Kutoka Butiama: Exclusive news

Kutoka Butiama: Exclusive news

Mkuu FMES,

Historia inasema dhahiri tuliburuzwa, je ni mpaka lini tutalia "utumwa" wa mawazo bila kuamka na kufanya mageuzi? Hata kama tulikulia katika "utumwa na unyonge" wa mawazo, ni vipi basi kila aliye kiongozi wa CCM ana kaugonjwa hako?

Mbaya zaidi ni kule kudanganyika kwa umma na unachokisema kuwa tumelelewa na "utumwa na unyonge wa mawazo", lakini CCM ya sasa inajua wazi kuwa FMES na wale 80% bado wanaamini kuwa wao ni "watumwa na wanyonge" wa mawazo hivyo tutumie vigezo hivyo hivyo kuhalalisha uharamia na ubabe wa chama kwa kujenga hofu kwa yule ambaye atakikosoa chama au kutishia usalama wa nchi kwa kuwaambia hawa "watumwa na wanyonge" kuwa mkichagua mwingine ambaye hana "baraka" zetu, mtaangamia!

Kina Kisori, Butiku, Iddi Simba, Anna Kilango, Mwakyembe na wengine ambao ni CCM ambao wameamka na kuanza kuhoji yale matumizi ya uonevu ya uongozi wa CCM wa kufanya kila mtu ni lazima awe "mtumwa na mnyonge" wa mawazo au kauli ni dalili wazi kuwa kuna mwamko mpya na ndio huu naushangilia.

Ni kweli hata Butiku na kelele zake zote si mtu kamili asiye na walakini, lakini kutoka kwake mekoni na kutamka wazi udhaifu wa chama ni swala la kupongezwa na si kukehebehiwa. Ilhali ni sawa na Mama Kilango au Kisori ambao sasa wanapata nguvu na sauti na kugundua kuwa "Utumwa na Unyonge" ulikuwa ni wa kujitakia na ulikomaa kutokana na mazingira ya awali.

Tulishafika pabaya, jahazi likagota mchangani, lakini wengine tumeamka na tunadai kwa Sauti za juu, tena kali zikiandamana na vinubi,baragumu na zumari, tunasema "enough is enough! Ndio maana hata nikatoa hoja kwa Kikwete kumsema kuwa "kosa ni kurudia, kulinda na kuendeleza makosa"!

Mimi sikimbilii historia tena au kuuliza fupa lililomshinda Mwalimu, Mwinyi na Mkapa eti limshinde Kikwete. Infact sasa hivi, kwa sauti zetu na uzalendo, tunampa Kikwete na wenzake wa CCM (hata upinzani) nyenzo za kutosha sana kuleta mageuzi ambayo yatamkomboa Mtanzania katika Utumwa na Unyonge ambao umemdumaza na kumfanya aendelee kunyanyaswa na Umasikini, Ujinga na Maradhi.

Swali kwao walioko Butiama, je pamoja na kasi yenu ya kudai mjisafishe na kuwa waadilifu, je mko tayari kubadilika na kuwa wenye mambo endelevu kwa maslahi ya Taifa na si maslahi ya Chama chenu?

Nitamjibu Kitila na Mkandara; Katiba ya CCM, Ilani zake za Uchaguzi, Miongozo na hata madniko na sera nyingi, zina kipa Chama kipaumbele kabla ya Serikali. Ndio maana nimehoji NEC na CC kuwa na nguvu kubwa kuliko Bunge! Kila tamshi wanalotoa CCM ni kuhusu Chama chao, its about them, only them and nation comes second!

That attitude needs to change and it is only the CCM leadership will be able to change such mentality and attitude. If they make those changes and stick to them, you will start seeing progress being made, Serikali will become Serikali ya Wananchi na si ya CCM na uwajibikaji kwa mujibu wa Katiba na Sheria za NCHI utarudi.

As of now, loyalty ya watendaji wa CCM na nidhamu yao ni kwa kuogopa vikao hivi viwili vinavyofanyika sasa hivi Butiama!
REJEA POSTING YANGU...PALE CCM WALIPOMTEMA ZITTO HUKO BUNGENI KWA MASLAHI YA KIUSHABIKI WA CHAMA NA KUYATELEKEZA MASLAHI MUHIMU YA TAIFA HADI HAPO JF ILIPOPIGA KELELE ZA KUFA MTU!NA NDIPO MH RAIS AKAUNDA TUME NA KUMPA ZITO A "SYMBOLIC POLE"
 
