Kutoka Butiama: Exclusive news

Kutoka Butiama: Exclusive news

Hii nimeipata kutoka kwenye gazeti la RA ...


Kumekucha Butiama


  • [*]Wajumbe waficha siri kubwa moyoni
    [*]Mijadala yanguruma hata kabla ya kikao
    [*]Kikao cha NEC kinafanyika leo, kesho
    [*]Nukuu za kauli za Nyerere kila mahali

na mayage s. mayage,butiama

KARIBU wajumbe wa NEC Musoma… Bila CCM madhubuti nchi itayumba. Hayo ni miongoni mwa maneno yaliyoyapamba mabango ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), yaliyotapakaa katika mji wa Musoma na vitongoji vyake, kuashiria kuanza kwa Kikao cha Halmashauri Kuu leo kijijini Butiama.

Kwa kuyaangalia mandhari tu ya mabango hayo, ni wazi yanaongeza hofu juu ya hatima ya chama hicho kuweza kugawanyika kufuatia tofauti za wazi kujitokeza kutokana na hali halisi ilivyo ndani ya chama hicho tawala.

Kikao cha NEC kinachoanza leo kimetanguliwa na vikao viwili, kile cha Sekretarieti ya chama hicho iliyokutana katika Ofisi ya CCM mjini Musoma jana, chini ya Katibu Mkuu wa CCM, Yussuf Makamba na Kamati Kuu iliyoongozwa na Mwenyekiti, Rais Jakaya Kikwete, kijijini Butiama jana jioni.

Kamati Kuu (CC) ya chama hicho ilipangwa kukutana jana jioni. Hata hivyo, kikao hicho hakikufanyika na badala yake, wajumbe walipewa makabrasha wakayasome ili washiriki kikamilifu kikao cha CC, ambacho kinaanza leo asubuhi, baada ya kuahirishwa jana jioni.

Pamoja na agenda za NEC kutajwa wazi kuwa ni pamoja na kuzungumzia hali ya kisiasa na muafaka wa kisiasa kati ya CCM na CUF, bado wajumbe wa kikao hicho wameelezwa kuwa na mambo mazito “vifuani” mwao wanayotarajia kuyaibua watakapopewa nafasi ya kuchangia ama kuuliza maswali.

Hali hiyo imeelezwa kuelemea zaidi katika hali tete ya kisiasa ambayo imetokana na matukio ya kashfa za ufisadi kuhusishwa kwa viongozi wa juu wa serikali na watendaji wao na hatua kuchukuliwa na Bunge na baadaye serikali, bila chama kuchukua hatua.

Kashfa mbili nzito zilizoitikisa CCM na serikali yake, ni ile ya mradi tata wa umeme wa dharura uliokabidhiwa kwa kampuni ya Richmond Development LLC na ile ya Akaunti ya Fedha za Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zote zikiihusisha kwa karibu mno serikali na chama tawala kupitia watendaji na wafadhili wake. Sakata la Richmond lilisababisha kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri wawili, Nazir Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha, ambao wote kwa kupishana waliongoza Wizara ya Nishati na Madini, iliyotekeleza upatikanaji wa mradi huo tata ambao umekua ‘wimbo’ kwa wananchi.

Rais Kikwete alilazimika kuunda upya baraza lake la Mawaziri, likiongozwa na Mizengo Pinda, ambaye aliunda timu ya wataalamu kutekeleza mapendekezo ya Kamati ya Bunge iliyochunguza mradi wa Richmond, wataalamu ambao wamekwisha kumkabidhi ripoti yao.

Habari kutoka katika vyanzo kadhaa vya ndani ya CCM, zinasema ripoti hiyo ya wataalamu wa Pinda, huenda ikajadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu cha jana jioni, hoja ambayo inaweza kuibua mjadala ndani ya vikao hivyo vya CCM, ambavyo kwa mara ya kwanza vinafanyika kijijini Butiama, alikozaliwa na kuzikwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.

Kufanyika kwa kikao hicho Butiama kumeibua hisia kutoka kwa baadhi ya wajumbe ambao katika mazungumzo yao yasiyo rasmi hapa mjini Musoma, wanasema kwamba Mwalimu Nyerere aliwakataa baadhi ya watu ambao sasa ndio wamesababisha kuchafuka kwa chama chao na serikali yake, na kwamba ni lazima chama kichukue hatua za haraka kujisafisha.

