Konny Joseph
Senior Member
- Aug 28, 2016
- 118
- 199
Kumekuwa na tabia kwa serikali kutengua uteuzi wa viongozi wa umma kwa tuhuma za kuhusika katika vitendo vya kihalifu.
Ila kwa bahati mbaya utenguzi huu huwa unatumika kama mbadala wa kutokuwashitaki viongozi hawa katika mahakama kulingana na makosa ya jinai waliyoyafanya.
Kwa misingi hiyo,utenguzi huu huwa hautumiki kwa maslahi ya umma ili kutoa nafasi kwa mamlaka kuchukua hatua zinazostahiki kwa wahusika.Badala yake zinatumika kuwalinda viongozi hao na mkono wa sheria kwa kuwahadaa wananchi kuwa kutumbuliwa ni hatua tosha kulingana na makosa waliyoyafanya.
Mamlaka zielewe kwamba kutumbuliwa sio mbadala wa adhabu ambayo mtu anapaswa kupewa anapotuhumiwa kwa makosa ya kihalifu.
Kutengua uteuzi wa kionhozi sio adhabu kama ilivyo kuteua sio takrima.
Viongozi wanaotuhumiwa kwa makosa ya jinai lazima hatua stahiki zichukuliwe kulingana na makosa yao.