Mnasema Mkapa hayupo Butiama ama mimi sijaelewa ?
Naona tunazinguana hakuna nyeti hata moja imeleak na leo mkutano ndio mwisho ,inaonyesha CCM imefanikiwa kuwazibiti wanavyanzo wa mtandao wa JF ambao walikuwa hawalazi damu kwa habari za ndani ,ambazo zilikuwa mwanzo hujitokeza hapa JF ,lakini sasa huonekana kwenye magazeti na kisha ndio JF.
Pengine ni matatizo ya internate ambayo bado hayajafika katika mikoa iliyopo vichochoroni ,huwezi kujua ,bado Tz haina mawasiliano ya internate na baadhi ya mikoa.Tunasubiri kuona yalioyojiri huko kwenye makutano makuu ya mafisadi.
 
Rev. Kishoka, yuko sawa.. kuwa Katiba ya CCM inasema wajibu wa mwanaCCM kwanza ni kwa chama chake na siyo nchi yake. Hili halina mjadala. Sasa naomba mumuombe radhi Mchungaji kwa kudhani ameexaggerate kwa kiasi kikubwa.
 
What the hell...? Yaani chama kinawekwa mbele ya taifa...na hakuna mtu aliyewahi kuhoji na kutaka hicho kipengele kibadilishwe? Na sijui ni nani aliyekuja na hiyo.....
 
What the hell...? Yaani chama kinawekwa mbele ya taifa...na hakuna mtu aliyewahi kuhoji na kutaka hicho kipengele kibadilishwe? Na sijui ni nani aliyekuja na hiyo.....

kuwekwa mbele nafikiri ni kwa maana kwamba chama kitumikie serikali (ndio maana chama kimewekwa mbele) maana lazima uwe na chama kuendesha serikali (najua pia kuna independents) lakini kwa mtazamo wangu ni kwamba ukiweka serikali mbele, then itabidi utumikie chama !

sasa mnataka katiba ibadilike serikali iwekwe mbele kutumikia chama au vice versa ?
 
kuwekwa mbele nafikiri ni kwa maana kwamba chama kitumikie serikali (ndio maana chama kimewekwa mbele) maana lazima uwe na chama kuendesha serikali (najua pia kuna independents) lakini kwa mtazamo wangu ni kwamba ukiweka serikali mbele, then itabidi utumikie chama !

sasa mnataka katiba ibadilike serikali iwekwe mbele kutumikia chama au vice versa ?


Sasa hivi kikubwa tunachokiona ni maslahi ya Chama yako mbele, au kwa usahihi zaidi maslahi ya core ya wana-CCM yaani wenye chama na wanaonufaika nacho, sujui kama wewe kada ni mmoja wao. Kwa hiyo Ukweli ni kuwa kwa CCM maslahi ya taifa ni jambo la tatu, kwanza ni maslahi ya wana CCM binafsi, then ya chama then ya taifa. Hapa hatuwezi kudanganywa hilo likowazi, Kwa hiyo mkuu Kada anza upya!
 
Rev. Kishoka, yuko sawa.. kuwa Katiba ya CCM inasema wajibu wa mwanaCCM kwanza ni kwa chama chake na siyo nchi yake. Hili halina mjadala. Sasa naomba mumuombe radhi Mchungaji kwa kudhani ameexaggerate kwa kiasi kikubwa.

Mwanakijiji,

Tuletee hicho kifungu basi, kwanini tuandikie mate wakati wino upo? Katiba ya CCM iko mtandaoni kwahiyo unaweza kuisoma na ukaleta kifungu tukijadili.

Ku interpret matendo ya viongozi wa CCM kama ndio maamuzi ya chama au ndivyo chama kilivyokubaliana ni makosa makubwa.

Nafikiri unaelewa maana ya Power, na kuanzia individuals, makampuni, kwenye nyumba mpaka kwenye vyama kunakuwa na power struggle. Politics ni aina moja wapo ya organisations kama organisations zingine na humo kuna power struggles kubwa. Power struggle ipo kwasababu malengo na expectations za individual haziko sawa. Ndio maana kila mtu huvutia kwake. Wengine wanasema organisations are rational, lakini ukweli hauko hivyo with 100%. So long as
individuals aims and expectations are different, suala la kwamba organisation kuwa rational sahau.

Ndio maana utasikia Democratic wakiwaambia Republicans kwamba wanajali maslahi ya chama chao na wala sio nchi. Utasikia Conservatives hapa UK wakiwaambia Labour hivyo hivyo na kinyume chake. Pia utasikia CHADEMA wakiwaambia hivyo CCM au CCM wakiwaambia CHADEMA. Au hata nyumbani, utasikia mama anamwambia baba anajali maslahi yake na wala hajali maslahi ya familia. nk.