Kauli za Mwalimu Nyerere zimekuwa zikirejewa na baadhi ya wajumbe wa NEC na wananchi, ikiwamo hiyo iliyotapakaa katika mabango katika barabara iendayo Butiama, ya kwamba “Bila CCM madhubuti, nchi itayumba.” Hiyo tu inaonyesha kwamba yapo mambo mazito yanayoweza kuibuka ili kukirejesha chama hicho kwenye misingi iliyoachwa na mwasisi wake.

Ukiacha hatua ya Katibu Mkuu, Yusuff Makamba kuitisha mkutano na waandishi wa habari na kufafanua ajenda na sababu za kufanyia kikao hicho Butiama, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, alikaririwa na magazeti jana akisema moja ya masuala yatakayojadiliwa ni maadili ya viongozi wa chama. Hilo halikuwa moja ya ajenda zilizotajwa na Makamba.Kwa ujumla kumekuwa na hali ya kutoaminiana miongoni mwa wana CCM na viongozi wao na kampeni za chini kwa chini zimekuwa zikifanyika ama kwa nia ya kuwamaliza baadhi ya watu au kuwabeba na kuwaokoa wana CCM waliotuhumiwa.

Wasiwasi huo unafuatia kuwapo tetesi za baadhi ya wana CCM kupendekeza kwa chama kuwachukulia hatua wale wote waliotajwa au kuhusishwa na ufisadi ili kukitenga chama na tuhuma hizo ambazo zinaelekea kuhatarisha mshikamano wa chama hicho.

Viongozi wote wa juu wa CCM, akiwamo Rais Kikwete na Waziri Mkuu Pinda, walikwisha kuwasili Butiama jana mchana tayari kwa vikao hivyo, huku kukiwa na taarifa kwamba kama ilivyo kawaida ya vikao vya NEC, waandishi wa habari hawataruhusiwa kuwamo ndani ya ukumbi wakati wa kikao.

Source: Mtanzania
 
kama watu wamefikia hatua ya kumtukuza nyerere kiasi hiki, nadhani next step itakuwa kumwabudu !

Mara nyingi uchangiaji wako ni ule wa kukosoa kile ambacho wengine wamesema! wewe ni hodari na bingwa wa kukosoa! mbona hatuoni upande wa pili wa kutoa mchango wa mambo mazuri hasa ukiyaanzisha wewe ili wengine wachangie???

Kutumia nguvu nyingi kukosoa huonyesha ujinga na upumbavu wakati mwingine!!

jifunze kuanzisha mada na wewe, sio siku zote unadandia kukosoa mada za wengine!! na si lazima anayeanzisha mada aandike kile ambacho wewe unakubaliana nacho!
 
Hoja hujibiwa na hoja, "CCM na unafiki wao" Hawa ni binadamu kama wewe na mimi, sioni tatizo liko wapi. Watanzania walio wengi wanajivunia marehemu Nyerere, kama baba wa taifa. Hii ni ishara ya kumuenzi na kumsamini Mwalimu. Mtu yeyote anyetaka kutembelea kaburi la Mwalimu anaweza kufanya hivyo, awe chadema, cuf nk, ni mapenzi yako tu. Kama wamekosa ama hawajakosa, tusikae kujadili mambo yasiyokua na maendeleo hapa. Nani hapa ni safi kabisa!? Wanaokwenda makanisani au misikitini sio kwamba hawatendi zambi (au tuwaite wanafiki?)...lakini hujakatazwa kwenda kanisani au msitikini ata kama ni fisadi, jambazi. Chuki binafsi hazitufikishi mbali..mijadala kama hii haimsaidii mtanzania kutoka kwenye umasikini, just a waste of time
 
Ndg zangu wa CCM mimi napenda kuwapa angalizo tena kwa nia nzuri kabisa ya kukiimarisha chama chenu.Kimila nadhani hapo mlipochagua kwenda ni mahali patakatifu ambapo hachezewi ovyo hilo naamini kila mtu analijua,na ndio maana watu wa dini mbalimbali wamekua wakienda kufanya ibada mbalimbali hapo.

