Kushindwa kwa maandamano ya CHADEMA ni karata muhimu kwa Rais Samia na CCM

Kushindwa kwa maandamano ya CHADEMA ni karata muhimu kwa Rais Samia na CCM

meningitis

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2010
Posts
8,425
Reaction score
4,768
images (3).jpeg

Ni wazi kuwa Chadema ilijaribu kucheza karata zake kisiasa kadri ilivyowezekana ili kujirudisha kwenye ramani ya siasa Tanzania.

Uchaguzi uliopita uliiacha chadema kwenye anguko kubwa yaani kutokuwepo kwenye eneo muhimu la kimaamuzi kupitia uchaguzi. Naamini baada ya kuliona hili viongozi wa CHADEMA walitafakari na kujipanga vyema ili waweze kurejea japo kwa kishindo katika uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Ajenda za ushindi katika uchaguzi zinajulikana zaidi niseme ni maswala ya huduma za jamii,maswala ya biashara ,uchumi wa mtanzamia mmoja mmoja na ikibidi kujenga hasira dhidi ya chama tawala.

Kwa upande wa ajenda za huduma za jamii Rais Samia amefanya mengi na ameyaeleza,kwa upande wa biashara amejitahidi kufanya vyema ikiwemo kupambana na majaribio kadhaa ya migomo iliyoratibiwa vyema na wapinzani ya wafanyabiashara .

Kwa upande wa uchumi pamoja na presha kubwa ya hali ya kidunia bado ameweza kuhimili.
kwa upande wa kuibua hasira za wananchi pia alifanya vyema kwa kuja na 4 Rs. CHADEMA imekosea kutumia turufu hii ya mwisho au niseme haikujiandaa vyema au pengine ni ugumu waliokutana nao kutoka kwa intelijensia ya Serikali ya Samia.

Hivi karibuni tumeshuhudia mabadiliko makubwa na kushtua au kushtukiza yaliolenga vyombo vya kiusalama na diplomasia ikiwemo kuondolewa kwa Makamba na Nape(Niliwahi kuhoji kama Nape alitaka kuandaa vonoco dhidi ya Magufuli)

Soma Pia:

Mabadiliko haya makubwa na ya hatari katika Taifa yasingeweza kupita hivi hivi bila misukosuko mikubwa.

Mwezi septemba tunajionea kashikashi kubwa inayotaka kumtokea Rais Samia ambayo unaweza kuifananisha na kashikashi nyingi zilizowahi kuwakuta kina Jakaya Kikwete na John Pombe Magufuli, mfano maandamano makubwa ya wamasai,Utekaji na mauji mfululizo yenye kuibua ghadhabu za umma na sasa jaribio la maandamano la CHADEMA .

Hata hivyo inaionekana Samia alijipanga mno tena sana.

Leo inaweza kuwa ni siku muhimu kwa Rais Samia kwa kufanikiwa kuzima jambo kubwa pengine Jaribio baya la kumuangusha. Ila kwa mafanikio haya naiona njia nyeupe kuekelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa na hatimaye 2025

FOR GTs ONLY
 
Ukiwa Rais usitake kumridhisha kila mtu mama samia alitaka kumridhisha kila mtu ilikua imebaki kidogo akutane na negative outcomes, unatukanwa mitandaoni unacheka cheka nyoosha mstari waende jela hata 15 kwa kosa la kutoa lugha ya matusi ili iwe mfano kwa wengine.

Ilikua imebaki kidogo waende wakampige makofi hukohuko Ikulu
 
View attachment 3104858

Ni wazi kuwa Chadema ilijaribu kucheza karata zake kisiasa kadri ilivyowezekana ili kujirudisha kwenye ramani ya siasa Tanzania...
Unajua maana ya kushindwa?

Kama maandamano yasingevamiwa na CHADEMA kujikuta wanakoswa wafuasi ktk maandamano yao, hiyo ndo wènye akili wangeiita kufeli kwa maandamano, lakin kwa sasa maandamano yamefanikiwa kwa kiwango cha juu sana
 
View attachment 3104858

Ni wazi kuwa Chadema ilijaribu kucheza karata zake kisiasa kadri ilivyowezekana ili kujirudisha kwenye ramani ya siasa Tanzania...

..Samia ametumia POLISI kuzima maandamano ya CHADEMA.

Alitakiwa ayazime kwa kujenga HOJA zenye ushawishi kupangua madai ya CHADEMA.

Jambo la kuangazia ni hatua ambazo Samia atachukua dhidi ya genge linalohusika na utekaji na mauaji.

Hoja nyingine ni kama Samia ataleta mabadiliko ya kweli ya Tume ya uchaguzi, na Katiba, na kutekeleza kwa vitendo 4R.

Kwa upande wa upinzani, kupanda, au kushuka kwao, kutategemea kama watakuwa na fedha, na rasilimali, za kutosha kufanya kampeni za ushindani dhidi ya CCM.

Samia sio mwanasiasa mzuri. Si mjenga hoja mwenye ushawishi ukilinganisha na wanaotarajiwa kusimama upande wa upinzani.
 
..Samia ametumia POLISI kuzima maandamano ya Chadema.

..alitakiwa ayazime kwa kujenga HOJA zenye ushawishi kupangua madai ya Chadema...
Maandamano huzimwa na nguvu ya dola ..hii ni principle
 
CCM inashinda kwa sababu ya power maana asilimia kubwa zito angekuwaga rais . Tundu lissu hapana ila lowasa angekuwa rais kuna watu wangewashinda CCM ila kwa msimu huu huyu mama amalizie tu miaka yake maana sija mwona anayefaa labda majaliwa.

Hata makamu wa rais anaweza ila chadema hakuna rais hapo. Kura yangu ili isipotee, Urais ni rais mama samia , ubunge atakegombea act wazalendo na madiwani ni huko kule ccm so akili hii sijashurutishwa na mtu nimetumwa na mimi mwenyewe
 
Ccm inashinda kwa sababu ya power maana asilimia kubwa zito angekuwaga rais . Tundu lissu hapana ila lowasa angekuwa rais kuna watu wangewashinda CCM ila kwa msimu huu huyu mama amalizie tu miaka yake maana sija mwona anayefaa labda majaliwa . Hata makamu wa rais anaweza ila chadema hakuna rais hapo. Kura yangu ili isipotee rais mama samia , ubunge atakegombea act wazalendo na madiwani ,huko kule ccm so akili hii sijashurutishwa na mtu nimetumwa na mimi mwenyewe
SweetyCandy mbona kama maji yamezidi unga ?
 
Back
Top Bottom