Katika mifano yote hiyo huwezi kusema with certainty kwamba katiba zao zinasema chama mbele kwanza na taifa baadaye. Au kwamba lengo lao ni kuweka maslahi ya chama mbele kuliko taifa.

Hiyo ni jitihada tu ya hayo makundi kulinda power waliyo nayo. Hata hapa JF unaweza kuona jinsi baadhi ya watu walivyo na power kubwa kuliko wengine na jinsi wanavyojaribu kutumia alliances mbalimbali ili kuilinda angalia mfano Mwanakijiji na Mwafrika wa Kike kwi kwi kwi!!! natania tu jamani, msije mkaniua bure.

Utakuwa very naive kuamini kwamba kwa mtindo wa sasa wa politics za Tanzania, chama kingine kitafanya tofauti. Wakiingia madarakani watafanya hivyo hivyo.

Kinachotakiwa kwasasa ni kwa Watanzania kuungana kuhakikisha suala la katiba linashughulikia ili kujaribu kuifanya serikali isiwe mahali pa
individuals kutumia njia mbalimbali zikiwemo haramu ili kubaki madarakani. Ni katiba na sheria tu ambazo zitafanya viongozi wetu waonekane wana aims na objectives zinazofanana na hivyo hata nchi yetu kuwa rational kwa kiasi fulani.
 
Tuletee hicho kifungu basi, kwanini tuandikie mate wakati wino upo? Katiba ya CCM iko mtandaoni kwahiyo unaweza kuisoma na ukaleta kifungu tukijadili
Iko hapa: [media]http://www.ccmtz.org/Katiba_ya_CCM____ENG_2005_.pdf[/media]
 
HABARI za uhakika zinasema kuwa baadhi ya marais na mawaziri wakuu wastaafu wa Tanzania wamegoma kwenda Butiama kushiriki vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM. Siku chache zilizopita, baadhi yao, chini ya Mzee Ali Hassan Mwinyi, walikuwa na kikao cha dharura kujadili namna ya kuinusuru CCM kutoka kwa mafisadi. Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye hawakualikwa. Wajumbe wa kikao cha Mwinyi waliazimia kutumia kikao cha Butiama kumlazimisha Rais Jakaya Kikwete achukue hatua mbili muhimu.

Kwanza, atumie mamlaka aliyonayo kuhakikisha vikao hivyo vinawavua uanachama wale wote waliotuhumiwa katika kashfa za EPA na Richmond. Pili, walitaka atumie nguvu hiyo hiyo, kumuondolea kinga Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, ili afikishwe mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili, na aweze kutoa ushahidi katika kesi ya Balozi Costa Mahalu ambaye amemtaja kama shahidi mkuu.

Ushauri walioupata kwa Mzee Joseph Sinde Warioba ni kwamba ikibidi, Mkapa aondolewe kinga kwa muda tu kwa ajili ya kesi ya Mahalu, halafu arejeshewe.

Katika kikao hicho, Mzee Mwinyi aliwashauri wenzake kwamba iwapo Kikwete atakataa kuchukua hatua hizo, itokee vurumai kubwa, hata kama itawalazimu kuivunja CCM na kuwa CCM A na CCM B. Wazo la CCM kuvunjika halikumpendeza Rais Mstaafu wa Zanzibar, Salmin Amour; kwa maelezo kuwa CCM ikivunjika itakuwa faida ya wapinzani, hasa Zanzibar.

Kwa hiyo, walikubaliana kuwa badala ya kuvunja chama, kama Kikwete hakubali ushauri wao, wao watagoma kushiriki kikao hicho. Alipokataa, kama walivyotarajia, wakaamua kutokushiriki.

Hata baada ya kuamua kutokwenda Butiama, hawakumtaarifu mwenyekiti wao (Kikwete). Alitaarifiwa na watu wa protokol walipokuwa wanaandaa usafiri wa wastaafu hao, huku kila mmoja akitoa udhuru wake papo hapo.

Baadhi yao, wakiwamo Mwinyi, Salim Ahmed Salim, Mkapa na Sumaye, wanasemekana kwenda nje ya nchi katika kipindi walichohitajika kwenda Butiama.

Sababu mojawapo ya Kikwete kukataa kuwachukulia hatua mafisadi wa EPA na Rihmond inasemekana ni hatua yake ya kuwalinda (au kuwaogopa) rafiki zake Edward Lowassa na Rostam Azizi ambao ni watuhumiwa wakuu wa Richmond. Na inasemekana sasa Kikwete amelazimika kuanza mkakati mpya wa kumbeba Lowassa, jambo ambalo limezua 'uhasama' kati yake (JK) na Spika wa Bunge, Samuel Sitta.

