Uchaguzi 2020 Kutoka viwanja vya CCM, Lindi: Membe atangaza nia ya Urais!

Uchaguzi 2020 Kutoka viwanja vya CCM, Lindi: Membe atangaza nia ya Urais!

Kiukweli Mwigulu ni jembe ukimlinganisha na Membe.Aliongea kwa muda mrefu tena akiwa na mipango mizuri hadi huchoki kumsikiliza tofauti na leo hotuba fupi halafu hakuna kitu.
KARIBU TUELEKEE 'CAANAN' NA LAMECK M. NCHEMBA! teh teh kwenye asali na maziwa.
 
Kama mtu katika dakika kama hii muhimu kabisa ktk maamuzi ya maisha yako na matumaini ya Watanzania unatoa speech nyepesi kama ile mtu huyu anafaa kuwa hata diwani?

Hata familia yake sidhani kama anaiongoza vizuri
 
Kamanda soma hii kiduchu.

Anawaonea huruma wenzao(Upinzani) kuwa tokea mfumo wa vyama vingi hawajawahi kushinda urais.

-Anawashangaa kuwa kila uchaguzi wanaweka mgombea yule yule ambaye anakuwa kama mfamle.

- Kila uchaguzi wanasingizia kuibiwa kura.

- Anasema kuwa wale wafalme hawataki kuachia ngazi na kubadilisha uongozi wa kifalme( Anaelezea sokosoko utakalopata kama ukitaka kugombea nafasi ya juu utafukuzwa kama panya).

- Anasema uongozi ule ule unaoshindwa miaka yote hawawezi kushinda,watachapwa asubuhi mapema.

Sasa Mkuu Ritz kwa nini awaongelee hao jamaa hata kabla hajapitishwa na chama chake?

Nilitegemea kwa kuwa tupo katika mapambano ndani ya chama chake angejikita sana huko, mfano jinsi gani atarudisha imani ya chama chake ambacho kwa matokeo ya serikali za mitaa yanaonesha hawakufanya vizuri kama chaguzi za nyuma.

Angeongea ni jinsi gani atawaunganisha makanda wa juu wa chama chake iwapo atapitishwa na chama chake.

Angeongelea jinsi ambavyo mathalani miladi ya chama itasimamiwa ili kukisaidia chama kutotegemea kwa sehemu kubwa ruzuku toka serikalini!
Angeongelea pia mathalani mianya katika chama chake na ataziziba vipi

Then mwishoni angeongelea maswala ya SERA kwa maana nini serikali yake itasimamia pamoja na uwepo wa ilani ya chama.

Kwa mlengi huo, angeonekana zaidi kama mtia nia wa sisiemu na sio kama tayari yeye ni mgombe mteule katika nafasi ya urais.

Cc Team Membe
 
Last edited by a moderator:
Iv membe amesahau yy n wazir wa mambo ya nje?
Anavyojnad atasaidia michezo, alkua wap kuanza nalo bado wazir wa mambo ya nje! Ata kupeleka vijana au kushawishi club kutoka nje kuchukua au kuanzsha taasis hapa nchi imesmshinda leo ajiwa rais ndo ataweza

Awa mawazir wanazid kuprove failure kwa uongoz wa j.k
 
Nakumbuka kwenye uzinduzi wa mkutano wa ACT - Wazalendo kule Mwanza kuna mbunge wa CCM alipata mualiko watu walipiga sana kelele kuwa ACT - Tanzania na CCM lao moja.

Sasa leo kulikoni tena kwenye mkutano wa Membe kutangaza nia ya kugombea urais kumejaa wabunge wa Ukawa.

Cc; Mkandara Mchambuzi Mag3 Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
Mara wengine wanaambiwa hawajui kuongea na hao wanaoambiwa wanajua kuongea wanaambiwa hawawezikutekeleza. Basi hata haieleweki mnachokitaka ni nini.
 
Pale ni kwa ajili ya kutangaza nia tu na kuomba ridhaa kwa chama. Zamani hayo mambo yalikuwa yakifanywa ndani ya chama ila kwa kuwa vikao kama halmashauri kuu inahusisha wana CCM wengi ndio maana wameweka huu utaratibu wa kujitangaza kupitia vyanzo mbalimbali. Hii inawahusu wana CCM tu. Huu mkutano sio wa kuwaomba kura kwa Watanzania....Watanzania tutawafuata baada ya kikao cha julai 12 na 13 kukaa.
Kwa hiyo pale alikuwa anaomba ridhaa kwa UKAWA, maana nusu ya hotuba yake amezungumzia Ukawa na nusu iliyobaki kaongelea matambiko na jinsi chama kilivyo na vyama rafiki vya nje.
 
Wewe kilaza...ilani ya chama ndio itasema mgombea wa CCM atafanya nini...ila hayo ya sera uwa hayasemwi siku ya kutanga nia...acha ushamba.

Mi na wewe nani Kilaza urais ni cheo cha kitaifa angewaomba wanachama Wa ccm Tanzania Kwa ujumla
 
Shughuli ya leo imepambwa na usanii mtupu.Sasa hao wasanii wanini?
 
Hizo hadithi za ccm hizo!!!! Wenyewe kwa wenyewe hawapatani hahahaaaaa
 
Membe hivi unatangaza nia au upo kwenye mkutano wa kampeni daahh!!

Na mm nimeshangaa sana, imekua kama ameshapitishwa tayari, kwa mtazamo wangu leo ilikua kutangaza nia sio kampeni, maanna amejipa mamlaka mengi mno kama vile chama kimeshampitisha au kama vile amedokezwa kwamba atapitishwa yeye. Bt ndio siasa bana kila mtu na utashi wake
 
Back
Top Bottom