Sasa nyie nendeni na unafiki wenu halafu mtaona matokeo yake,mtajuta kwa kupeleka hicho kikao Butiama.Ni lazima mtoke na maamuzi ambayo ni matarajio ya watanzania na sio kubembelezana.
 
Mimi Naamini Baada Ya Wana Jf Kurusha Makombora Mzito Kuhusu Tuhuma Za Ufisadi Yaliyopelekea Baadhi Ya Wadau Wa Jf Kukamatwa Na Na Polisi Basi Fisadi Nao Wakaamua Kumtumbukiza Mtu Wao Ambaye Wanamuita Kada Mpinzani Ili Apambane Na Wana Jk Lakini Sisi Tunasema Vita Ni Mbele
 
If your a CCM Member then you should think careful the role that this party has made in our country. It is very difficult to take this, we are really poor with no sign of a through way. What is going on in our Economy, social services and polical arena in general. Where is our strength?
The people who went to Butiama and now cheating through their action are bad people than the Mafisadi you know. If something bad is appening and you are the one who can make a differend not saying anything to stop it is turning back to your country. CCM is not a political party of Will. Not the country, village or an individual need to have it. It is a party of victims whose supporters have northing to praise but Green Tshirts they used to wear. That is how it is. Nyerere died while challenging Mkapa Regine, those people you see where there. A unlawful acted regime that inherited the country one of the waste government to trust and see.
Tell, me we have a budget of Six trellion, we are at the last quoter, what did we get on the budget any far? I just remember Ministers using it to tour the country. What are those praises of wonderful budget, larger party of it set for infrastructure development? We don't get any even conclusion of tenders. What as a nation we can prosper with a party whose government gives on a fake budget to its people? Those leaders you see trust everything even the worse part of it.
kuweka maua sio bigi deal, pengine (sina uhakika) walifanya hivyo mara ya mwisho hivyo picha hawakupigwa, it just happened kwamba kikao hiki kinafanyika butiama, hivyo wakaamua kwenda kumkumbuka muasisi wa chama chao !
hata wewe unaweza kwenda kuweka maua, na SIDHANI KUWEKA MAUA KATIKA KABURI LA NYERER NI UNAFIKI ! NAKATAA ! ebu kama utaweza kuikuza hiyo picha naomba ufanye hivyo halafu nitajie mafisadi unaowaona wewe katika hiyo picha ! Picha hiyo hiyo uliyoweka !

(Najua mafisadi wengine watapigwa picha wakiweka maua hizo labda zaweza kutoka siku 1-2-3 from now) lakini kilichokufanya mainly uandike ni hiyo picha, so plz call out a few names ya hao unaowaita wanafiki !

yule wa kati kati kafanana na kinana, sijui kama ni yeye !
 
Wajumbe wetu Mlio Butiama nini kinaendelea? Lunyungu, Mpaka kieleweke, Halisi, Mzee wanakijiji? Tuanatoa macho hapa hatujui nini kinaendelea huko?
 
Wajumbe wetu Mlio Butiama nini kinaendelea? Lunyungu, Mpaka kieleweke, Halisi, Mzee wanakijiji? Tuanatoa macho hapa hatujui nini kinaendelea huko?
Simu ya mmoja wa watu niliotarajia wangenipa updates haipatikani. Dakika chache zilizopita kanitumia ujumbe kuwa "Kamati kuu walikuwa wanaendelea na kikao chao Musoma kilichoanza asubuhi na walikuwa hawajamaliza hadi ananitumia ujumbe huo na wajumbe walio Butiama hawajui nini kinaendelea".

Sasa endapo kutakuwa na jipya nitakuarifuni na naamini kuna members ambao wana mpya basi naamini watatudadavulia.

