Kutoka Singida hadi Dar es Salaam kwa matumaini ya kupata msaada wa elimu

Kutoka Singida hadi Dar es Salaam kwa matumaini ya kupata msaada wa elimu

Inaendelea......

Basi siku hiyo ndio ikaisha hivyo nami nipo kimya tu sikutaka kumshirikisha mtu yeyote hata rafiki yangu ninaelala nae geto moja pia sikumwambia, Basi baada Kama week moja hivi yule mzee alikuja na Gari akashuka hapo alikuwa kavaa miwani nyeusi fulani akaniita njoo kijana wangu nikaenda akaniambia vipi Kuna mtu unamdai nikamjibu hapana, je Kuna mtu anakudai nikasema ndio maana hela ya kazi siku mbili sijakabidhi na ninazo zote Basi akaniambia utamkabidhi Nani Sasa nikamwambia Kuna mtu hapa naweza mkabidhi atampa ni mwaminifu tu.

Baada ya kumjibu maswali hayo nikamuuliza kwani mie naenda wapi kwa mda huu baba angu akaniambia unaenda Tabora shuleni, ukweli hapa sikuamini ninachokisikia masikioni mwangu ghafla machozi yananitoka nikamuuliza ni kweli inawezekana ? Je jina langu bado lipo kweli huko akaniambia wewe nenda shuleni Kama bado unapenda kusoma nikamwambia napenda sana kusoma.

Baada ya hapo nimekabidhi hela nikaandika kibarua kidogo kumwaga rafiki yangu tulikuwa wote getoni maana hakuwa na simu na kipindi hicho wenye simu ni wa kuhesabu maana hata huyo mzee sijui Kama alikuwa nayo maana sikumuona akiwa nayo hata kidogo,
tulianza safari Hadi karume pale nikaambiwa chagua viatu pair 4 hivi nikachagua akalipa mzee tukaondoka Hadi kwenye mashuka akanunua nakuweka kwenye bag tukaanza safari Hadi ubungo nikakatiwa ticket tukaondoka tukaenda nikapelekwa kwa Dada mmoja hivi nikatambulishwa nikaambiwa huyu dada atakupeleka stand asubuhi, mzee akaniuliza wewe una sh ngapi hapo mfukoni nikamwambia Nina laki na nusu akaniambia hiyo inakutosha kabisaa njiani mahitaji mengine utayapata shuleni.

Basi kesho yake safari ikaanza Kama siku tatu hivi ndio nikaingia Tabora kumbuka kipindi hicho kwanzia dodoma ni vumbi mwanzo mwisho, nilifika stand pale Tabora maana nilikuwa nimeambiwa ukishuka chukua daladala ya baiskeli mpka hapo shuleni utapokelewa Basi nami niliuliza watu hapo Tabora boys ni wapi nikachukuliwa na daladala Hadi hapo shuleni nikapelekwa ofsi ya mkuu wa shule nikapokelewa na second master akaniuliza wewe ndio Fulani nikasema ndio, basi akaniambia wewe umekuja kusoma au umekuja kuiona shule tu alafu urudi nikamwambia nimekuja kusoma.

Hapo nakumbuka ilikuwa umebaki week moja tu mitahani ya mwezi wa sita ianze Basi nikapelekwa kwa mkuu wa shule nikaambiwa utakaa hapa mpaka shule ikija kufunguliwa ndio utaenda bwenini nikaona hapa sawa na kwenye Chumba tulikuwa wawili na jamaa mmoja alikuwa form six basi tukawa tunapiga story ananitia moyo sana nikaanza kukopy notes na kusoma karibia usiku kucha week likakata , mkuu wa shule aliporudi alinikuta kidogo nimechangamka akaniambia vipi unaweza kufanya mitihani na wenzio nikasema ndio naweza kujaribu akasema sawa Basi jiandae jumatatu mitahani unaanza.

Nami bila kinyongo nilipiga msuli haswa wa kusoma huku yule jamaa wa form six akinitia moyo na kunifundisha sana tena kwa bidii kweli jtatu ikafika nami huyo kwenye Chumba Cha paper nikazama hapo ndipo nilianza rasmi kumwogopa Mungu kwani kila siku nilikuwa naingia kwenye Chumba Cha mtihani nimefunga na haya ndio matokeo yangu ya mtihani wa mwezi wa sita form one nikiwa nimefika shuleni week mbili kabla ya mitahani kuanza,

MATHEMATICS: A 100
PHYSICS. A 95
CHEMISTRY A 98
BIOLOGY. A 100
GEOGRAPHY A 100
HISTORY. A 100
CIVICS. A 98
ENGLISH F 15
KISWAHILI A 100