Kumeguka kwa wastaafu, hasa Mzee Mwinyi, kutoka kambi ya Kikwete, si habari ndogo. Inafikirisha na kuzua maswali magumu juu ya hatima ya chama na uongozi mzima wa Kikwete. Hadi habari hii inaandikwa, wastaafu walioonekana Butiama wakati kikao cha Kamati Kuu kinaendelea ni Rashid Kawawa, John Malecela na Gharib Bilal. Walio Butiama tuletee habari kuhusu Joseph Sinde Warioba na Cleopa Msuya.

Kutoka: http://www.ngurumo.blogspot.com/
 
Mkuu FMES,

Historia inasema dhahiri tuliburuzwa, je ni mpaka lini tutalia "utumwa" wa mawazo bila kuamka na kufanya mageuzi? Hata kama tulikulia katika "utumwa na unyonge" wa mawazo, ni vipi basi kila aliye kiongozi wa CCM ana kaugonjwa hako?

Mbaya zaidi ni kule kudanganyika kwa umma na unachokisema kuwa tumelelewa na "utumwa na unyonge wa mawazo", lakini CCM ya sasa inajua wazi kuwa FMES na wale 80% bado wanaamini kuwa wao ni "watumwa na wanyonge" wa mawazo hivyo tutumie vigezo hivyo hivyo kuhalalisha uharamia na ubabe wa chama kwa kujenga hofu kwa yule ambaye atakikosoa chama au kutishia usalama wa nchi kwa kuwaambia hawa "watumwa na wanyonge" kuwa mkichagua mwingine ambaye hana "baraka" zetu, mtaangamia!

Kina Kisori, Butiku, Iddi Simba, Anna Kilango, Mwakyembe na wengine ambao ni CCM ambao wameamka na kuanza kuhoji yale matumizi ya uonevu ya uongozi wa CCM wa kufanya kila mtu ni lazima awe "mtumwa na mnyonge" wa mawazo au kauli ni dalili wazi kuwa kuna mwamko mpya na ndio huu naushangilia.

Ni kweli hata Butiku na kelele zake zote si mtu kamili asiye na walakini, lakini kutoka kwake mekoni na kutamka wazi udhaifu wa chama ni swala la kupongezwa na si kukehebehiwa. Ilhali ni sawa na Mama Kilango au Kisori ambao sasa wanapata nguvu na sauti na kugundua kuwa "Utumwa na Unyonge" ulikuwa ni wa kujitakia na ulikomaa kutokana na mazingira ya awali.

Tulishafika pabaya, jahazi likagota mchangani, lakini wengine tumeamka na tunadai kwa Sauti za juu, tena kali zikiandamana na vinubi,baragumu na zumari, tunasema "enough is enough! Ndio maana hata nikatoa hoja kwa Kikwete kumsema kuwa "kosa ni kurudia, kulinda na kuendeleza makosa"!

Mimi sikimbilii historia tena au kuuliza fupa lililomshinda Mwalimu, Mwinyi na Mkapa eti limshinde Kikwete. Infact sasa hivi, kwa sauti zetu na uzalendo, tunampa Kikwete na wenzake wa CCM (hata upinzani) nyenzo za kutosha sana kuleta mageuzi ambayo yatamkomboa Mtanzania katika Utumwa na Unyonge ambao umemdumaza na kumfanya aendelee kunyanyaswa na Umasikini, Ujinga na Maradhi.

Swali kwao walioko Butiama, je pamoja na kasi yenu ya kudai mjisafishe na kuwa waadilifu, je mko tayari kubadilika na kuwa wenye mambo endelevu kwa maslahi ya Taifa na si maslahi ya Chama chenu?

Nitamjibu Kitila na Mkandara; Katiba ya CCM, Ilani zake za Uchaguzi, Miongozo na hata madniko na sera nyingi, zina kipa Chama kipaumbele kabla ya Serikali. Ndio maana nimehoji NEC na CC kuwa na nguvu kubwa kuliko Bunge! Kila tamshi wanalotoa CCM ni kuhusu Chama chao, its about them, only them and nation comes second!

That attitude needs to change and it is only the CCM leadership will be able to change such mentality and attitude. If they make those changes and stick to them, you will start seeing progress being made, Serikali will become Serikali ya Wananchi na si ya CCM na uwajibikaji kwa mujibu wa Katiba na Sheria za NCHI utarudi.