Invisible
 
Hoja hujibiwa na hoja, "CCM na unafiki wao" Hawa ni binadamu kama wewe na mimi, sioni tatizo liko wapi. Watanzania walio wengi wanajivunia marehemu Nyerere, kama baba wa taifa. Hii ni ishara ya kumuenzi na kumsamini Mwalimu. Mtu yeyote anyetaka kutembelea kaburi la Mwalimu anaweza kufanya hivyo, awe chadema, cuf nk, ni mapenzi yako tu. Kama wamekosa ama hawajakosa, tusikae kujadili mambo yasiyokua na maendeleo hapa. Nani hapa ni safi kabisa!? Wanaokwenda makanisani au misikitini sio kwamba hawatendi zambi (au tuwaite wanafiki?)...lakini hujakatazwa kwenda kanisani au msitikini ata kama ni fisadi, jambazi. Chuki binafsi hazitufikishi mbali..mijadala kama hii haimsaidii mtanzania kutoka kwenye umasikini, just a waste of time

Nani alikwambia kuna chuki binafsi!? 😕
Hawa CCM tangu Mwalimu afariki miaka 9 iliyopita sera zake zote ambazo alikuwa akizithamini na kupendwa na Watanzania wengi wameziacha kwa kuwa "zimepitwa na wakati".

Wakaja na sera za kusaini mikataba ya kifisadi ya IPTL, Richmonduli, Songa, Netgroup na kukupua mabilioni ya shilingi toka BoT.

Wahusika wote wa mikataba hiyo ya kifisadi bado wanaogopwa kutajwa na kuchukuliwa hatua za kisheria eti nchi "italipuka" kama watatajwa!

Pia wakasaini mikataba ya kifisadi ya madini ambayo haina maslahi yoyote kwa Watanzania na wanaonufaika ni wageni.

Sasa wameona umaarufu wa CCM unaporomoka kwa kasi kubwa sana kila kona ya nchi wanataka kuwadanganya Watanzania eti wanamuenzi Mwalimu kwa kuweka maua kwenye kaburi lake! Humuenzi Mtu kwa kuweka maua kwenye kaburi bali kwa kuendeleza yale ambayo aliyapa kipaumbele katika uhai wake na kuungwa mkono na wengi aliowaongoza.

Wakati huo huo asilimia kubwa ya vingunge wote wa CCM ambaye hawataki kabisa kuzungumzia chochote kuhusiana na ufisadi wa Mkapa wakati alipokuwa Rais kwa kufanya biashara akiwa Ikulu, kutumia wadhifa aliokabidhiwa na Watanzania kujitajirisha yeye na mafisadi wenzie na kujipatia Kiwira Coal Mining katika mazingira ya kutatanisha. Mwalimu angekuwa hai angelisema hili kwa marefu na mapana. Na huku siyo kumuenzi Mwalimu kwa kuunyamazia ufisadi ambao uko wazi kabisa.

Leo unasema eti ni chuki binafsi! kwa hiyo chochote kila tunachohoji kuhusu CCM ni chuki binafsi! Mkishashindwa hoja ndiyo zenu hizo eti tuna chuki binafsi bahati nzuri Watanzania wa 2008 siyo wale wa mwaka 47 wanajua kuchanganua mambo kwa kina.
 
I mean vijana mnaonekana kuwa mmekata tamaaa kabisaa, no mimi bado, ndio kwanza vijana wengi tunaofanana nao wameingia huko NEC, hilo linanipa moyo sana kuwa kuna mwanga mbele, sasa mimi nilitegemea kuwa hapa JF mahali pa wasomi na wachambuaji wakali wa siasa zetu tutajitokeza kutoa ushauri mzito kwa wajumbe mategemeo yetu huko Butiama, binafsi nilitegemea mawazo hayo tuyapeleke kwa wajumbe hao maana kuna kina Nape, John Mongella, Asha Baraka, Sister Dogo(Visiwani) na wengineo hawa ni washikaji tunaweza kuwatumia ujumbe anytime wakaufikisha huko Butiama, wakishindwa ndio tuwale nyama, lakini vijana mnalia mno hata mkutano wenyewe haujawa, vipi wakuu?

Too much negativity, hebu tujaribu kuangalia on the otherside of the coin, kisiasa bongo tumetoka mbali sana wakuu, leo wabunge wa CCM wanamgomea waziri kupitisha muswaaada wa nishati, Waziri Mkuu anasutwa bungeni mbele ya public na kujiuzulu, I mean Roma haikujengwa kwa siku moja wakuu, hebu tuwe positive angalau kidogo, tuwapoe nafasi wajumbe wajiweke sawa na tuwape mawazo, mimi ninayakaribisha na ninaaahidi nitayafikisha as always do, lakini so far we are not offering anything positive kwa wajumbe wetu.

