Kutoka kuwa Mkurugenzi wa TISS na kuwa IGP hii imekaaje?

Nani mwenye cheo kikubwa? je mtu kwa mfano akitolewa kuwa mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama wa taifa TISS na kupewa u-IGP inakuwa imekaaje? je anakuwa kapanda cheo au kashushwa cheo nani mkubwa kati ya Mkurugenzi wa TISS na IGP maana duh.!
Hivi ni vyombo vya ulinzi na usalama
  1. Top Mkuu wao ni CinC- Amiri Jeshi Mkuu
  2. CDF ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi
  3. DGIS ni Mkuu wa jeshi la usalama
  4. IGP ni Mkuu wa jeshi la polisi
  5. Commissioner of Magereza
  6. Commissioner of Uhamiaji
  7. Commissioner of Zimamoto
  8. Commissioner wa Tume ya madawa kulevya
P
 
Hivi kumbe kuna jeshi la usalama
 
9. Ongezea TAKUKURU hao wote kama ulivyowataja ni Line Officers. Anyway Kulwa na Dotto nani Mkubwa vile??
 

Hivi kati ya Amiri jeshi na Amiri jeshi mkuu, cheo kipi ni sahihi kwa C in C?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Wote wako sawa na hata huduma zao ziko sawa. Na hata wakistaafu bado wana pata huduma sawa hadi wafe. Na wana haki sawa kutoa taarifa kwa mkuu wanchi..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
IGP yuko juu, miaka 20+ nyuma TISS haikuwepo isipokuwa ilikuwa ni tawi maalumu la jeshi la polisi, alivyoingia Rais Mkapa ndio hii Taasisi ikaundwa na kutolewa jeshi la polisi na kuanza kujitegemea na vilevile ikahamishiwa wizara ya utumishi na utawala bora,

Kwa hiyo mtu wa TISS anaweza kufanya kazi jeshi la polisi hususani kwenye upande wa kukusanya taarifa na kuzichambua (UPELELEZI) na vilevile mtu mwenye taaluma ya upelelezi wajeshi la polisi anaweza akafanya kazi TISS kama kutakuwa na tofauti ya kazi zao basi ni kidogo sana.
 
Pascal Mayalla, inaonekana muundo wa TISS kisheria ulifanyiwa kazi wakati wa Rais Mkapa.

Either huku nyuma taasisi hiyo ilikuwa chini ya Mzee Mzena, Col. Hassy Kitine, Ag DGIS Augustine Mahiga, Lt. Gen. Imran Kombe then mabadiliko kisheria yakafanyika wakati wa Apson.

Je wakati huo, kitengo kisheria kilikuwa kikitambulika kwa jina gani??

Naomba kuwasilisha


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo kwenye commisioner of magereza ungeandika commisioner of prisons, na huyo wa migration ukaandika commissioner of shifting
 
Mkuu unajua tunakuamini sana humu,ila sasa unatuchanganya unaposema kuna jeshi la usalama wa taifa,halafu DGTS hawezi kuwa wa tatu kiprotocali kabla ya IGP.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…