti ni kama kufananisha na mtu na Viwango vya Uungu!
 
Mkuu, Kawe Alumn anasemaje kwani?
 
Kwangu sio ujinga ni upunguani! Vijana wa tz tukatae kuongozwa na mawazo ya kizee km ya kessy!
 
Japo sijasoma hilo gazeti, ila nilitarajia kuona list ya majina angalau mawili ya wanaoweza kumpita magufuli kwa utendaji wake.

Au ungetaja hata lwa kwako.
 
"Lakini tatizo lao kubwa ni IQ yao kuwa chini sana below the bottom line" .
Wapumbavu,Hawajitambuwi,Wapo wapo tu.
 
Hii inamaanisha mambo yafuatayo:
1. CCM imeshindwa kuwatengeneza viongozi wapya ktk kipindi chote cha utawala wao kama wanavyokuwa wakijigamba; maana hata huyu wanayemsifia anasema alikuwa ana 'beep' tu, kwa maneno mengine hakuandaliwa wala siyo zao la mfumo wa chama.
2. Kati ya wanachama zaidi ya mil 12 wanaotajwa kuwa ni wa CCM hayupo mwenye akili na uwezo wala maono bora juu ya nchi hii zaidi ya Mwenyekiti wao
3. Wanaotetea hoja hiyo, hawaelewi maana ya mfumo wa Democracy; kwamba kama ndani ya chama chao hawajaona mwenye akili anayefaa kupokea kijiti basi waruhusu vyama vingine viwasimamishe wenye akili tuwapime kwa miaka mitano iliyopangwa.
4. Mwisho, hawaamini ktk taaluma, vipawa, uwezo na dhamira njema walizonazo wananchi zaidi ya mil 50 ambao wanaweza kuleta mageuzi makubwa zaidi ya haya yanayoonekana sasa, ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.
 
watanzania tumechoshwa,kwa kifupi watanzania hawaitaji ccm Wala chadema Wala chama chochote, wanahitaji serikali ya magufulu tu.hata Kama magufuli atakuwa mgombea binafsi wananchi wataelekea huko huko.vyama tunavyochagua ndivyo vilivyotufikisha hapa kwenye umaskini huu.
 
Ukiona unamwona huyu mtu kama mungu ujue huna akili
Japo sijasoma hilo gazeti, ila nilitarajia kuona list ya majina angalau mawili ya wanaoweza kumpita magufuli kwa utendaji wake.

Au ungetaja hata lwa kwako.
 
Misukule FC indicators of dictatorship is ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…