Tuwape nafasi wakuu!

FMES,

Mimi nimekulia ndani ya kuipenda CCM, Yes CCM Asili ambayo ilikuwa inasimamia Utu hata kama ilikuwa na mafupi, lakini kipaumbele kilikuwa watu. Kadri miaka inavyokwenda, CCM inageuka Sura na kuwa Nyang'au!

Alichosema Bin Maryam kuwa CCM (NEC/CC) ni Politburo, ni kitu nilichosema hata nilipotoa mchango wangu kuhusu Jaka Mwambi na Mapuri ambao ni makada kupelekwa nchi asisi za Ujamaa ambazo CCM zao (China and Russia) zimeng'ang'ania madaraka na hata kumiliki uchumi na si Taifa.

Katiba ya CCM inaweka Chama mbelena si Taifa, Katiba inasema mwanachama na kiongozi wajibu wake na uaminifu wake ni kwa Chama kwanza na si Taifa. Hili ni kosa, ndio maana nasema nakuwa vigumu kwa Bunge kuwa na nguvu kuliko NEC! Ndio maana unaona watu wengine hukimbilia kugombea NEC na si Ubunge!

This is backwards and moribund and it has to stop! CCM is no longer the party of the mass, Wakulima na Wafanyakazi. CCM is now the party of those elite who make it to NEC and CC! Priority and loyalty is given to those who stand together to defend the brass and not the mass!

The mass is forgotten, left behind unattended until every political menstrual cycle, that is when you see CCM becoming active again singing praises about themselves "we have courage, we liberate our country, we are strong, trust us" like John McCain banner and with free booze, food and green and yellow Tshirt using taxpayer money, the Mass say Amen and vote CCM again!

The decay of original vision for CCM to be party of the mass and work for the Interest of Utaifa has sidelined most of us and we do not trust current CCM leadership. Yes it is good for people like Viane (John Mongela, Nape and young guns to get into the club, however if the core Mantra of CCM does not change and put Tanzania and Tanzanians first and foremost before CCM interests, then John, Nape and all young guns in 5 years or less than that, they will be practicing the same stuff that their party elders are doing today! John will just be like Kingunge or Makamba!

Hivyo basi, napenda kutofautiana na mtazamo wako mkuu na kuona kuwa CCM inachofanya ni sawa. I beg to differ with you respectfully!

Respect Mkuu!
 
Basically hakuna any fundamental problem ya Gavana kuitwa kwenye kikao cha CCM (Mind you kuitwa, siyo kulala nao mpaka anapoteza professional integrity yote na any moral standing)

My thing is awe na equal access kwa wote, kesho CHADEMA wakitaka kumuita na kumhoji kuhusu EPA aweze kwenda kwenye mkutano wa CHADEMA na kujibu maswali kama alivyoenda CCM, kama CHADEMA wanahitaji access na document fulani za serikali wapatiwe kama wanavyopatiwa CCM. Kama documents ziko classified basi hata CCM nao wasipate,kama CCM wanaomba hela za kampeni BOT basi hata CHADEMA nao waweze kupata vile vile.Kama ni mwiko kuomba pesa za kampeni BOT basi wote CCM na CHADEMA wasiweze kupata hela.

Sio tunakuwa na double standards, huku CCM wana rules zao na vyama vingine vina rules zao.

My fear ni kwamba CCM ina abuse position kama ruling party kupata undue advantage na access ya BOT.Kuanzia election funds mpaka access na governor.It should not be like that.

Pundit,

This is my point and my friend Mtanzania thinks I am paranoid!

Why would CCM leaderhip clan have more powers to summon an executive of any institution but our parliament or other organs can not? If the parliament is being told that stay away from probing Buzwagi contract, but NEC can receive the original copy and even CEO of Barrick show up in Chimwaga to give some explanation, then to whose interest does the Governer Ndulu govern? Is it to CCM or Tanzania?

