Mkuu Wangu Kishoka,
Heshima mbele mkuu, maneno yako hapo juu mengi ni kweli isipokuwa tu hujasema tatizo lilipoanzia mpaka tukafikia hapa tulipo. Toka tulikotoka TANU/CCM kilikuwa ni chama kilichokuwa chini ya uongozi wa kiongozi mmoja, viongozi wengine wote walikuwa wameaminishwa kuwa hawakuwa na uwezo wa kuweza kuwa viongozi wa kufikiri independently, wananchi wote tulikuwa tunafuata idea za huyu kiongozi mmoja, bila ya kuuliza wala kukataa, sasa siku alipoondoka ulitegemea itokee miujiza?
I mean, matatizo tuliyonayo sasa as a nation, ni yetu wenyewe lakini unapotaka kwenda deep as of your analysis kwa maoni yangu ni we have to go deep pia kutafuta why tupo tulipo, kabla ya kutafuta solution. Ukweli ni kwamba matatizo yetu ni vivuli vyetu wenyewe taifa zima no one to be spared. Baada ya kututawala for about 23 years chini ya chama kimoja, one day the kiongozi akaamua kutoka, akatuchagulia wa kumrithi ambaye wa all know kuwa hakuwa na uwezo wa kutosha kama tulivyoambiwa, lakini haikutosha kiongozi akatuchagulia tena kiongozi mwingine, huyu sasa ndiye hasa aliyechangia big time kutufikisha tulipo, lakini na yeye pia akatuchagulia kiongozi tuliye naye sasa, OH my God!
Now here we are, a confused nation with absolutely no idea tunachofanya, then comes wananchi kama wewe na ku-act as if you are from the Mars, kwamba haya matatizo tuliyonayo yameanza jana au juzi, kumbe unajua ukweli kuwa ni malimbikizo ya uongozi mbovu toka tulipopata uhuru, na wananchi tusioelewa kitu kuhusu nchi yetu wenyewe! Idea ya kuiweka CCM mbele kuliko taifa be honest mkuu viongozi wetu wameitoa wapi kama sio kwa waliowatangulia? Wakati hizi tabia zinapandiwa mbegu wananchi tulikuwa so happy about it bila ya kujua kuwa zilikuwa ni mbegu mbaya sana kwa our nation's future, kuna waliojaribu kuonya lakini wakatupwa na tukaambiwa ni viongozi wabaya sana na hawafai, sasa kwa sababu alisema tuliyemuamini na taifa letu ikawa amina, we never questioned the leader, I mean haiwezekani kuwa viongozi kuanzia Kambona, Karume, Bibi Titi, Eli Anangisye, Kassanga Ntumbo, Chief Fundikira, Bakari Seif, Seif Hamadi, Aboud Jumbe, Dr. Masha, walikuwa hawana vision au akili ya kujua kuwa baadhi ya maamuzi yaliyokuwa yakifanywa huko nyuma yalikuwa na madhara mbele ya safari,
Mkuu I can go on and on, lakini the messaage is the same kuwa hatuko hapa kwa bahati mbaya, na wote yaaani taifa zima tumehusika kwa njia moja au nyingine kufika tulipo, sasa tunahitaji kutafuta njia za kujitoa tulipo, lakini still either hatuelewi how, au hatuaminiani kiasi kwamba tuko radhi kuwaacha hao hao waliohusika kwa karibu kutufikisha hapa tulipo waendelee na uongozi, I mean CCM ni chama cha siasa sio cha dini au charity, so is Chadema au CUF, sasa kama kila anyeeenda kuingia kwenye uongozi anaishia kuwa sawa na wale wa zamani, inasema nini kuhusu sisi wananchi?
Mkuu ninakubaliana sana na analysis yako nzito kuhusu CCM, isipokuwa tu nina tatizo kuwa hukuangalia deeep kuona matatizo ya viongozi wetu ndani ya CCM yametokea wapi, na pia hutoi mapendekezo ya kutosha of what to do next, maana nina wasi wasi kuwa hiyo inaweza kutufanya wote tukawa part of the very problem we are trying to address, kwa sababu hatutoi applicable solution ambazo ni fit kwa mazingara yetu kijamii na kisiasa, na pia hatusemi na kukubali kuwa tumefikaje tulipo.
Sikusema kuwa CCM inachofanya ni sawa, isipokuwa nimesema kuwa tuwapewe nafasi kwanza, maana recently angalau wameonyesha kuanza kubadilika pole pole, as opposed na kasi ambayo tungependa wawe nayo kwenye kubadilika.
Ahsante Mkuu