As of now, loyalty ya watendaji wa CCM na nidhamu yao ni kwa kuogopa vikao hivi viwili vinavyofanyika sasa hivi Butiama!

Mkuu wangu Kishoka,

Ninaweza kusema unaongea Utopian kwi kwi kwi!!! Inaelekea maandishi ya akina Walter Rodney uliyasoma sana A-level (Ni utani tu).

Serikali ya wananchi? Unaota, hakuna serikali ya wananchi mahali popote.
Wananchi wote hatuwezi kuongoza, badala yake tuna outsource hiyo kazi na kukipa chama kimoja ili kiongoze kwa niaba yetu.

Kama ilivyo kwenye shirika, unapotaka ku outsource kazi, unaangali nani atatimiza hiyo kazi kwa ufanisi zaidi kwa faida yako. Kukiwa na washindani wengi wenye sifa, hapo unakuwa na nafasi kubwa ya kupata kampuni inayofaa na itakayowajibika.

Tatizo la Tanzania na nchi nyingi za Afrika, kwanza ni kwamba sisi wananchi hatujui hizo kazi tunazotaka ku outsource zifanywe vipi, yaani hata sisi wenyewe tungeamua tuzifanye huenda tungevurunda. Pili kwenye pool la hao tunaotaka kuwapa kazi, kuna wahusika wachache sana. Hakuna competition ya kutosha, matokeo yake tunajikuta tunaipa kampuni ile ile hata kama inavurunda.

Hapa kuna mambo mawili yanatakiwa kufanyika, kwanza ni kuongeza uwezo wa wananchi kuelewa mambo. Civil societies ikiwemo JF ina kazi ya kuhakikisha wananchi mpaka vijijini wanaelemika ili wanapoamua ku outsource uongozi wa nchi, wafanye maamuzi ya busara na kukipa chama ambacho kitasaidia nchi kwenda mbele. Kama ulivyosema kwenye maandishi yako hapa ndio pana shida sana. Usitegemee CCM watataka kuwaamsha wananchi, ukiamini hivyo utakuwa very naive. CCM wangependa wananchi waendelee kuwa wajinga wajinga, waendelee kuimba chama chetu nk. Kwa kufanya hivyo wanajijengea mazingira ya kuongoza milele. Lengo la vyombo kama JF ni kinyume na CCM, lengo letu sisi liwe kuwakomboa hawa wananchi kimawazo ili waelewe haki zao za msingi ikiwa ni pamoja na kwamba CCM wamewekwa madarakani ili wawasaidie wananchi na sio kinyume chake.

Jambo la pili ni kuhakikisha kwamba wananchi wakielewa wanataka kampuni (chama) ya aina gani basi kwenye pool la vyama, kunakuwa na vyama vingi ambavyo vinashindana kwa ubora kiasi kwamba wanaweza kuchagua chama kinachofaa. Hapa ni sawa na makampuni ya mobiles Tanzania. Kwanza inatakiwa wananchi waelewe haki zao ikwemo kujua dakika moja inagharimu pesa ngapi, ubora wa network na services zingine. Kazi ya pili ni kwamba kuna mashirika mengi ambayo yanashindana kwa sifa hizo, vodacome, celtel,ttcl nk. Hapa napo tuna matatizo makubwa. Kwasasa labda vyama tunavyoweza kusema japo vinasifa za kuitwa vyama ni CCM, CHADEMA na CUF. Ushindani hapo uko chini sana na inafika mahali wananchi hawana choice na hivyo kuirudisha CCM. Muungano wa vyama vya upinzani hapa ungetusaidia sana ili tuwe na vyama viwili vyenye nguvu vikishindania hii tender ya kuongoza nchi.

Ni kutokana na kufanyika kwa mambo mawili hapo juu, vyama vyetu vitaanza kujiosha ili viweze kuchagulika. Wale ambao hawajisafishi vizuri, ukifika uchaguzi wanatupwa nje, wanaishia kuwa kama Mobitel. Mambo hayo mawili yakishindwa kufanyika CCM watendelea kugawana dividends kubwa na kusahau quality au services kwa customers wao. Wanajua wananchi hawawezi kuwatema.

Kuna watu wanasema matumizi ya vyombo vya dola, hiyo ni kweli. Chukulia hilo kama ni monopoly kwenye mashirika ya umma, lakini kukiwa na ushindani wa kweli hata monopoly haifanyi kazi. Ndio maana Malawi, Zambia, Kenya na kwingineko, siku ilipofika watawala waling'olewa.

Binafsi naamini muhimu ni hayo mambo mawili niliyoyataja hapo juu.