Baada ya matokeo hayo mkuu wa shule alinambia unastahili kutunzwa kwa gharama yeyote nikasema sawa akaninunulia saa Kama zawadi na maisha yakasonga mbele miaka iliyofuata ikawa napita kwenye kipindi kigumu sana hasa kwenye likizo mda mwingi nilikuwa naweza shinda bila kula na mda mwingine tukifunga shule nami naenda kutafuta vibarua kwa mfano niliendaga huko wilaya ya Uyui kata ya Loya kuvua samaki na mwaka mwingine pia nikaenda huko kuvuna mpunga sikurudi nyumbani maana nilikuwa naogopa kurudi home likizo najua nikirudi naweza nusirudi shuleni tena.



Itaendeleaa.....
 
Inaendelea......

Basi siku hiyo ndio ikaisha hivyo nami nipo kimya tu sikutaka kumshirikisha mtu yeyote hata rafiki yangu ninaelala nae geto moja pia sikumwambia, Basi baada Kama week moja hivi yule mzee alikuja na Gari akashuka hapo alikuwa kavaa miwani nyeusi fulani akaniita njoo kijana wangu nikaenda akaniambia vipi Kuna mtu unamdai nikamjibu hapana, je Kuna mtu anakudai nikasema ndio maana hela ya kazi siku mbili sijakabidhi na ninazo zote Basi akaniambia utamkabidhi Nani Sasa nikamwambia Kuna mtu hapa naweza mkabidhi atampa ni mwaminifu tu.

Baada ya kumjibu maswali hayo nikamuuliza kwani mie naenda wapi kwa mda huu baba angu akaniambia unaenda Tabora shuleni, ukweli hapa sikuamini ninachokisikia masikioni mwangu ghafla machozi yananitoka nikamuuliza ni kweli inawezekana ? Je jina langu bado lipo kweli huko akaniambia wewe nenda shuleni Kama bado unapenda kusoma nikamwambia napenda sana kusoma.

Baada ya hapo nimekabidhi hela nikaandika kibarua kidogo kumwaga rafiki yangu tulikuwa wote getoni maana hakuwa na simu na kipindi hicho wenye simu ni wa kuhesabu maana hata huyo mzee sijui Kama alikuwa nayo maana sikumuona akiwa nayo hata kidogo,
tulianza safari Hadi karume pale nikaambiwa chagua viatu pair 4 hivi nikachagua akalipa mzee tukaondoka Hadi kwenye mashuka akanunua nakuweka kwenye bag tukaanza safari Hadi ubungo nikakatiwa ticket tukaondoka tukaenda nikapelekwa kwa Dada mmoja hivi nikatambulishwa nikaambiwa huyu dada atakupeleka stand asubuhi, mzee akaniuliza wewe una sh ngapi hapo mfukoni nikamwambia Nina laki na nusu akaniambia hiyo inakutosha kabisaa njiani mahitaji mengine utayapata shuleni.

Basi kesho yake safari ikaanza Kama siku tatu hivi ndio nikaingia Tabora kumbuka kipindi hicho kwanzia dodoma ni vumbi mwanzo mwisho, nilifika stand pale Tabora maana nilikuwa nimeambiwa ukishuka chukua daladala ya baiskeli mpka hapo shuleni utapokelewa Basi nami niliuliza watu hapo Tabora boys ni wapi nikachukuliwa na daladala Hadi hapo shuleni nikapelekwa ofsi ya mkuu wa shule nikapokelewa na second master akaniuliza wewe ndio Fulani nikasema ndio, basi akaniambia wewe umekuja kusoma au umekuja kuiona shule tu alafu urudi nikamwambia nimekuja kusoma.

Hapo nakumbuka ilikuwa umebaki week moja tu mitahani ya mwezi wa sita ianze Basi nikapelekwa kwa mkuu wa shule nikaambiwa utakaa hapa mpaka shule ikija kufunguliwa ndio utaenda bwenini nikaona hapa sawa na kwenye Chumba tulikuwa wawili na jamaa mmoja alikuwa form six basi tukawa tunapiga story ananitia moyo sana nikaanza kukopy notes na kusoma karibia usiku kucha week likakata , mkuu wa shule aliporudi alinikuta kidogo nimechangamka akaniambia vipi unaweza kufanya mitihani na wenzio nikasema ndio naweza kujaribu akasema sawa Basi jiandae jumatatu mitahani unaanza.

