Kushika sana dini kunaweza kukupeleka kubaya. Rafiki yangu aliacha kazi ya Ualimu baada ya Mkuu wa Shule kumtaka anyoe ndevu

Kushika sana dini kunaweza kukupeleka kubaya. Rafiki yangu aliacha kazi ya Ualimu baada ya Mkuu wa Shule kumtaka anyoe ndevu

Ni jirani yetu huko nyumbani kwetu, pia kuna kaurafiki kwa mbali baina yetu. Likizo sometimes tulikuwa tunajisomea pamoja kwakuwa tulikuwa darasa moja.

Jamaa akawa teacher wa serikali baadaye. Sasa nasikia walimu wana miiko mingi kutokana na mazingira yao ya kazi, sometimes wanakuwa walezi.

Sasa jamaa hakuacha sunnah ya Mtume akafuga ndevu vizuri. Mkuu wa shule akamwambia Mr nyoa hizo ndevu hii shule ni secular, jamaa akakataa.

Alipoona anazidi kuhimizwa kunyoa uchebe na sometimes kutishiwa kufutwa ajira akamwahi boss wake akaandika 24 hrs resignation letter, mkuu wa shule akaipitisha, na Mkurugenzi akamaliza kazi.

Jamaa sasa kwa moyo mweupe analima kijijini. Kaka yake aliyemsomesha wamegombana baada ya jamaa kupiga kalamu chini lakini anasema hawezi kurudi.
Ndevu mpaka Prince Harry anafuga.Nyinyi sijui mna nini na ndevu.
Zamani mababu zetu mliwalazimisha mpaka kubadili majina na dini ili wasome.Kama wasingetokea mashujaa wakakataa sijui tungekuwa wapi leo hapa Tanzania
 
Atakuwa anakula ndevu zake sahiv kama chakula.Kuna watu wahovyo sana kutaka kulazimisha mambo yao Kila sehemu Kwa kuhisi ndiyo wenye haki kumbe ujinga TU.
Kama huyo mwalimu mkuu anayeingiza chuki zake kwa waajiriwa wenzake
Wapi imeandikwa kuwa ndevu si maadili ya mwalimu
mnaona jeans na vimini mnavyovaa nyinyi ndio maadili ya ualimu.
Acheni ujinga huo.
 
Sio lazima ,hata ukienda kwao kweny taasisi zao sio wote wanafuga ,wengine hawana kabisa kutokana na maumbile yao.

Mi nakumbuka kuna rasta mmoja mwanae hakusoma kwa vile aliambia akate nywele ndio aanze darasa la kwanzq ,walikataa kabisa yaani.
Rasta haziruhusiwi kwa sheria!
Na pia..
Kama nilivyosema tu inategemea na Madhehebu kila Dhehebu lina itikadi zake na kuna Ulazima wake katika kufanya mambo..
Na hata hizo Taasisi inategemea ni za Dhehebu gani
 
Dini ni moja ya majanga tuliyoachiwa Waafrika. Mitaani usiku mnene watu wanahubiri na vipaza sauti unajiuliza watu wanapumzika saa ngapi? misikiti inatumia vipaza sauti usiku mnene. Washauri wawe wastaarabu utakachoambulia pengine wanaweza kukukata shingo kabisa
hahahahahaa
dini imeleta msala afirika
 
Ni jirani yetu huko nyumbani kwetu, pia kuna kaurafiki kwa mbali baina yetu. Likizo sometimes tulikuwa tunajisomea pamoja kwakuwa tulikuwa darasa moja.

Jamaa akawa teacher wa serikali baadaye. Sasa nasikia walimu wana miiko mingi kutokana na mazingira yao ya kazi, sometimes wanakuwa walezi.

Sasa jamaa hakuacha sunnah ya Mtume akafuga ndevu vizuri. Mkuu wa shule akamwambia Mr nyoa hizo ndevu hii shule ni secular, jamaa akakataa.

Alipoona anazidi kuhimizwa kunyoa uchebe na sometimes kutishiwa kufutwa ajira akamwahi boss wake akaandika 24 hrs resignation letter, mkuu wa shule akaipitisha, na Mkurugenzi akamaliza kazi.

Jamaa sasa kwa moyo mweupe analima kijijini. Kaka yake aliyemsomesha wamegombana baada ya jamaa kupiga kalamu chini lakini anasema hawezi kurudi.
Kuna maza fulani alikuwa anaishi karibu na chuo cha butimba, nasikia alikuwa askari nilikuwa namwona akiuza mboga mboga, kumbe aliacha kazi baada ya kulazimishwa kuwa anafanya kazi siku ya sabato. Maza alikuwa anatembeza mboga pale shule iliyopikwa anatuletea tunanunua na kumix kwenye ugali.
 
Kuna maza fulani alikuwa anaishi karibu na chuo cha butimba, nasikia alikuwa askari nilikuwa namwona akiuza mboga mboga, kumbe aliacha kazi baada ya kulazimishwa kuwa anafanya kazi siku ya sabato. Maza alikuwa anatembeza mboga pale shule iliyopikwa anatuletea tunanunua na kumix kwenye ugali.
Hatari
 
Inaongelea dini gani ?

Kwenye Uislamu kama ndevu unazo ni lazima kuzifuga kama huna kabisa, hii Sheria haikuhusu.

Kufuga ndevu ni Sunnah za mitume wote.
umesema sunna, kivipi iwe lazima? mbona mnafanya waislam wengine waonekane kituko? ndevu sio lazima kufuga japo pia haipendezi kwa (mwanaume kunyoa kabisa pakabaki kama shavu kwa mtazamo wangu)
 
Back
Top Bottom