Sasa wacha sisi JF tutumie nguvu zetu, uwezo wetu kuharakisha mabadiliko kwa kuwa cheche ya mawazo mapya na elimu kwa wananchi na sio matusi au kuandika mambo ambayo hayaungwi mkono na facts. Pili tujiandae kushiriki
kutafuta tender ya uongozi ili tukipata tuwaonyeshe wananchi, tunaweza ku deliver better services kuliko hao viongozi wao wa sasa. Tusitegemee hata siku moja kwamba CCM au CHADEMA watakuja kupata malaika ambaye atasaidia kubadilisha mfumo wetu wa uongozi. Tunatakiwa kuwalazimisha hawa viongozi wetu ili wabadilike. Wanataka uongozi (power) hivyo wakiona wasipobadilika, watakosa huo uongozi, watabadilika tu.
 
Iko hapa: [media]http://www.ccmtz.org/Katiba_ya_CCM____ENG_2005_.pdf[/media]

Tina,

Asante kwa link ya CCM. Nilichotaka ni kifungu kipi kwenye hiyo katiba? Mimi nimepitia sijaona kitu kama hicho. Utatusaidia kama utataja hicho kifungu.
 
Kwa kuzingatia matamko mbalimbali ya JK na She-Makamba sioni kama kuna maamuzi mazito yatatolewa butiama, why?

1. JK hajaonyesha political will kuwashughulikia mafisadi ndio maana katika hotuba aliyotoa kwa wazee wa ccm dar mwezi Feb baada ya lowassa kuachia ngazi hakutoa karipio zaidi ya kusema ni ajali ya kisiasa.So dont expect lowassa na mafisadi wengine kuchukuliwa hatua yoyote zaidi ya kupongezwa kwa uamuzi waliochukua kujiuzulu

2. She-Makamba keshasema hakuna mwanachama atafukuzwa.

3.Mabadiliko ya itikadi na sera hayatakuwepo maana JK Keshaliweka wazi.Kwa hiyo tutegemee wanachama kuwa watiifu na kutoa kipaumbele kwa ccm kwanza kabla ya kufikiria taifa.Kwa msingi huu tutaendelea kuwa na wabunge wa ccm makondoo wasiohoji na kuwa Rubber stamp na "Mr Yesman"

4. CCM Imepata fedha za kifisadi za EPA so siyo rahisi kutoa uamuzi ambao utakuwa wa kujinyonga. Je mwizi anaweza kujihukumu?

5. Sioni uwezekano wa kukemea maovu ya Nkapa na yonah kufanya biashara ikulu. Mtakumbuka JK alisema "Mwache nkapa apumzike kwa amani". Na pia mtakumbuka katiba inaziba mianya ya kumshitaki rais mstaafu labda jk aondoe kinga. Je ataweza? kwanza nkapa hajaenda butiama. Tusubiri maumivu zaidi kwenye umeme tanpower/kiwira wakianza kuuza umeme kwa tanesco.Mhh kasheshe

6. Mpasuko zanzibar. Natabiri ccm zanzibar hawatakubali serikali mseto maana kumpa seif uwaziri kiongozi ni kumpa nguvu kushinda 2010.Je ccm wapo tayari kwa hilo?

Haya wazee wa jamvi tuendelee kutega sikio kusikia tunachotarajia toka butiama.
 
Kwa kuzingatia matamko mbalimbali ya JK na She-Makamba sioni kama kuna maamuzi mazito yatatolewa butiama, why?

1. JK hajaonyesha political will kuwashughulikia mafisadi ndio maana katika hotuba aliyotoa kwa wazee wa ccm dar mwezi Feb baada ya lowassa kuachia ngazi hakutoa karipio zaidi ya kusema ni ajali ya kisiasa.So dont expect lowassa na mafisadi wengine kuchukuliwa hatua yoyote zaidi ya kupongezwa kwa uamuzi waliochukua kujiuzulu

2. She-Makamba keshasema hakuna mwanachama atafukuzwa.

3.Mabadiliko ya itikadi na sera hayatakuwepo maana JK Keshaliweka wazi.Kwa hiyo tutegemee wanachama kuwa watiifu na kutoa kipaumbele kwa ccm kwanza kabla ya kufikiria taifa.Kwa msingi huu tutaendelea kuwa na wabunge wa ccm makondoo wasiohoji na kuwa Rubber stamp na "Mr Yesman"

4. CCM Imepata fedha za kifisadi za EPA so siyo rahisi kutoa uamuzi ambao utakuwa wa kujinyonga. Je mwizi anaweza kujihukumu?