Nami bila kinyongo nilipiga msuli haswa wa kusoma huku yule jamaa wa form six akinitia moyo na kunifundisha sana tena kwa bidii kweli jtatu ikafika nami huyo kwenye Chumba Cha paper nikazama hapo ndipo nilianza rasmi kumwogopa Mungu kwani kila siku nilikuwa naingia kwenye Chumba Cha mtihani nimefunga na haya ndio matokeo yangu ya mtihani wa mwezi wa sita form one nikiwa nimefika shuleni week mbili kabla ya mitahani kuanza,

MATHEMATICS: A 100
PHYSICS. A 95
CHEMISTRY A 98
BIOLOGY. A 100
GEOGRAPHY A 100
HISTORY. A 100
CIVICS. A 98
ENGLISH F 15
KISWAHILI A 100

Baada ya matokeo hayo mkuu wa shule alinambia unastahili kutunzwa kwa gharama yeyote nikasema sawa akaninunulia saa Kama zawadi na maisha yakasonga mbele miaka iliyofuata ikawa napita kwenye kipindi kigumu sana hasa kwenye likizo mda mwingi nilikuwa naweza shinda bila kula na mda mwingine tukifunga shule nami naenda kutafuta vibarua kwa mfano niliendaga huko wilaya ya Uyui kata ya Loya kuvua samaki na mwaka mwingine pia nikaenda huko kuvuna mpunga sikurudi nyumbani maana nilikuwa naogopa kurudi home likizo najua nikirudi naweza nusirudi shuleni tena.



Itaendeleaa.....
Mkuu story yako ni nzuri sana na inasisimua. Nilisoma pale tabora boys 2013 hadi 2015 (advance). Tupo pamoja mkuu!!
 
Itiririshe kwa speed ya umeme ,sijui kwa nini hapo kwenye kutoa kijitabu kumenipa simanzi kidogo.Stori kali sana.
 
Itiririshe kwa speed ya umeme ,sijui kwa nini hapo kwenye kutoa kijitabu kumenipa simanzi kidogo.Stori kali sana.
Hapo kwenye uandishi wa kitabu ndio sijajaliwa kuandika labada nitaweza kutafuta mtu aniandikie mkuu
 
Hapo kwenye uandishi wa kitabu ndio sijajaliwa kuandika labada nitaweza kutafuta mtu aniandikie mkuu
Nilikuwa namaanisha pale upo kwa fundi halafu yule mzee anakuuliza maswali kuhusu kupenda shule ukamwambia hata hapa na kijitabu najisomea.Asante.
 
Inaendelea....

Wakati naendelea na shule kwa mapito magumu sana hasa nyakati za likizo Kuna likizo moja ambayo nipatwa na tukio sitalisau maishani mwangu,
Ilikuwa likizo ya mwezi wa kumi na mbili nikiwa tumefunga shule sikubaki hapo shuleni maana nipata rafiki mmoja fundi ujenzi alikuwa ameajiriwa na kampuni moja hivi la ujenzi hivyo huwa wanaenda saiti kwa mda mrefu so kaniomba nikawe nalala getoni kwake mkaa upo gunia mbili na unga kiasi so nitakuwa naenda kufanya vibarua napata hata mboga kidogo.

Nikiwa getoni hapo siku moja asubuhi nikaamka asubuhi na mapema maana nilipewa dili la kwenda kufyeka pale hospital ya mkoa Kitete , basi nilipofika nilikabidhiwa kwanja na kupewa kipande na malipo ni jioni unapewa 5000 hivyo nikakomaa sana huku nyumbani nimetoka hamna kitu sijala Ila nikajikaza sana mpaka saa 10 hivi nikamaliza, nikaenda kuomba malipo yangu yule jamaa mwenye tenda sikumkuta ofsini nikaambiwa Hadi kesho basi nikaondoka mpaka home kulikuwa na akiba kidogo ya unga kidogo nikawasha Moto nikakoroga uji wa chumvi nikanywa nikalala mpka asubuhi nikaenda ili nipewe hela yangu nikapate chakula maana nilikuwa nimezidiwa na njaa.

Baada ya kufika kwenye kiofisi Cha mwenye tenda ya kufyeka nikaambiwa jamaa amepata dharura mpaka week ijayo hapo ndipo nilichanganyikiwa, wazo lilikuja kwa Nini nisiende maeneo ya kipalapala huko Kuna mashamba mengi ya mihogo naweza omba mihogo kadhaa hivi nikatafuna na mingine nikaja chemsha, wazo hili lilipata kibali akilini mwangu nikatembea mpka huko, hapa najua wenyeji wa Tabora mtakuwa mnaelewa vizuri mazingira hayo miaka ya 98 Hadi 2005 hivi palivyokuwa na vichaka tu hakuna watu wengi.