Yes CCM has mandate by elections of 2005 to be Chama madarakani, but it is Serikali and its body that needs to be on top and not otherwise!

I am not sure if as Taifa we have transitioned well into the new political spectrum of multipartyism and democracy. CCM is still leading and controlling all the political scenarios and our government as if that CCM is the mighty one, the Messiah, the Grand Puba of politics, Alpha and Omega of our lives!
 
butiama%252B1.jpg

Vigogo chama tawala Tanzania( CCM) wakiweka mataji ya maua katika kaburi la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, nyumbani kwake Mwitongo, Butiama kabla ya kuanza mkutano wao.

Chama kimejaa mafisadi ambao Mwalimu angekuwa hai angewasemea hovyo, leo wanajifanya eti wanaenda kutoa heshima zao kwenye kaburi la Mwalimu. Wana heshima gani hawa kwa Mwalimu! wakati wanafanya tofauti na Mwalimu alivyokuwa kama kiongozi ambaye alikuwa na maadili na wala hakuwa na tamaa ya utajiri au kuishi maisha ya fahari kubwa kuliko wale aliotuongoza. CCM acheni unafiki na usanii wenu

Mimi namba litokee tetemeko na mvua kubwa kama lile lililotokea siku alipofariki Mwalimu Julius pale Mwitongo, ili hawa jamaa wasutwe nadhiri zao!
 
Kikao kimemalizika,inasemekana usalama wa Taifa wametumia zana za kisasa walizoachiwa na joji Kichaka kuzima mawasiliano ,hakuna mawasiliano kabisa musoma nzima ,hali ni tete ,kuna baadhi ya magego ya CCM wameondoka na kurejea makwao ,hakijulikani kitu gani haswa kilichowaondoa,nimejuliswa kwa njia ya GPRS ,ghali sana hivyo maneno yalikuwa ni ya haraka kama sekunde thelathini tu , pia hali ya hewa haikuruhusu mawasiliano yawe ya kusikika vizuri ,huenda ikawa sikusikia vizuri kati ya kuondoka na kuwasili.
 
Kama nilivyoahidi: Wajumbe wamewasili muda si mrefu tokea Musoma, kikao kimeanza na JK anatoa hutuba fupi sasa

Points to note are as follows:

Mkapa, Mwinyi na Sumaye hawajahudhuria katika kikao hiki Butiama.

Dr. Shein kafiwa hatoweza kuwepo katika kikao hiki.

More info to come
 
Kauli za Mwalimu Nyerere zimekuwa zikirejewa na baadhi ya wajumbe wa NEC na wananchi, ikiwamo hiyo iliyotapakaa katika mabango katika barabara iendayo Butiama, ya kwamba “Bila CCM madhubuti, nchi itayumba.” Hiyo tu inaonyesha kwamba yapo mambo mazito yanayoweza kuibuka ili kukirejesha chama hicho kwenye misingi iliyoachwa na mwasisi wake.

Ukiacha hatua ya Katibu Mkuu, Yusuff Makamba kuitisha mkutano na waandishi wa habari na kufafanua ajenda na sababu za kufanyia kikao hicho Butiama, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, alikaririwa na magazeti jana akisema moja ya masuala yatakayojadiliwa ni maadili ya viongozi wa chama. Hilo halikuwa moja ya ajenda zilizotajwa na Makamba.Kwa ujumla kumekuwa na hali ya kutoaminiana miongoni mwa wana CCM na viongozi wao na kampeni za chini kwa chini zimekuwa zikifanyika ama kwa nia ya kuwamaliza baadhi ya watu au kuwabeba na kuwaokoa wana CCM waliotuhumiwa.

Source: Mtanzania

Ukichukulia kwa wepesi ile kauli ya Mwalimu "Bila CCM madhubuti, nchi itayumba", watu na hasa wana CCM watadai kuwa hii ni ishara kuwa ni CCM pekee yenye yamini na uwezo wa kuongoza nchi. Lakini ukichunguza kwa undani matamshi haya ukweli wake yanasema kuwa kama CCM haitakuwa imara, kwa kuwa adilifu na kulitumikia Taifa na si kutumikiwa na Taifa, nchi itapata misukosuko. Nchi itayumba kwa kuwa CCM (TANU/ASP) ndio chama asili ambacho tumekuwa nachi tangu uhuru. CCM imekuwa ni Baba na Mama kwa Watanzania.