5. Sioni uwezekano wa kukemea maovu ya Nkapa na yonah kufanya biashara ikulu. Mtakumbuka JK alisema "Mwache nkapa apumzike kwa amani". Na pia mtakumbuka katiba inaziba mianya ya kumshitaki rais mstaafu labda jk aondoe kinga. Je ataweza? kwanza nkapa hajaenda butiama. Tusubiri maumivu zaidi kwenye umeme tanpower/kiwira wakianza kuuza umeme kwa tanesco.Mhh kasheshe

6. Mpasuko zanzibar. Natabiri ccm zanzibar hawatakubali serikali mseto maana kumpa seif uwaziri kiongozi ni kumpa nguvu kushinda 2010.Je ccm wapo tayari kwa hilo?

Haya wazee wa jamvi tuendelee kutega sikio kusikia tunachotarajia toka butiama.

Mkuu umeanisha mambo vizuri kabisa, lakini ukiangalia kwa undani, inaonekana JK anataka kukwepa yale anayotakiwa kufanya, na kama akikwepa kuwachukulia hatua mafisadi, kama ikiikwepa EPA au akiirashia rashia mkutanoni, akimkalia kimya Nkapa, na baya zaidi akiukalia kimya muafaka na kupoteza nafasi hii, for sure itaonekana wazi kabisa kuwa hafai kuwa rais, na hafai kuwa mwenyekiti wa CCM, na atakuwa ameweka greenlight kwa watu kuitafuta nafasi hiyo 2010. Hizo issues ni kidonge kichungu ambacho anatakiwa kukinywa ili aweze, kutibu ugonjwa uliopo ndani ya chama na kwenye Uongozi wake.
Kusikiliza anayosema Makamba ni sawa na kujisumbua, yule mzee ni story nyingi ambazo hazina substance, achana naye hata haoni umuhimu wa kiti alichonacho na hana hata busara ya kumshauri mwenyekiti la maana.
Kweli Butiama inaweza kuwa Begining of the End.
 
Inasikitisha sana kuona nchi yetu sasa hivi haishughulikii tena maendeleo ya nchi. Rais na Mawaziri wake wako bize kujibu tuhuma za ufisadi, kuchambua mapungufu ya serikali ya awamu ya tatu na blah blah nyingi tu.

Hakuan juhudi zozote za makusudi katika kuinua uchumi katika sekta mbalimbali. Sasa hivi mabaya ya serikali ya awamu ya nne yamefunikwa na habari za ufisadi na kashfa kubwa kubwa kama Richmond. Mfumuko wa bei unazidi kuongezeka, bei ya mafuta bado iko juu licha ya serikali kuondoa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), miundombinu ni mibovu kupindukia, hasa kwa wakazi wa Dar es Salaam (Usiulize kuhusu vijijini kwani huko neno miundombinu ni msamiati).

Pia wagonjwa bado walala chini mahospitalini na wengine kufa kila siku kwa kukosa pesa za kununulia dawa, wanafunzi bado wanakaa chini na idadi yao imeongezeka maradufu kutokana na mpango wa MEM na MES.Mashule hayana vitabu na vifaa vingine vya kufundishia. Walimu hawatoshi na waliopo wanaishi katika mazingira duni hasa kwa shule za vijijini. Kilimo, ambacho ndio uti wa mgongo wa taifa kinazidi kudorora na pesa za kukiboresha zimechotwa na wajanja pale BOT.

Kwa kifupi safari hii tuna serikali ya "saa mbili kamili usiku". Nina maanisha serikali ya kwenye taarifa ya habari ya saa mbili kamili usiku pale ambapo kila kiongozi anajitahidi kupata "media coverage" ili aonekane anafanya kazi. Tume zinaundwa kila siku, tena sio za kufanya R&D, hapana! Ni za kuchunguza pale ambapo mambo yamekosewa, kuna wizi na kadhalika. Hapo wanatumia pesa za walipa kodi. Nina wasiwasi kwamba pesa za EPA zitarudishwa na wezi wa serikali ya awamu ya tatu, halafu zitaibiwa tena na mafisadi wa serikali ya awamu ya nne! The work done might be ZERO. Tunakwenda wapi?

Naomba kuuliza swali moja kwa JK. Tangu aingie madarakani, atutajie kitu kimoja tu kikubwa na cha manufaa kwa uchumi wa taifa hili ambacho amekifanya. Hapa nazungumzia Uchumi.
 
Naomba kuuliza swali moja kwa JK. Tangu aingie madarakani, atutajie kitu kimoja tu kikubwa na cha manufaa kwa uchumi wa taifa hili ambacho amekifanya. Hapa nazungumzia Uchumi.