Basi nilitembea Hadi huko pamoja na mchoko na njaa kweli nikakuta shamba la mihogo Safi kabisa nikatazama labda Kama Kuna mji ulioko karibu nikaombe kupewa mihogo hakuna, basi niliamua Sasa kuiba nikaingia nikavuta shina la kwanza mihogo ni mikubwa mno shina moja tu lilinitosha nikachukua mda wakati naanza kuondoka nimeifunga vizuri na mwingine nakula Mara nasikia mwano wa mwizi looh kuangalia mbele watu wanakuja nyuma pia Kuna watu aisee nguvu ziliniishia nikakaa chini watu wakafika wengine wakata nisipigwe kwanza nipelekwe mlimani nikahojiwe vizuri, wengine tumuue hapahapa na kidhibiti anacho.

Itaendeleaa
 
Inaendelea.....

Baada ya kuulizwa maswali mengi na kipigo Cha hapa na pale nikajieleza sana lakini wapi watu hawakunilewa hata kidogo, ikafika wakati nikakata tamaa nikawaambia Kama yote nimewaambia na hamjaweza kuamini basi naomba mniue tu ili nife kuliko kupata maumivu ya kupigo namna hii kateni hata panga moja tu shingoni mtakuwa mmeridhika baada ya maneno hayo nikaona wakatulia kidogo wakashauriana kwamba Kama amesema ni mwanafunzi kwa Nini tusimpeleke shuleni ili tukajiridhishe, wengine wakasema tumwache tu atakuwa amekoma.

Basi katika mashauriano hayo Kuna mtu mmoja ni mwenyeji wa eneo Hilo lakini ni afisa kilimo na mifugo wilaya Uyui kata ya Loya kwa Sasa ni marehemu alikuwa na ndugu yake katibu tawala wilaya ya Nzega mlemavu wa mguu hivi sijui yupo wapi huyu, basi yule afisa kilimo aliomba yeye anichukue na kunipeleka Police wakakubali kwa haraka sana, na Mimi nikachukua mihogo yangu maana walinipa niondoke nayo nikakaa kwenye pikipiki huyoo mpka karibu na shule jamaa kasimamisha pikipiki akaniambia hebu nileze ukweli wa hili Jambo kabla sijakufikisha police nikampa story yangu mwanzo mwisho akaniambia hebu twende kwenye geto uliloachwa na huyo rafiki yako basi nikampeleka tukafika akamuuliza baba mwenye Nyumba akasema kijana huyu alitambulishwa kwangu na kijana ambae ndio mwenye chumba hiki kuwa ni mwanafunzi atakuwepo hapa mpka shule ikifinguliwa, hapo afisa kilimo nikamuona akawa mnyonge Fulani hivi tukaingia ndani chumbani nikamwonyesha nguo na daftari zangu na paper za mitihani yangu hapo akaamini kabisa na kuniambia pole sana huku nakumbuka nae akinipiga vibao kadhaa kule porini.

Baada ya afisa kilimo kuwa mpole akaniambia Sasa mdogo wangu pole sana nakuahidi kukusaidia, nikasema sawa akanipa Kama elfu 30000/= na kuniambia hii naomba ununue mahitaji ya chakula hapa na kesho ujiandae mapema Kuna sehemu nitakupeleka, basi nikachukua maji nikawasha Moto nikajikanda Yale maeneo niliyopigwa na maumivu na makali nikajikanda nikamaliza nikaoga na kuchemsha mihogo yangu nikala kwa soda nikashiba nikalala mpaka kesho asubuhi saa 3 hivi huyu afisa kilimo kaja na watu Kama watu kumbe mmoja ndio huyo afisa tawala wakanichukua na kunipeleka pale mkoani nikakalishwa kwenye ofisi moja nikahojiwa maswali mengi sana.

Baada ya maswali nikaambiwa unamuona huyu mama nikasema ndio basi utakuwa ukiishiwa mahitaji unakuja kwa huyu mama atakupa unachohitaji nikafurahi sana nikatoka hapo Nina amani kweli na baada ya hapo tukaagana mie nikawa narudi getoni nikiwa nimefuata road ya gereza mahabusu nikaona Gari inasimama mbele yangu anatoka mkuu wa shule akaniambia vipi kijana mbona huji hata kunisalimia siku hizi nikawa nimenyamaza tu Sina majibu,

Akaniambia Kuna hela imetumwa toka dar twende nyumbani ukachukue nikaingia kwenye Gari huyoo mpaka kwake nikapewa Kama laki na nusu hivi looh nilifurahi mno nikamwambia mkuu naomba unitunzie hii laki ngoja mie nichukue hamsini inanitosha kabisa.

Itaendeleaa........
 
Back
Top Bottom