Ikiwa CCM itakosa mwelekeo na kushindwa kuwa madhubuti ndani ya chama kwa kuwa na uongozi bora wenye kulinda maslahi ya nchi na si maslahi binafsi, basi Watanzania watayumba sawa na leo ukimwambia Mkristo kuwa Yesu si mwana wa Mungu na ukadhihirika wazi kuwa Yesu si Mwana wa Mungu na mkombozi!

Kinachoshangaza kingine ni kupingana kwa kauli kati ya Katibu Mkuu na Makamu Mwenyekiti kuhusiana na moja ya ajenda kubwa za Kikao hiki. Hili nalo laashiria mgawanyiko mkubwa na ukosefu wa umoja hivyo kuthibitisha kuwa CCM sasa hivi si madhubuti.

Ninachojiuliza mimi Kasisi ni hili, je Upinzani uko wapi dakika hii kuchukua Tunu inayodondoka kutoka mdomo wa CCM? Kwa nini Upinzani hautumii fursa hii kujiuza kwa nguvu zote na kuikebehi CCM? Je Upinzani kama wananchi wanasubiri matokeo Jumatatu usiku kujua kuwa CCM imejipatia ushindi wa uchaguzi 2010 kwa kujisafisha katika kikao hiki cha Butiama? Yetu macho!
 
Kama nilivyoahidi: Wajumbe wamewasili muda si mrefu tokea Musoma, kikao kimeanza na JK anatoa hutuba fupi sasa

Points to note are as follows:

Mkapa, Mwinyi na Sumaye hawajahudhuria katika kikao hiki Butiama.

Dr. Shein kafiwa hatoweza kuwepo katika kikao hiki.

More info to come

asante kwa info
Kuna sababu zozote zilizotolewa kwa kutokufika kwao
 
Just curious, why do we always appear to be obsessed and overwhelmed by these CCM meetings? Do we expect anything different from their usual ways doing things: cover up, mockery, manipulation of truth and lies, n.k? It seems like some people are expecting some CCM gurus to be fired, have you asked yourself for what and how will that help JK ovecome his shameful incompetence? Do you still doubt that the root of our problems is systemic rather than a problem of a few unscrupulous individuals in CCM? And finally, what makes it good for Mkapa, Mwinyi and Sumaye not to have attended this business as usual CCM meeting?
 
1. Yes CCM Asili ambayo ilikuwa inasimamia Utu hata kama ilikuwa na mafupi, lakini kipaumbele kilikuwa watu. Kadri miaka inavyokwenda, CCM inageuka Sura na kuwa Nyang'au! Katiba ya CCM inaweka Chama mbelena si Taifa, Katiba inasema mwanachama na kiongozi wajibu wake na uaminifu wake ni kwa Chama kwanza na si Taifa. Hili ni kosa,

Mkuu Wangu Kishoka,

Heshima mbele mkuu, maneno yako hapo juu mengi ni kweli isipokuwa tu hujasema tatizo lilipoanzia mpaka tukafikia hapa tulipo. Toka tulikotoka TANU/CCM kilikuwa ni chama kilichokuwa chini ya uongozi wa kiongozi mmoja, viongozi wengine wote walikuwa wameaminishwa kuwa hawakuwa na uwezo wa kuweza kuwa viongozi wa kufikiri independently, wananchi wote tulikuwa tunafuata idea za huyu kiongozi mmoja, bila ya kuuliza wala kukataa, sasa siku alipoondoka ulitegemea itokee miujiza?

I mean, matatizo tuliyonayo sasa as a nation, ni yetu wenyewe lakini unapotaka kwenda deep as of your analysis kwa maoni yangu ni we have to go deep pia kutafuta why tupo tulipo, kabla ya kutafuta solution. Ukweli ni kwamba matatizo yetu ni vivuli vyetu wenyewe taifa zima no one to be spared. Baada ya kututawala for about 23 years chini ya chama kimoja, one day the kiongozi akaamua kutoka, akatuchagulia wa kumrithi ambaye wa all know kuwa hakuwa na uwezo wa kutosha kama tulivyoambiwa, lakini haikutosha kiongozi akatuchagulia tena kiongozi mwingine, huyu sasa ndiye hasa aliyechangia big time kutufikisha tulipo, lakini na yeye pia akatuchagulia kiongozi tuliye naye sasa, OH my God!