Atakuambia amemleta rais Bush. Kwao rais Bush na ombaomba ya misaada ndio uchumi.

Tuna tatizo kubwa sana.
 
Pengine ni matatizo ya internet ambayo bado hayajafika katika mikoa iliyopo vichochoroni ,huwezi kujua ,bado Tz haina mawasiliano ya internate na baadhi ya mikoa.Tunasubiri kuona yalioyojiri huko kwenye makutano makuu ya mafisadi.

..labda mkoani kwenu,musoma internet ipo!

..taja mikoa ambayo haina internet tz?
 
HABARI za uhakika zinasema kuwa baadhi ya marais na mawaziri wakuu wastaafu wa Tanzania wamegoma kwenda Butiama kushiriki vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM. Siku chache zilizopita, baadhi yao, chini ya Mzee Ali Hassan Mwinyi, walikuwa na kikao cha dharura kujadili namna ya kuinusuru CCM kutoka kwa mafisadi. Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye hawakualikwa. Wajumbe wa kikao cha Mwinyi waliazimia kutumia kikao cha Butiama kumlazimisha Rais Jakaya Kikwete achukue hatua mbili muhimu.

Kwanza, atumie mamlaka aliyonayo kuhakikisha vikao hivyo vinawavua uanachama wale wote waliotuhumiwa katika kashfa za EPA na Richmond. Pili, walitaka atumie nguvu hiyo hiyo, kumuondolea kinga Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, ili afikishwe mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili, na aweze kutoa ushahidi katika kesi ya Balozi Costa Mahalu ambaye amemtaja kama shahidi mkuu.

Ushauri walioupata kwa Mzee Joseph Sinde Warioba ni kwamba ikibidi, Mkapa aondolewe kinga kwa muda tu kwa ajili ya kesi ya Mahalu, halafu arejeshewe.

Katika kikao hicho, Mzee Mwinyi aliwashauri wenzake kwamba iwapo Kikwete atakataa kuchukua hatua hizo, itokee vurumai kubwa, hata kama itawalazimu kuivunja CCM na kuwa CCM A na CCM B. Wazo la CCM kuvunjika halikumpendeza Rais Mstaafu wa Zanzibar, Salmin Amour; kwa maelezo kuwa CCM ikivunjika itakuwa faida ya wapinzani, hasa Zanzibar.

Kwa hiyo, walikubaliana kuwa badala ya kuvunja chama, kama Kikwete hakubali ushauri wao, wao watagoma kushiriki kikao hicho. Alipokataa, kama walivyotarajia, wakaamua kutokushiriki.

Hata baada ya kuamua kutokwenda Butiama, hawakumtaarifu mwenyekiti wao (Kikwete). Alitaarifiwa na watu wa protokol walipokuwa wanaandaa usafiri wa wastaafu hao, huku kila mmoja akitoa udhuru wake papo hapo.

Baadhi yao, wakiwamo Mwinyi, Salim Ahmed Salim, Mkapa na Sumaye, wanasemekana kwenda nje ya nchi katika kipindi walichohitajika kwenda Butiama.

Sababu mojawapo ya Kikwete kukataa kuwachukulia hatua mafisadi wa EPA na Rihmond inasemekana ni hatua yake ya kuwalinda (au kuwaogopa) rafiki zake Edward Lowassa na Rostam Azizi ambao ni watuhumiwa wakuu wa Richmond. Na inasemekana sasa Kikwete amelazimika kuanza mkakati mpya wa kumbeba Lowassa, jambo ambalo limezua 'uhasama' kati yake (JK) na Spika wa Bunge, Samuel Sitta.

Kumeguka kwa wastaafu, hasa Mzee Mwinyi, kutoka kambi ya Kikwete, si habari ndogo. Inafikirisha na kuzua maswali magumu juu ya hatima ya chama na uongozi mzima wa Kikwete. Hadi habari hii inaandikwa, wastaafu walioonekana Butiama wakati kikao cha Kamati Kuu kinaendelea ni Rashid Kawawa, John Malecela na Gharib Bilal. Walio Butiama tuletee habari kuhusu Joseph Sinde Warioba na Cleopa Msuya.

Kutoka: http://www.ngurumo.blogspot.com/

Sina hakika kuhusu authenticity na accuracy ya hii post, lakini kama ni kweli basi Mwinyi ataenda down in history kama statesman na Kikwete asipoangalia anaweza kukosa nomination ya CCM come 2010.
 
Back
Top Bottom