Now here we are, a confused nation with absolutely no idea tunachofanya, then comes wananchi kama wewe na ku-act as if you are from the Mars, kwamba haya matatizo tuliyonayo yameanza jana au juzi, kumbe unajua ukweli kuwa ni malimbikizo ya uongozi mbovu toka tulipopata uhuru, na wananchi tusioelewa kitu kuhusu nchi yetu wenyewe! Idea ya kuiweka CCM mbele kuliko taifa be honest mkuu viongozi wetu wameitoa wapi kama sio kwa waliowatangulia? Wakati hizi tabia zinapandiwa mbegu wananchi tulikuwa so happy about it bila ya kujua kuwa zilikuwa ni mbegu mbaya sana kwa our nation's future, kuna waliojaribu kuonya lakini wakatupwa na tukaambiwa ni viongozi wabaya sana na hawafai, sasa kwa sababu alisema tuliyemuamini na taifa letu ikawa amina, we never questioned the leader, I mean haiwezekani kuwa viongozi kuanzia Kambona, Karume, Bibi Titi, Eli Anangisye, Kassanga Ntumbo, Chief Fundikira, Bakari Seif, Seif Hamadi, Aboud Jumbe, Dr. Masha, walikuwa hawana vision au akili ya kujua kuwa baadhi ya maamuzi yaliyokuwa yakifanywa huko nyuma yalikuwa na madhara mbele ya safari,

Mkuu I can go on and on, lakini the messaage is the same kuwa hatuko hapa kwa bahati mbaya, na wote yaaani taifa zima tumehusika kwa njia moja au nyingine kufika tulipo, sasa tunahitaji kutafuta njia za kujitoa tulipo, lakini still either hatuelewi how, au hatuaminiani kiasi kwamba tuko radhi kuwaacha hao hao waliohusika kwa karibu kutufikisha hapa tulipo waendelee na uongozi, I mean CCM ni chama cha siasa sio cha dini au charity, so is Chadema au CUF, sasa kama kila anyeeenda kuingia kwenye uongozi anaishia kuwa sawa na wale wa zamani, inasema nini kuhusu sisi wananchi?

Mkuu ninakubaliana sana na analysis yako nzito kuhusu CCM, isipokuwa tu nina tatizo kuwa hukuangalia deeep kuona matatizo ya viongozi wetu ndani ya CCM yametokea wapi, na pia hutoi mapendekezo ya kutosha of what to do next, maana nina wasi wasi kuwa hiyo inaweza kutufanya wote tukawa part of the very problem we are trying to address, kwa sababu hatutoi applicable solution ambazo ni fit kwa mazingara yetu kijamii na kisiasa, na pia hatusemi na kukubali kuwa tumefikaje tulipo.

Sikusema kuwa CCM inachofanya ni sawa, isipokuwa nimesema kuwa tuwapewe nafasi kwanza, maana recently angalau wameonyesha kuanza kubadilika pole pole, as opposed na kasi ambayo tungependa wawe nayo kwenye kubadilika.

Ahsante Mkuu
 
It seems like some people are expecting some CCM gurus to be fired, have you asked yourself for what and how will that help JK ovecome his shameful incompetence?

Note JK's message in Butiama (a few seconds ago):

"NEC kwa kawaida huwa ni kikao kizito na kinachotoa maamuzi mazito; kwahiyo wanaofikiria kuwa kuna maamuzi mazito yatatokea hawajakosea. Lakini hayatakuwa maamuzi ya kubadili maamuzi ya kisera na kiitikadi katika uchumi au kisiasa; hatutabadili na kuanza kutaifisha mali au kubadili na kufuta siasa ya vyama vingi."

Sasa kazi kwenu kuutafsiri usemi huo
 
Back
Top Bottom